Sababu mbalimbali zinazopelekea Mjamzito kutokwa damu ukeni

Sababu mbalimbali zinazopelekea Mjamzito kutokwa damu ukeni

Sina pa kwenda

Senior Member
Joined
Nov 18, 2010
Posts
113
Reaction score
15
Habari wanajamvi jamani hivi inawezekana mama mjamzito wa miezi minne kutokwa na damu? Na kama ndio inatokana na nini?

Msaada please

=========
Similar Cases

Mjamzito anatokwa na damu. Rangi ni brown, inatoka kidogo tu, sio kama ya period, tumbo haliumi kabisa. Umri ni 29 ni mimba ya kwanza, sijawahi kuugua ugonjwa wa zinaa. Kama UTI ni ugonjwa wa zinaa niliugua mwaka jana mwezi kama wa sita hivi.

Kazi ngumu hapo ndio sielewagi ni zipi maana kazini na kuishia kwa kiti na kazi za kawaida. Sijawahi ugua homa muda mrefu sana, safari ndefu hapana, stress za kawaida sana hizi ugomvi wa hapa na pale.

Nilienda hospital Dr. akaniambia nikacheki kwanza Ultra sound nikaenda check ikaonekana hamna shida akanipa dawa zinaitwa Duphaston basi ndio naendelea kumeza ila sasa sijaelewa maana sasa imetokea mara ya pili thats why nimekuja kuuliza kabla sijarudi tena hospital maana appointment na Dr. Jumamosi ya 24/03/2013

Msaada wadau,

Mwanamke anapokuwa mjamzito na anatokwa na damu mara moja moja na wakati mwingine maji anakuwa na tatizo gani?

Wasalaam,

Kuna dada ana mimba ina miezi 3 na wiki mbili na hili amelijua siku chache zilizopita kuwa ana mimba na sababu ya kutokujua hadi inafika umri huo ni kwamba na alikua anapata hedhi kama kawaida japo anadai damu ilikuwa inatoka kdogo sio nyingi kama ilivyo kawaida na mpaka sasa hivi hali bado iko hivyo.

Hospitali kaenda kaelekezwa akanunue dawa ya kukata na mimba bado ipo.

Naomba kujua inawezekana mwanamke ana mimba na bado akatokwa damu? Na nini sababu yake na madhara yake pia kama damu itaendelea kutoka.

Naombeni msaada wa ushauri kwenu wataalam.

Wenye taaluma au uzoefu mnisaidie ni dalili ya nini? Siku za kujifungua alizoandika nesi zimepita kama wiki moja, but maumivu ya kiuno na nyonga na tumbo yanakuja na kutoweka, then damu kidogo na whitish mucus inafuata.What is that? Msaada pls...

========
Ushauri:

Kutokwa damu kipindi cha ujauzito ni hali hatarishi, inawezekana ni dalili ya kutaka kuharibika kwa mimba au complications za mimba tu. Mama aidha hutokwa damu kwa kiasi kidogo(matone) au kiasi kikubwa, haswa kipindi cha miezi 3 ya kwanza ya mimba (first trimester) mpaka miezi 3 ya mwisho( third trimester). Takwimu zinaonesha kuwa asilimia 25 ya wamama wajawazito wanatokwa na damu kipindi cha miezi 3 yao ya mwanzo (first trimester).

Mama anapotokwa damu huambatana na maumivu chini ya tumbo, kizunguzungu, kushindwa kuona vizuri na kuishiwa nguvu.

Mimba inapotungwa inapofika wiki ya 4 yai linakuwa fertilized na kushikilia uterine wall, hiyo hali inaweza msababishia mama kupata damu nyepesi kwa muda na baadae itakata(implantation bleeding). Implantation bleeding inakuwa damu nyepesi.

Damu inapotoka kiasi kidogo cha matone (spotting) hapo inaweza matatizo kama ya infection au dalili ya kuharibika kwa mimba ila damu inapotoka kwa wingi hiyo inakuwa hali nyingine kabisa.

Complication nyingine zinazoweza sababisha mama kubleed damu kwa wingi ni:-

1. Kuharibika kwa mimba. Mjamzito anapotokwa damu kwa wingi yenye madonge makubwa au madogo kidogo hiyo ni ishara kubwa ya kuharibika kwa mimba.

2. Kuharibika kwa placenta(kondo) kunachangia mama kutokwa damu.

3. Yai kutungwa nje ya mji wa mimba (ectopic preganancy). Mimba inapotungwa nje ya mfuko wa uzazi na badala yake inakuja kutungwa kwenye mirija ya uzazi(fallopian tube) hapo nafasi ya kulea mimba na kukuzia mpaka miezi 9 ni ndogo, hiyo hali inamletea mama kupata damu kwa wingi. Ndio mana Wizara ya Afya inashauri mama unapopata mimba toa taarifa kituo cha afya usisubirie ikue miezi 4-5 ndio uanze clinic.

4. Kondo(placenta) kuwa na matatizo kwenye ukuta wa uzazi.

5. Mabadiliko ya mwili yanachochewa na homoni(hormonal changes), inasababisha mama kutokwa damu matone madogo madogo (spotting).

