Sababu za Tanzania kupitwa kimaendeleo na nchi nyingine

Sababu za Tanzania kupitwa kimaendeleo na nchi nyingine

Nyerere alisema ili tuendelee twahitaji
Ardhi (tunayo)
Siasa safi (je tunayo?)
Watu (wapo au tupo. Ila tuna uwezo kiasi gani kuyatawala mazingira yetu kwa kukuza uzalishaji wenye tija)
Siasa safi (hapa tuna mjadala mkubwa sana. Polepole ameweka wazi siasa ndani ya chama cha zina mizengwe, uchawi, fitna; ukizubaa tu, ndio hivyo. JK wakati mmoja akiwa mkulu, aliweka wazi wanachama wa chama chake hawaachiani glass za vinywaji).

Ukiona tumefika pahala ambapo "kuna wale na sisi", tuna makundi ya Urais yalianza toka 1994 enzi za boys2men,wakaja wana-mtandao, mara mtandao ukafa kukawa na virungu chungu mzima, maana yake, nchi hii inahitaji reforms za "kufa mtu"

Rwanda PK kajitahidi sana kuiweka nchi kwenye ramani ya Afrika na ulimwenguni.

Tanzania tunakwama kwa kukosa nini kifanyike ili rasilimali watu izalishe kwa tija na kufanya biashara kukidhi mahitaji ya soko la ndani na then twende walau soko la EA na SADC.

Mpaka sasa elimu yetu ni a for apple na sio elimu yenye maswali kama apple zinatoka SA kuja hapa kwa miaka mingi, kwa ukubwa wa ardhi ya nchi hii ambayo ni virgin, nini tufanye ili ndani ya miaka 10 ijayo Tz iwe kwenye ramani ya exports ya apple zenye ubora kwa nchi zaidi ya 15 (8 za jirani & SADC)

Tuna viongozi wanaosaidia wakulu wenye fikra za nini nifanye niendelee kumpendeza mkulu. So, ni matamko, mipango, kuonekana kwa media ila ukipima kuna effors ndogo sana kukuza uzalishaji wa kibiashara.

Tunalima mahindi kila mwaka mpaka yanakosa soko, kwanini kusifanyike tafiti kule kwenye ukanda mahindi yanakubali tukazalisha breed inayokamuliwa mafuta ili ku-cover deficit ya mafuta ya kula worth 600bn kwa mwaka?
Watawala wetu badala ya kufikiri wa picha kubwa, wanawaza viwanda vidogo. Na kuna mmoja na masters holder akiwa waziri akawa anasema machine ya kuponda tofali au cherehani ni kiwanda kidogo. Very low sense of accountability.

Tukipata strategic thinkers kwenye leadership, tunaweza kusogea haraka sana. Ila kama ni hawa waimba hiena hiena na wale wanajiita "mimi ni chawa wa ...." mimi nina degree 4, tunazidi kuchelewa sana.
Nini kifanyike? Jamii ndo iamuke itoke kwenye ujinga kama ni elimu watu wa zamani wengi hawakupata elimu na ndo tatizo lilianzia hapo walisoma wachache na haohao kupata ajira moja kwa moja na vizazi vyao wamewapa elimu nzuri na ajira ni zawao tu maana wale waliokosa elimu hawakuona uzuri na umuhimu wa kuwapa watoto wao elimu nzuri labda watoto waliolazimisha kusoma kwa lazima au kwa msaada ndo tunaona wanavyeo nao wanajipendelea tu, hivyo tukazanie elimu za vizazi vyetu Kwanza Ili wengi waelimike na kujitambua na mazingira ya kuwekeza yataleta faida imagine mpaka Sasa bado tunaishi kizamani kwa kupoteza muda tu kama mtu kulima kwa jembe la mkono mazao kidogo yasiyo na faida, kushinda mtu anazunguka na mifugo kama vile na yeye ni mfugo badala ya kutengeneza au kuzalisha chakula cha mifugo na kufuga kisasa tena kama kampuni inayojitosheleza na mahitaji ya mifugo yake Sasa watu wenye akili za kizamani kama hizi wataweza kuzungusha uchumi kiasi cha wenye madaraka kutetemeka na kufanya mambo makubwa? Maana watu wakifanya mambo kisasa yanaleta ajira nyingi sana mfano elimu ya English medium inaajili watu wengi kuliko hizi za kata na hata huduma zingine kama kilimo kikiwa kisasa kinaleta pesa nyingi na ajira nyingi.
 
