Safari ya Lissu kuelekea Nairobi ilikuwa ni mateso na vilio, Spika Ndugai usitoneshe vidonda

Ahsante sana mkuu kwa kuliweka hili vizuri.
 
Salary Slip nilikuona siku hile,poleni sana kwa kadhia hii,na namuombea rais wangu wa tls na mtani wangu maisha marefu!
Na wale waliohusika na uovu huu iwe kwa kutenda,kuwaza au kunena ile albadiri ya kesho iwatendee sawa sawa na yale waliyomtendea Lissu!
 
U remind me back!!30 yrs ago!!In a good class of Moral Theology!!I little cry for yr theological Concepts!!
 
Duh! Haya mambo yanatokea Tanzania tu. Kwa kweli mchawi wetu alishakufa na mganga pia na mitishamba yao na uchawi, yaani tuna speed ya kujitoa ufahamu. Ccm adui mkubwa mno taifa hili.
 
Wewe Jisambaa la wapi unatia aibu hivyo?
 
Asante Barafu! Naweza kusema bila hofu kwamba kwa sasa Taifa linaendeshwa kishetani zaidi! Ni aibu kubwa kuwa na Viongozi aina ya Ndugai!
Ndugai alipewa amri hadharani ya kuwashughulikia wapinzani, haikuchukua muda wabunge waliochaguliwa na Wananchi kwa kura halali wakafukuzwa! Kibaya zaidi akapigiwa simu za pongezi kutoka kwa waliomtuma! Kichwa kikapanuka! Leo anatamba na kutetea kasoro ya serikali na Bunge kutomsaidia Lissu!
Esther Bulaya aliyeongoza maombi kwa Afya ya Spika hayupo Bungeni leo, kashughulikiwa na Spika aliyemuombea kwa Mungu! Naamini shetani anamkejeli Mungu wetu kwa kumponya kiumbe huyu!
Wenzetu huomba uongozi kulitumikia Taifa, lkn kuna wengine wapo kwenye uongozi kutumikia kikundi cha watu!
Ipo siku Taifa hili la Nyerere litapata Uhuru wake kamili! Siku zinahesabika!
Mwenyezi Mungu hajawahi kushindwa na viumbe dhaifu!
 
Mungu awabariki sana. Watu wake mliompigania Lisu kuokoa uhai wake dhidi ya mashetani yaliyokusudia kumuua.
 
Why all these hate comments?!!
 
Asante sana barafu, kwa post hii umelitendea haki hili jamvi letu pendwa la JF. Ni muda mrefu nimejiuliza ni wapi ilipoenda JF yetu ile ya miaka ilee hadi nikajikuta na mimi naingia kwenye mipasho ya ajabu ajabu na kuanza kukimbizana na vichaa nikisahau wanaotusoma watashindwa kuona tofauti. Hii post yako imenizindua, imeniamsha lakini zaidi ya yote imenipa faraja...hongera sana.

Ninachoomba ni kitu kimoja, turuhusu tuisambaze huu mchango wako uwafikie wengi wakati huu tunapomuombea Mh. Tundu Lissu apone haraka. Tunaomba Mungu amnusuru kutoka mikononi mwa watesi wake wanaotamba mitaani kama vile Tanzania imetekwa na kuwa ngome yake shetani. Turuhusu tuitafsiri na kuisambaza hii ripoti yako ili raia wema wajue kinachoendelea.

Mungu akubariki sana barafu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…