Rwanda ifikapo 2026 watakuwa na umeme wa nyuklia wa bei nafuu na uhakika. Sisi tunashindwa nini wakati madini ya nyuklia tunayo kibao?

Sijui kama tunaliweza hilo Tanzania hilo tumwachie huyo mwanaume aendelee tu.
 
Madini ya nuclear ndo madini gani na yanapatikana wapi hapa tanzania?
Nimetumia lugha ambayo mswahili wa kawaida ataweza kuielewa. Si unajua wengi sayansi ni kizungumkuti kwao.

Nilimaanisha kisayansi madini yafuatayo:
  • Uranium atomic number 92 in the periodic table with the symbol U.
  • Plutonium atomic number 94 in the periodic table with the symbol Pu.

Madini haya yanapatikana kwa wingi huko Namtumbo (Mkuju river), Bahi, Galapo, Minjingu, Mbulu, Simanjiro, Lake Natroni, Manyoni, Songea, Tunduru, Madaba na Nachingwea. Hayo yaliyoko tu huko Mkuju river wingi wake peke yake unaifanya Tanzania kuwa kati ya top ten Afrika in terms of uranium deposits. Mto huo wa Mkuju uko ndani ya eneo la Selous Game Reserve ambako hata hilo bwawa la umeme la Nyerere linapatikana. Warusi wako huko tangie enzi za Kikwete waki extract madini hayo wakitumia teknolojia ya kisasa kabisa inayoitwa in-situ recovery (ISR) technology na kuyapeleka wanakotaka pamoja na huko kwenye vinu vya Rwanda.
 
Kuwekeza kwenye vinu vya kufua nishati ya umeme kwa kutumia nuclear ni must , hasa ukizingatia nchi yetu ilivyokubwa na matumizi yanaongezeka kila siku ya nishati ya umeme , ukiangalia pia hata mabadiliko ya tabia ya nchi , umeme wa maji si wa kutegemea sana ,ni lazima tuwekeze kwenye vyanzo vya nishati vya uhakika kama nuclear .
 
deposit ya mkuju ni sandstone hosted mkuu, and thus not amenable to isl/isr, only rollfront types of uranium deposit are amenable to isl, hao warusi walinunua hyo projec kutoka mantra na ni kama ilikuwa bahati mbaya kwao kwani kpind hcho bei ya uranium ilishuka ghafla kutokana na kile kinu cha japan kuleta shida, hakuna uchimbaji unaoendelea mkuju mkuu wangu iwe isl or conventiona open cut mining ambayo ndo method ingetumika pale mkuju
 
KIGALI, Rwanda (AP) β€” Rwanda’s atomic energy board says it has signed a deal with a Canadian-German company to build its first small-scale nuclear reactor to test what the company asserts is a new nuclear fission approach in one of the world’s most densely populated countries.

Rwandan officials said Tuesday that the reactor won’t produce any electricity for the country’s grid. Instead, it will explore the technology developed by Dual Fluid Energy Inc. to address the need for low-carbon energy.

If all goes well, officials said, Rwanda and the company could set up a production line of such reactors in the central African nation as the country turns to nuclear power to help meet growing energy needs and adapt to climate change.

Amandla...
 
Tatizo ni CCM!! Nakuhakikishia mbelen tutauziwa umeme na Mr tall!!
 
Mbona kama tunaongea lugha moja ila tunatofautiana kwenye uelewa wa hisabati na sayansi. Twende taratibu utaelewa:
NB: 1 GW ni sawa na 1,000 MW.

Wewe unasema hizo nuclear power plant (aka kinu) ndogo zinagharimu $ 1.0 billion sawa na TZS 2.5 trillion na zina uwezo wa kuzalisha 300 MW.

Mimi nimesema nuclear power plant ya size ya kawaida inauwezo wa kuzalisha 1,000 MW yaani mara tatu ya hizo ndogo za kwako. Hivyo na gharama yake itakuwa si zaidi ya mara tatu ya hizo ndogo ie $ 3.0 sawa na TZS 7.0 trillion

Bwawa la umeme la Nyerere lina uwezo wa kutoa 2,115 MW sawa na 2.1 GW na limetugharimu $ 2.9 billion sawa na TZS 7.0 trillion. Maana yake ni kuwa umeme wa kiasi cha JNHPP ungaliweza kuzalishwa na vinu viwili vya size ya kawaida kwa bei, kwa calculation zako, ya $ 6.0 billion sawa na TZS 15.0 trillion.