Huu mjadala ni wa moto sana , ni kweli kabisa hali ya nchi inasikitisha sana ukilinganisha na rasilimali tulizo nazo .
Tatizo hizo rasilimali tunazosema tunazo hatuna maamuzi nazo hivyo kama jamii Kwanza ijiangalie kifamilia ipambane kutumia muda vizuri kujiletea maendeleo na kukataa kutumia muda vibaya kwa mambo ya wengine inatakiwa mtu ajute muda wake unapokuwa umetumika vibaya kwaajili ya mambo yasiyompa faida.
 
Kutumia kiingereza kufundisha watoto wetu ni moja ya sababu ya sisi kuwa maskini
Hapana kabisa kiingereza ni lazima tangu watu walipoanza kwenda kutafuta shule za kiingereza nje na mwisho kuzileta hapa nchini ndo unaona hata matumizi ya vitu vya kisasa na teknologia ndo vinaingia nchini kwa Kasi sana maana hata simu za kiswahili sijaona na teknologia ipo kwa kiingereza zaidi Sasa unataka watu warudi kwenye kusomewa barua, mikataba na matumizi ya vitu kwa kutumia wakalimani wa Nchi za nje jamani? Hapana kabisa kiingereza ni lazima kwa Kila mtu maana tumechoka kuwa na wajinga wengi hivi hata Tv za nyumbani sizinamfumo wa kiingereza Sasa kwanini tujiweke kwenye mazingira ya ujinga? Na hicho kiswahili kinachotumika na Nchi moja yenye akili moja na wakati kiingereza kinatumika na wengi na wenye akili tofauti?
 
Sasa tusiangalie Nchi peke yake kupitwa na familia nayo ijiangalie pia kwanini ipitwe kimaendeleo? Familia ikiwa na watu waliosoma vizuri na vipato vizuri itakuwa rahisi kuisema serikali ilete maendeleo yenye viwango vya watu wanaopenda kuishi vizuri.

hili ndio watu wengi hatuliangalii, tunapenda kuwanyooshea vidole walioko madarakani ilihali nao wametoka miongoni mwetu, tabia zile zile walizonazo ndio tulizonazo huku uraiani....

Tabia za wizi, uzinzi, uongo, usaliti, umalaya, unafiki, uchawi nk hizi ni tabia ambazo wote tuko nazo huku uswahili na sisi ndio tunaweza kuwa viongozi tukaendekeza ujinga huohuo..

La msingi ni watu katika ngazi ya familia kulea familia katika misingi inayowaweka mbali na tabia za hovyo hovyo kama wizi, uzinzi, uchawi nk....wote tukiyasimamia haya basi tutakuwa na jamii imara..
 
Mkuu ungefafanua kwasbb kiingereza chenyewe hatukijui, tuna ongea kiswahili nakujua kiswahili kwa 98% ila elimu bado duni ushindani wa kazi za kimatafa bado sana ugunduzi na ubunifu hamna ujuzi hamna, kwahiyo tatizo sio kiingereza tatizo ni kitu kingine kabisa.
Tatizo ni elimu ya kikalekale kama historia Fulani isiyo na ukweli kwasababu watu wengi walikuwa wajinga wakawa wanaogopa wengine wasiwe welevu wakawazidi ndo yote haya bado yameganda kwenye vichwa, ndo maana bado tunaogopa kizazi kipya kikijua kiingereza kikawa na maarifa ya kimataifa kitatuzidi welevu na kutushangaa kwanini tunaishi kama wanyama wasio na maarifa, mtu kuchezea muda kwa kukaa shambani siku nzima kwa kulima tuta moja eti ndo ufahari badala ya kutumia majembe ya kisasa na kulima mazao mengi kwa muda mfupi na muda mwingine ukatumika kwa mambo mengine ya uchumi, ona Leo gesi ilivyookoa upishi wa muda mfupi lakini bado Kuna watu wanaona kutumia Kuni ndo ufahari yaani akili hazitumiki kabisa.
 
