Sad Truth: Sijivunii na mama wa mtoto wangu

Sad Truth: Sijivunii na mama wa mtoto wangu

Yaani [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] mishangingi inajua kukamata wanaume.
Yaani kuna lishangingi limoja limeingilia familia yetu kuna siku tulikuwa msibani mama mkubwa akauliza "hivi huyu ni linani mbona hafananinii na sisi wote hapa"
Mishangingi bana inakuwa unique sana
[emoji23][emoji1787][emoji1787]
 
.......Baada ya kutoka kwa yule Maza, sikuendelea muda mrefu kupiga ushanta pale sokoni, ndio likaja lile wazo la kwenda mgodini Msumbiji ( yaliyoendelea after hapo yapo kwenye ile story). Huku nyuma yule Maza, mimba ilikua hadi akajifungua, Mimi sina habari, maana nilihisi ingetoka, sikuwa na simu na hatuna mawasiliano. Inaonekana baada ya kuanza malezi, alikuja akawa anaona kero na usumbufu.

Ile mtoto kuumwa umwa, clinic etc. Hapo nadhani ndio lilimjia wazo la kumpeleka mtoto home kwetu. Wazazi wangu walikuwa wanaishi mkoani, tena kijijini sio town. Kipindi nafanya kazi kwa yule Maza, alikuwa ananijua taarifa zangu nyingi, mfano kwetu tupo wangapi, majina ya wazee wangu, Kijiji walichopo n.k. Unajua ubaya au uzuri wa vijijini, ukifahamu taarifa za mtu, unaweza ukafika hadi anapoishi kwa kuulizia tu. Basi ndicho alichofanya yule Maza, alifanya jitihada hadi akafika home kabisa. Matukio mengi yaliyotokea wakati sipo, nilipata taarifa zake toka kwa sister, mama, baba na wadogo zangu wengine, kwa nyakati tofauti tofauti.

Yule Maza alipofika home, alikaribishwa vizuri tu. Unajua kijijini kwetu mgeni ukifika ambaye hawakujui kabisa, wala hawakuulizi umefata nini, wao wanakukirimu, then wanakupa nafasi. Sasa yule Maza baada ya ukaribisho, ndio akajitambulisha, akaniulizia Mimi, akaambiwa sijaonekana pale nina kama miaka miwili. Akawaambia kuwa ananifahamu vizuri, na huko nilipokuwa nimeacha mtoto ambae ndio yule. Unajua pamoja na utukutu wangu, Mimi ni kipenzi cha wote kwenye familia yetu. Ile habari ya kuwa yule mtoto ni wangu, wakaipokea vizuri, tena ukiangalia Wana muda mrefu hawajaniona. Dada angu alifurahi sana, hapo ndo akaomba mtoto ambebe, maana muda wote alikuwa bado kashikwa na yule Maza. Sasa wakati yule Maza anaendelea kuongea nao pale, Mama yangu akauliza mama wa mtoto yuko wapi, mbona hajaja? Yule Maza ndo kuwafungukia kuwa yeye ndio mama wa mtoto. Mshua kusikia vile alinyanyuka kwenye kiti kama vile amepigwa shoti, akawa anamwangalia yule Maza akihisi ameskia vibaya, dada na mama wao wakabaki wametoa macho. Yule Maza akarudia tena kauli yake, kuwa yule mtoto ni wangu, na yeye ndio nimezaa nae. Unaambiwa mama yangu alipiga ukunga mmoja mkubwa sana.

Baba alitoka sebleni speed mpaka chumbani kwake, then akatoka kabeba kibegi kama anasafiri. Mama akamuuliza, "Baba nanii unaenda wapi?" Mshua akawajibu huku anaondoka, kuwa anaenda serikali za mtaa kwa ajili ya ule mgogoro wa ardhi. (Huu mgogoro ulikuwa ni wa muda mrefu sana, na mshua alikuwa kila akiitwa anakataa kwenda, siku hiyo ndo akaona aitikie wito). Akawa anasisitiza, akirudi asimkute yule Maza.

