Naam mkuu, you are very right, mimi kama shabiki mkubwa wa soka naangalia timu inavyocheza na katika soka ninachoshangilia ni mpira kutinga wavuni. Ninachojali ni matokeo na timu hata kama inacheza vizuri namna gani lakini kama ama hawafungi au hawalindi goli lao wasifungwe basi kwangu haifai. Baada ya leo nakiri timu ya England bado changa na Kombe la dunia wataendelea kuiota tu hadi watakapokomaa.
Mkuu kuanzia hatua ya makundi, wengine tumekuwa tunatathmini timu kwa uchezaji na ushindi, kuna wakati tulikera watu na kuitwa 'hater' lol
Hatua za mwanzo nilitamani timu za Afrika zitolewe. Ilikuwa ni fedheha siyo aibu tena
Egypt- Akili ilikuwa kwa Salah. Mfumo wa uchezaji wa kukimbiza mipira. Hakuna pattern
Tunisia- Hawaeleweki wanacheza mchezo gani zaidi ya kulinda goli. Ushambulizi zero
Nigeria- Wanauwezo wa kumiliki mpira hawana uwezo wa kuzuia mashambulizi
Hawakuwa na wachezaji wanaoweza kufunga isipokuwa yule mmoja wa mbele
Hatukuona Nigeria ya Peter Rufai, Okocha, Sunday Olisei, Amunike n.k
Senegal- Dah, hawa walipita pita huku Afrika ilikuwa aibu kwakweli
Morocco- Hawana tofauti na Egypt kwa uchezaji, mpira wa kukimbiza
Hatukuwahi kuona ile Cameroun ya akina Makanaki, mfede, Roger Miller au Ghana 2010
Afrika ilikuwa ni aibu katika mabara yote bila kumung'unya maneno
Japan na Korea- Timu zimeonyesha mchezo tofauti sana. Wanakasi sana na waliweza kuwashangaza wapinzani wao. Ni timu zitakazosumbua sana Qatar 2022
Timu nilizozipa nafasi zilikuwa Brazil,Croatia na Uruguay, Potugal na Spain.
Ilipofika knock out nilibaini timu za kuogopwa kama Serbia, Belgium na Sweden
Kiwango cha timu hizo hakiwezi kulinganishwa na timu yoyote ya Afrika au Asia
Brazil- Wanakanyaga soka, hawataki kukabwa ,hujiangusha angusha wapate dead ball au penalty. Akili zote walimkabidhi Neymar aliye prove si lolote
William au Macello wangeweza kuwa vyanzo vya magoli.
Waliwaogopa Neymar na Coutinho.Mipira yote wanasubiri kuwapatia hao wawili.
Argentina- Hawakuwa katika kiwango wakimtegemea Messi pekee.
England- Walipita pita kutokana na makundi, kiwango kilikuwa kidogo
Mashabiki walidhani England inaundwa na 'PL' na kuweka matumaini ya uongo
Harry Kane na chapuo zote hakuwa na lolote la maana. Anasubiri cross hachezeshi timu
Ufaransa- Wanamchezo usiotabirika. Wana uwezo wa kuzuia na kujenga mashambulizi toka nyuma. Wanacheza na viungo sana. Mabeki wana uwezo wa kupanda.
Forward yao ni nzuri kwa counter attack, wakikuotea huchomoi kwa ball possession yao na ile counter attack ya kasi
Croatia- Kama Serbia, Belgium na Sweden wanakanyaga mpira wanajua nini wanataka
Wana umiliki wa mpira na uhakika wa pasi, tatizo kubwa kwa Mfaransa
Croatia kwenda fainali si bahati ni 'mission'. Kama kuna mtu anaweka dau mahali, Croatia ni eneo la kuwekeza. Nikitazama na Ufaransa, naona Croatia mabingwa wa Dunia