Kuna vita ya kagera iliturudisha nyuma sana na pia kuzisaidia nchi za kusini mwa Africa kupigania uhuru wao nayo ilichangia
miaka 40 tangu vita ya kagera hatuja rekabisha uchumi watu kweli, kipindi hicho nchi nyingi kama Zimbabwe SA nk zilikua hazijapata uhuru, zimepata uhuru na kutupita, kwanini Tz hatuende mbele kiuchimi?
 
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:

1 - Kushabikia mno siasa kuliko uchumi
2 - Kupuuza elimu na rasilimali watu
3 - Kupuuza kilimo ambacho ndiyo mategemeo ya wengi
4 - Kutokuwa na viongozi wengi wenye upeo wa fikra na exposure (matokeo yake kiongozi mmoja anadiriki kudai kujua kila kitu, mungu mtu)
5 - Kutokuwa na dira, stability ya sera za uongozi (kila kiongozi anaanza upya)
6 - Kupuuza Kiingereza (hii watu hawataifahamu, lakini ni kweli nchi za Afrika ambazo raia wake wengi wanafahamu Kiingereza,

Kifaransa, Kireno, Kijerumani, Kispaniola, Kiarabu, huwa akili zao, taste zao zimeendelea zaidi kwa vile wana nchi za kuiga zilizoendelea kuliko wao.

Hii ni kwa sababu raia hao ni rahisi ku 'incoporate' fikra mpya kama zile zilizoko kwenye nchi hizo zilizoendelea. Katika nchi za Afrika zilizoendelea sana katika kukumbatia fikra mpya: Social media, capital ventures, masoko ya hisa, Bitcoin na innovations za aina mbali mbali ni zile zenye uelewa mkubwa wa lugha hizo.

Nimetazama katika nchi 15 za Afrika zinazotabiriwa kuona mapinduzi makubwa ya 'start up tech ventures' Tanzania haimo! Hakuna shaka ni kwa sababu ya lugha. Ukitazama matumizi ya Twitter, WhatsApp, na social platforms nyingine katika nchi za Kenya na Uganda utaona namna gani Tanzania iko nyuma. Lugha!

Hii haina maana tusijivunie Kiswahili na tusifundishe kwa Kiswahili. Tatizo ni kwamba bado hatujakifanyia kazi Kiswahili kiasi ambacho kinastahiki kuwa lugha ya kufundishia. Huwezi kupata hata vitabu 10 vya rejea kwa katika fani yeyote!
Ukisema nchi imeendelea ni vigezo gani unavyotumia? Kama GDP si kigezo kimoja - tutajie hivyo vigezo vya kusema nchi imeendelea kuliko Tz. Yaani wewe maendeleo ni kuchukua fikra/ mambo ya ulaya na kuleta Tanzania.
 
Umeongea kishabiki bila hoja yoyote ya maana, umeshindwa kuunganisha doti kuhusiana na utawala wa ccm na umaskini wa watanzania ambao wamefikia hatua ya kuona fahari kwa kuwaita "Wanyonge". Poor you.

Wewe ndo pumba kwa kuwa unadanganyika kuwa Chama ndo Shida ya maendeleo yetu. Utasubiri sana. Hata hivyo Tz tuko vizuri. Sijui unajifananisha na nani. You can not have it all my brother.

Viongozi Ni wachache sana kuliko hao mliopo maofisni na wakamilishaji miradi. Huko ndo wanaiba sana hela zetu na kujenga.

Wanaopindisha mambo wengi wako mkoani na wilayani. Hao Ni wanachama wa vyama vyote.

Wavivu Ni wanachama wa vyama vyote

Wengi tumesoma ulaya na Marekani. Vyuo Bora. Lakini tukirudi tunataka tuibe haraka au tunakutana na wale wa la saba la mwaka 1947, kila ukipendekeza mabadiliko Utaskia wenzako ulitukuta na utatuacha.

Akitoke kiongozi mkali wa kutaka actions. Mnaanza wenyewe siasa.

Watz mmejiroga. Na siku mtakayokubali kukaa chini kajitafakari na kuacha kunyoesheana vidole ndo siku ya ushindi.
 
