Marie Antoinette
JF-Expert Member
- Jan 28, 2019
- 426
- 412
Kutokana na vita vinavyoendelea mashariki mwa DRC,tarehe 26 na 27 January 2025, watu 5 nchini Rwanda walipoteza maisha kutokana na risasi na makombola yaliyotua nchini Rwanda, mjini Rubavu unaopakana na Goma, na kusababisha vifo vya watu 5 nyumba na majengo ya shule vikiharibika.
Kwenye mkutano wa maraisi wa nchi za Afrika mashariki, raisi wa Rwanda Paul Kagame, aliahidi kutolifumbia macho jambo hilo, na kwamba atajibu mapigo, akisema hilo bado linafuatiliwa.
Tangazo la serikali leo tarehe tatu, baada ya tathmini ya maafa yaliyotokana na mabomu hayo, limebainisha kuwa mpaka sasa , watu 15 ndo wamepoteza maisha. Huku jumla ya watu 160 wakijeruhiwa, badhi wamesharuhusiwa na kurudi majumbani kwao, na wengine 6 hali zao zikiwa ni mbaya. Nyuma na shule vilivyohalibika, tangazo hilo limesema vina thamani ya faranga za Rwanda milioni 150.
Kwenye mkutano wa maraisi wa nchi za Afrika mashariki, raisi wa Rwanda Paul Kagame, aliahidi kutolifumbia macho jambo hilo, na kwamba atajibu mapigo, akisema hilo bado linafuatiliwa.
Tangazo la serikali leo tarehe tatu, baada ya tathmini ya maafa yaliyotokana na mabomu hayo, limebainisha kuwa mpaka sasa , watu 15 ndo wamepoteza maisha. Huku jumla ya watu 160 wakijeruhiwa, badhi wamesharuhusiwa na kurudi majumbani kwao, na wengine 6 hali zao zikiwa ni mbaya. Nyuma na shule vilivyohalibika, tangazo hilo limesema vina thamani ya faranga za Rwanda milioni 150.