Rupia: Hazina ya Mjerumani

Rupia: Hazina ya Mjerumani

Habari wanabodi!!

Kuna tetesi ambazo zilishavuma sana kwa kipindi kirefu sana hapa nchini huku baadhi ya wenzetu wakijitokeza sehemu mbalimbali kuthibitisha tetesi hizo.

Inadaiwa kabla ya wajerumani kukimbia Tanganyika wakati wa Vita ya kwanza ya Dunia baina yao na waingereza na kujikuta wakishindwa vibaya katika vita hiyo walikuwa wamemiliki hazina na Mali nyingi ndani ya eneo lao lililojulikana Germany East Africa Terrirory.

Haikuwa rahisi baada ya kushindwa vita hivi kuondoka na mali zao zote kwenda nazo Ujerumani. Hivyo basi, mali na hazina nyingi inasemekana zilifinywa maeneo mbalimbali hapa nchini. Kuna ambazo zilifichwa chini ya milima, kwenye mahandaki na kwingineko kama habari zilizotufikia zilivyokuwa zikienea.

Kuna watu ambao walijaribu Mara kwa Mara kuzifikia hazina hizi lakini hakuna aliyewahi kujitokeza na kutabainisha kuwa alifanikiwa kupata hata kipande kidogo cha hazina hizo. Kuna wengi ambao pia walikuja na madai kuwa kwenye maeneo hayo kuna ushirikina mkubwa ambao wajerumani waliufanya hivyo ni vigumu kuweza kufikia hazina hzo bila idhini yao.

Nakumbuka kipindi cha nyuma kuna jamaa mmoja alitoa ushuhuda huko sehemu za tabora kuwa wajerumani walifika na kwenda kuchukua baadhi ya Mali walizoziacha na walifanikiwa na haikuonekana kama ilikuwa ni kazi kubwa kwa upande wao. lakini wananchi wa maeneo hayo wamejaribu kuzifikia hizo hazina kwa miaka bila mafanikio.

Hii inanipeleka niwaze kuhusiana na nchi ya Misri. Kupitia filamu mbalimbali tumekuwa tukiaminishwa nchi ya misri hususani kwenye zile pyramid zake kuna hazina kubwa ikiwemo dhahabu ambayo huwezi kukisia utajiri wake.

Swali ni je, habari kuhusu hizi Mali za wajerumani zilizofichwa ni za kweli? Zimefichwa maeneo gani? Kwanini wazawa hatuwezi kuzifikia hizi Mali? Je, hii nadharia ya ushirikina kwenye maeneo haya ni ya kweli? Ni kweli pia kuwa wajerumani huwa wanafika kuchukua hizi Mali zao walizoficha.

Lets contribute na tujifunze
 
Moja kwa moja utawaza kuhusu rupia(rupee ya mjerumani) na pesa nyingine za kale na yale yanayosemwa kuzihusu hasa kwenye habari nzima za kichawi
Watu wamezinguka na kuzinguliwa hasa watu wametapeliwa na wengine kufa wakitafuta hivi vitu vinavyotajwa kuwa na thamani kubwa

Ukweli huu hapa na si pesa tu bali na vitu vingine vya kale
1. Aina ya malighafi iliyotumika
Wakati huo vilitengenezwa vitu imara sana kutokana na upatikanaji wa malighafi ya kutosha ...vitu kama vyombo vya bati na chuma urembo kama bangili mikufu pete nk leo hii ukivipata na kuviyeyusha kila kimoja unaweza kutengeneza kumi kupitia hicho kimoja

2. Uhifadhi
Wajerumani kwa hapa kwetu walikuta malighafi vito na madini ya kutosha sana! Kutokana na uhifadhi hafifu wakati huo vingi ya hivi vitu viliwekwa tu majumbani mwao wakiviandaa kuvidafirisha kwao
Vita ya pili ya 1939-45 iliwachanganya mno na walipoelekea kushindwa waliamua kuficha mali yote kwenye mashimo makubwa mashambani misituni kwenye mahandaki na milimani kusikofikika kwa urahisi kisha wakawaua watu karibia wote walioshiriki na wanaojua yale maficho wakasepa
Huku kote mali hizo zilihifadhiwa kwenye vyumba imara vilivyojengwa kwa zege gumu hasa ili iwe ngumu kuchimbua ama kuvunja na kama ni mapangoni yalikuwa mapango ya mbali hasa milimani na misituni