Mama na dada wakabaki na yule Maza pale, hawaelewi wafanye nini. Yule Maza yeye katulia tu anawachora. Mama mara kaingia jikoni, mara chumbani, mara nje ili mradi hakuwa na utulivu. Yule Maza nae kila akitaka kumuita dada angu, alikuwa anamuita "Wifi", hapo ndio mama angu anazidi kuvurugwa. Dada nae akitaka kumuita yule Maza "Wifi" akili inakataa, ulimi unakuwa mzito. Siku hiyo mshua hakurudi home, na bi mkubwa Wala hakukumbuka kumuulizia. Dada ilibidi ampe kampani mama, akalala chumbani kwake ili kumpunguzia mawazo. Yule Maza akalala chumba cha dada. Niliivuruga sana familia yangu.

Usiku wakati wapo chumbani mama na dada huku, dada akawa anamwambia mama, labda yule Maza anawatania tu au amepotea nyumba, wasubirie pakuche waongee nae vizuri. Mama akawa anabisha, kuwa yule Maza hajakosea nyumba. Akawa anamwambia dada "Hivi katika kuzunguka kwako kote pua za namna ile ulishawahi kuziona wapi kama sio kwenye ukoo wa baba ako?, Yule mtoto ni wa hapa, cheki pua yake, tena nahisi ni wa baba ako, wanamsingizia tu mwanangu kwavile hayupo, we huoni baba ako alivyokimbia hapa?"

Katika kukua kwangu, hakuna siku ambayo niliona baba na mama wakigombana sababu ya swala la uaminifu. Hii ni kwa mara ya kwanza niliwaingiza katika mgogoro wa aina hiyo. Nakumbuka kipindi niko mdogo sana, tulikua tunatoka sokoni na mshua, wakati tupo njiani alitokea mwanamke from nowhere akamchapa Kofi la maana mshua, then akasepa bila kuongea chochote. Mshua alibaki ametoa macho tu, hata mimi nilibaki surprised maana sikuelewa imekuwaje kuwaje, nilishindwa kumuuliza mshua, nikatarajia ataongea kitu, nae hakuwahi niambia chochote mpaka leo. Lile tukio lilionwa na wengi, maana ilikuwa asubuhi, story zikamfikia mama. Aliniuliza sana, nikawa nakataa kuwa hapajatokea kitu kama hicho, so kitendo cha huyu Maza kuja na mtoto alaf anasema wangu, basi mama akaona ni yale yale tu, tunafichiana na mshua, yule mtoto ni wa baba, na yule Maza ni mchepuko [emoji26][emoji26][emoji26].

Kesho yake mshua alipiga simu kuuliza kama yule Maza ameondoka, alivyoambiwa bado yupo, faza akasema anaenda kumtembelea mdogo wake anaumwa, akirudi asimkute yule Maza. Jioni kabisa alirudi, tena baada ya kufatwa na mdogo wangu kuwa Kuna ugomvi home, mama anasema yule ni mke mdogo wake( baba), so mshua alikuwa anaitwa akamchukue mchepuko wake na mtoto wa uzeeni. Baba kufika home, anaingia sebleni kwa hasira, anapokewa na kelele. Yule Maza nae anamwambia "Afadhali mkwe umekuja". Ile kauli ya kuitwa mkwe ndo inazidi kumchanganya Baba, Mama nae anaona kama wanamuigizia. Kiufupi pakawa vululu vululu. Kipindi wao wanajiandaa kukaa kikao wajadili vizuri ili swala, yule Maza akawaaga kuwa anaondoka, kikao cha familia hakimuhusu. Akamuacha mtoto, akaondoka wala hana wasi wasi. Mshua wetu jinsi alivyo, akiwa katika hali ya kawaida, akitaka kumuongelea Mama yetu, huwa anatumia maneno kama "Mama fulani", "Kamuite Mama", "Mama yupo?" n.k Ila akishavurugwa, yule anakuwa sio mama yetu tena, bali ni mke wake. Utasikia anasema, nitawafukuza wote nibaki na mke wangu, au oeni mpeleke stress kwa wake zenu, niachieni mke wangu. Kiufupi mshua anamuelewa sana mke wake, na mkewe (Mama yetu) analijua ilo, lakini kizaa zaa nilicholeta kilisahaulisha vyote, mama akawa haelewi kitu.

