Pro LowassaWacha aisome namba mpuuzi Sana huyu jamaa
Ametumika vya kutosha kipindi Cha utawala wa Kikwete na Mkapa kuchafua watu na kueneza propaganda.
Kwani amount ya pesa inayotakiwa kuwa declared ukiwa unaingia nchini ni kiasi gani?(KES 491,700 X 23) + (USD 8000 x 2314) = TZS 28,411,327.80.
Kosa kubwa hapo ni kupita njia za panya. Ila hiyo hela mbona ya maandazi tu!!!
Kwani amount inayotakiwa kuwa declared ukiwa unaingia nchini ni kiasi gani?Kosa kubwa hapo ni kupita njia za panya. Ila hiyo hela mbona ya maandazi tu!!!
Kwa sababu Kubenea ni mwanahabari hivyo kukamatwa kwake ni habari. Isiwe tena kuanzisha lawama zisizo na ukweli bali uzushi tu. Wako wengi mahabusi/gerezani wakisubiri/kukabiliwa na kesi za aina hiyo.Kama Wahusika wameamua kuwa na Umakini huu basi usiwe unaishia tu kwa Wanasiasa tena wa Upinzani kwani unafanywa na wengine wengi tu.
Mtanzania ameingia Tanzania sio kihalali? Sijae
Ndio mkuu, jamaa alikuwa anatoka "kuuza nchi kwa vipande ishirini vya fedha!"Kumbe interest yao ni mambo mengine !
Mimi nilikuwa nasema hilo la kutoka kwenda nchi jirani na kurudi!Huku kwetu ni maisha ya kawaida kabisa na tunaenda kama tunavyoenda chooni!Wengine hadi kuhemea tunahemea nchi jirani!
Kauzaje nchi?Ana hati za ardhi ambazo anaweza kuuza na sehemu ya Tanzania ikawa inamilikiwa na wakenya?Nieleweshe hapo!Ndio mkuu, jamaa alikuwa anatoka "kuuza nchi kwa vipande ishirini vya fedha!"
I will give you a very cantangerous punishmentHii ndio ile walimu walikuwa wanatutishia enzi zile za Mwalimu kwa kutwambia "I will deal with you perpendicularly".
Vitu vingi vinakua haviingii kabisa kichwani, yaani moja haikai mbili nayo tia maji. Katika kipindi kama hiki kwa nini mtu anakuwa anakosa umakini na kuacha nafasi za kutunguliwa, ni kama kumpa adui yako risasi ilhali unajua kwamba given a chance anakumaliza.TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA SAED AHMED KUBENEA
Mnamo tarehe 5/9/2020, Jeshi la Polisi Tanzania lilimkamata SAED AHMED KUBENEA akiwa katika gari la abiria lenye namba ya usajili T. 645 DKR akitokea kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya, eneo la Namanga akielekea Arusha mjini.
Mara baada ya upekuzi, mtuhumiwa huyo alikutwa, pamoja na vitu vingine, Dola za Marekani Elfu Nane (USD 8000), Shilingi za Kenya Laki Nne Tisini na Moja Elfu Mia Saba (KES 491,700), Shilingi za Kitanzania Elfu Sabini na Moja (TZS 71,000/-), tiketi ya basi la Super Couch lenye namba ya usajili KCP 4230 ya tarehe 05/09/2020 kutoka Nairobi, Kenya kwenda Namanga, ‘Memorandum of Understanding’ kati ya Hali-Halisi (Tanzania) na Buni Media Limited (Kenya), Risiti ya malipo ya hoteli iitwayo After 40 Hotels Limited iliyopo Nairobi, Kenya yenye jina la Kubenea, Saed Ahmed kama mgeni kuanzia tarehe 3/9/2020 hadi 5/9/2020 na. Pasi yake ya kusafiria (Passport).
Mara baada ya kukamatwa, mtuhumiwa alieleza kuwa alifika mkoani Arusha tarehe 2/9/2020 akitokea Dar es Salaam na kufikia katika hoteli iliyopo Arusha mjini. Alieleza zaidi kuwa, tarehe 3/9/2020, alienda kulala kwa Kaka yake tarehe 3/9/2020, na tarehe 4/9/2020 alienda Namanga na kupokea fedha taslimu tajwa hapo juu kutoka kwa raia wa Kenya.
Hata hivyo, mara baada ya kupitia Ushahidi uliokusanywa nimebaini kuwa:-
1. Mtuhumiwa SAED AHMED KUBENEA hakufikia katika hoteli aliyoitaja Arusha mjini, wala kulala kwa Kaka yake kama alivyoeleza.
2. Mtuhumiwa tajwa alivuka Mpaka usio rasmi na kuelekea Nairobi nchini Kenya na kisha kurejea nchini Tanzania bila kutumia Mpaka rasmi mnamo tarehe 5/9/2020.
3. Mtuhumiwa tajwa aliingiza nchini Fedha za Kigeni (foreign currency) bila kutoa tamko rasmi la kisheria kinyume na masharti ya Kanuni za the Anti-Money Laundering (Cross - Border Declaration of Currency and Bearer Negotiable Instruments) Regulations, 2016 zikisomwa pamoja na Kifungu cha 28B(1)(a) cha Sheria ya Kuzuia Utakasishaji wa Fedha Haramu, Na. 12 ya Mwaka 2006.
Hivyo, leo tarehe 7/9/2020, mara baada ya kujiridhisha na uwepo wa ushahidi wa kutosha dhidi ya mtuhumiwa tajwa, sambamba na misingi ya kikatiba inayoniongoza kama ilivyoanishwa katika Ibara ya 59B(4)(a) hadi (c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, nimeidhinisha mashtaka yafuatayo dhidi ya mtuhumiwa SAED AHMED KUBENEA:-
a. Kuingia nchini Tanzania kinyume na Sheria ya Uhamiaji, Sura ya 54 Marejeo ya mwaka 2016; na
b. Kuingiza nchini fedha za Kigeni bila kutoa tamko kinyume na Kanuni za Utoaji Tamko la Fedha Mpakani za mwaka 2016.
View attachment 1561443
View attachment 1561444
Lengo sio kumfunga hapo lengo lao ni kumkomoa kwa kumpotezea muda tu.Kesi dhaifu sana hii, hizi ndio kesi za kuwapa ujiko mawakili
Nitashangaa sana kama wengi hamuoni udhaifu wa mashtaka haya.
Kwahiyo hapa ni kushikishana adabu tu.hahaha kampuni ya kuuza "zana za kivita"
View attachment 1561571
Kubenea ndio ameuza Loliondo gate?Ndio mkuu, jamaa alikuwa anatoka "kuuza nchi kwa vipande ishirini vya fedha!"
Hii ndio ile walimu walikuwa wanatutishia enzi zile za Mwalimu kwa kutwambia "I will deal with you perpendicularly".
Kubenea alikua anagombea Kinondoni nasio ubungo, alihama jimbo.Kubenea amehama Chadema na kuhamia ACT, na kwa uhasama pale Ubungo.
Chadema Ubungo imepasuka sababu ya ishu yake na Boni (mtu wa Mbowe).
ACT Ubungo ndo chama pekee kilichomuwekea Boni pingamizi pamoja na wagombea wote udiwani wa CHADEMA UBUNGO. Hili pingamizi la ACT ndo limemuengua Boni kugombea ubunge Ubungo. Kitu ambacho hakiwezi kufurahisha akina Mbowe.
Kwahiyo sidhani kama Kubenea anashirikiana na Lissu, ili hali akina Mbowe na wenzake wanammind.