Bado bei hii si mbaya kwani hizo nuclear power plant hazina changamoto ya kuishiwa hiyo uranium iliyomo kwenye hivyo vinu. Half life ya uranium ni 4.5 billion years. Kinachotokea ndani ya hivyo vinu ni kugongana kwa neutrons na atoms za uranium. Mgongano huo unaitwa fission na hutoa joto la kuzalisha mvuke (steam) ambao ndiyo huzungusha turbine generator ya kutoa umeme. Hakuna kinachopotea au kuungua ndani ya humo kwenye nuclear power plants. Changamoto ya umeme wa maji ni kamq ambavyo tunashuhudia kwa mabwawa kuishiwa maji wakati wa kiangazi au ukame.

Usimikaji wa hivyo vinu vya nuclear power plant ni rahisi kuliko ule wa kutengeneza mabwawa kama hilo la JNHPP. Gharama kubwa huwa ni uranium ya high grade (aka weapon grade) ambayo bei yake maradufu ya bei ya dhahabu. Bei ya kilo moja ya hii uranium - isotope 238 ni $ 100,000 kwa kilo moja. Ninachosema ni kuwa sisi Tanzania tunayo kwa wingi hii uranium, hivyo usimikaji wa nuclear power plant hapa kwetu utakuwa rahisi sana, ni chini ya nusu ya ile uliyo kokotoa hapo juu. Assuming of course kwamba hakutakuwa na ufisadi au mikataba mbovu katika muradi huo. Uranium hii ilishaanza kuwa extracted na kampuni ya Urusi (state owned) tangia mwaka 2013 baada ya kununua kutoka kampuni binafsi ya Fredrick Kibodya et al waliokuwa wanamiliki uranium deposits zilizomo mto Mkuju huko Namtumbo. Kampuni hiyo ya Kibodya et al ilijulikana kwa jina la Mantra Tanzania Limited. Kampuni ya serikali ya Russia iliyonunua deposits hizo inaitwa Rosatom, ni 100% owned by the state of Russia na inauzoefu wa zaidi ya miaka 70 kwenye shughuli ya ku extract uranium and plutonium.

Usimikaji wa hivi vinu vya nuclear power plant 2huchukua muda mfupi, ndani ya miezi sita, siyo kama ule wa ujenzi wa mabwawa ya umeme. Ndiyo maana unaweza kununua hata ka kinu kadogo ka matumizi yako binafsi kenye kilo moja tu ya uranium- 238 ambako katakuzalishi muda wote 24,000,000 units (kWh) za umeme. Kilo moja ya mineral oil (gasoline) au gesi inatoa 12 units baada ya kuungua, kilo moja ya makaa ya mawe inatoa 8 units tu za umeme baada ya kuungua. Nuclear power generators do not burn fuel just like hydo power generators.

Nadhani sasa tunazungumza lugha moja ya kisayansi na siyo ile ya wana si hasa.

 
Kusimika kinu cha nyuklia ni pesa yako tu ndani ya mwaka umemaliza maana vingine ni kama pre fabricated. Ila kwenye fuel lazima tununue nje zenye yield nzuri hasa Urusi ambao wanauza fuel rods hadi Ufaransa.
Gharama ni kama zilezile sababu maintenance cost ya HEP ni ndogo sana na haihitaji kununua fuel ila inategemea uwepo wa mvua. Gharama za nyuklia ni za juu kidogo, kupozea kinu, ukaguzi na usalama na wataalamu ni ghali zaidi ila umeme wake ni uhakika.
Kwa haraka if everything is constant ni bora kwenda na HEP kuliko nuclear. Kama ingekuwa sivyo basi China isingejenga maelfu ya mabwawa ya umeme wakati inayo uranium fuel na inajua kujenga reactors
 
Tumeshindwa kutengeneza hata tooth picks itakuwa kwenye miradi mikubwa kama hiyo?
 
