Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,734
- 5,750
Taifa letu linatia aibu sana, maana ni kama hatuko ulimwengu wa karne ya ishirini na moja, ambayo inataka kuwe na usawa kwa binadamu wote. Maana hakuna ambaye ni special zaidi ya mwingine.
Kuna watu wanaua raia wenzao, wanatesa raia wenzao wakiwa mahabusu na kuwapiga mpaka wanakuwa vilema, lakini hawachukuliwi hatua, kisa tu ni wateule wa rais au watumishi wa umma.
Kwa mujibu wa katiba ya JMT ibara ya 37 watumishi wa umma wote wanafanya kazi kwa niaba ya rais.
Tunaposikia polisi, askari jeshi, wakuu wa wilaya na wengine wote wakitesa na kuua watu, tufahamu wanafanya kwa niaba ya rais.
Ila hapa Tanzania mpaka watulishi wa umma mpaka wachukuliwe hatua kwa makosa wanayofanya kwa niaba ya rais ni ngumu sana.
Tunashuhudia watu wakiuliwa na askari au watumishi wa umma lakini hakuna hatua za kisheria zikichukuliwa,labda tu jumba bovu limuangukie mtu kama Sabaya Ole Sangayi.
Kuna watu wanaua raia wenzao, wanatesa raia wenzao wakiwa mahabusu na kuwapiga mpaka wanakuwa vilema, lakini hawachukuliwi hatua, kisa tu ni wateule wa rais au watumishi wa umma.
Kwa mujibu wa katiba ya JMT ibara ya 37 watumishi wa umma wote wanafanya kazi kwa niaba ya rais.
Tunaposikia polisi, askari jeshi, wakuu wa wilaya na wengine wote wakitesa na kuua watu, tufahamu wanafanya kwa niaba ya rais.
Ila hapa Tanzania mpaka watulishi wa umma mpaka wachukuliwe hatua kwa makosa wanayofanya kwa niaba ya rais ni ngumu sana.
Tunashuhudia watu wakiuliwa na askari au watumishi wa umma lakini hakuna hatua za kisheria zikichukuliwa,labda tu jumba bovu limuangukie mtu kama Sabaya Ole Sangayi.