Ile kauli ya mchuma janga ula na wakwao, hapa ndio niliona. Msala wangu, tabu imeenda kwa familia. So yeyote anayesoma hapa, namshauri awe makini sana na mambo anayofanya, asirudishe mzigo kwa familia.

Wazazi at last walikuja wakaelewana, Ila wakashindwa kuamua kuhusu mtoto. Baba alikua hataki kabisa kukubali kuwa yule mtoto nimezaa na yule Maza. Mama nae akawa anasema kuhusu mtoto, anauhakika kabisa ni wetu, Ila kuhusu mama wa mtoto ndo hawezi sema chochote mpaka Mimi niulizwe. Katika ile story niliyokuwa naelezea hustle zangu, Kuna kipindi nilikutana na mshua ghafla bila kutarajia, alaf mshua akanikazia. Kipindi Mimi namwangalia mshua kwa hudhuni nikitegemea atanionea huruma, kumbe yeye alikua anajaribu kutafakari hii ng'ombe (Mimi) ndo kweli imezaa na yule Maza? Akaniacha nikaendelee kusota kwanza. Alaf alivyorudigi home Wala hakuwaambia kama tulikutana

Hatimae nikarudi nyumbani. Siku niliyorudi home kwa mara ya kwanza toka niondokage, ndo nilijua kuwa kumbe mshua ni kichaa zaidi yangu........
Akakuangalia halafu akakausha
 
.... Unajua katika kipindi chote cha msoto, sio kwamba sikuwa na mahusiano, la, yalitokea mahusiano mengi tu japo hayakudumu muda mrefu kama ya yule Maza. Hii ilitokana na kutotulia sehemu moja muda mrefu, lakini pia sababu nyingine kubwa ni shimo aliloacha yule Maza. Kila niliyekuwa nakutana nae alikua hatoshi, anapwaya. Huku kujuta ninakojuta sasa, kulianza baada ya yeye kufahamika home na Mimi kurudi nyumbani. Lakini kabla ya hapo nilikua namkumbuka sana, tena Ile ya kumkumbuka then una wish angekua karibu yako. Nahisi wanaosemaga mapenzi yamezaliwa Tanga, hawapajui uzaramuni. Kiufupi yule Maza alikuwa kwenye akili yangu, na hata nilipofahamu kuwa mimba haikutoka na alijifungua salama, nilijihisi furaha.

Unajua mwanamke akiwa hataki kusex, hata umlazimishe vipi ni ngumu kunyanyua hisia zake, sana sana utaishia kumuumiza maana mwili haupo tayari. Ila mwanaume hata uwe umechoka kama punda, mwanamke anaweza kukufanya mwenyewe kwa hiari yako usahau uchovu wako, then ushughurike. Na yeye ndio anachagua umalize baada ya muda gani. Kwa ufupi naweza sema kipindi natoka na yule Maza ni kama vile nilikuwa tuition, maana alikuwa ananielekeza kila kitu, mara fanya hivi, weka kwa hivi, hapa fanya kwa hivi, hutakiwi kufanya hiki n.k. Kwa kupitia yeye ndio nilijua kuwa, kwa mwanamke mwanya ni urembo, Ila kwetu wanaume mwanya una kazi tofauti kabisa. Na mwanaume ukiwa na mwanya na kiganja kilichokamilika, basi unaweza kumlidhisha mwanamke yeyote yule chini ya jua.


