Russia World Cup 2018: France crowned World Champions after defeating Croatia 4-2

Russia World Cup 2018: France crowned World Champions after defeating Croatia 4-2

It's coming HOME,
It's coming HOME
Premier League is coming home on your TV next month not the World Cup .Like I Said this WC will go to the Underdog. I want Croatia to win it now.

DonDonald

Damn I'm gutted.... but these kids deserve our applause for what they have achieved, because before the tournament started nobody gave them a chance to reach this stage (Media, Pundits, Fanatics, Haters)

They did the country proud, better days to come SOON
 
Naam mkuu, you are very right, mimi kama shabiki mkubwa wa soka naangalia timu inavyocheza na katika soka ninachoshangilia ni mpira kutinga wavuni. Ninachojali ni matokeo na timu hata kama inacheza vizuri namna gani lakini kama ama hawafungi au hawalindi goli lao wasifungwe basi kwangu haifai. Baada ya leo nakiri timu ya England bado changa na Kombe la dunia wataendelea kuiota tu hadi watakapokomaa.
Mkuu kuanzia hatua ya makundi, wengine tumekuwa tunatathmini timu kwa uchezaji na ushindi, kuna wakati tulikera watu na kuitwa 'hater' lol

Hatua za mwanzo nilitamani timu za Afrika zitolewe. Ilikuwa ni fedheha siyo aibu tena

Egypt- Akili ilikuwa kwa Salah. Mfumo wa uchezaji wa kukimbiza mipira. Hakuna pattern
Tunisia- Hawaeleweki wanacheza mchezo gani zaidi ya kulinda goli. Ushambulizi zero

Nigeria- Wanauwezo wa kumiliki mpira hawana uwezo wa kuzuia mashambulizi
Hawakuwa na wachezaji wanaoweza kufunga isipokuwa yule mmoja wa mbele
Hatukuona Nigeria ya Peter Rufai, Okocha, Sunday Olisei, Amunike n.k

Senegal- Dah, hawa walipita pita huku Afrika ilikuwa aibu kwakweli
Morocco- Hawana tofauti na Egypt kwa uchezaji, mpira wa kukimbiza

Hatukuwahi kuona ile Cameroun ya akina Makanaki, mfede, Roger Miller au Ghana 2010
Afrika ilikuwa ni aibu katika mabara yote bila kumung'unya maneno

Japan na Korea- Timu zimeonyesha mchezo tofauti sana. Wanakasi sana na waliweza kuwashangaza wapinzani wao. Ni timu zitakazosumbua sana Qatar 2022

Timu nilizozipa nafasi zilikuwa Brazil,Croatia na Uruguay, Potugal na Spain.
Ilipofika knock out nilibaini timu za kuogopwa kama Serbia, Belgium na Sweden

Kiwango cha timu hizo hakiwezi kulinganishwa na timu yoyote ya Afrika au Asia

Brazil- Wanakanyaga soka, hawataki kukabwa ,hujiangusha angusha wapate dead ball au penalty. Akili zote walimkabidhi Neymar aliye prove si lolote

William au Macello wangeweza kuwa vyanzo vya magoli.
Waliwaogopa Neymar na Coutinho.Mipira yote wanasubiri kuwapatia hao wawili.

Argentina- Hawakuwa katika kiwango wakimtegemea Messi pekee.

England- Walipita pita kutokana na makundi, kiwango kilikuwa kidogo
Mashabiki walidhani England inaundwa na 'PL' na kuweka matumaini ya uongo

Harry Kane na chapuo zote hakuwa na lolote la maana. Anasubiri cross hachezeshi timu

Ufaransa- Wanamchezo usiotabirika. Wana uwezo wa kuzuia na kujenga mashambulizi toka nyuma. Wanacheza na viungo sana. Mabeki wana uwezo wa kupanda.

Forward yao ni nzuri kwa counter attack, wakikuotea huchomoi kwa ball possession yao na ile counter attack ya kasi

Croatia- Kama Serbia, Belgium na Sweden wanakanyaga mpira wanajua nini wanataka
Wana umiliki wa mpira na uhakika wa pasi, tatizo kubwa kwa Mfaransa

Croatia kwenda fainali si bahati ni 'mission'. Kama kuna mtu anaweka dau mahali, Croatia ni eneo la kuwekeza. Nikitazama na Ufaransa, naona Croatia mabingwa wa Dunia
 
Croatia ndo ameishia hapo...kombe linaenda kwa ufaransa....defence ya France imesimama sana...forward za France ni hatar tupu hawafanyi makosa ya kijinga kama waingereza mnapata nafas af mnacheka Cheka na gori...mapema sana kombe linatua Paris .....watu tuendelee na mambo mengine
 
Pale ambapo hata mkoloni wa dunia anapoteza Kwa timu ndogo kama Croatia inatutia moyo sisi Africa kuwa kutolewa mapema Kwa timu zetu sio Kwa kizembe ni mchezo Tu kama wa tatumzuka
Croatia sio timu ndogo ni wazuri sema miaka ya hivi karibuni walipotea japo hawajawahi kuchukua WC
 
Wazee wa It's coming home wamejitahidi hadi kufika nusu fainali, ila walijisahau na kuanza kupiga kelele kutuaminisha wana timu bora kuliko zote..

It's coming home!! Coming home what? Maybe fourth position...
 
Kakaa!we ulikua kwa malkia!?
Naam khaswa tafuta thread yoyote inayozungumzia the three lions utanikuta. Kiukweli hatua tuliyofikia tunajipongeza khaswa jinsi watu walivyo kuwa wanatubeza kwa miaka mingi mpaka bezo likageuka chuki ni jambo jema sana. Lengo lilikuwa kufika fainali ila asie kubali kushindwa si mshindani hapo tulipoishia wengi walitamani tena magwiji ila hawakusogea.
 
Naam khaswa tafuta thread yoyote inayozungumzia the three lions utanikuta. Kiukweli hatua tuliyofikia tunajipongeza khaswa jinsi watu walivyo kuwa wanatubeza kwa miaka mingi mpaka bezo likageuka chuki ni jambo jema sana. Lengo lilikuwa kufika fainali ila asie kubali kushindwa si mshindani hapo tulipoishia wengi walitamani tena magwiji ila hawakusogea.

Pole sana akhui,,kiukweli mmejitahidi sana mlipofikia...timu zilizopewa nafasi kubwa zimeshindwa hata kufika robo final. Hongereni sana. Next time insha Allah
 
Kwa hali ilivyo croatia ni wazi croatia anamfunga leo England na kwenda kubeba worldcup kirahisi against France

Pia ikumbukwe rekodi zinaonyesha kila baada ya miaka 20 kombe la dunia hupata bingwa mpya na kwa timu zilizobaki ni wazi croatia ndio bingwa mpya mwenyewe kwani France na England wote wameshawahi kubeba kombe hili

Kuchukua ubingwa kwa Croatia pia itasaidia kuuonyesha ulimwengu ubora wa kiungo Luka Modric ambaye amekuwa underated kwa muda mrefu na wanazi wa soka

Tukutane baadae saa 3 kamili kuthibitisha haya

Tumuombee Croatia abebe mkuu
 
Back
Top Bottom