3. Dhana ya majoka na viumbe wa ajabu
Huko kwenye hayo maficho kuna baadhi ya watu walisalimika hivyo wakasimulia vizazi vilivyofuata
Kizazi cha kusaka utajiri wa haraka kikaona fursa na kuamua kuchangamkia dili. ..Wajerumani hawakuweka ulinzi wowote wa majoka! Hao ni viumbe tu walijitwalia makazi huko ambako ndio maisha yao yaliko
Watu walioenda bila tahadhari waliumwa na hayo madubwana na kupoteza maisha! Waliosalimika walitimua mbio na kuunda stories za kufikirika

4. Dhana ya uchawi na majini
Kwa wale waliosaka kwenye mahandaki na mashimo marefu yenye vyumba vilivyojengwa kwa zege , baada ya kufanikiwa kuvunja hayo mazege na kutaka kuingia ndani nao walikutana na mauzauza ya kila aina
Unajua ni kwa nini? Sehemu yoyote yenye mfumo wa nyumba ama chumba isiyokaliwa na binadamu roho zinazotangatanga na mapepo hufanya makazi yao kumbuka ile mada ya kutakasa makazi! Hivyo ukiingia huko lazima ukutane na vitu vya ajabu...Mjerumani hahusiki kabisa!

5. Uamuzi wa kufanya kafara ama tambiko kabla ya kuchimba ama kuingia pangoni
Wengi walitafuta waganga wa kienyeji kwenye hili na hawakufanikiwa. ..waliofanikiwa walifanikiwa kwa ujanja tuu....ukienda kwenye pango misituni ukachinja mnyama ukapiga manyanga automatically mkiondoka ile nyama italiwa na kuna wakati manyanga huleta kelele na kufukuza mnyama yoyote aliyeko pangoni...ndio maana baada ya kafara hamuingii siku hiyo hiyo bali kesho yake nk
Wale wa kwenye mashimo NA mahandaki ni ibada tu ya kuziomba roho ziondoke ama kuzifukuza kwa kutumia mitishamba na harufu wasizozipenda....mkikutana na roho korofi mtachezea kichapo mpaka muache kila kitu na kutimua mbio kali sana

6. Ukweli hasa ni UPI?
Baada ya vita ya pili kukoma na baadae Uhuru wajerumani walishindwa kurudi kwa ubabe hivyo wakatumia njia za kijanja kurudi
Unajua waliondoka na ramani zote kule mali zilikofichwa hivyo walirudi kuzichukua kwa njia ya kununua yale maeneo na kuyaendeleza kwa kujenga shule vyuo hospital nk ama miradi ya barabara ufugaji na kilimo
Kwa njia hii walichukua vyao kiulaini mno

7. Thamani na umaarufu wake ni UPI!?
Vitu vya kale kwa wenzetu vina thamani kubwa sana....wenzetu wana utaratibu wa kuweka vituo vya antiques na kuchaji watalii pesa ndefu kuviangalia . kila kimoja kinakuwa kimeandikiwa historia yake. Kwa hiyo wakija huku kuvitafuta wengi huenda kuviuza kwenye hayo maduka kwa bei kali mno

8. Nguvu ya utajiri
Biashara imevamiwa , vitu vya kale haviwezi kukupa utajiri wa miujiza ..havina huo uwezo bali kuna baadhi kutokana na malighafi iliyotumika kuvitengeneza vina mvuto kwenye ulimwengu wa giza kama mabangili ya shaba

9. Usumbufu
Kuna watu wanawachezea wenzao shere na kuwasumbua bila sababu.. Miaka hiyo pesa ilitengenezwa kwa mpango maalum(nadhani hata sasa) na zilitengenezwa kwa miaka... Kuna miaka pesa hazikutengenezwa. Sasa mtu anakupa dili na kukuahidi kukupa pesa ndefu ukimletea rupee ya mwaka fulaniView attachment 526110

10. Hitimisho
Kuna baadhi ya sehemu kulikofichwa hizo mali wafichaji walinuizia ama kufanya mambo ya giza ili atakayejaribu kuchukua ama apate madhara au asizione kabisa...lakini kwa sehemu kubwa ni habari zilizotiwa chumvi nyingi