6. Kushiriki tendo la ndoa uume akigonga kwenye mlango wa uzazi kunaweza msababisha mama kutokwa damu kidogo (matone). Mama akiona iyo hali ni vizuri kuacha kushiriki tendo la ndoa muda kwanza.

7. Maambukizi yanapompata kupitia ukeni au cervix kama U.T.I, kaswende, gonorea n.k ni rahisi kutokwa damu kipindi cha miezi 3 ya kwanza (first trimester). Mama mwenye infections anatakiwa kuwahi hospital ili kuokoa maisha yake na mtoto, infetions husababisha watoto kuzaliwa na ulemavu (kuona,kusikia n.k)

8. Mama anapofanyiwa vipimo na mkunga au daktari na kuwekea kidole ndani ya uke kunaweza msababishia kutokwa damu matone.

9. Mama anapojifungua kabla ya week 37(preterm labor) atasikia kutanuka kwa uke kunakoweza ambatana na damu, kuhara, maumivu ya mgongo na mvuto kwenye nyonga.

Muhimu:

Unapoona damu inakutoka haijalishi kidogo au nyingi, wahi hospital sababu hujui nini kimesababisha na inaweza kuwa dalili ya kuharibika kwa mimba. Kwa matibabu utafanyiwa ultra sound na vipimo vingine vya ukeni na tumboni n.k kujua tatizo ni nini.
 
Damu ya namna gani?

>Kuona matone kwenye chupi?
>Nyingi kama ya period au zaidi?
>Na je, imeambatana na maumivu ya tumbo?
>Umri wako na ni mimba yako ya ngapi?
>Magonjwa ya zinaa?
>Umefanya kaz ngumu?
>Umekuwa na homa hivi karibuni au sasa?
>Stress?
>Safari ndefu?

Kuna vitu vingi vya kujiuliza mpaka ufikie kusema huenda ni ya kawaida(Kutanuka kwa mfuko wa uzazi) hata hivyo tatizo hilo huwatokea wachache.
 
ni miongoni mwa dalili za hatari za ujauzito na pindi litokeapo nenda hospital mapema jamani watu hawaendi clinic eeh.
 
Mjamzito anatokwa na damu. Rangi ni brown, inatoka kidogo tu, sio kama ya period, tumbo haliumi kabisa. Umri ni 29 ni mimba ya kwanza, sijawahi kuugua ugonjwa wa zinaa. Kama UTI ni ugonjwa wa zinaa niliugua mwaka jana mwezi kama wa sita hivi.

Kazi ngumu hapo ndio sielewagi ni zipi maana kazini na kuishia kwa kiti na kazi za kawaida. Sijawahi ugua homa muda mrefu sana, safari ndefu hapana, stress za kawaida sana hizi ugomvi wa hapa na pale.

Nilienda hospital Dr. akaniambia nikacheki kwanza Ultra sound nikaenda check ikaonekana hamna shida akanipa dawa zinaitwa Duphaston basi ndio naendelea kumeza ila sasa sijaelewa maana sasa imetokea mara ya pili thats why nimekuja kuuliza kabla sijarudi tena hospital maana appointment na Dr. Jumamosi ya 24/03/2013
 
Iwapo damu inatoka kuna vitu vikubwa viwili vinavyohitaji uchunguzi.
1. Je, mtoto bado yuko hai?
2. Je, placenta imekaa sehemu gani na haijaanza kutoka?

Ili kujua hayo unahitaji kufanyiwa kipimo cha ultrasound.
Kipimo hiki ni muhimu sana kwa sababu kama placenta imekaa kwenye njia ya kutokea mtoto kuna hatari ya kupoteza damu nyingi na pengine hata kupoteza maisha wakati wa kujifungua.
 
Iwapo damu inatoka kuna vitu vikubwa viwili vinavyohitaji uchunguzi.
1. Je, mtoto bado yuko hai?
2. Je, placenta imekaa sehemu gani na haijaanza kutoka?

Ili kujua hayo unahitaji kufanyiwa kipimo cha ultrasound.
Kipimo hiki ni muhimu sana kwa sababu kama placenta imekaa kwenye njia ya kutokea mtoto kuna hatari ya kupoteza damu nyingi na pengine hata kupoteza maisha wakati wa kujifungua.



Kama nilivyokwambia nimeenda hospital wakaniambia mtoto na placent iko vizuri tu, wakasema ni kawaida Hormon zinakuwa bado hazijazoea hali ya ujauzito, sasa jana usiku nilipita kwa mabonde nafika nyumbani nakutana na damu kidogo na hakutoka tena nimelala nimeakma hamna kitu ila ntaenda hospital nilikuwa nataka kujua
 
Je ulifanya tendo na baba kijacho hivi karibuni?
 