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:

1 - Kushabikia mno siasa kuliko uchumi
2 - Kupuuza elimu na rasilimali watu
3 - Kupuuza kilimo ambacho ndiyo mategemeo ya wengi
4 - Kutokuwa na viongozi wengi wenye upeo wa fikra na exposure (matokeo yake kiongozi mmoja anadiriki kudai kujua kila kitu, mungu mtu)
5 - Kutokuwa na dira, stability ya sera za uongozi (kila kiongozi anaanza upya)
6 - Kupuuza Kiingereza (hii watu hawataifahamu, lakini ni kweli nchi za Afrika ambazo raia wake wengi wanafahamu Kiingereza,

Kifaransa, Kireno, Kijerumani, Kispaniola, Kiarabu, huwa akili zao, taste zao zimeendelea zaidi kwa vile wana nchi za kuiga zilizoendelea kuliko wao.

Hii ni kwa sababu raia hao ni rahisi ku 'incoporate' fikra mpya kama zile zilizoko kwenye nchi hizo zilizoendelea. Katika nchi za Afrika zilizoendelea sana katika kukumbatia fikra mpya: Social media, capital ventures, masoko ya hisa, Bitcoin na innovations za aina mbali mbali ni zile zenye uelewa mkubwa wa lugha hizo.

Nimetazama katika nchi 15 za Afrika zinazotabiriwa kuona mapinduzi makubwa ya 'start up tech ventures' Tanzania haimo! Hakuna shaka ni kwa sababu ya lugha. Ukitazama matumizi ya Twitter, WhatsApp, na social platforms nyingine katika nchi za Kenya na Uganda utaona namna gani Tanzania iko nyuma. Lugha!

Hii haina maana tusijivunie Kiswahili na tusifundishe kwa Kiswahili. Tatizo ni kwamba bado hatujakifanyia kazi Kiswahili kiasi ambacho kinastahiki kuwa lugha ya kufundishia. Huwezi kupata hata vitabu 10 vya rejea kwa katika fani yeyote!
Sababu zote ulizotoa siyo sahihi; sababu kubwa ni kuwa Tanzania tunapenda sana shortcut, ambayo ndiyo inayozalisha hayo uliyotaja. Kwa mfano, tamaa ya shortcut inafanya kila mtu awe shabiki wa kisiasa ili aambulie chochote kule. Ukisema ubane shortcuts zote nchini ili kila mtu afuate njia inayotakiwa, utapata taabu sana. Dira ipo, ila kushorcuts katika utekelezaji wa dira hiyo ndilo tatizo. Kufahamu kiingereza siyo tatizo kwani Cote d'ivoire hawaongei kiingereza lakini umewaweka katika listi yako. Lugha ya kiingereza itakuja yenyewe kwa mtu iwapo ataona anaihitaji; kwa mfano wanamuziki wengi tanzania siku hizi wanajua kiingereza kwa sababu wanakihitaji.

Ondoa shortcut zote na mold watu kujua kuwa inabidi wafanye kazi kweli ili kujipatia riziki halali siyo kwa njia za mkatomkato, utaona nchi inaendelea haraka sana.
 
Uchumi wa wachuuzi, tutegemee nini??
Ukiwe mwekezaji TRA wanalala na kuamka na wewe. Kodi utitiri! Bora kulipa 20elfu ya kitambulisho cha ujasiliamali! Uishi kibishi

Hapa tunakosea sana. Labda tuwe na Mawaziri waliowahi kufanya biashara. Au waende field kufanya biashara kwa muda flani, wawe wakulima, hata wawe Machinga, wajifunze kabla ya kuwa Mawaziri.

Tunaweza kupata sera zitakazo wasaidia Watanzania wengi.
 
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:

1 - Kushabikia mno siasa kuliko uchumi
2 - Kupuuza elimu na rasilimali watu
3 - Kupuuza kilimo ambacho ndiyo mategemeo ya wengi
4 - Kutokuwa na viongozi wengi wenye upeo wa fikra na exposure (matokeo yake kiongozi mmoja anadiriki kudai kujua kila kitu, mungu mtu)
5 - Kutokuwa na dira, stability ya sera za uongozi (kila kiongozi anaanza upya)
6 - Kupuuza Kiingereza (hii watu hawataifahamu, lakini ni kweli nchi za Afrika ambazo raia wake wengi wanafahamu Kiingereza,

Kifaransa, Kireno, Kijerumani, Kispaniola, Kiarabu, huwa akili zao, taste zao zimeendelea zaidi kwa vile wana nchi za kuiga zilizoendelea kuliko wao.

