Saed Kubenea atiwa mbaroni. Afikishwa Mahakamani kwa kuingia nchini kinyume na Sheria, utakatishaji fedha na kupelekwa rumande

Saed Kubenea atiwa mbaroni. Afikishwa Mahakamani kwa kuingia nchini kinyume na Sheria, utakatishaji fedha na kupelekwa rumande

Mahakama inahitaji ushahidi wa Kubenea kwenda Kenya na kurudi kwa njia ya panya na si vinginevyo.

Kesi ya Zombe Jaji aliwaambia upande wa mashtaka wakawatafute wauwaji wawalete mahakamani, Zombe hakuuwa mtu lakini alishtakiwa kwa kesi ya mauwaji.

Wengi humu bado hamuelewi kwa nini watu wengi hawafungwi mahakamani bado hamjajuwa mahakama hasa huwa inahitaji nini ili kumfunga mtu.
Ulivyo kiazi, wewe utadhani ndiyo mahakama. Unaulizwa huko mahakamani atafika baada ya miaka mingapi? Uchaguzi utakuwa umeisha. Ni kama kusubiri binti aliyezaliwa leo ili umuoe akiwa na miaka 2o, je, unauhakika atakuwa hai au wewe dushe litakuwa linawika wakati huo?
 
Anavunja Sheria kwa koti la Upinzani

Akilalamika eti wananyanyaswa.

Sasa kisa cha kutumia njia za panya kuingia Kenya na kutoka nini

Isijekuwa anafanya Mambo ya Ugaidi hapa.
Ndo wale wale na mwenzie aliyekiri kosa kwa DPP! tukiwaambia upinzani wanatumika na mabeberu wanashupaza shingo! Magu 5 tena
 
Kubenea kapokea kiinua mgongo zaidi ya TZS 200 million, kufanya money laundering ya TZS 28 million haijaeleweka
Haa! We hujasikia muheshimiwa Waziri kwenda kukopa pikipiki unashangaa hili?

Hapo hakuna uonevu toka kupitia mpaka rasmi gonga passport yako vizuri na kurudi Fanya vivohivyo...bahati nzuri Kenya hakuna Visa hapo...unaenda tu kama Ilala...kama amevunja sheria...sheria ifuate mkondo wake tu haina jinsi.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

YAH: KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA SAED AHMED KUBENEA

Mnamo tarehe 5/9/2020, Jeshi la Polisi Tanzania lilimkamata SAED AHMED KUBENEA akiwa katika gari la abiria lenye namba ya usajili T. 645 DKR akitokea kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya, eneo la Namanga akielekea Arusha mjini.

Mara baada ya upekuzi, mtuhumiwa huyo alikutwa, pamoja na vitu vingine, Dola za Marekani Elfu Nane (USD 8000), Shilingi za Kenya Laki Nne Tisini na Moja Elfu Mia Saba (KES 491,700), Shilingi za Kitanzania Elfu Sabini na Moja (TZS 71,000/-), tiketi ya basi la Super Couch lenye namba ya usajili KCP 4230 ya tarehe 05/09/2020 kutoka Nairobi, Kenya kwenda Namanga, ‘Memorandum of Understanding’ kati ya Hali-Halisi (Tanzania) na Buni Media Limited (Kenya), Risiti ya malipo ya hoteli iitwayo After 40 Hotels Limited iliyopo Nairobi, Kenya yenye jina la Kubenea, Saed Ahmed kama mgeni kuanzia tarehe 3/9/2020 hadi 5/9/2020 na. Pasi yake ya kusafiria (Passport).

Mara baada ya kukamatwa, mtuhumiwa alieleza kuwa alifika mkoani Arusha tarehe 2/9/2020 akitokea Dar es Salaam na kufikia katika hoteli iliyopo Arusha mjini. Alieleza zaidi kuwa, tarehe 3/9/2020, alienda kulala kwa Kaka yake tarehe 3/9/2020, na tarehe 4/9/2020 alienda Namanga na kupokea fedha taslimu tajwa hapo juu kutoka kwa raia wa Kenya....
Hakuna kesi hapo,si amekamatwa Tanzania?
Huyu hajaenda kenya, kisheria. bado yuko Tanzania.
Hizo pesa alizonazo ni maandalizi ya safari yake ya kwenda Kenya.
Pesa za kenya na US kanunua Tanzania kwenye Bureau De Change ili atumie safarini.
Labda iwe hana Risiti, ndio kidoogo atakuwa matatani kwa kuwa na fedha za kigeni bila kuwa na Receipt..
Ajiandae kurudi Dar kuendelea na Kampeni pale Kinondoni.
Pia yawezekana kaja Arusha kwa jamaa yake kukopa pesa ili ajiwezeshe kwenye kampeni zake.
CCM BANA janja janja ili wapate mtelezo, mwka huu tuko na nyinyi bega kwa bega.
NI YEYE TUU- Lisu 2020
Magufuli OUT
 
Hivi kubenea nae alitusaliti?
Wapum.bavu mtaisoma namba mwaka huu, hakuna rangi hamtaiona, alitumwa kurekebisha pesa na mengineyo ya kampeni, jiiteni Chama Cha Wananchi tu kama Yanga ilivyohiita Timu ya Wananchi wakati ilipikuwa inategemea kutembeza bakuli kwa wananchi kujiendesha.