** ***

Siku niliyofika home, baada ya mapokezi na ukaribisho mama aliendelea kuniuliza habari za huko nitokako, story za hapa na pale. Hapa ndo nikaanza kuhisi Kuna kitu hakipo sawa. Maana maongezi ya mama yalikuwa hayajanyooka, ilikua ni kama mtu anayelazimisha story ili kuzuia jambo fulani lisitokee. Tulivyokuwa wadogo, Mama alikua akitaka tusisinzie kabla ya kula ucku, basi alikuwa anakupa vikazi vya ajabu ajabu, mara kamwage maji, kalete dekio, sogeza hiki, fanya kile ilimradi usisinzie. Basi hii siku niliyorudi story zake ndio zilikuwa za mtindo huo, kuzuia kitu fulani kisitokee, japo sikuwa nakijua.

Kumbe alikua anajaribu kumblock Baba asipate nafasi ya kuongea na Mimi. Kwa ninavyomjua mshua wangu, akiwa na jambo lake sharti lifanyiwe kazi kwanza, so pale hapakutakiwa kukucha hadi nimpe majibu ya maswali yote aliyokuwa nayo, japo mpaka time hiyo sikuwa najua chochote.

Wakati naendelea kupiga story na Mama, mshua uvumilivu ukamshinda, akatukatisha, "Kama mnataka kuzungumza mje tukae sebleni tuzungumze wote, hata mimi huku nina mengi ya kuzungumza". Mama ikabidi amwambie chakula ndio kinamalizikia kuiva, nile, nipumzike, tutaongea kwa urefu asubuhi. Mshua alivyosikia habari za kuongea asubuhi ikabidi aje jikoni na yeye. Mzee wangu huwa haingiagi jikoni, Ila siku hiyo aliingia. Mama akamwambia kama amechoka sana alale, then asubuhi ataongea na Mimi vizuri. Baba akawa mkali "Yani mtu alitaka kuniulia mke wangu alafu nisubirie mpaka asubuhi ndo nimuulize wakati namuona hapa?". Ile kauli ikanishangaza kidogo, alaf nikahisi labda kwavile niliondokaga home bila wao kujua nimeenda wapi pengine ilimpa Mama presha, ndo maana Baba anasema nilitaka kumuua mkewe. Kumbe bhana kile kizaa zaa kilichotokana na yule Maza kuja home, summary ya mshua ni kwamba nilikua na lengo la kutaka kumuua mkewe. Dada ndo alikujaga kunipa story kuwa baada ya yule Maza kuwasusia mtoto na kusepa, ilibidi wao kama familia wajadiliane inakuwaje kuhusu hatma ya mtoto. Mama na Dada wakawa wanasema hawana jinsi, yule mtoto itabidi familia imlee, Mshua akawa anapinga kuwa arudishwe kwa yule Maza.

Ilibidi na kaka zangu wengine waitwe pale home kujadiliana namna gani lile linatatuliwa. Maana Baba alishaamua mtoto arudishwe Dar. Mpaka siku hiyo ya kikao, zilishapita kama wiki mbili tokea yule Maza aondoke, lakini mshua alikua bado hataki kuamini kama nimezaa na yule Maza. Yeye fikra zake ni kwamba nilitia mimba alafu kwa uoga, nikakimbia. Sasa yule aliyekuja na mtoto ni mama wa Binti niliyempa mimba. Baba akawa anawashauri inabidi Mimi nitafutwe, then taratibu zifatwe ili Binti niliyezaa nae akabidhiwe kwetu kihalali. Dada akajiribu kuwaambia kuwa kwa jinsi yule Maza alivyokuwa anaongea nae, ni dhahiri yeye ndio mama wa mtoto. Kaka yangu mkubwa akasema kwa jinsi Dunia ya sasa ilivyo, kuchaguliana mke au mchumba ishapitwa na wakati, kwavile dogo (Mimi) amechagua, huyo ndo shemeji yetu, sioni tatizo juu ya ilo. Kauli za "shemeji", "wifi" na "mkwe" Baba ndio alikua hataki kuziskia kabisa. Mwisho wa kikao, wakaamua Dada akakae nae, mpaka akue kue kidogo then ndo ataenda kuishi pale kwa Babu na Bibi.