Hii ni kwa sababu raia hao ni rahisi ku 'incoporate' fikra mpya kama zile zilizoko kwenye nchi hizo zilizoendelea. Katika nchi za Afrika zilizoendelea sana katika kukumbatia fikra mpya: Social media, capital ventures, masoko ya hisa, Bitcoin na innovations za aina mbali mbali ni zile zenye uelewa mkubwa wa lugha hizo.

Nimetazama katika nchi 15 za Afrika zinazotabiriwa kuona mapinduzi makubwa ya 'start up tech ventures' Tanzania haimo! Hakuna shaka ni kwa sababu ya lugha. Ukitazama matumizi ya Twitter, WhatsApp, na social platforms nyingine katika nchi za Kenya na Uganda utaona namna gani Tanzania iko nyuma. Lugha!

Hii haina maana tusijivunie Kiswahili na tusifundishe kwa Kiswahili. Tatizo ni kwamba bado hatujakifanyia kazi Kiswahili kiasi ambacho kinastahiki kuwa lugha ya kufundishia. Huwezi kupata hata vitabu 10 vya rejea kwa katika fani yeyote!
Sababu kubwa ni moja; UONGOZI MBOVU NA HOVYO WA CHAMA CHA MAPINDIZI.
 
Swali la lugha sio kwamba tujue Kiswahili au Kingereza. It is not EITHER OR, but it is rather BOTH AND.
Watanzania wanaomaliza elimu ya sekondari na kuendelea waweze kuandika na kuzungumza Kiswahili na Kiingereza.

Watoto wanaosoma international schools wanakuwa na hiyo hali ya kumudu lugha zote mbili. Na they are relatively highly employable.

Viongozi wetu wengi wanajua kwamba mtoto ni vizuri ajue lugha zote mbili kwa ufasaha. Ndiyo maana karibu wote wanasomesha watoto wao English Medium Schools. Wasidanganye wananchi kwamba Kiingereza sio muhimu.

Nimependekeza huko nyuma kwamba wafanyakazi wa serikali kuu lazima watakiwe kuwa fluent in both languages. This can be ensured during employment interviews.

Tutakuwaje taifa linalotegemea mchango mkubwa toka utalii wakati front line workers kwenye hiyo sekta (maofisa wa Uhamiaji, Polisi, people in the hospitality industry) ni zero kwenye luhga za kimataifa?
Ni muhimu kuangalia English kama ni sehemu moja muhimu itayowasaidia Watanzania to be proper connected to Duniani, kujifunza mengi, kufanya biashara za kimataifa, kupata elimu.

Internet, Science, technology, historia ya Afrika, ya dunia imeandikwa kwenye lugha ya Kiingereza.

Hata uchumi, ajira, biashara zinaweza kuimarishwa kwa kujua kiingereza.
 
Hapana kabisa kiingereza ni lazima tangu watu walipoanza kwenda kutafuta shule za kiingereza nje na mwisho kuzileta hapa nchini ndo unaona hata matumizi ya vitu vya kisasa na teknologia ndo vinaingia nchini kwa Kasi sana maana hata simu za kiswahili sijaona na teknologia ipo kwa kiingereza zaidi Sasa unataka watu warudi kwenye kusomewa barua, mikataba na matumizi ya vitu kwa kutumia wakalimani wa Nchi za nje jamani? Hapana kabisa kiingereza ni lazima kwa Kila mtu maana tumechoka kuwa na wajinga wengi hivi hata Tv za nyumbani sizinamfumo wa kiingereza Sasa kwanini tujiweke kwenye mazingira ya ujinga? Na hicho kiswahili kinachotumika na Nchi moja yenye akili moja na wakati kiingereza kinatumika na wengi na wenye akili tofauti?

Ajabu nyingine ni kwamba mahakama zetu, maagizo mengi ya serikali, hukumu muhimu, vitu muhimu vinaandikwa Kiingereza wakati wengi hawajuhi hata wamehukumiwa nini, document zinasema nini? Mawakili nao wana- struggle to intepret hukumu.
 
