Uchaguzi 2020 Ruzuku ya CHADEMA yanunulia magari ya kampeni

Uchaguzi 2020 Ruzuku ya CHADEMA yanunulia magari ya kampeni

Mlihoji sana ruzuku inakwenda wapi. Haya ni baadhi tu ya maandalizi ya uchaguzi magari 25 mapya ya kupigia kampeni


MAGARI mengine mapya 25 ya Chama kwa ajili ya maandalizi ya Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2020 yamefika Dar es salaam.
sio ni yeye tena mzigo m4c , biashara kibiashara biasharani
 
Ha ha ha aa! Naona nimegusa pasipogusika. Hata hivyo, Mkuu, unaweza kunisaidia kurejesha utimamu wa akili zangu kwa kujibu swali hili

"Je. bilioni 10 za ela za kitanzania ambayo ni sehemu ya ruzuku imetumika kufanya nini!?"
Kabla ya kukujibu huo utumbo, nakutaka ulete uthibitisho kwamba bilioni 10 zimeshatumika. Kama hazijatumika, kuna tatizo gani?
 
Tuwekee na kadi za hayo magari tuond mmiliki wake ni nani, maana nasikia magari yote yana jina la Mbowe, baada ya uchaguzi anachukua magari yake.
Aliyekusikilizisha ulishindwa kumwambia akuoneshe hizo kadi zinazoonesha umiliki wa hayo magari ni ya Mbowe.?
 
usijitoe faham beberu linalozungumziwa hapa unalijua, chadema ni wapinzani uchwara kila kitu wanapinga bt hata siku moja hatujasikia wakipinga kupokea ruzuku hapo ndo mnapaswa mjiongeze nyie mbulula mnaopa support
Kwa taarifa yako ruzuku ni kodi ya watanzania woote ipo kikatiba kila chama kinapewa kulingana na vigezo!!
Acha ujuha na wivu wa kike!!
Mlileta HADI TAKUKURU kuchunguza matumizi ya ruzuku bado tuu hamjaridhika??
Bado vitatua vifaa vingine vya kampeini subiria!!
 
Well & good. Tunaomba huko mbeleni badala ya kununua magari zaidi, ni vyema wakajenga ofisi kila mkoa. Nina uhakika hayo magari hayapungui 70m@, lakini 70m tunaweza kununua eneo la heka moja+ kila mkoa kwa bajeti isiyozidi 10m. Na kujenga ofisi ya 60m, ambayo mbali ya jengo, kutakuwa na eneo kubwa la wazi nyuma ambalo litaezekwa kwa bati na kutumika kama sehemu ya mikutano ya ndani. Ukishakuwa na ofisi za kudumu, ni rahisi chama kuendelea kuwa na sehemu sahihi za kukutana, hata nyakati za hujuma. Hiyo itapelekea kutokuhitaji vibali kwa ajili vya mikutano ya ndani. Na kwa hapa Dar Nina uhakika ikitengwa 500m, kuna uwezekano wa kujenga jengo la ghorofa mbili au tatu litakalokuwa ofisi za kisasa za chama.
Mkuu tindo sidhani kama kuna mtu anayekataa suala la ujenzi wa ofisi za chama isipokuwa halipaswi kuwa kipaumbele namba moja kwa sasa.

Kama ulivyoshauri 'mbeleni huko' ni sahihi kabisa. Baadhi ya watu wanapigwa porojo kwamba Cdm haifai kupewa nchi sababu haina ofisi.

Well, wangejenga ofisi nchi nzima kisha wakati kama huu wa uchaguzi wangetumia majengo kuwafikia wananchi?

Ni ukweli kwamba chama bado hakijawa na rasilimali za kutosha kufanya kila jambo hivyo issue ya vipaumbele ni muhimu sana, so far so good [emoji111][emoji111]
 
Jamani MAHIDRA zetu 4 by 4 za kijani hazijatoka tu bandarini??
 
Mlihoji sana ruzuku inakwenda wapi. Haya ni baadhi tu ya maandalizi ya uchaguzi magari 25 mapya ya kupigia kampeni


MAGARI mengine mapya 25 ya Chama kwa ajili ya maandalizi ya Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2020 yamefika Dar es salaam.
CCM wametuambia chama chao ni cha uongozi nyie ni vyama vya uchaguzi inatakiwa muwajibu kwa hoja
 
kwa akili hizi ni ngumu kuujua ushenzi wa beberu, jiulize tu kwanini tangu tupunguze kuchukua mikopo nakutumia pesa za ndani mbona mabeberu yanang'aka sana? wale hawataki mwafrika ajitawale ndo maana wameunda mifumo kandamizi itakayotufanya kua duni daima.
Wewe umeadhiriwa na utopolo unaozungumza na viongozi wako kwenye majukwaa.Kama makusanyo ya Kodi ni 1 T kwa mwezi na mishahara tu ya wafanyakazi unalipa 700B a month,niambie hiyo fedha ya ndani ya kutumia inatoka wapi? Lakini pia hivi unakumbuka nani alificha takwimu za kukopa? Je ni yule anayesema anatumia pesa za ndani au ni beberu? Hii corona ikiendelea na mpango and Mr jalala wasipate nafasi ya kwenda kutembeza bakuri kwa beberu just wait uone Ile budget ya matirioni Kama atatekelezwa hata kwa 30%
 
Nawakubali Chadema lakini kwenye ofisi hapana
Bila kuwa priority huwezi kupiga hatua....

CDM mpo makini sana kwenye hili hasa la ujenzi wa chama...bila movements huwezi kuwafikia watanzania walio wengi kwa huu muda mfupi wa kampeni ukizingati jamaa aliwapiga pini miaka 5 huku yeye akifanya siasa kila siku.
 
Welk said na je go Hilo la ghorofa floor moja kuwa ukimbizi wa mikutano.

Yap, kuna jengo na tajiri yangu mmoja limejengwa kwa gharama ya 420m, lina ghorofa tatu, kisha ndani wakaweka partition kulingana na mahitaji husika ya idara mbalimbali. Chini ya bilioni 1 na miundombinu ya tehama eg, computers, printers, Wi-Fi, PABX nk.
 
Nadhani jambo ambalo chadema imekosea 2015-2020 ni uwekezaji mdogo.

Kwa sababu
1. Walikua na wabunge wengi
2. Walikua na wanachama wengi
3. Walikua na ruzuku kubwa


Ujenzi wa chama ni muhimu sana kuliko ofisi na vitega uchumi japo inabidi wabalance.

Tusilinganishe na ccm ambayo ofisi nyingi zilijengwa kwa fedha ya walipa kodi na 1992 wakapora kama mali zao.

Mkuu kwa siasa hizi za Meko unajengaje chama wakati kuna zuio la kufanya siasa, wabunge karibu wote wamebambikwa kesi mahakamani, wengine wamepigwa risasi nk nk.

Ni kweli Cdm ilikuwa na wabunge wengi kwa idadi ila kiuhalisia unapokuwa na watu aina ya Lijualikali, Silinde, Kubenea, Mwambe, Mollel, Kalanga, Ole Millya, Gekul, Waitara pamoja na wengine wa viti maalum utafanya nini cha maana?
 
Back
Top Bottom