* * ****** ***


Mimi nilivyorudi nyumbani, yule mwanangu hakuwepo, alikuwa bado anaishi kwa Dada. Baada ya Mama kushauri niulizwe asubuhi, Baba alikubali. Usiku ule tukaongea habari tofauti kabisa. Kulivyokucha, katika story ndo akaniuliza kama katika movements zangu sijaacha mtoto sehemu, yani alianzia mbali sana, nahisi alitaka kuona nitasemaje. Mimi nikamuelezea tu kuwa nina mtoto wa kiume Dar. Baba akaniambia "Mtoto sio shida, vipi kuhusu mama ake? " The way alivyo uliza tu nikikumbuka na hali ya jana yake usiku, nikahisi kuna kitu akipo sawa. Ikabidi nimuwahi kwa kumwambia ukweli, maana Mzee wetu jinsi alivyo, kwa sisi watoto wakiume, tukikoseaga huwa anatengeneza mazingira ya kupigana. Na ikitokea hiyo chance, bila mama kuingilia, anaweza akakuua.

Wakati naendelea kujielezea, akanikatisha "Hebu ngoja kwanza legend, hivi unajiskia unachokiongea?" Nikashangaa ilo jina la legend. Mshua sasa kujizuia kukaisha, akaanza kutema nyongo. "Hivi unajua yule Maza kama angekua kazaliwa familia ya Mama ako, basi angekua mtoto wa pili kama sio wa kwanza" " Wadogo zake mama ako hakuna hata mmoja anayempata kwa umri", " Hivi ule unene wake ndo ulokuchanganya au?" Mzee aliongea sana, akawa anasema watoto wake wote wamerithi tabia kwake, sijui ilikuaje Mimi nikarithi ujombani. Ile kauli Mama akaamua kuitolea ukimya "Yani ukoo wenu (wa baba) ulivyo na damu kali, Sina hata mtoto mmoja aliyefata kwetu, tena mmeniharibia hadi Binti yangu na pua zenu zisizojua kujificha, tafuta namna nzuri ya kuelewana na mwanao, ujombani hapahusiki". Kauli ya Mama bado kidogo inifanye nicheke, nikajizuia, ila mshua akakiona hicho kitendo. Sijakaa hata sawa, alinivaa mzima mzima, akanipiga kichwa cha kifua. Wote kama tulivyo tukaenda mpaka chini. Sijakaa sawa, akaniweka kichwa kingine cha uso tukiwa pale pale chini, nataka kujiweka sawa, akaniwahi na kabali. Mzee wangu hana pumzi, ila ana nguvu sana za mikono, maana tushapigana nae mara kadhaa. Kitendo cha yeye kuniwahi na kabali, nikajisemea kimoyo moyo, "Leo hapa Mama asipoingilia nakufa". Nilijitahidi kadiri nilivyoweza, Ila wapi. Mama nae baada ya kuona tunapigana, akataka kuja. Kumbe Mzee alishajua anachotaka kufanya, so aliacha kamfungia Mama kwa nje. Mama ametoka jikoni mbio ili aje nje kuamulia, anakuta mlango wa nje umefungwa, zunguka upande wa pili, nako hivyo hivyo. Akasogea dirishani anabwata tu. Mzee alinipiga kabali mpaka nikanya. Alivyoona hali yangu tete ndo akaniachia, then akanyanyuka fasta, akakunja ngumi kwa ajili ya pambano rasmi. Mama analalama "Utaniulia mwanangu" Baba anamjibu "Huyu sio mtoto, alichelewa tu kuzaliwa, acha niende nae sawa". Muda huo Mimi ndo natafuta pumzi maana nilikuwa hoi, faza wala hajali ndo kwanza anarusha ngumi. Alinipiga moja kwenye jicho, sitokaa niyasahau yale maumivu. Ikabidi nianze kujitetea, Ila nilichezea sana vitasa vya tumbo na mbavu. Mzee alipoona pumzi inamuishia, akaanza kutafuta namna ya kunipiga kabali tena ili avute pumzi, nikawa nishamsoma maana ndio ilikua kawaida yake, mkipigana anakuwahi kwanza kwenye pua ili kukukata moto, so nikawa naichunga pua yangu, na yeye anachunga yake. Huku na kule, akanipiga tena kwenye jicho lile lile, sijakaa vizuri,akanipiga mtama then akaniwahi na kabali. Nikaona hapa nisipokuwa makini nakunya tena

Muda huo Mama anahaha tu dirishani, kelele zake zinamezwa na kelele za mifugo. Na eneo letu ni kubwa, majirani wako mbali. Dingi nae ndio kwanza anazidi kukaza mikono......



