Saed Kubenea atiwa mbaroni. Afikishwa Mahakamani kwa kuingia nchini kinyume na Sheria, utakatishaji fedha na kupelekwa rumande

Saed Kubenea atiwa mbaroni. Afikishwa Mahakamani kwa kuingia nchini kinyume na Sheria, utakatishaji fedha na kupelekwa rumande

Sasa hapa Tunduma mbona tunatakiwa kukamatwa karibia wakazi wote wa hapa?
Kuingia na kutoka nchi jirani kwetu kawaida mno na hatujui sheria inatuchukuliaje?
Sehemu zote za mpakani kubinjuka kawaida
Wenyeji wa pande zote mbili wanazijua chocho

Ova
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

YAH: KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA SAED AHMED KUBENEA

Mnamo tarehe 5/9/2020, Jeshi la Polisi Tanzania lilimkamata SAED AHMED KUBENEA akiwa katika gari la abiria lenye namba ya usajili T. 645 DKR akitokea kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya, eneo la Namanga akielekea Arusha mjini.

Mara baada ya upekuzi, mtuhumiwa huyo alikutwa, pamoja na vitu vingine, Dola za Marekani Elfu Nane (USD 8000), Shilingi za Kenya Laki Nne Tisini na Moja Elfu Mia Saba (KES 491,700), Shilingi za Kitanzania Elfu Sabini na Moja (TZS 71,000/-), tiketi ya basi la Super Couch lenye namba ya usajili KCP 4230 ya tarehe 05/09/2020 kutoka Nairobi, Kenya kwenda Namanga, ‘Memorandum of Understanding’ kati ya Hali-Halisi (Tanzania) na Buni Media Limited (Kenya), Risiti ya malipo ya hoteli iitwayo After 40 Hotels Limited iliyopo Nairobi, Kenya yenye jina la Kubenea, Saed Ahmed kama mgeni kuanzia tarehe 3/9/2020 hadi 5/9/2020 na. Pasi yake ya kusafiria (Passport).

Mara baada ya kukamatwa, mtuhumiwa alieleza kuwa alifika mkoani Arusha tarehe 2/9/2020 akitokea Dar es Salaam na kufikia katika hoteli iliyopo Arusha mjini. Alieleza zaidi kuwa, tarehe 3/9/2020, alienda kulala kwa Kaka yake tarehe 3/9/2020, na tarehe 4/9/2020 alienda Namanga na kupokea fedha taslimu tajwa hapo juu kutoka kwa raia wa Kenya.
Hata hivyo, mara baada ya kupitia Ushahidi uliokusanywa nimebaini kuwa:-

1. Mtuhumiwa SAED AHMED KUBENEA hakufikia katika hoteli aliyoitaja Arusha mjini, wala kulala kwa Kaka yake kama alivyoeleza.

2. Mtuhumiwa tajwa alivuka Mpaka usio rasmi na kuelekea Nairobi nchini Kenya na kisha kurejea nchini Tanzania bila kutumia Mpaka rasmi mnamo tarehe 5/9/2020.

3. Mtuhumiwa tajwa aliingiza nchini Fedha za Kigeni (foreign currency) bila kutoa tamko rasmi la kisheria kinyume na masharti ya Kanuni za the Anti-Money Laundering (Cross - Border Declaration of Currency and Bearer Negotiable Instruments) Regulations, 2016 zikisomwa pamoja na Kifungu cha 28B(1)(a) cha Sheria ya Kuzuia Utakasishaji wa Fedha Haramu, Na. 12 ya Mwaka 2006.

