Rwanda yafunga Parokia 47 za Kanisa Katoliki

Rwanda yafunga Parokia 47 za Kanisa Katoliki

Nawaza sana nchi ndogo mnoo kama Rwanda ambayo kieneo ni ndogo kuliko hata mkoa wa Pwani hapa Tanzania (huenda kieneo haifiki hata nusu ya mkoa wa Pwani), inawezaje kuwa na nyumba rasmi za ibada maelfu kwa maelfu. Yaani kama Kanisa Katoliki pekee Rwanda lina Parokia zaidi ya 231 (Kanisa katoliki ni mfano mzuri zaidi katika kujipanga kiutarabu wa kujenga nyumba zake za Ibada), hizo ni nyingi mnoo katika eneo la nchi kama Rwanda. Mleta mada anaeleza mpaka sasa Rwanda imeshafungia zaidi ya nyumba za ibada 10000.

Kwa utiriri huo, tukubali tu, Afrika (Rwanda ikiwa ni mfano halisi) tuna shida kubwa mnoo kuhusu ulevi wa kidini, tumegeuza dini kuwa kishaka cha kulewa ili kujisahaulisha matatizo yetu.
Jimbo kuu la Tabora ambalo ni kubwa kuliko nchi ya Rwanda lina parokia 30 tu
 
Serikali ya Rwanda imezifunga Parokia 47 za Kanisa Katoliki kwa madai ya kukiuka kanuni na sheria za nchi hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti ambayo imetolewa na Maaskofu wa Kanisa Katoliki, inasema kuwa suala la uhuru wa kuabudu limekuwa changamoto kubwa nchini Rwanda.

Ripoti hiyo inasema kuwa kati ya Parokia 231 zilizopo nchini humo, 47 tu ndizo ambazo zimefungwa kutoka katika Dayosisi tisa.

Hadi kufikia mwanzano mwa mwezi wa Septemba mwaka huu, Serikali ya Rais Paul Kagame ilikuwa imeyafunga Madhehebu na Misikiti takribani 10,000 kwa kile ilichokiita kukiuka sheria za nchi hiyo
Watu wenye makananisa wanatumia mambo ya kiimani kuwaumiza waumini. Safi Kagame wapambanie watu wako. Piga spana kama wanachofanya nikinyume na utaratibu.
 
Angeongeza Bars za pombe na nyama choma, Casino + gambling, na brothel houses. Uchumi muhimu, wale wadada wote wakiwa baa maid tuta hamia Rwanda.
Tatizo ni kwamba hizo so called "dhambi" ulizoorodhesha hapo juu zinafanyika sana ndani ya so called "nyumba za ibada"
 
Alafu usichokijua msikiti ni tofauti na kanisa kwamba ukipata sehemu we unafungua tu unaanza kupiga hela,, msikiti sio wa shekhe bali ni waumini,, hebu nitajie shekhe yoyote unaemjua wewe anaemiliki msikiti, na kwenye imani ya kiislam kigezo sio degree huku ni kufuata mafundisho ya kiislam kama yalivyoagizwa na mungu so hizo degree zake ukiingia msikitini unaziacha nje
Hivi nyie mbona huaga wagumu hivo kuelewa when it comes to issues za dini yenu? Nani kasema kwenye Uislam lazima uwe na degree? Kagame ndio kapanga hivo; huna elimu dunia, achana na uongozi wa dini. Sio sheria ya dini, ni utaratibu wake Kagame. Unadhani hata Roman Catholic (haya makanisa alioyafungia hapa) na wenyewe huaga kuna kanisa la mtu? Makanisa yao yapo chini ya taasisi, taasisi ndio zinayaendesha, viongozi wake (mapadre) wameajiriwa na wamefunzwa hasa kuhusu dhehebu lao but Kagame kapita nao. By the way, Waislamu Rwanda is only 1% ya population na mostly ni wahamiaji.
 
Jimbo kuu la Tabora ambalo ni kubwa kuliko nchi ya Rwanda lina parokia 30 tu
Usitizame ukubwa eneo tu angalia na idadi ya watu mkoa wa tabora wako milion 3tu, lkn nchi ya rwanda wako milion 10. Sasa hapa uoni kwamba ni tofauti, mfano nchi ya canada na tanzania. Tanz inaingia mara nne kwa canada kieneo, lkn canada idadi ya watu ni milion 30tu tanz wako 60.
 
Back
Top Bottom