Ukisema nchi imeendelea ni vigezo gani unavyotumia? Kama GDP si kigezo kimoja - tutajie hivyo vigezo vya kusema nchi imeendelea kuliko Tz. Yaani wewe maendeleo ni kuchukua fikra/ mambo ya ulaya na kuleta Tanzania.
Nakujibu maana wewe wataka kujua, si wale wanaotukana!
Ili nchi iitwe imeendelea, kwanza wananchi wake waoneshe wameendelea. Unaweza kulipima hili katika mambo yanayoonekana na mambo dhahania. Yanayoonekana kama, per capita income (kila Mtanzania angalau awe anapata wastani wa sh. milioni 12 kwa mwaka, sawa na $ 4,500 ( sh. elfu 33 au $12.5 kwa siku). Au kwa maneno mengine: ana uwezo wa kula milo mitatu ya wastani- inayoendana na matakwa ya mwili. Kwa hilo tu, nakuhakikishia hata asilimia 10 ya Watanzania hawalimudu. Tazama per capita ya nchi zinazofanana nasi kwa idadi ya watu, ujue nani kaendelea. Ufaransa $42,900 UK : $ 41,100 Kenya: $1,500.... Hapa Tanzania $ 980 kwa mwaka! (au dola 12 kwa mwezi badala ya siku moja)!
Maendeleo mengine yanapimwa kwa idadi ya watu waliosoma (vizuri), Idadi ya watu wanaohudumiawa na daktari mmoja nk. Katika yote hayo, tuko nyuma mno----twaishi ishi tu.
Utasema: lakini maendeleo kama hayo huchukua muda! Ni kweli. Ila narudia kichwa cha habari kwamba kutokana na vitu tulivyonavyo ingekuwa tuishavuka kwenye pato la dola 12 kwa mwezi, ingekuwa tuishafika kwenye pato la dola 12 kwa siku. Nchi nyingi zimefanya hivyo ambazo hazina tulivyonavyo.
 
Nakujibu maana wewe wataka kujua, si wale wanaotukana!
Ili nchi iitwe imeendelea, kwanza wananchi wake waoneshe wameendelea. Unaweza kulipima hili katika mambo yanayoonekana na mambo dhahania. Yanayoonekana kama, per capita income (kila Mtanzania angalau awe anapata wastani wa sh. milioni 12 kwa mwaka, sawa na $ 4,500 ( sh. elfu 33 au $12.5 kwa siku). Au kwa maneno mengine: ana uwezo wa kula milo mitatu ya wastani- inayoendana na matakwa ya mwili. Kwa hilo tu, nakuhakikishia hata asilimia 10 ya Watanzania hawalimudu. Tazama per capita ya nchi zinazofanana nasi kwa idadi ya watu, ujue nani kaendelea. Ufaransa $42,900 UK : $ 41,100 Kenya: $1,500.... Hapa Tanzania $ 980 kwa mwaka! (au dola 12 kwa mwezi badala ya siku moja)!
Maendeleo mengine yanapimwa kwa idadi ya watu waliosoma (vizuri), Idadi ya watu wanaohudumiawa na daktari mmoja nk. Katika yote hayo, tuko nyuma mno----twaishi ishi tu.
Utasema: lakini maendeleo kama hayo huchukua muda! Ni kweli. Ila narudia kichwa cha habari kwamba kutokana na vitu tulivyonavyo ingekuwa tuishavuka kwenye pato la dola 12 kwa mwezi, ingekuwa tuishafika kwenye pato la dola 12 kwa siku. Nchi nyingi zimefanya hivyo ambazo hazina tulivyonavyo.
Huu ndiyo uhalisi mkuu!Kuna watu wengi sana wana wabeza marais Mwinyi na Kikwete kwa kuwa kwao uchumi wa mtu mmoja mmoja siyo kigezo cha maendeleo ya nchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo sio elimu duni dunia nzima nchi zote zilizoebdelea technolojia huguduliwa na watu binafsi sio serikali zao

Tanzania tumesomesha mijitu kibao nchi hizo zinazosifiwa kwa elimu kubwa kuanzia chekechea hadiI PhD lakini hawana LA maana walilogundua kubadilisha kuanzia maisha yao wenyewe wanadandia siasa tu wawe akina Tundu Lisu au mbatia ambao walisoma ulaya kwenye elimu bora ni waganga njaaa tu kama wasoma kayumba.