Hivyo, leo tarehe 7/9/2020, mara baada ya kujiridhisha na uwepo wa ushahidi wa kutosha dhidi ya mtuhumiwa tajwa, sambamba na misingi ya kikatiba inayoniongoza kama ilivyoanishwa katika Ibara ya 59B(4)(a) hadi (c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, nimeidhinisha mashtaka yafuatayo dhidi ya mtuhumiwa SAED AHMED KUBENEA:-

a. Kuingia nchini Tanzania kinyume na Sheria ya Uhamiaji, Sura ya 54 Marejeo ya mwaka 2016; na
b. Kuingiza nchini fedha za Kigeni bila kutoa tamko kinyume na Kanuni za Utoaji Tamko la Fedha Mpakani za mwaka 2016.

View attachment 1561443
View attachment 1561444

UPDATE: KESI YA KUBENEA YAAHIRISHWA HADI SEPTEMBA 21

Saed Kubenea amefikishwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha ambapo anakabiliwa na kwa makosa mbalimbali ikiwemo utakatishaji fedha na kuziingiza nchini bila kibali

Kubenea anatuhumiwa kukiuka Sheria za kuvuka mpaka kwenda Kenya na kurejea nchini kwa kutumia njia zisizo rasmi

Kutokana na kosa la kutakatisha fedha kutokuwa na dhamana, amepelekwa rumande hadi Septemba 21, 2020 kesi hiyo itakapotajwa

Wamemshika pabaya. Wakati wengine wakiendelea na kampeni, yeye atakuwa anapambana na kesi huku akiwa anasota rumande.
ACT iungane na vyama pinzani ili kumpigia kampeni mgombea mwingine maana huyu atapigwa tarehe za mwezi kwa mwezi hadi uchaguzi upite.
Wasipo kuwa makini hilo jimbo litachukuliwa na sisiem
 
We akili huna, hata kama wewe ni mtanzania kuna namna ya kuingia tanzania. Njia ya kuingia Tanzania ni kupotia mpaka rasmi. Sasa yeye kaingia kupitia isivyo halali, ni lazima akamatwe kwa kuwa hawajui kabeba nini
Muulize kwani yeye Kurudi kwake huwa anapitia Madirishani!?

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Like serious?! Yaani tiketi, MoU na risiti ndio ushahidi wa kuthibitisha aliingia na kutoka Kenya bila kufuata sheria?!

What kama Kubenea kilichomtoa Dar ni safari ya kikazi/kibiashara kati ya Hali-Halisi na Buni Media ya Kenya lakini kwavile Halisi ni kampuni akaamua kutaka kuwadanganya wabia wenzake wa Halisi kwamba alienda Nairobi na akalala hotel ili hatimae achikichie pesa ya nauli na ya hotel?!

Lakini badala ya kwenda hadi Nairobi, partners wa Kenya (Buni Media) wakamaliza kila kitu kwa upande wao, including MoU signing kisha wakampa mtu ambae alileta hiyo MoU including anything else hadi mpakani upande wa KE na ndipo Kubenea nae akaifuata akiwa upande wa TZ kisha akarudi na kupanda basi ambako ndimo walimkuta na kumkamata?!

Hivi yule mtu aliyekuwa mpakani upande wa KE, akifunga mizigo labda kwenye mfuko kisha akaurushia upande wa Tanzania na hatimae Kubenea kuchukua mzigo husika ina maana hapo itakuwa aliingia Kenya na hatimae kurudi TZ kwa njia isiyo halali?!
Kumbuka Kubenea ametoa maelezo Polisi. Hayo uyasemayo siyo maelezomaliyotoa Polisi. Don't make speculations
 
Hizo pesa si angetumiwa tu kwa account namba yake ya Benki ama hata ya MTU wake wa karibu, ni pesa ndogo sana
 
Kwanini unaamini risiti ni proof kuwa alikuwa Nairobi?
1. Risiti ya Hotel: Alikuwa ana mpango wa kwenda kulala Nairobi akamwomba mwenyeji wake amchukulie chumba cha kulala halafu atakuja kumrudishia fedha zake. Lakini kwa bahati mbaya hakwenda hivyo mwenyeji akamletea mpaka pale mpakani ili amrudishie fedha zake. Pia tiketi ya basi alikuja nayo mwenyeji wake mpaka Namanga. ambako walisaini hiyo MoA.
Akapanda basi kwa tiketi kwa jina la Saed Kubenea mpaka Namanga😂😂 Na apliyemletea MoU akavuka kwa njia za panya kukutana na Kubenea😂😂
 
Hajaonewa, tatizo ni mchoyo na mbinafsi.

