Said Lugumi avunja ukimya kuhusu tuhuma za ufisadi zinazoikabili kampuni yake

Said Lugumi avunja ukimya kuhusu tuhuma za ufisadi zinazoikabili kampuni yake

Usikute aliyeleta mada hii ni msomi kweli kweli na mmoja wapo wa watu muhimu serikalini,lakini ona ujinga aliouandika. Hili taifa limekula hasara kama huyu bwana alisoma kwa fedha za walipa kodi, bora hata hizo fedha zingekutumika kununulia magari ya kubebea taka ngumu ktk jiji la Dar,zingesaidia sana.
 
Kwa hiyo mtoto Kabwe aliposemewa pale na Makonda halafu akatumbuliwa hadharani na huyo "Baba" hana haki ya kusikilizwa kama Lugumi? Au Kabwe ni mtoto wa Kambo na Lugumi ni mtoto wa ndoa?

Rais Magufuli anapenda sana sifa, anapenda sana media na kuonekana. Kama angekuwa na kifua angemtumbua Lugumi, lakini tumeambiwa "sio kila jipu la kutumbuliwa". Hizi double standards ndio zitamshusha Magufuli chini ni suala la muda. Mazuri yote anayofanya katika kukusanya kodi na kubana matumizi yatasahaulika
 
Umenena vyema sana .....baada ya principle of natural justice kufuatwa tusubr vyombo huska vituletee Majibu sahihi
Natural justice kwa Lugumi lakini kwa Wilson Kabwe hakuna! Double standard at its best. Kwa hiyo Magufuli anaangalia utashi wake kutumbua na sio kufuata standard operating procedure....

Bila katiba ya Warioba huyo Magufuli ataishia njiani tu, majipu anayo hadi Ikulu
 
Hi conflict of interest. Mwenye kampuni ni mkwe wa ex IGP. Hii peke yake inatakiwa kufuta hiyo contract na kumfugulia mashtaka IGP. Tatizo la pili ni kuchelewa kukamilisha hiyo kazi. Said ni mwizi na baba mkwe ni mwizi. Hawa watachngesha lakini mwisho watafika mahakamani tu. Huu sio utawala wa kuoneana aibu.
 
Kwa hiyo mtoto Kabwe aliposemewa pale na Makonda halafu akatumbuliwa hadharani na huyo "Baba" hana haki ya kusikilizwa kama Lugumi? Au Kabwe ni mtoto wa Kambo na Lugumi ni mtoto wa ndoa?

Rais Magufuli anapenda sana sifa, anapenda sana media na kuonekana. Kama angekuwa na kifua angemtumbua Lugumi, lakini tumeambiwa "sio kila jipu la kutumbuliwa". Hizi double standards ndio zitamshusha Magufuli chini ni suala la muda. Mazuri yote anayofanya katika kukusanya kodi na kubana matumizi yatasahaulika
Kwani lugumi ameajiriwa na magufuli. Kabwe ni muajiriwa wa serikali kwaiyo rais anaweza kumfukuza wakati wowote. Sasa lugumi atamfukuza kwenye kampuni yake? Kwani hiyo kampuni inamilikiwa na magufuli?
 
yawezekana waliofaidika hasa ni IGP wakati huo, waziri wakati huo na wakuu Wa vitengo. watafutwe wahojiwe
 
Kwani lugumi ameajiriwa na magufuli. Kabwe ni muajiriwa wa serikali kwaiyo rais anaweza kumfukuza wakati wowote. Sasa lugumi atamfukuza kwenye kampuni yake? Kwani hiyo kampuni inamilikiwa na magufuli?
Hivi kumbe bangi zako zinakueleza majizi yanafukuzwa kazi!!! Mbulumundu at its best.