.Hata ma diaspora yaliyobaki nje yakapata elimu bora huko yaliko yanajitwika mabox tu misiba ikitokea inakuja kutuchangisha Huku Tanzania haina hela milofa tu
Hahahaaaa...umeua mkuu
 
Shida nyingine kubwa ni siasa kuingilia mipango mwisho wa siku tunakuwa brainwashed na politics.

Tukitaka tupate maendeleo lazima tuache huo utopolo wa siasa uchwara na turuhusu professionalism ifanye Kazi na wanasiasa wa mobilise funds na kuwamobilise watu waunge mkono ndio tutoke hapa..

Wachumi tuna muarobaini wa wapi pa kuanzia ila shida ni siasa uchwara.

Lazima tuvunje "poverty circle" kwanza.
Agreed with you
 
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:

1 - Kushabikia mno siasa kuliko uchumi
2 - Kupuuza elimu na rasilimali watu
3 - Kupuuza kilimo ambacho ndiyo mategemeo ya wengi
4 - Kutokuwa na viongozi wengi wenye upeo wa fikra na exposure (matokeo yake kiongozi mmoja anadiriki kudai kujua kila kitu, mungu mtu)
5 - Kutokuwa na dira, stability ya sera za uongozi (kila kiongozi anaanza upya)
6 - Kupuuza Kiingereza (hii watu hawataifahamu, lakini ni kweli nchi za Afrika ambazo raia wake wengi wanafahamu Kiingereza,

Kifaransa, Kireno, Kijerumani, Kispaniola, Kiarabu, huwa akili zao, taste zao zimeendelea zaidi kwa vile wana nchi za kuiga zilizoendelea kuliko wao.

Hii ni kwa sababu raia hao ni rahisi ku 'incoporate' fikra mpya kama zile zilizoko kwenye nchi hizo zilizoendelea. Katika nchi za Afrika zilizoendelea sana katika kukumbatia fikra mpya: Social media, capital ventures, masoko ya hisa, Bitcoin na innovations za aina mbali mbali ni zile zenye uelewa mkubwa wa lugha hizo.

Nimetazama katika nchi 15 za Afrika zinazotabiriwa kuona mapinduzi makubwa ya 'start up tech ventures' Tanzania haimo! Hakuna shaka ni kwa sababu ya lugha. Ukitazama matumizi ya Twitter, WhatsApp, na social platforms nyingine katika nchi za Kenya na Uganda utaona namna gani Tanzania iko nyuma. Lugha!

Hii haina maana tusijivunie Kiswahili na tusifundishe kwa Kiswahili. Tatizo ni kwamba bado hatujakifanyia kazi Kiswahili kiasi ambacho kinastahiki kuwa lugha ya kufundishia. Huwezi kupata hata vitabu 10 vya rejea kwa katika fani yeyote!
Umesahau 1 muhimu. KATIBA BORA. Katiba iliyopo ni ya CCM chama Twawala.Bila kuwa na Katiba mpya tofauti na hii ya 1977 inayoibeba SerikalI ya CCM basi Maendeleo Tanzania ni sawa na ndoto za Alinacha.
 
Umeongea kishabiki bila hoja yoyote ya maana, umeshindwa kuunganisha doti kuhusiana na utawala wa ccm na umaskini wa watanzania ambao wamefikia hatua ya kuona fahari kwa kuwaita "Wanyonge". Poor you.
Achana nae, kwani humjui kuwa ni kada wa chama tawala humu jf?
 
Hapana kabisa kiingereza ni lazima tangu watu walipoanza kwenda kutafuta shule za kiingereza nje na mwisho kuzileta hapa nchini ndo unaona hata matumizi ya vitu vya kisasa na teknologia ndo vinaingia nchini kwa Kasi sana maana hata simu za kiswahili sijaona na teknologia ipo kwa kiingereza zaidi Sasa unataka watu warudi kwenye kusomewa barua, mikataba na matumizi ya vitu kwa kutumia wakalimani wa Nchi za nje jamani? Hapana kabisa kiingereza ni lazima kwa Kila mtu maana tumechoka kuwa na wajinga wengi hivi hata Tv za nyumbani sizinamfumo wa kiingereza Sasa kwanini tujiweke kwenye mazingira ya ujinga? Na hicho kiswahili kinachotumika na Nchi moja yenye akili moja na wakati kiingereza kinatumika na wengi na wenye akili tofauti?
Nakuelewa vizuri mkuu
 
Back
Top Bottom