JUMAPILI NJEMA
Jr[emoji779] [emoji781]
Hivyo vitu yani madini nikweli yaliachwa mi hapa binafsi kijijin kwetu kwa utashi Wangu kijijin kwetu kuna sehemu kulikuwa na becone fulani alafu nondo ikawa imechomoka juu tukawa hatuelewi walikuja jamaa fulani ambao kati yao mmoja alikuwa wa maeneo ya kwetu alikuwa someone informed na mwingine alikuwa ni mzungu wengine hatukuwajua that was 1985 na wqlikuja mchana sa8 tukichunga hapo wakafanya yakwao pale kichotokea baada ya kupomoa hixo zege la nguvu walitoa chupa fulani zilikuwa na tobo chini ambalo ukingiza kidole kinazama chupa zilikuwa na red mercury yule jamaa wa kwetu a lichenga Magorofa mpaka Leo yupo sasa jiulize red mercury 1gram ni million ngapi na Walitoa chupa 5 za lita 2...
 
Kiukweli mm bado sina uhakika kama yapo kwasababu BINAFSI sijafuatilia kiundani na sikutilia maanani kwa kuwa kuna mengine kama hayakuniingia akilini(niliona ni mepesi sana), ILA ninachofahamu hadi sasa kuna eneo nilienda kulingana na maelezo niliyopewa nikakuta kuna dalili za hiyo kitu.

ILIKUWAJE:
Nilivoulizia zile alama ktk mawe kule mwanza(mawe mengi yana alama za michoro km chokaa, mfano alama ya jiwe ambalo maji yalikua yakitiririka kupitia hapo kisha yakakauka)..... Maelezo nlopewa yaliendana na hicho mshana jr alichosema, ila jamaa alikua na ushahidi zaidi, kwa kuwa alinifundisha maana ya alama zote kuanzia hiyo michoro ya chokaa, aina ya miti, mchanga.... na alinipitisha ktk maeneo yote yaliyo karibu ili kuona mifano halisi.

Kwa ufukunyunyu wangu siku moja nikaenda mbali sana huko nyegezi af unapanda huko ndani ndani. Nikachagua moja ya alama na kuanza kufatilia kadri alivyonieleza..... nikakuta kuna mahali kuna jiwe(ama zege hivi) kama limeegeshwa...... nilipologonga.... ulitoka mlio mithili kuna uwazi kwa chini....sikufatilia zaidi ya hapo kwa kuwa nilijawa hofu........ ila ipo siku nitakwenda na team tukafanye mambo.

Maeneo yenye hizi mambo mengine unakuta ni kambi za jeshi, na kwa maelezo ya jamaa waliofanikiwa kupata hazina hii ni wajeda wakubwa tu(haiwekwi wazi) ingawa wao walitumia njia rahisi ya kununua maji(au mafuta) toka kwa familia za kijerumani zinazojua maswala haya(hii ni kwa mujibu wa maelezo ya jamaa).

Masharti ya kuingia maeneo haya.

1. Usisex wala kujielekeza sana na mawazo ya sex kwa muda usiopungua miezi6(maana yake uwe masafi(pure), kuna uwezekano ukiwa bikra unafanikiwa zaidi) pia usiwe na mawazo ya chuki, hasira.
2. Ukiwa eneo hili hamtakiwi kula kula(kama ni kula mkalie mbali huko)
3. Usiende kwa mganga kwa nia ya kudhuru(wapo waganga wanaoelewa hilo na wanajua namna ya kuwashauri)
4. Mnapoenda, msiwe na mawazo ya kidhuluma(yani km ni mgawo, uwe sawa sawa kama mlivokubaliana)
5. Uwe jasiri, vile vitu unapokutana navyo ni vitisho tu, havidhuru, mtu anadhurika kwa woga wake na panic, na pia utakapoogopa na kupiga kelele ndo mauza uza yanapozidi.
6.Msiwe waropokaji, hapa jamaa alisema utakaposema sema habar hizo kwa wasiohusika(kwamba mna mzigo) utakua unapotea potea....
7. Haitakiwi kelele, msiongee ongee, mnatakiwa kuweka akili yote katika jambo mnalofanya(ikiwezekana mjifunze kuwasiliana kwa ishara kabla hamjaingia)

Kikubwa hapa ni kuwa waangalifu kwa mazingira yanayokuzunguka, kuchunga hali ya hatari ili usidhurike na vitu halisi mfano nyoka, wanyama, wadudu na mawe kuporomoka.
Mbona Sasa Tunakufa Maskin Nawaka Upo Embu Fanya Makeke Twende Huko

Mshana Jr Atatupa Elim Zaid

Cc: Mshana Jr
 
Back
Top Bottom