Russia World Cup 2018: France crowned World Champions after defeating Croatia 4-2

Teh teh teh nimeamua kujitoa mhanga nina Imani na vijana wangu akina Kante pogba Nadhani watawadhibiti vilivyo De Bruyne,Lukaku na Hazard na kazi itakuwa imeisha.Huku Dogo Mbape akiendelea kuleta shida pale mbele,ila Giroud Huwa simuelewi elewi
Giroud hatabiriki na ni ngumu kueleza kwanin yupo kikosini .... tutaona baadae.
 
Ukiangalia nchi/timu zote zilizochukua kombe la dunia, utagundua kuwa kulikuwa na ile inaitwa golden generation. Kwa mfano brazil ile ya kina pele % kubwa ni walewale ndio walichukua kombe mara zile tatu. Kina Didi, Vava, Pele, Garincha Zagalo n.k.

1978 Argentina wanachukua kombe wakiwa na kizazi cha dhahabu, kina Valdano, Burcharga na 1986 wanarudia wakiwa wameongeza mastaa kibao akiwepo Diego Maradona, na Caniggia.

1990 Ikawa kama hii ya 2018 timu kibao zilienda zikiwa ma mastaa kibao. Uingereza ya Shilton, Paul Parker, Peter Birdslay, Terry Butcher, Chriss Wadle, Garry Liniker na wengine.

Ujerumani ya Ruddy Voller, Klinsmann, Andreas Brehme, Lother Matheus nk.

Argentina ya Maradona, Ganigia, Valdano, Burchagga nk

94. Brazili ya wakali kina bebeto, Cufu,Romario,, Leonardo, Aldair marius Santos, Captain Dunga, Mazinho, Mauro Silva, Rai nk.

98. France ya Zizou, Lizarazu, Desaily, Libouf, Deschamp, Karembeu,Viera na kina Hendry.
2002. Brazili ya kina Di lima, GAUCHO, Rivaldo nk

2006. Italia ya Pirlo Canavarro, Gatuso, Zambrota na wakali kobao. Fabio Grosso na Vincenzo Ianquitta.

2010. Spaini hii ndio ilikuwa nuksi. Kila mtu analijua hilo. Spain hii ilichukuwa euro 2008, ikachukua world cup 2010, na euro tena 2012. Mastaa kibao Xavi,Iniesta,Puyol,Avid Villa nk.

2014. Germani ya Khadera, Ozil, Gotze, Muller, closer, na nyota kibao.

Sasa 2018. Nchi zenye mastaa na walipewa nafasi ya kushinda ni Brazil, Belgium,France, Argentina na German ambao %kubwa ndio walishinda 2014. Baadhi zimeondolewa. Zilizobaki ni france na Belgium. England ina nyota lakini hawafikii hata wa croatia.

Kwa maoni yangu nusu fainali hii mshindi kati ya france na belgium ndio ataibuka mikono juu. England watapata tabu sana kwa croatia. Na nina uhakika watatolewa maana watakuwa na pressure kuliko Croatia.
 
Umenena vyema
 
Maelezo mazuri
 
Leo nitatupia posts Kwa fujo usiku najua wengi mtalala na viatu mtakuwa mnasoma tu posts Kwa mbali kama hamuoni Ila muwe mnalike kuonyesha uwepo wenu
Hahahaaa. Mie huwa sipendi kuchanganya kuangalia na kuandika hivyo Mkuu we tupia tu posts zako ila kesho asubuhi mie nitakuwa wa kwanza kukutembezea dole gumba kwenye kila Post Mkuu.
 
Baada ya Argentina kutolewa binafsi ladha imepungua sana tena sana...kwa brazil ni kawaida tu ni kama australia na panama
Hahahaaa. Kaka watonesha kidonda cha Sesten ujue. [emoji12] [emoji12]

Sababu anadai Brazil kutolewa mashindanoni ndio maajabu badala ya kuchukua Kombe. Hahaaaa.

Hivi maajabu yanakujaje wakati wapo matop zaidi yake wameshatolewa na ilikuwa jambo la kawaida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…