Raisi angeamuru Lugumi akamatwe haraka na kufikishwa mahakamani ambako mahakama kama ikimkuta na hatia anafungwa. Lakini wanufaika wa Lugumi Charles Kitwanga na yule jamaa wa NIDA ni watumishi wa serikali ambao Magufuli anaweza kuwatumbua bila ganzi
 
1461301223121.jpg
1461301237004.jpg
 
Alitakiwa aweke vifaa katika vituo 180-> ,akalipwa cash money.
Sasa huyu ndugu yeye ameweka vifaa katika vituo 14 tu.na fedha ameweka kwa pocket yake!.anaonewaje?
 
hapa watu tunaambiwa tuzibe midomo yetu na tujenge nchi huku wala nchi ni wengine kabisaa hata buumu hawalijui I mean wameishia std 7 ila tu ujanja ujanja wao unawaweka mjini.then huku kijijin mnatwambia tumuulize mtendaji mapato na matumiz ya serilali yetu ya kijiji. Ebu sasa wao waonyeshe mfano waanze na mapato na matumizi ya hizo bil 37 jinsi zilivyotumika ambapo zingeweza kununua 740 john Deere tractor tena new model mpyaa kabisa ambazo zingesaidia kuinua sekta ya Kilimo nchini
HATUDANGANYIKI LISEMWALO LIPO !
 
Hatimae kampuni ya LUGUMI imejitokeza na kuelezea taarifa mbalimbali zinazoenea kwenye mitandao ya kijamii na kuita taarifa hizo ni za uzushi.
Yani kampuni INA profile hovyo kabisa ndo imepewa tender ya almost 40 billion tsh? Kha Tanzania noma sana.

Sehemu ya taarifa hii inasema nanukuu;

“Hivi karibuni kumekuwa na habari zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kwa namna ambayo inapotosha ukweli kuhusu kampuni yetu iliyotekeleza mradi huu muhimu kwa nchi yetu na, mradi wa AFIS. Aidha taarifa hizo katika mitandao na magazeti mbalimbali imekuwa ikitoa habari zisizo na ukweli wowote kuhusu mtendaji mkuu Bwana Said H. Lugumi.

Ukweli ni kwamba mnamo mwaka 2011 Jeshi la Polisi liliingia mkataba na kampuni ya Lugumi Enterprises Limited wa kufunga mitambo ya utambuzi kwa kutumia alama za vidole (AFIS) katika vituo vya Polisi kwa mujibu wa matakwa ya Jeshi. Vituo vilikuwa nchi nzima Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.”


Pia kuna sehemu ya taarifa hii inazidi kuchanganua nanukuu;

“Kwa mantiki hiyo basi, mambo yaliyo mengi yalitajwa katika vyombo vya habari si ya kweli na ni upotoshaji mkubwa na ni muhimu kuyapuuza, na kuendelea na shughuli za kawaida za ujenzi wa taifa. Ni katika muktadha huo huo tunapenda kuujulisha umma kwamba tuhuma nyingi za uzushi zimetungwa kumwelekea Mtendaji Mkuu Bwana Said H. Lugumi ikiwemo kuzushiwa kutoroka na kukamatwa nje ya nchi na kadhalika. Taarifa hizo ni uzushi mtupu, ni za kupuuza, Mkurugenzi wetu nchini na anaendelea na shughuli zake za kawaida”.

Soma zaidi kupitia viambatanisho hivi.

View attachment 340959

View attachment 340961
 
Tuliwaambia wanalindana, tayari wameshapata ''ulinzi''

Hawaelezi tenda waliipata lini, kwanini wamelipwa 100% kazi ikiwa bado n.k.

Hawa CCM na Watumbua majipu ni wale wale, wanalindana ndio maana mafisadi wanatamba. Hii serikali haiwezi kuwa tofauti na zingine

Wanalindana! kesho anatumbuliwa Anne K Watanzania wanashangilia

Wameshawalinda tayari, kama ilivyo kwa kashafa nyingine
Tukiwatumbua Mbowe anasusa bunge na kudai katiba haifuatwi! Wacha kumsema Lugumi, tunatekeleza katiba sasa, amepewa muda wa kujieleza na uchunguzi unaendelea.
 