Narudi kumalizia....

Mzee alinipiga kabali mpaka nikanya. Alivyoona hali yangu tete ndo akaniachia, then akanyanyuka fasta, akakunja ngumi kwa ajili ya pambano rasmi. Mama analalama "Utaniulia mwanangu" Baba anamjibu "Huyu sio mtoto, alichelewa tu kuzaliwa



[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
[mention]Kelsea [/mention] njoo huku[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
We jamaa sijawah kukuzingatia[emoji28][emoji28]


Kwahyo ile kabali ikikua kama mtihani wa moko
Alipokunja ngumi ndio mkaanza necta[emoji28][emoji23][emoji23][emoji23]
 
.... Unajua katika kipindi chote cha msoto, sio kwamba sikuwa na mahusiano, la, yalitokea mahusiano mengi tu japo hayakudumu muda mrefu kama ya yule Maza. Hii ilitokana na kutotulia sehemu moja muda mrefu, lakini pia sababu nyingine kubwa ni shimo aliloacha yule Maza. Kila niliyekuwa nakutana nae alikua hatoshi, anapwaya. Huku kujuta ninakojuta sasa, kulianza baada ya yeye kufahamika home na Mimi kurudi nyumbani. Lakini kabla ya hapo nilikua namkumbuka sana, tena Ile ya kumkumbuka then una wish angekua karibu yako. Nahisi wanaosemaga mapenzi yamezaliwa Tanga, hawapajui uzaramuni. Kiufupi yule Maza alikuwa kwenye akili yangu, na hata nilipofahamu kuwa mimba haikutoka na alijifungua salama, nilijihisi furaha.

Unajua mwanamke akiwa hataki kusex, hata umlazimishe vipi ni ngumu kunyanyua hisia zake, sana sana utaishia kumuumiza maana mwili haupo tayari. Ila mwanaume hata uwe umechoka kama punda, mwanamke anaweza kukufanya mwenyewe kwa hiari yako usahau uchovu wako, then ushughurike. Na yeye ndio anachagua umalize baada ya muda gani. Kwa ufupi naweza sema kipindi natoka na yule Maza ni kama vile nilikuwa tuition, maana alikuwa ananielekeza kila kitu, mara fanya hivi, weka kwa hivi, hapa fanya kwa hivi, hutakiwi kufanya hiki n.k. Kwa kupitia yeye ndio nilijua kuwa, kwa mwanamke mwanya ni urembo, Ila kwetu wanaume mwanya una kazi tofauti kabisa. Na mwanaume ukiwa na mwanya na kiganja kilichokamilika, basi unaweza kumlidhisha mwanamke yeyote yule chini ya jua.


** ***

Siku niliyofika home, baada ya mapokezi na ukaribisho mama aliendelea kuniuliza habari za huko nitokako, story za hapa na pale. Hapa ndo nikaanza kuhisi Kuna kitu hakipo sawa. Maana maongezi ya mama yalikuwa hayajanyooka, ilikua ni kama mtu anayelazimisha story ili kuzuia jambo fulani lisitokee. Tulivyokuwa wadogo, Mama alikua akitaka tusisinzie kabla ya kula ucku, basi alikuwa anakupa vikazi vya ajabu ajabu, mara kamwage maji, kalete dekio, sogeza hiki, fanya kile ilimradi usisinzie. Basi hii siku niliyorudi story zake ndio zilikuwa za mtindo huo, kuzuia kitu fulani kisitokee, japo sikuwa nakijua.

