Jack HD
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 851
- 1,168
Habari wanabodi!!
Kuna tetesi ambazo zilishavuma sana kwa kipindi kirefu sana hapa nchini huku baadhi ya wenzetu wakijitokeza sehemu mbalimbali kuthibitisha tetesi hizo.
Inadaiwa kabla ya wajerumani kukimbia Tanganyika wakati wa Vita ya kwanza ya Dunia baina yao na waingereza na kujikuta wakishindwa vibaya katika vita hiyo walikuwa wamemiliki hazina na Mali nyingi ndani ya eneo lao lililojulikana Germany East Africa Terrirory.
Haikuwa rahisi baada ya kushindwa vita hivi kuondoka na mali zao zote kwenda nazo Ujerumani. Hivyo basi, mali na hazina nyingi inasemekana zilifinywa maeneo mbalimbali hapa nchini. Kuna ambazo zilifichwa chini ya milima, kwenye mahandaki na kwingineko kama habari zilizotufikia zilivyokuwa zikienea.
Kuna watu ambao walijaribu Mara kwa Mara kuzifikia hazina hizi lakini hakuna aliyewahi kujitokeza na kutabainisha kuwa alifanikiwa kupata hata kipande kidogo cha hazina hizo. Kuna wengi ambao pia walikuja na madai kuwa kwenye maeneo hayo kuna ushirikina mkubwa ambao wajerumani waliufanya hivyo ni vigumu kuweza kufikia hazina hzo bila idhini yao.
Nakumbuka kipindi cha nyuma kuna jamaa mmoja alitoa ushuhuda huko sehemu za tabora kuwa wajerumani walifika na kwenda kuchukua baadhi ya Mali walizoziacha na walifanikiwa na haikuonekana kama ilikuwa ni kazi kubwa kwa upande wao. lakini wananchi wa maeneo hayo wamejaribu kuzifikia hizo hazina kwa miaka bila mafanikio.
Hii inanipeleka niwaze kuhusiana na nchi ya Misri. Kupitia filamu mbalimbali tumekuwa tukiaminishwa nchi ya misri hususani kwenye zile pyramid zake kuna hazina kubwa ikiwemo dhahabu ambayo huwezi kukisia utajiri wake.
Swali ni je, habari kuhusu hizi Mali za wajerumani zilizofichwa ni za kweli? Zimefichwa maeneo gani? Kwanini wazawa hatuwezi kuzifikia hizi Mali? Je, hii nadharia ya ushirikina kwenye maeneo haya ni ya kweli? Ni kweli pia kuwa wajerumani huwa wanafika kuchukua hizi Mali zao walizoficha.
Lets contribute na tujifunze
Kuna tetesi ambazo zilishavuma sana kwa kipindi kirefu sana hapa nchini huku baadhi ya wenzetu wakijitokeza sehemu mbalimbali kuthibitisha tetesi hizo.
Inadaiwa kabla ya wajerumani kukimbia Tanganyika wakati wa Vita ya kwanza ya Dunia baina yao na waingereza na kujikuta wakishindwa vibaya katika vita hiyo walikuwa wamemiliki hazina na Mali nyingi ndani ya eneo lao lililojulikana Germany East Africa Terrirory.
Haikuwa rahisi baada ya kushindwa vita hivi kuondoka na mali zao zote kwenda nazo Ujerumani. Hivyo basi, mali na hazina nyingi inasemekana zilifinywa maeneo mbalimbali hapa nchini. Kuna ambazo zilifichwa chini ya milima, kwenye mahandaki na kwingineko kama habari zilizotufikia zilivyokuwa zikienea.
Kuna watu ambao walijaribu Mara kwa Mara kuzifikia hazina hizi lakini hakuna aliyewahi kujitokeza na kutabainisha kuwa alifanikiwa kupata hata kipande kidogo cha hazina hizo. Kuna wengi ambao pia walikuja na madai kuwa kwenye maeneo hayo kuna ushirikina mkubwa ambao wajerumani waliufanya hivyo ni vigumu kuweza kufikia hazina hzo bila idhini yao.
Nakumbuka kipindi cha nyuma kuna jamaa mmoja alitoa ushuhuda huko sehemu za tabora kuwa wajerumani walifika na kwenda kuchukua baadhi ya Mali walizoziacha na walifanikiwa na haikuonekana kama ilikuwa ni kazi kubwa kwa upande wao. lakini wananchi wa maeneo hayo wamejaribu kuzifikia hizo hazina kwa miaka bila mafanikio.
Hii inanipeleka niwaze kuhusiana na nchi ya Misri. Kupitia filamu mbalimbali tumekuwa tukiaminishwa nchi ya misri hususani kwenye zile pyramid zake kuna hazina kubwa ikiwemo dhahabu ambayo huwezi kukisia utajiri wake.
Swali ni je, habari kuhusu hizi Mali za wajerumani zilizofichwa ni za kweli? Zimefichwa maeneo gani? Kwanini wazawa hatuwezi kuzifikia hizi Mali? Je, hii nadharia ya ushirikina kwenye maeneo haya ni ya kweli? Ni kweli pia kuwa wajerumani huwa wanafika kuchukua hizi Mali zao walizoficha.
Lets contribute na tujifunze