Sisi tunataka tutengeneze silaha za nuklia kwanza then ndo tuhamie kwenye umeme πŸƒπŸΎβ€β™‚οΈπŸƒπŸΎβ€β™‚οΈπŸƒπŸΎβ€β™‚οΈ
 
Tumeshindwa kutengeneza hata tooth picks itakuwa kwenye miradi mikubwa kama hiyo?
Si mradi mkubwa kiasi hicho unachofikiria. Kama tumethubutu na kuweza kujenga SGR ya umeme, hizo nuclear power plants ni kitu kidogo sana. Na uzuri wa awamu hii raisi wetu anapendwa sana na mataifa makubwa ulimwenguni hususani USA na China ambazo ziko tayari kumwezesha ili kuonesha dunia na hasa Africa kwamba wanawake wanaweza kuliko hata wanaume! Lazima Tanzania tuioneshe Afrika kwamba maraisi wanawake ni bora mara mia kuliko marais madume. Ni raha iliyoje kuwa na raisi mama, tena anayetoka Zenji!. Wakina Biteko msimuangushe raisi wetupendwa. Hakikisheni mwaka mmoja ujao Tanzania ina umeme wa nyukilia. Achaneni kabisa na hizo fossil fuels za gesi kuwa chanzo kikuu cha umeme wetu kwani zina madhara makubwa kwa tabia nchi na umeme wake ni wa bei kubwa sana. Funga kabisa hayo ma gas fuelled electrical generators yaliyopo hapo Kinyerezi baada ya ku switch on nuclear power electrical generators na hydro power electrical generators za bwawa la Nyerere. Uranium na plutonium tunazo za kumwaga ila zinachotwa bure na hiyo kampuni ya Russia huko Mkuju River. Zungumzeni na Putin atuwekee hivyo vinu vya nuclear power generators tutamlipa kilogram 100 za uranium plus 50 kilograms za plutonium akatengenezee mabomu ya nyuklia kumwangamiza adui yake Ukraine plus USA! Vita ya panzi ni neema kwa kunguru. Tuwe kunguru kwenye hii vita ya Ukraine. Tusiwe majani ambayo huumia fahari wawili wanapogombana.
 
Hakuna nchi yenye madini ya nuclear Duniani. Hakuna. Ni mara ya kwanza kusikia Tanzania Ina madini kibao ya nuclear. Yapo wapi hayo madini?! Ficha ujinga kidogo.
 
Hakuna nchi yenye madini ya nuclear Duniani. Hakuna. Ni mara ya kwanza kusikia Tanzania Ina madini kibao ya nuclear. Yapo wapi hayo madini?! Ficha ujinga kidogo.
Nimesema nimetumia lugha ambayo mtazania wa kawaida ataielewa. Ningesema madini ya uranium atomic number 92 abbreviated U92 au plutonium atomic number 94 abbreviated Pu94 au uranium- radioisotope 238 of high weaponry grade hatungalielewana isipokuwa kwa wachache kama wewe unayejua periodic table.
 
Hakuna nchi yenye madini ya nuclear Duniani. Hakuna. Ni mara ya kwanza kusikia Tanzania Ina madini kibao ya nuclear. Yapo wapi hayo madini?! Ficha ujinga kidogo.
Usiwe serious sana mkuu.. naamini jamaa amemaanisha madini ya Uraniam ndo yanatoa hiyo nishati ya nuclear
 
Usiwe serious sana mkuu.. naamini jamaa amemaanisha madini ya Uraniam ndo yanatoa hiyo nishati ya nuclear
Kuna watu wanakaza sana mafuvu hapa jamvini . Mtoa mada ameeleweka na alishasema katumia hiyo term "madini ya nyuklia " ili kupanua wigo wa mjadala hata sisi tulioishia darasa la nne tujue anazungumzia nini.
 
"South Africa is the only nuclear operator in Africa with two reactors at its Koeberg NPP totalling almost 2000MWe" from Google
 
Hivi mabaki ya nyukilia si yana athari zake na namna ya kuhifadhi na utupwaji wake. Ambayo hutupwa huku afrika Kwa kulipwa na mataifa Makubwa , Kwa baadhi yetu kupewa chenji kidogo
 
Tangu 1961 - 2023, serikali ya CCM inahangaika na uhaba wa matundu ya choo kwenye shule za msingi na sekondari.
Sasa huo umeme wa nyuklia watauweza kweli?
Mama anayewwze kupanga mambo ya jikoni na kuwa na vikoba hawezi shindwa kuendesha nchi. Hata vitumbua ishirini vikiungua , anaweza kuvitupa na kuanza tena. Vivyo hivyo ndivyo ataiongoza nchi .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…