Kumbe alikua anajaribu kumblock Baba asipate nafasi ya kuongea na Mimi. Kwa ninavyomjua mshua wangu, akiwa na jambo lake sharti lifanyiwe kazi kwanza, so pale hapakutakiwa kukucha hadi nimpe majibu ya maswali yote aliyokuwa nayo, japo mpaka time hiyo sikuwa najua chochote.

Wakati naendelea kupiga story na Mama, mshua uvumilivu ukamshinda, akatukatisha, "Kama mnataka kuzungumza mje tukae sebleni tuzungumze wote, hata mimi huku nina mengi ya kuzungumza". Mama ikabidi amwambie chakula ndio kinamalizikia kuiva, nile, nipumzike, tutaongea kwa urefu asubuhi. Mshua alivyosikia habari za kuongea asubuhi ikabidi aje jikoni na yeye. Mzee wangu huwa haingiagi jikoni, Ila siku hiyo aliingia. Mama akamwambia kama amechoka sana alale, then asubuhi ataongea na Mimi vizuri. Baba akawa mkali "Yani mtu alitaka kuniulia mke wangu alafu nisubirie mpaka asubuhi ndo nimuulize wakati namuona hapa?". Ile kauli ikanishangaza kidogo, alaf nikahisi labda kwavile niliondokaga home bila wao kujua nimeenda wapi pengine ilimpa Mama presha, ndo maana Baba anasema nilitaka kumuua mkewe. Kumbe bhana kile kizaa zaa kilichotokana na yule Maza kuja home, summary ya mshua ni kwamba nilikua na lengo la kutaka kumuua mkewe. Dada ndo alikujaga kunipa story kuwa baada ya yule Maza kuwasusia mtoto na kusepa, ilibidi wao kama familia wajadiliane inakuwaje kuhusu hatma ya mtoto. Mama na Dada wakawa wanasema hawana jinsi, yule mtoto itabidi familia imlee, Mshua akawa anapinga kuwa arudishwe kwa yule Maza.

Ilibidi na kaka zangu wengine waitwe pale home kujadiliana namna gani lile linatatuliwa. Maana Baba alishaamua mtoto arudishwe Dar. Mpaka siku hiyo ya kikao, zilishapita kama wiki mbili tokea yule Maza aondoke, lakini mshua alikua bado hataki kuamini kama nimezaa na yule Maza. Yeye fikra zake ni kwamba nilitia mimba alafu kwa uoga, nikakimbia. Sasa yule aliyekuja na mtoto ni mama wa Binti niliyempa mimba. Baba akawa anawashauri inabidi Mimi nitafutwe, then taratibu zifatwe ili Binti niliyezaa nae akabidhiwe kwetu kihalali. Dada akajiribu kuwaambia kuwa kwa jinsi yule Maza alivyokuwa anaongea nae, ni dhahiri yeye ndio mama wa mtoto. Kaka yangu mkubwa akasema kwa jinsi Dunia ya sasa ilivyo, kuchaguliana mke au mchumba ishapitwa na wakati, kwavile dogo (Mimi) amechagua, huyo ndo shemeji yetu, sioni tatizo juu ya ilo. Kauli za "shemeji", "wifi" na "mkwe" Baba ndio alikua hataki kuziskia kabisa. Mwisho wa kikao, wakaamua Dada akakae nae, mpaka akue kue kidogo then ndo ataenda kuishi pale kwa Babu na Bibi.


* * ****** ***


Mimi nilivyorudi nyumbani, yule mwanangu hakuwepo, alikuwa bado anaishi kwa Dada. Baada ya Mama kushauri niulizwe asubuhi, Baba alikubali. Usiku ule tukaongea habari tofauti kabisa. Kulivyokucha, katika story ndo akaniuliza kama katika movements zangu sijaacha mtoto sehemu, yani alianzia mbali sana, nahisi alitaka kuona nitasemaje. Mimi nikamuelezea tu kuwa nina mtoto wa kiume Dar. Baba akaniambia "Mtoto sio shida, vipi kuhusu mama ake? " The way alivyo uliza tu nikikumbuka na hali ya jana yake usiku, nikahisi kuna kitu akipo sawa. Ikabidi nimuwahi kwa kumwambia ukweli, maana Mzee wetu jinsi alivyo, kwa sisi watoto wakiume, tukikoseaga huwa anatengeneza mazingira ya kupigana. Na ikitokea hiyo chance, bila mama kuingilia, anaweza akakuua.