Hatimae kampuni ya LUGUMI imejitokeza na kuelezea taarifa mbalimbali zinazoenea kwenye mitandao ya kijamii na kuita taarifa hizo ni za uzushi.

Sehemu ya taarifa hii inasema nanukuu;

“Hivi karibuni kumekuwa na habari zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kwa namna ambayo inapotosha ukweli kuhusu kampuni yetu iliyotekeleza mradi huu muhimu kwa nchi yetu na, mradi wa AFIS. Aidha taarifa hizo katika mitandao na magazeti mbalimbali imekuwa ikitoa habari zisizo na ukweli wowote kuhusu mtendaji mkuu Bwana Said H. Lugumi.

Ukweli ni kwamba mnamo mwaka 2011 Jeshi la Polisi liliingia mkataba na kampuni ya Lugumi Enterprises Limited wa kufunga mitambo ya utambuzi kwa kutumia alama za vidole (AFIS) katika vituo vya Polisi kwa mujibu wa matakwa ya Jeshi. Vituo vilikuwa nchi nzima Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.”


Pia kuna sehemu ya taarifa hii inazidi kuchanganua nanukuu;

“Kwa mantiki hiyo basi, mambo yaliyo mengi yalitajwa katika vyombo vya habari si ya kweli na ni upotoshaji mkubwa na ni muhimu kuyapuuza, na kuendelea na shughuli za kawaida za ujenzi wa taifa. Ni katika muktadha huo huo tunapenda kuujulisha umma kwamba tuhuma nyingi za uzushi zimetungwa kumwelekea Mtendaji Mkuu Bwana Said H. Lugumi ikiwemo kuzushiwa kutoroka na kukamatwa nje ya nchi na kadhalika. Taarifa hizo ni uzushi mtupu, ni za kupuuza, Mkurugenzi wetu nchini na anaendelea na shughuli zake za kawaida”.

Soma zaidi kupitia viambatanisho hivi.

View attachment 340959

View attachment 340961[/QUO
h
Hatimae kampuni ya LUGUMI imejitokeza na kuelezea taarifa mbalimbali zinazoenea kwenye mitandao ya kijamii na kuita taarifa hizo ni za uzushi.

Sehemu ya taarifa hii inasema nanukuu;

“Hivi karibuni kumekuwa na habari zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kwa namna ambayo inapotosha ukweli kuhusu kampuni yetu iliyotekeleza mradi huu muhimu kwa nchi yetu na, mradi wa AFIS. Aidha taarifa hizo katika mitandao na magazeti mbalimbali imekuwa ikitoa habari zisizo na ukweli wowote kuhusu mtendaji mkuu Bwana Said H. Lugumi.

Ukweli ni kwamba mnamo mwaka 2011 Jeshi la Polisi liliingia mkataba na kampuni ya Lugumi Enterprises Limited wa kufunga mitambo ya utambuzi kwa kutumia alama za vidole (AFIS) katika vituo vya Polisi kwa mujibu wa matakwa ya Jeshi. Vituo vilikuwa nchi nzima Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.”


Pia kuna sehemu ya taarifa hii inazidi kuchanganua nanukuu;

“Kwa mantiki hiyo basi, mambo yaliyo mengi yalitajwa katika vyombo vya habari si ya kweli na ni upotoshaji mkubwa na ni muhimu kuyapuuza, na kuendelea na shughuli za kawaida za ujenzi wa taifa. Ni katika muktadha huo huo tunapenda kuujulisha umma kwamba tuhuma nyingi za uzushi zimetungwa kumwelekea Mtendaji Mkuu Bwana Said H. Lugumi ikiwemo kuzushiwa kutoroka na kukamatwa nje ya nchi na kadhalika. Taarifa hizo ni uzushi mtupu, ni za kupuuza, Mkurugenzi wetu nchini na anaendelea na shughuli zake za kawaida”.

