Uchaguzi 2020 SADC yaipongeza Tanzania kwa kuendesha Uchaguzi halali

Uchaguzi 2020 SADC yaipongeza Tanzania kwa kuendesha Uchaguzi halali

Mbona Watanzania wenyewe walikuwepo kwenye vituo vya kupigia kura? Wameona kura kwenye mabegi zikiletwa kwenye vituo, wameona mawakala wa vyama vya upinzani wakifukuzwa, wameona mawakala wa vyama vya upinzani wakinyimwa utambulisho, nk. Picha zimepigwa na video pia?

Hata kabla ya uchaguzi, Watanzania waliona vyombo vya habari zikitangaza habari za CCM na Magufuli tu, wagombea wa vyama vya upinzani wakienguliwa wengine kwa kutekwa ili muda wa kurudisha fomu upite, nk. Hawa SADC ndio nani na wakaa nchi gani? Kama ubeberu upo basi ndio huu wa SADC kuja kuwaambia Watanzania uchaguzi eti ulikuwaje. Ni kichekesho.
mambo ya kushangaza yanayoendelea TZ.
 
Jukwaa la Tume za Uchaguzi la SADC limeipongeza serikali ya Tanzania kwa kuendesha Uchaguzi halali.

Jukwaa hilo linaundwa na tume za uchaguzi za mataifa 14 ya SADC.

Tamko lililotolewa na jukwaa hilo kutoka makao makuu yake yaliyopo Botswana, linasema NEC na ZEC zimeendesha uchaguzi huru, wa haki, unaoaminika na uliogubikwa na uwazi wa hali ya juu.

Aidha, jukwaa hilo limezitaka nchi wanachama wa SADC kujifunza kiwango cha juu cha demokrasia kilichooneshwa na Tanzania na Zanzibar kwenye chaguzi kuu zake za mwaka 2020.
Angalia kauli ya waangalizi wa nje walicho kisema
Screenshot_20201101-142855.jpg
 
Jukwaa la Tume za Uchaguzi la SADC limeipongeza serikali ya Tanzania kwa kuendesha Uchaguzi halali.

Jukwaa hilo linaundwa na tume za uchaguzi za mataifa 14 ya SADC.

Tamko lililotolewa na jukwaa hilo kutoka makao makuu yake yaliyopo Botswana, linasema NEC na ZEC zimeendesha uchaguzi huru, wa haki, unaoaminika na uliogubikwa na uwazi wa hali ya juu.

Aidha, jukwaa hilo limezitaka nchi wanachama wa SADC kujifunza kiwango cha juu cha demokrasia kilichooneshwa na Tanzania na Zanzibar kwenye chaguzi kuu zake za mwaka 2020.
Sasa jamani izonchi zinazounda hilo genge chaguzi zao uwazipo huru ?ilitujuwe maoni yao nikweli mfano kamavile china akosoe au Asifie mimi sishikichochote hapo labda ningesikia marekani tu
 
Usipende kutusemea wa Tanzania eti sisi wa Tanzania!!! Au wewe dada yako na mumewe ndio wa Tanzania wote?
Kwahiyo wafuasi, wapenzi, wafurukutwa na wanachama wa chadema na ACT ni warundi?
 
Mbona Watanzania wenyewe walikuwepo kwenye vituo vya kupigia kura? Wameona kura kwenye mabegi zikiletwa kwenye vituo, wameona mawakala wa vyama vya upinzani wakifukuzwa, wameona mawakala wa vyama vya upinzani wakinyimwa utambulisho, nk. Picha zimepigwa na video pia?

Hata kabla ya uchaguzi, Watanzania waliona vyombo vya habari zikitangaza habari za CCM na Magufuli tu, wagombea wa vyama vya upinzani wakienguliwa wengine kwa kutekwa ili muda wa kurudisha fomu upite, nk. Hawa SADC ndio nani na wakaa nchi gani? Kama ubeberu upo basi ndio huu wa SADC kuja kuwaambia Watanzania uchaguzi eti ulikuwaje. Ni kichekesho.
Kwa nini wakati mwingine unajitoa ufahamu, mbona hapa upo vizuri?

CHADEMA na ACT-Wazalendo walikuwa na nafasi nzuri sana ya kuzuia uchaguzi wakati haya uliyoorodhesha hapa yanatokea,; na sio wakati huu baada ya kuruhusu UCHAFUZI kufanyika.

Ilikuwa ni rahisi zaidi kudhibiti uchafuzi huo katika vituo vyote vya kupigia kura na kusimamisha uchaguzi kila mahali, badala ya kusubiri kura zihesabiwe na matokeo haramu kutangazwa ndipo maandamano yafanyike.

Maandamano haya hayatabadili chochote, sana sana yatakuwa ya kuwaumiza tu baadhi ya majasiri watakaojitoa mhanga kuitetea nchi hii.
 
SADC ni muungano wa madikteta tupu ukitoa Kenya na S. Africa
Aiseee!
Kenya nao wamo?

Unawaweka wapi Botswana, Namibia, na hata Malawi kwa sasa hivi?

Ila inashangaza kwa SADC kutoa taarifa ya namna hii. Hawa ni Secretariat waliotoa taarifa, na hata taarifa yenyewe naona ni ya kujiumauma na aibu nyingi.
 
Ingekuwa vyema zaidi kama ungesema " baadhi ya watanzania"!!!!
Umeona ripoti ya wazungu??? Yaani hata wazungu wameona ubatili, wewe hujauona?? Jiwe alikataliwa kwa kiwango kikubwa Sana.
 
Umeona ripoti ya wazungu??? Yaani hata wazungu wameona ubatili, wewe hujauona?? Jiwe alikataliwa kwa kiwango kikubwa Sana.
Shida Wazungu hawaishi Tanzania, kuna watu kibao wanaomkubali Magufuli wengine hawako hata mitandaoni ukipata bahati ya kukutana na watu mbalimbali/tofautitofauti unaweza ukashangaa idadi ya watu wanaomkubali!! Ndo maana nikasema ni heri kusema baadhi ya Watanzania
 
Back
Top Bottom