Kama nilivyokwambia nimeenda hospital wakaniambia mtoto na placent iko vizuri tu, wakasema ni kawaida Hormon zinakuwa bado hazijazoea hali ya ujauzito, sasa jana usiku nilipita kwa mabonde nafika nyumbani nakutana na damu kidogo na hakutoka tena nimelala nimeakma hamna kitu ila ntaenda hospital nilikuwa nataka kujua

Hapo sijaelewa aliyekwambia hivyo alikuwa anamaanisha nini ila kwa jinsi unavyoelezea unatakiwa kupata mapumziko kwa kipindi fulani. Usipande na kushuka mabonde au tunaweza kusema "take it easy"
 
Hapo sijaelewa aliyekwambia hivyo alikuwa anamaanisha nini ila kwa jinsi unavyoelezea unatakiwa kupata mapumziko kwa kipindi fulani. Usipande na kushuka mabonde au tunaweza kusema "take it easy"

Yule mtu wa Ultra sound aliniambia hivyo ni vitu vya kawaida mwili unakuwa haujazoea, sinakuwa nimezoea kublid so bado mazoea ya huo ujauzito ndio maana inakuwa hivyo.
 
Yule mtu wa Ultra sound aliniambia hivyo ni vitu vya kawaida mwili unakuwa haujazoea, sinakuwa nimezoea kublid so bado mazoea ya huo ujauzito ndio maana inakuwa hivyo.

hayo maelezo sio sahihi.
Lakini cha msingi ni kwamba hali yako inaendelea vizuri, so just take it easy.

Unapobleed wakati wa siku zako maana yake ukuta wa kifko cha uzazi unabomoka, ili mzunguko wa kuujenga tena uanze upya. Hicho ndio chanzo cha damu za hedhi.

Kipimo cha ultrasound hakina uwezo wa kutoa hali ya hormon mwilini mwako.
 
hayo maelezo sio sahihi.
Lakini cha msingi ni kwamba hali yako inaendelea vizuri, so just take it easy.

Unapobleed wakati wa siku zako maana yake ukuta wa kifko cha uzazi unabomoka, ili mzunguko wa kuujenga tena uanze upya. Hicho ndio chanzo cha damu za hedhi.

Kipimo cha ultrasound hakina uwezo wa kutoa hali ya hormon mwilini mwako.


Yaah kikubwa naendelea vizuri, asante sana kwa msaada wako barikiwa sana.
 
Hi Sina pa Kwenda!

Nimelielewa vizuri swali lako na pia nimesoma ushauri mbali mbali uliotolewa na wana jamvi! Nikiwa kama daktari, kutokwa na damu kwa mwanamke wakati wa ujauzito (katika umri wowote wa mimba) sio jambo la kawaida, achilia mbali kama tumbo linauma, haliumi, damu ni kama ya hedhi au ni fresh etc etc.... kuendelea kutoka kwa damu kunaweza kuwa na madhara kwa mama na kwa mtoto aliye tumboni. Sababu zinaweza kuwa nyingi.....ni vema kufanyiwa uchunguzi wa kina hospitalini! Napenda kukushauri uende hospitali mapema na kama inawezekana basi umwone Gynaecologist/Obstetrician!
 
Hi Sina pa Kwenda!

Nimelielewa vizuri swali lako na pia nimesoma ushauri mbali mbali uliotolewa na wana jamvi! Nikiwa kama daktari, kutokwa na damu kwa mwanamke wakati wa ujauzito (katika umri wowote wa mimba) sio jambo la kawaida, achilia mbali kama tumbo linauma, haliumi, damu ni kama ya hedhi au ni fresh etc etc.... kuendelea kutoka kwa damu kunaweza kuwa na madhara kwa mama na kwa mtoto aliye tumboni. Sababu zinaweza kuwa nyingi.....ni vema kufanyiwa uchunguzi wa kina hospitalini! Napenda kukushauri uende hospitali mapema na kama inawezekana basi umwone Gynaecologist/Obstetrician!

Asante sana by the Clinic ninayoenda ni pale Mbuyuni kwa Mgaya baada ya kupata majibu ya Ultra sound akaniapa hizo dawa Duphaston na niomuone baada ya kumaliza hiyo dozi ambayo ni trh 24 this month ila ntaenda leo jioni kwa ajili ya kujua shida zaidi maana sasa hv damu imetoka mara ya pili
 
Good! Prof Mgaya is my medical school teacher and he is a good gynaecologist. You see...it is the second time now you are seeing this bleeding. Again...Please see him today and you will let us know the progress! All the best!
 
Good! Prof Mgaya is my medical school teacher and he is a good gynaecologist. You see...it is the second time now you are seeing this bleeding. Again...Please see him today and you will let us know the progress! All the best!

Asante kwa mara nyingine! ntarudi hapo kesho kutoa mrejesho!
 
Habari wanajamvini jamani hivi inawezekana Mama Mjamzito wa miezi minne kutokwa na damu! na kama ndio inatokana na nini! Msaada plz

Kama alivyojibu The secretary - hiyo ni dalili ya kuwa ujauzito wako upo hatarini sana - Katika hali ya kawaida damu yaweza kutoka kutokana na sababu mbalimbali lakini The worst case scenario yawezekana umepatwa na PPROM - Preterm Premature Rapture Of Membrane - Tiba ya hili tatizo mara nyingi huwa ni "bed rest" hadi utakapojifungua kwa wanaobahatika kujifungua...!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom