Safari yako ndefu kuendesha gari bila kupumzika ni ipi?

Safari yako ndefu kuendesha gari bila kupumzika ni ipi?

Ila kuna madereva wengine hawanaga uungwana kabisa, either kwakutokufahamu ama kwa makusudi mtu unamflash lakini yeye kangangania full afu mitaa kama ya treni, mi nikishaonaga hivi ni mguu kati tu nanyunyiza mpaka nitakapopita ndio nakiwasha tena.
Kuna viraka tyre ya kushoto ama lami imebomoka inshort huwa ni wakati mgimu sana
 
Mwaka juzi FEB, 2020 Nikiwa na RAV 4 Old model yangu nilikua natoka mwanza to singida, nilianza safari saa 8 usiku.

Nilipofika maeneo ya ZIBA - TABORA mida ya saa 11 alfajiri nikakutana na lori mbele yangu kama mita 50 ghafla likaibuka lori jingne kwa nyuma ya lile lori mbele yangu linaOvertake, hapo nipo 110 km/hr, nilishika breki nikavuta na Hand brake kwa nguvu zoteee, aseee Lile Lori lilininusa si zaid ya sentimeta 10 linigonge upande wangu.

Nilisimamisha gari nikashuka pale nikakojoa mkojo kama lita 5, mwili unatetemeka, jasho linanitoka wakati ni alfajiri kuna baridi.

Nikasimama pale kama dakika 20 nazungumza pekeangu kama kichaa, natoa matusi makali huku natoa maneno ya kumshukuru Mungu hapo hapo.

Tokea siku hiyo nikasema wallah sitothubutu tena kuendesha gari usiku.
Dah lita 5 [emoji28][emoji28]
 
Wakuu heshima kubwa sana kwenu. Nimekumbuka mengi sana tangu nimeanza kusafiri umbali mrefu kwa gari binafsi.

Safari zangu kila baada ya miezi 3 nafanya kati ya Dar na Mara kikazi na huwa nasafiri na gari yangu binafsi and nikiwa peke yangu. Napenda kuendesha usiku so hiwa naanza safari yangu dar es salaam saa kumi jioni.

Ninachofanya huwa natega pale maeneo ya veta kuna IT kibao nakula vichwa vyangu vy shinyanga ama mwanza ama musoma elf 50 naweka kibindoni laki 2. Huwa nafika musoma kesho yake mida ya saa saba mchana.

Ila huwa nina nusi saa ya kulala nikivuka singida maeneo ya shelui alfajiri. Bila kusahau energy 2 na kopo za lita na nusu za maji 2 za kumix energy nazinywa safari nzima polepole ili kukimbiza usingizi.

Dar-Iringa-Dar siku moja
 
Back
Top Bottom