Sababu ya Diamond kuwazidi wasanii wenzake kwenye kutoa vipaji vipya

Pamoja na mapungufu mengi aliyonayo Diamond ila bado atabaki kuwa msanii namba moja aliyeibadilisha sana bongo fleva,imeanza kupata thamani na inajulikana world wide,muziki wetu umeongezeka thamani zaidi,miaka michache nyuma Diamond alishawahi kusema hawezi kufanya show hapa tz chini ya milioni kumi watu walimbeza hususani watu wa media na mapromota wa muziki,alisusia baadhi ya show na tuzo za media kama clouds na eat radio/tv sababu kubwa ikiwa malipo kiduchu,leo hii anachukua zaidi ya hela ile aliyoikataa kwa show,wasanii wengi wakaanza kuamka kiakili,tuzo za kimataifa kwa wasanii wa bongo fleva ilikuwa ndoto,collabo za kimataifa zilikuwa ndoto kuzipata, Diamond alijua kujibrand mapema kwa sababu alijua alichokiitaji,leo hii muziki wetu at least unazungumziwa Africa sio kama miaka michache nyuma,ila kiukweli kwa sasa tukiacha ushabiki kimuziki Diamond graph yake imeshuka ukimlinganisha na diamond yule wa kuanzia 2012_2018,sio yeye tu hata wale waliosumbua Africa kwa hits kama tekno,kcee,iyanya,na wengineo, hawezi kuwa na watu wote watakaompenda ila tusisubiri mtu afe ndio tumsifie kijana amepambana kuliko wasanii wengi wa bongo fleva,tuna wasanii wakubwa na wasanii wakongwe Diamond ni msanii mkubwa ktk nchi hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo alipomtaja Harmonize naona umepita kama hupaoni.
 
vyote ulivyozungumza kaiga kwa ALIKIBA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
JE DIAMOND ALITOLEWA NA NANI?..linaweza likawa ni swali la kwanza ambalo majibu yake yatakwepwa kwa kiasi kikubwa ili kuendelea kumtengenezea huyu bwana u Mungu mtu.
1.kasema zuchu ana nyimbo za kutosha huenda ikawa ni fact ila kwenye suala la "NYIMBO KALI" kidooogo Tafadhali.
2.Kusema wakaona wakati huu wa CORONA ndo wakati "SAHIHI" fikiria vizuri.
3.Ukimsifu diamond kwa kutumia nguvu kubwa kwa PUCHU kwamba hata insta ya diamond imekuwa kama fan page ya zuchu so ni Ku mbrand au kumsapot sidhan coz nguvu hiyo hatukuiona kwa msanii yyte wa WCB nadhani kaona kwa uimbaji wake na Muziki wa sasa inahitaji nguvu kubwa kumsukuma ama la itatokea kama ya lavalava na queen darlin dadaye.
4.Kusema PUCHU kwa muda mfupi kafika levo za NANDY,RUBY NA VANESSA ni kuwatusi hao madada coz hadi sasa kinamchombeba PUCHU si uwezo wa kuimba Bali ni FAN BASE ya WCB.
5.Kutengeneza brand ya kujitegemea haina maana kutoshirikiana na wenzako kwenye nyimbo zake kama n hivyo boss wao Diamond nadhani kwa TZ ndo msanii anaongoza kwa kolabo za nje sasa yy brand yake haijitegemei kwa kuwa hutegemea zaidi kushirikisha??
6.Si kweli kwamba zuchu kaiteka bongofleva hadi sasa kwateka mashabiki wa WCB kwa kuwa ni bidhaa yao mpya na wanataka waiingize sokoni kwa kishindo kusema ukweli hakuna alichofanya kilichoshtua tasnia zaidi ya kusainiwa wasafi na si kwa uimbaji ukizingatia ana tone ya taarabu katika mirindimo ya bongofleva.

TUKIRUDI KWA KIBA.
Mara zote jamaa mmekuwa mkimpuuzisha kwenye industry na kumfanya aonekane si kitu lakini katika mioyo nadhani ndo mpinzani wa Diamond anayeogopwa zaidi kuanzia na boss wao hadi shabiki wa mwisho kabisa wa WCB kwa sababu hadi sasa sijaona sababu ya kuendelea kumlinganisha DIAMOND na ALIKIBA kama kweli mnajiaminisha DIAMOND kamzidi Kila kitu ALIKIBA ni mpuuzi pekeyake ataendelea na kushindanisha watu wa uzani huo tofauti na hapo labda my admit kwamba KIBA NI MWIBA NA NDO MAANA MMEKUWA MKIMUANDAMA WAKATI WOTE.

Kuna hoja kwamba Kiba akimtoa msanii wake lazima aimbe nae Sina uhakika na hili coz k 2ga katoa "UNANIONA" na "HAWAPENDI" sidhan kama kuna sauti ya KIBA pale lakini sikatai GUBU na MASOZY kashiriki kwa hiyo huwa inategemea siyo kwamba ni lazima, Kila strategy hii ingetumiwa na DIAMOND ingepigiwa upatu na watu wa dizaini ya mtoa mada.

Kwamba wasanii wa Kings wakitoa ngoma wanakaa muda mrefu inaezekana ndo strategy yao wao and u can't force them to do like others au kama unavyoona ww inafaa,ki2ga alisikika kwenye masozy kaja kusikika tena kwenye hizo mbili na kapokelewa kwa stahiki yake si kama unavyotaka kutuaminisha kwamba wanaanza upya si kweli.

Kwamba Kiba kwenda intavyuu na wasanii wake si sawa..iangalie hii to both sides mzee attention inayokuwepo akiwepo KIBA na wakiwepo wasanii wake peke yao hata ww uambiwe intavyuu atakuwepo PUCHU au atakuwepo PUCHU na DIAMOND nadhani unaona kabisa uzito ni tofauti japo strategy hii angetumia Diamond mtoa mada ungepiga upatu.

Kwamba wasanii wa ALIKIBA Hawana matukio...why matukio?..acha Muziki uongee why matukio ili utengeneze attention?.. Kama unatengeza matukio ili usikike Basi huamini Muziki wako na unajua wazi bila matukio hausikiki.

Lastly bt not least Mashabiki wa WCB huwa mnahisi ua brilliant from top to toe bt not that,wakati mwingine mahaba mnapeleka mbele kuliko uhalisia na huwa mnataka kujiaminisha na kutuaminisha kwamba huu Muziki wa Tanzania kwa sasa ni Mali yenu maana mnaamini na mnataka kutuaminisha kwamba hakuna yyte NJE YA WCB anaeweza Muziki au biashara ya Muziki that's not true na tutaendelea kuwaweka sawa kila mnapoteleza kama huyu bwana mtoa huu ushuzi...TUKUMBUKE DODO IS STILL TRENDING there tchao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera si kwa gazeti hili😀
Yataka moyo, yote hii kutaka kutuamisha Domo na WCB si lolote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…