Sababu kubwa 2 kwanini Miziki wa Tanzania kwa sasa ni Fake, Mgumu na Mbovu

Hata bongo movie wakati wa Kanumba hizi mboyoyo zilikuwepo, hata hao waigizaji wakawa wanasema waneshaipiku Nollywood 🀣🀣
 
Perfect πŸ’―πŸ’―πŸ’― πŸ‘πŸ‘πŸ‘
 
acha kufananisha waumini wa gwajima na vitu vya kijinga
 
Mkuu deal nyingi za wasanii unazoziona kuna watu wa kati ambao hula zaidi yako. Na kama hutaki hawakupi, anatafutwa mwingine.

Why hujiuluzi kwanini Harmonize kapata endorsement kibao kuliko Kiba ?

Kwanza kibiashara Tanzania bado hakuna ushindani huo mkuubwa kiasi kwanba mpaka makampuni yawe that aggressive kwenye marketing.

Hata wasipompa msanii endorsement biashara zao zinaenda, so huna cha kuwafanya hata wakikupa pesa kidogo
 
Hata USA pako hivo. Bila wadau wa mziki ( Media na Label) hutusui... Na ukipigwa chini na Label basi jua utakuwa na khali mbaya kimuziki hata USA pia.
Muziki wa mainstream upo hivo Dunia nzima. Na huwezi kuwa juu siku zote kwenye muziki. Wasanii Wapya wanavyozidi kuja basi wale wa zamani ambao hawataki kubadilika kimuziki basi wanajikuta nje ya mstari.
 
Hata USA pako hivo. Bila Label hutusui... Na ukipigwa chini na Label basi una khaki mbaya hata USA pia.
Muziki wa mainstream upon hivo Dunia nzima.
Kwamba dunia nzima media ndio zinazomiliki wasanii, studio, kuandaa matamasha na hao hao ndio promoters kiasi kwamba wasanii wasiokuwa kundi lolote wakiwemo wachanga hawapati nafasi ?
 
Kwamba dunia nzima media ndio zinazomiliki wasanii, studio, kuandaa matamasha na hao hao ndio promoters kiasi kwamba wasanii wasiokuwa kundi lolote wakiwemo wachanga hawapati nafasi ?
Bongo hapa Media ndo zinafanya kazi kama mapromota (kupromote music) bila Media mziki utasua sua kufika mbali (nation wide).
Recording Label huwa zinafanya kazi kwa Ukaribu na Media.
Hivo kama Label hazina Ukaribu na Media basi Label itapata ugumu flani kusambaza kazi. Hususani Label ambazo hazina Loyal fanbase kubwa..
Kwa hiyo unarudi pale pale kuwa Media ina mchango mkubwa katika Supply Chain ya Muziki.
Na Media nao ni wafanyabiashara wanataka pesa. Ndo maana wanaandaa matamasha yao na kupromote wasanii.

Kwa KIFUPI, Mziki popote duniani haujawahi kuwa mrahisi kwa Msanii Mchanga hata KIDOGO.
Kama haushikamani na wadau (Media, Label) basi imekula kwako.
unaweza kutoka bila wadau kwa kutegemea kuTrend kwenye INTERNET, lakini ni ngumu ngumu mno, ila inawezekana.!
Lakini ukiwa na Wadau (Media, Label) basi ni rahisi kushikwa mkono na hapo itategemea Ubunifu wako Kimziki jinsi ya ku-maintain.
Maana unawezashikwa mkono na bado usiwe juu kivile sababu mziki wako umeshindwa kupenya mainstream.
 
Mkuu si wote wamefanikiwa, lakini mtu kama Diamond huwezi sema hajafanikiwa.

Hata kama waliofanikiwa ni wachache lakini huwezi fananisha na zamani.

Mtu kama Juma nature angekuwepo enzi hizi nadhani angekuwa zaidi ya diamond.
Juma Nature ni overated.
 
Kusaga master minder..Babu Tale anaweza nini
 
He is just a puppets,

Basi sawa.
 
Mkuu jitahidi uwe na valid info
 
Juma Nature ni overated.
Muziki huwa haunaga Formula, unaweza piga sana mistari konzi na hata usitusue wala nini..
Kuna watu wana Calibre ya kupendwa tu na jamii. Kupendwa nako ni KIPAJI ujue.πŸ˜€
Na hii ipo hata MITAANI, MASHULENI etc. huwa kuna watu inatokeaga wanapendwa na kukubalika tu, Mpaka unabaki unajiuliza How? Why? na Jibu usipate!!
Ukitangaza sehemu Juma Nature atakuwepo kutoa burudani ya Muziki basi PANAJAA watu shaziiii!!
Nature alikuwa Sauti flani hivi, akishikilia CHORUS utapenda mwenyewe.. Na ile Style yake Rap Katuni flani. Juma Nature ndo Msanii aliyekuwa anapendwa zaidi Miaka ya 2001-2007. Kipindi hicho nipo shule ya msingi.
Tofauti ya Diamond na Nature ni kwamba Diamond yeye alikuwa anawekeza zaidi Pesa zake kupata COLABO na Wasanii Wakubwa wa Nigeria ili kuhakikisha anaiteka Africa Kimziki pia.
Wakati Nature yeye alikuwa anakubalika Bongo tu.
Msanii mwingine ambaye alikuwa na Calibre ya Kupendwa alikuwa Mr.Nice.
Mr.Nice alichomzidi Juma Nature ni kuwa Mr. Nice alitusua mpaka Kenya na Uganda kote humo akawa msanii mkubwa.
ila kwa Bongo, Juma Nature was The Star. TANZANIA ONE. Vile viwanja vyote sugu vilivyokuwa havijai Nature akiwepo tu vinajaa shazi.
Mimi mwenyewe mpaka Leo ukiniuliza kwa nini Utotoni nilikuwa namkubali sana Juma Nature kwa kweli Sina Jibu.
πŸ˜€πŸ˜€
 
Kuna wasafi tv na wasafi media do you know the difference?!
Wasafi Tv na Wasafi media ,mbona kitu kile kile sawa sawa kusema mamba na reptilia kwani wasafi TV ipo ndani ya Wasafi Media ambayo ndani yake unapata na radio.

Wasafi Media=Wasafi TV +Wasafi Radio.

Sababu TV na radio zote ni aina ya Broadcasting media.

Au kama una document nyingine ambayo updated tuwekee.
 
Deals na Endorsement zinatafutwa pia ujue. Usizani unakaa tu kisa wee msanii mkubwa basi zitakufata.πŸ˜€πŸ˜€ Zitafute nyingi kisha kula Percentage yako, Ni Ngumu sana kula hii Cake kwa 100% pekee yako hasa ukiwa msanii ambaye huna Loyal fanbase kubwa..
Binafsi, naona kibiashara ni bora kuwekeza kwa Harmonize sababu yuko Active na anajua kujiMix kutafuta Makeke na Headlines. Kitu Ambacho ni kizuri kibiashara.
Alikiba yupo Tuli sana. Yaani tuliiiii sana. entertainment industry inahitaji makeke na hamsha hamsha. Hivyo kibiashara ni bora kumpa deals Harmonize.
 
Kwamba dunia nzima media ndio zinazomiliki wasanii, studio, kuandaa matamasha na hao hao ndio promoters kiasi kwamba wasanii wasiokuwa kundi lolote wakiwemo wachanga hawapati nafasi ?
Ndio hivyo, Ila wenyewe wanamedia nyingi zenye nguvu tofaut na sisi unakuta Ni mbili tu, pia Kuna promoters wengi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…