Watu kama Kubenea hapendi hata kuona kuna kijana ana millioni mfukoni

Vitu kama hivyo unawatuma tu vijana wako kwenda kukuchukulia pesa sehemu.

Tuache uchoyo matokeo yake ndio haya.
Mkuu ungekuwa wewe ungemtuma kijana?hivi unawajua Watanzania linapokuja suala la uaminifu? mtume mtu hata laki mbili na ndio kwa heri. Nashindwa kwanini mtu kama Kubenea ameshindwa kufuata taratibu na akaingia kwenye mtego wa kitoto, kwani angefuata njia halali na kutaja /kujaza fomu kuhusu hizo pesa yasingemkuta hayo yote.
 
Hapa ndipo ninapokuona wewe ni wakili kanjanja, inawezekana vipi umkamate raia wa Tanzania ndani ya Tanzania na halafu umshtaki kwa kuingia Tanzania isivyo rasmi? Are you mad?

Hivi huko CCM huwa mnavutishwa bangi gani ya kuwatowa akili?
Sheria hujui nyamaza! Kuna utaratibu wa kutoka na kuingia nchini mwako!! Siyo unapitia njia za panya ni kosa la uhamiaji mkuu!
 
Kamuandika sana Lowasaa kuhusu ufisadi.

Akaja kumsafisha ndani ya usiku mmoja tu.

Kamuandika ssna Zitto kwamba ni msaliti, anatumika na usalama na CCM. Na ACT imeanzishwa na CCM kupambana na CDM.

Lakini hivi karibuni alihamia huko huko ACT kwa Zitto!
😂😂
 
Kushikwa kwa kubenea ni pigo kubwa kwa Lisu
Lissu anakusumbua akili sana ndugu yangu, nimekuja kugundua unampenda sana, ndio mana mda wote yuko kichwani kwako

Kwa siku jina la lissu unaandika zaidi ya mara 50, naamini hata bwana ako atakuwa anapata wivu sana sababu ni lazima keshaliona hili
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

YAH: KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA SAED AHMED KUBENEA

Mnamo tarehe 5/9/2020, Jeshi la Polisi Tanzania lilimkamata SAED AHMED KUBENEA akiwa katika gari la abiria lenye namba ya usajili T. 645 DKR akitokea kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya, eneo la Namanga akielekea Arusha mjini.

Mara baada ya upekuzi, mtuhumiwa huyo alikutwa, pamoja na vitu vingine, Dola za Marekani Elfu Nane (USD 8000), Shilingi za Kenya Laki Nne Tisini na Moja Elfu Mia Saba (KES 491,700), Shilingi za Kitanzania Elfu Sabini na Moja (TZS 71,000/-), tiketi ya basi la Super Couch lenye namba ya usajili KCP 4230 ya tarehe 05/09/2020 kutoka Nairobi, Kenya kwenda Namanga, ‘Memorandum of Understanding’ kati ya Hali-Halisi (Tanzania) na Buni Media Limited (Kenya), Risiti ya malipo ya hoteli iitwayo After 40 Hotels Limited iliyopo Nairobi, Kenya yenye jina la Kubenea, Saed Ahmed kama mgeni kuanzia tarehe 3/9/2020 hadi 5/9/2020 na. Pasi yake ya kusafiria (Passport).

Mara baada ya kukamatwa, mtuhumiwa alieleza kuwa alifika mkoani Arusha tarehe 2/9/2020 akitokea Dar es Salaam na kufikia katika hoteli iliyopo Arusha mjini. Alieleza zaidi kuwa, tarehe 3/9/2020, alienda kulala kwa Kaka yake tarehe 3/9/2020, na tarehe 4/9/2020 alienda Namanga na kupokea fedha taslimu tajwa hapo juu kutoka kwa raia wa Kenya.
Hata hivyo, mara baada ya kupitia Ushahidi uliokusanywa nimebaini kuwa:-

1. Mtuhumiwa SAED AHMED KUBENEA hakufikia katika hoteli aliyoitaja Arusha mjini, wala kulala kwa Kaka yake kama alivyoeleza.

2. Mtuhumiwa tajwa alivuka Mpaka usio rasmi na kuelekea Nairobi nchini Kenya na kisha kurejea nchini Tanzania bila kutumia Mpaka rasmi mnamo tarehe 5/9/2020.

3. Mtuhumiwa tajwa aliingiza nchini Fedha za Kigeni (foreign currency) bila kutoa tamko rasmi la kisheria kinyume na masharti ya Kanuni za the Anti-Money Laundering (Cross - Border Declaration of Currency and Bearer Negotiable Instruments) Regulations, 2016 zikisomwa pamoja na Kifungu cha 28B(1)(a) cha Sheria ya Kuzuia Utakasishaji wa Fedha Haramu, Na. 12 ya Mwaka 2006.

Hivyo, leo tarehe 7/9/2020, mara baada ya kujiridhisha na uwepo wa ushahidi wa kutosha dhidi ya mtuhumiwa tajwa, sambamba na misingi ya kikatiba inayoniongoza kama ilivyoanishwa katika Ibara ya 59B(4)(a) hadi (c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, nimeidhinisha mashtaka yafuatayo dhidi ya mtuhumiwa SAED AHMED KUBENEA:-

a. Kuingia nchini Tanzania kinyume na Sheria ya Uhamiaji, Sura ya 54 Marejeo ya mwaka 2016; na
b. Kuingiza nchini fedha za Kigeni bila kutoa tamko kinyume na Kanuni za Utoaji Tamko la Fedha Mpakani za mwaka 2016.

View attachment 1561443
View attachment 1561444

UPDATE: KESI YA KUBENEA YAAHIRISHWA HADI SEPTEMBA 21

Saed Kubenea amefikishwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha ambapo anakabiliwa na kwa makosa mbalimbali ikiwemo utakatishaji fedha na kuziingiza nchini bila kibali

Kubenea anatuhumiwa kukiuka Sheria za kuvuka mpaka kwenda Kenya na kurejea nchini kwa kutumia njia zisizo rasmi

Kutokana na kosa la kutakatisha fedha kutokuwa na dhamana, amepelekwa rumande hadi Septemba 21, 2020 kesi hiyo itakapotajwa
[/QUOT

Hili la mtanzania kukamatwa ndani ya tanzania na kushitakiwa kwa kosa la kuingia tanzania bado sijalielewa vizuri.
Kwa nchi nyingi huwa kuanzia $10,000 ndio inatakiwa kutoa taarifa.
Kwa mujibu wa sheria za TZ unatakiwa kutoa taarifa ukiwa na kiasi gani?
 
Aliyekuwa mbunge wa Ubungo kijana Said Kubenea yuko Mahabusu kwa kosa la kuingiza kiasi kikubwa fedha bila kutoa Maelezo yake.Pia anatakiwa kujibu tuhuma ya kwenda nje ya nchi Na kurudi bila kufuata taratibu za mipaka.
Je hizo ndio fedha za kuchochea vurugu au za nini?
Kwani azifate Kenya?
 
Idiot Gvnt since Tz became free from colonialist
Nimesoma baru hiyo inasema hivi
1599505562238.png

1599505579025.png


Kwa hiyo kama kavunja sheria hizo, basi tuiache sheria ichukua mkondo wake.

Hii ina maana kuwa tayari ACT imeshapoteza kiti cha Kionondoni
 
Back
Top Bottom