Wakati naendelea kujielezea, akanikatisha "Hebu ngoja kwanza legend, hivi unajiskia unachokiongea?" Nikashangaa ilo jina la legend. Mshua sasa kujizuia kukaisha, akaanza kutema nyongo. "Hivi unajua yule Maza kama angekua kazaliwa familia ya Mama ako, basi angekua mtoto wa pili kama sio wa kwanza" " Wadogo zake mama ako hakuna hata mmoja anayempata kwa umri", " Hivi ule unene wake ndo ulokuchanganya au?" Mzee aliongea sana, akawa anasema watoto wake wote wamerithi tabia kwake, sijui ilikuaje Mimi nikarithi ujombani. Ile kauli Mama akaamua kuitolea ukimya "Yani ukoo wenu (wa baba) ulivyo na damu kali, Sina hata mtoto mmoja aliyefata kwetu, tena mmeniharibia hadi Binti yangu na pua zenu zisizojua kujificha, tafuta namna nzuri ya kuelewana na mwanao, ujombani hapahusiki". Kauli ya Mama bado kidogo inifanye nicheke, nikajizuia, ila mshua akakiona hicho kitendo. Sijakaa hata sawa, alinivaa mzima mzima, akanipiga kichwa cha kifua. Wote kama tulivyo tukaenda mpaka chini. Sijakaa sawa, akaniweka kichwa kingine cha uso tukiwa pale pale chini, nataka kujiweka sawa, akaniwahi na kabali. Mzee wangu hana pumzi, ila ana nguvu sana za mikono, maana tushapigana nae mara kadhaa. Kitendo cha yeye kuniwahi na kabali, nikajisemea kimoyo moyo, "Leo hapa Mama asipoingilia nakufa". Nilijitahidi kadiri nilivyoweza, Ila wapi. Mama nae baada ya kuona tunapigana, akataka kuja. Kumbe Mzee alishajua anachotaka kufanya, so aliacha kamfungia Mama kwa nje. Mama ametoka jikoni mbio ili aje nje kuamulia, anakuta mlango wa nje umefungwa, zunguka upande wa pili, nako hivyo hivyo. Akasogea dirishani anabwata tu. Mzee alinipiga kabali mpaka nikanya. Alivyoona hali yangu tete ndo akaniachia, then akanyanyuka fasta, akakunja ngumi kwa ajili ya pambano rasmi. Mama analalama "Utaniulia mwanangu" Baba anamjibu "Huyu sio mtoto, alichelewa tu kuzaliwa, acha niende nae sawa". Muda huo Mimi ndo natafuta pumzi maana nilikuwa hoi, faza wala hajali ndo kwanza anarusha ngumi. Alinipiga moja kwenye jicho, sitokaa niyasahau yale maumivu. Ikabidi nianze kujitetea, Ila nilichezea sana vitasa vya tumbo na mbavu. Mzee alipoona pumzi inamuishia, akaanza kutafuta namna ya kunipiga kabali tena ili avute pumzi, nikawa nishamsoma maana ndio ilikua kawaida yake, mkipigana anakuwahi kwanza kwenye pua ili kukukata moto, so nikawa naichunga pua yangu, na yeye anachunga yake. Huku na kule, akanipiga tena kwenye jicho lile lile, sijakaa vizuri,akanipiga mtama then akaniwahi na kabali. Nikaona hapa nisipokuwa makini nakunya tena

Muda huo Mama anahaha tu dirishani, kelele zake zinamezwa na kelele za mifugo. Na eneo letu ni kubwa, majirani wako mbali. Dingi nae ndio kwanza anazidi kukaza mikono......



Narudi kumalizia....
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji2][emoji23][emoji23][emoji23]
" Hebu ngoja kwanza legend"

Haahaaahaa

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom