Uchaguzi 2020 Sababu zinazofanya Magufuli apendwe na Watanzania wengi

Uchaguzi 2020 Sababu zinazofanya Magufuli apendwe na Watanzania wengi

EllySkyWilly

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2020
Posts
2,204
Reaction score
2,085
Habari ndugu zangu wana JamiiForums.

Katika uzi huu nitaelezea sababu zinazofanya Magufuli apendwe na watanzania wengi zaidi.

Mimi mwenyewe binafsi najikuta sana navutiwa na mwanasiasa mchapakazi Dkt Magufuli kama ilivyo kwa watanzania wengine hili hata wanasiasa wa vyama upinzani wanalijua na hata wanachama pia wa vyama vya upinzani wanalielewa vilivyo maana lipo wazi.

Sababu ni hizi hapa
1. Magufuli ni Rais wa Afrika, kila pembe ya dunia inamtazama huyu Rais wa namna ya tofauti katika bara hili. Ndiye Rais aliyebaki kuwa na misimamo chanya dhidi ya bara la Afrika katika kujipatia maendeleo ya kiuchumi. Anatamani bara la Afrika liwe kama ulaya.

2. Magufuli ni mchapakazi sio mvivu anajituma kufanya kazi. Amejitoa kwa udi na uvumba kuisimamia Tanzania sio kazi ndogo. Na ni watu wachache Sana duniani wenye uwezo kama huo.

3.Magufuli ana kipaji cha uongozi. Na hili limethibitishwa na jinsi anavyo weza kusimamia kila wizara inayo hitaji kusimamiwa. Hachoki anaendelea kubuni mbinu za kusimamia zaidi mpaka Tanzania iendelee.

4. Magufuli ni mzalendo na kila mtanzania anaamini Magufuli akikabidhiwa Tanzania basi Tanzania itakuwa imewekwa mahali salama salimini.

5. Magufuli ni mcha Mungu. Ni Rais na kiongozi mwenye hofu ya Mungu. Na anayo imani kubwa sana kuwa Mungu ndiye kila kitu katika maisha. Na muda wote analiombea taifa letu toka moyoni sio mdomoni tu.

6. Magufuli ameondoa rushwa na maadili mabovu kazini.

7. Magufuli amefanya makubwa sana amefufua makampuni yetu makubwa, amehimiza na kujenga viwanda mbalimbali Tanzania vidogo kwa vikubwa. Viwanda vya kila namna vimejengwa katika awamu ya tano kwenye kila wilaya.

8. Anajenga mradi mkubwa Afrika wa kufua umeme utakao chochea maendeleo makubwa ya viwanda kama Ulaya.

9. Anajenga reli ya kisasa itakayo chochea usafirishaji wa malighafi na watu vitu ambavyo vitachochea ukuaji mkubwa wa uchumi na biashara.

10. Amerudisha Elimu bure kuanzia shule ya msingi mpaka chuo kikuu. Watoto wetu sasa wanasoma bure kwa kutumia pesa ya serikali ya awamu ya tano.

11. Kwenye serikali ya Magufuli hakuna utakatishaji wa pesa tena za serikali au taasisi.

12. Amebuni mbinu mpya za kukusanya mapato pamoja na kupokea fedha kwenye taasisi mbalimbali, kwenye halmashauri za wilaya na mikoa. Njia ambazo mtu hana uwezo tena wa kuiibia serikali.

13. Naomba niishie hapa mambo mengine yapo kwenye hizi audio.

Hizi audio zinazo sababu za nyongeza ambazo zinafanya watanzania wengi kumpenda na kumkubali Magufuli.





Mitano tena kwa Magufuli.

Screenshot_20200919_021320.jpg
 
Jibu haya maswali

2 Ni Raisi gani ambaye hakuwahi kuwa mchapakazi?

4 Ni nani ambae sio mzalendo?

7 Kampuni gani kubwa iliyofufuliwa?

8. Kila raisi alijenga miradi ya umeme, inaonyesha ulikuwa hujazaliwa

9. Hata mabeberu walijenga reli

10. Elimu kweli ni bure?

11. Iko wapi 1.5T, mbona baadhi ya Taasisi hazifanyiwi ukaguzi
 
Jibu haya maswali

2 Ni Raisi gani ambaye hakuwahi kuwa mchapakazi?

4 Ni nani ambae sio mzalendo...

Naomba nichukue fursa hii kujibu maswali yako kama ifuatavyo,

2. Hata marais wa miaka ya nyuma wanajua na wanamwamini Magufuli kwamba ni mchapakazi na hana mchezo katika kazi. Hivyo hiyo sababu inajibu swali lako unaloniuliza.

4. Watanzania wanamchukulia Magufuli kama mzalendo kwasababu anaipenda Tanzania pamoja na watu wake na rasilimali zote zilizomo Tanzania. Magufuli anachukia watu wanaoibia Tanzania na wasioipenda Tanzania na anaiombea Tanzania kwa moyo wa dhati.

7. Kampuni zilizofufuliwa ni TTCL, ATCL n. k

8. Mradi wa umeme anayojenga Magufuli ndio utakaoondoa kabisa shida ya umeme Tanzania.

10. Elimu ni bure kabisa bila hata senti watoto wa ndugu zangu wote wanasoma bure kabisa. Wazazi wamebaki kuzaa tu kuhusu kusomesha waiachie serikali ya awamu ya tano na sita
 
Kura atakazopata mgombea wenu mwaka huu ni zile atakazo zawadia na Tume ya Uchaguzi.
Hata mumpambe vipi, HAKUBALIKI. Na sababu kubwa ni hulka yake ya ubabe na kupenda kujiamulia kila kitu.
Na wapinzani wanajua kura watampa zotee Magufuli number one ni Rais wa Afrika

Naipenda sana hiyo korasi
 
Naomba nichukue fursa hii kujibu maswali yako kama ifuatavyo,

2. Hata marais wa miaka ya nyuma wanajua na wanamwamini Magufuli kwamba ni mchapakazi na hana mchezo katika kazi. Hivyo hiyo sababu inajibu swali lako unaloniuliza.

4. Watanzania wanamchukulia Magufuli kama mzalendo kwasababu anaipenda Tanzania pamoja na watu wake na rasilimali zote zilizomo Tanzania. Magufuli anachukia watu wanaoibia Tanzania na wasioipenda Tanzania na anaiombea Tanzania kwa moyo wa dhati.

7. Kampuni zilizofufuliwa ni TTCL, ATCL n. k

8. Mradi wa umeme anayojenga Magufuli ndio utakaoondoa kabisa shida ya umeme Tanzania.

10. Elimu ni bure kabisa bila hata senti watoto wa ndugu zangu wote wanasoma bure kabisa. Wazazi wamebaki kuzaa tu kuhusu kusomesha waiachie serikali ya awamu ya tano na sita

2 Hujajibu swali

4 Hujajibu swali

7 Tangua ATCL ifufuliwe, tuambie faida iliyopatikana

8 Hivi nyie watu huwa mnasomeaga wapi, hivi mtu mzima unakubali kudanganywa hivi na wewe unadanganyika

10 Kumbe ni watoto wa ndugu zako, wangekuwa ni wa kwako mwenyewe, ungejua kuwa haujui. Elimu bure ni propaganda za majukwaani. Mabeberu walishawahi kusema, There's no such thing as 'free'
 
Unapofanya maamuzi ya kufanikiwa lazima uweke vipaumbele kama sera ya taifa , katiba mpya , . Tofauti na hapo utabaki una bidii sana , lakini hupigi hatua maana kuna vitu vingi mno katika safari yako ya mafanikio siyo bidii tu. south africa na nchi nyingi za africa zina bidii sana , lakini huoni walipo .
 
Kura atakazopata mgombea wenu mwaka huu ni zile atakazo zawadia na Tume ya Uchaguzi.
Hata mumpambe vipi, HAKUBALIKI. Na sababu kubwa ni hulka yake ya ubabe na kupenda kujiamulia kila kitu.
Haya mkuu ngoja tusubiri October tu
 
Unapofanya maamuzi ya kufanikiwa lazima uweke vipaumbele kama sera ya taifa , katiba mpya , . Tofauti na hapo utabaki una bidii sana , lakini hupigi hatua maana kuna vitu vingi mno katika safari yako ya mafanikio siyo bidii tu. south africa na nchi nyingi za africa zina bidii sana , lakini huoni walipo .
Mkuu unaweza kuizungumzia China kwanini inapiga maendeleo haraka kuliko mataifa mengine duniani
 
Hata sisi tulikuwa kama wewe ila baadae tukabadilika baada ya kuona hatumuelewi.
 
Ninachompendea huyu Rais ni tabia yake ya Kuongea Kilugha na Watanzania. Jamaa ni mkabila hasa.
 
Back
Top Bottom