Mlipitishia kwa wale watetezi wenu wa haki za usho.ga wao wanaita haki za binadamu, accounts zikazuiwa na wakatangaza kusitisha shughuli zao nchini, huko nako mnakotegemea hakitapita kitu jipangeni, JPM anawaonesha ni jinsi gani yuko makini linapokuja swala la usalama wa Taifa, lakini pia kusimamia sheria, kanuni na taratibu.
 
Sirari boarder wananchi wa pande zote huwa wanaingia tu,sijui siku hizi.
basi hilo ni kosa, kila nchi ilinde mipaka yake. Baadae tunaanza kuona ugaidi unaingia nchini, halafu tunaanza kutafuta mchawi. wakati kuna maeneo tena yanajulikana watu wanapita na kupituka watakavyo
 
Pamoja na kuwa alijitoa CHADEMA na kujiunga ACT-Wazalendo, hii isiwe sababu ya sisi wa upande wa upinzani kufurahia yaliyomkuta kwani safari ya kuelekea Oktoba 28 bado inaendelea.

La msingi kuliko yote ni kuwa,tusimuhumu ili hali hatujasikia chochote kutoka Kwake na tusiwe kama ni wageni katika nchi hii.

Subirini kuona hiyo kesi itavyoendeshwaa na zaidi hatima ya kesi yenyewe.

Tujipe muda
 
Hapa ndipo ninapokuona wewe ni wakili kanjanja, inawezekana vipi umkamate raia wa Tanzania ndani ya Tanzania na halafu umshtaki kwa kuingia Tanzania isivyo rasmi? Are you mad?

Hivi huko CCM huwa mnavutishwa bangi gani ya kuwatowa akili?
Wakati mwingine mnajitoa ufahamu. Mtuhumiwa ameingia na kutoka nchini Kenya bila taarifa zake kuwapo mpakani. Ushahidi ni risiti ya Hotel aliyolala Nairobi, Memorandum of Understanding iliyosainiwa Nairobi na tiketi ya basi alilopanda toka Nairobi kwenda Namanga, unashangaa nini? maana yake Usafiri wake wa kwenda na kurudi ulikuwa ni wakuishia Namanga na kisha kuvuka kutumia njia za Panya, njia haramu.
 
Huyu Mganga alipaswa kumshughulikia kwanza Kangi Lugola kabla ya Kubenea au ndiyo double standards.
 
Wakati mwingine mnajitoa ufahamu. Mtuhumiwa ameingia na kutoka nchini Kenya bila taarifa zake kuwapo mpakani. Ushahidi ni risiti ya Hotel aliyolala Nairobi, Memorandum of Understanding iliyosainiwa Nairobi na tiketi ya basi alilopanda toka Nairobi kwenda Namanga, unashangaa nini? maana yake Usafiri wake wa kwenda na kurudi ulikuwa ni wakuishia Namanga na kisha kuvuka kutumia njia za Panya, njia haramu.

..itategemea wamemkamatia wapi.
 
Hizo lazima zitakuwa pesa za kampeni. Swali je; Nani huko Kenya anataka Kubenea awe mbunge na kwa manufaa gani? AU katumwa na nani?
Umeona mbali sana. Pia CCM na Kubenea ni kitu kimoja. Inawezekana Kubenea anahongwa kuwili kuwili. Sasa atanyea debe hadi January 2021 ndio atatoka.

Amemsaliti bwana wake CCM kwa bwana mwingine wa kiKenya.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
 
Buni Media angalia bodi ya wakurugenzi wa hiyo kampuni ambayo Kubenea alikamatwa na "mkataba wa makubaliano" nao! Mkurugenzi wake kila kukicha ni kuishambulia serikali yetu na viongozi wake!
Kwamba huyo Mkurugenz anaandika ya uongo?
 
Wacha aisome namba mpuuzi sana huyu jamaa

Ametumika vya kutosha kipindi Cha utawala wa Kikwete na Mkapa kuchafua watu na kueneza propaganda.
Alimchafua sana mgombea wetu wa URAIS kamanda Lowasa kabla akina Lissu na Mbowe hawajapiga lile dili.
 
Nina wasiwasi, amount ya pesa on him ni kidogo sana kuwarrant an arrest,
Kuingia na kutoka njia ya panya, kunataka red handed caughting, au ushahidi wa video footage
Ha ha ha umenikumbusha ushahidi wa Msigwa na Lema. Waliweka kwenye flashi kabisa kisha wakaukabidhi TAKUKURU.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom