Safari katika barabara za Tanzania ni Changamoto

Grand Canyon

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2020
Posts
545
Reaction score
1,191
Kwa kweli matrafiki ni wengi sana barabarani. Hawatoi elimu kuhusu matumizi ya barabara, lugha yao ni kupiga faini tu.

Inachosha kwa kweli.

Nimewahi kufanya safari ya usiku sikuona traffic hata mmoja. Lakini nilifika salama.

Lakini mchana ni balaa. Mfano wanasimama na camera yao kwenye kibao cha 50. Wanataka ukifika kibao hicho uwe 50 net.

Mfano nikiwa spidi 130 nikaona kibao cha 50 kweli inawezekana kushusha spidi kutoka 130 hadi 50 ndani ya mita 30 baada ya kuona kibao?

Si bora wakae mita 50 kutoka kwenye kibao ili kutoa nafasi kwa dreva ya kushusha spidi bila kushika breki kwa nguvu?

Inachosha sana.
 
Matrafiki bora wapo Botswana kwanza kibao chao kinasoma 80km/h harafu mbele kama mita kadhaa ndio unakutana na hiki cha 60km/h yaani unaweza kupunguza hata ukiwa mwendokasi ila nao wanakaa maporini kama Bongo tu uzuri wake hawabadiliki miaka nenda rudi...
 
Wanazingua sana hawa matrafiki wa bongo.
 
Sipendelei kabisaa ku drive long distance usiku, yan iwe imenibid tu ila huwa sipendelei hii kitu.
Na enjoy zaid day time ride
 
Changamoto nyingine: Unaanza kuovertake sehemu sahihi. Kabla hujamaliza mstari myoofu unaanza. Je ughairi kuovertake na kurudi nyuma au umalizie? Ukimalizia unapigwa faini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…