Mwenyekiti Ufipa st amekusikia
Ruto ni Magufuli wa Kenya
Na hili ndio kosa chadema wanataka kulifanya, kujikomba kwa mama Samiah kwa uongo wa maridhiano. Shauri zao. Wajitenge mapema na mama Samiah hana jipya kwao, atawazungusha na baadae kuwatosa wabaki wanalia. CCM haijawahi kuipenda CHADEMA hata siku moja. Mtu wa karibu amshauri Mbowe.
Madesa yamechanganyika hapa. Au nasema uongo ndugu zangu?Walamba asali ni Tundu Lisu, Mbowe, Zito Kabwe, Nape, Makamba & Co.
Madesa yamechanganyika hapa. Au nasema uongo ndugu zangu?
Watu hubadilika. Zaidi sana picha tu mkuu? Suala siyo itikadi? Kama ni itikadi huyo mwamba ni huyu hapa in black and white:
Raila uses friendship with Magufuli to win over voters
Siyo kweli, Uhuru Kenyata na Raila wamekampeni pamoja kama team na Uhuru Kenyata ndiyo bosi wa Mbowe, Tundu na CCM ya sasa hivi!
Raila alikuwa rafiki chanda na pete wa mwendazake. Yupo kwenye records akisema akichukua nchi atakuwa kama mwendazake.
Mwendazake hajawahi kuwa na cha kufanya na Mbowe wala Lissu. Itoshe kusema sera za mwendazake ambazo ni msingi wa sera za baba hazijawahi kuwa msingi wa hao unaoonekana kuwakasirikia mno kutokea kusikojulikana.
Ukombozi wa nchi hii unawahitaji wenye moyo.
Somo la Ruto ni la manufaa kwetu ukiwamo wewe kama nawe umechoshwa na walamba asali wetu na tozo zao.
Raila na Uhuru wamekampeni dhidi ya Ruto, kama ni kweli Raila alikuwa team Magufuli, Mbowe alifwata nini kwa Raila Nairobi ? Mbowe na Tundu ni adui wa Magufuli wanamshambulia mpaka leo hii sasa iweje Mbowe aende kumtembelea Raila? Mbona hakukutana na Ruto popote pale?
Usichanganye mambo, kupenda sera za Magufuli siyo kumpenda Magufuli, ni vitu viwili tofauti, hata Samia akizidiwa huongelea sera za Magufuli ingawaje humnanga kila apatapo nafasi!
Kwani Chadomo wakiingia hawatalamba asali ila watalamba pilipili?Walamba asali wamejisahau. Wamedhani sisi tunayo furaha mno wao na familia zao wakiendelea kujimilikisha nchi na kujineemesha.
Tozo hizi wanazo turundikia sisi, zina ridhaa gani nasi?
Ruto na jamii ya Wakenya iliyochoka mno na madhila kama ya kwetu, ilisimama imara vilivyo kuwakataa walamba asali wa namna ya kwetu:
View attachment 2329076
Kujizatiti kupata utawala wa haki na usawa kwa hakika inawezekana.
Kwani kwa huyu huoni wanolamba asali ni nani?Kwani Chadomo wakiingia hawatalamba asali ila watalamba pilipili?