Soma zaidi kupitia viambatanisho hivi.

View attachment 340959

View attachment 340961
hahahahahahaha Kweli bongo hatari, umbea kila kona jambo hata halina ukweli watu wanapayuka na kulivalia njuga. Duuuuuh haya sasa wambea wote kazi kwenu.
 
Hatimae kampuni ya LUGUMI imejitokeza na kuelezea taarifa mbalimbali zinazoenea kwenye mitandao ya kijamii na kuita taarifa hizo ni za uzushi.

Sehemu ya taarifa hii inasema nanukuu;

“Hivi karibuni kumekuwa na habari zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kwa namna ambayo inapotosha ukweli kuhusu kampuni yetu iliyotekeleza mradi huu muhimu kwa nchi yetu na, mradi wa AFIS. Aidha taarifa hizo katika mitandao na magazeti mbalimbali imekuwa ikitoa habari zisizo na ukweli wowote kuhusu mtendaji mkuu Bwana Said H. Lugumi.

Ukweli ni kwamba mnamo mwaka 2011 Jeshi la Polisi liliingia mkataba na kampuni ya Lugumi Enterprises Limited wa kufunga mitambo ya utambuzi kwa kutumia alama za vidole (AFIS) katika vituo vya Polisi kwa mujibu wa matakwa ya Jeshi. Vituo vilikuwa nchi nzima Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.”


Pia kuna sehemu ya taarifa hii inazidi kuchanganua nanukuu;

“Kwa mantiki hiyo basi, mambo yaliyo mengi yalitajwa katika vyombo vya habari si ya kweli na ni upotoshaji mkubwa na ni muhimu kuyapuuza, na kuendelea na shughuli za kawaida za ujenzi wa taifa. Ni katika muktadha huo huo tunapenda kuujulisha umma kwamba tuhuma nyingi za uzushi zimetungwa kumwelekea Mtendaji Mkuu Bwana Said H. Lugumi ikiwemo kuzushiwa kutoroka na kukamatwa nje ya nchi na kadhalika. Taarifa hizo ni uzushi mtupu, ni za kupuuza, Mkurugenzi wetu nchini na anaendelea na shughuli zake za kawaida”.

Soma zaidi kupitia viambatanisho hivi.

View attachment 340959

View attachment 340961
hahahahahahaha wabongo kweli noma, kila jambo tunalivalia njuga kuliongelea hadi basi wakati halina ukweli wowote.Kweli wabongo kwa Uzushi tumepitiliza.Ifike pahala tuache uzushi lol.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Ndugu waandishi wa habari , nimewaita hapa leo ili niweze kutoa ufafanuzi wa mambo kadhaa kwa niaba ya Kampuni yetu ya LUGUMI ENTERPRISES LTD, kwa siku kadhaa kumekuwa na habari mbali mbali za kuchafua na kudhalilisha Kampuni yetu pamoja na Mimi Said Lugumi ambaye ni Mkurugenzi Mkuu.

Nitafafanua mambo yafuatayo kama majibu ya kadhia ambayo sisi na Washirika wenzetu katika shughuli zetu za kibiashara tumekutana nayo ,

Kampuni ya LUGUMI ENTERPRISES LTD ilipewa zabuni ya kufunga na kusambaza mitambo ya kuhakiki alama za vidole mnamo mwaka 2011 na kazi tuliifanya kwa kushirikiana na Washirika wenzetu wa kibiashara nje ya Nchi Kampuni za BIOMETRICA LLC (USA) na BIOLINK (RUSSIA) , tumefanikiwa kufunga na kusambaza mfumo wa alama za vidole (AUTOMATED FINGER PRINTS IDENTIFICATION SYSTEM – AFIS ) katika maeneo yote ya Nchi yetu na kwa uadilifu kama ambavyo mkataba ulivyohitaji.

Pamoja na kashfa nyingi dhidi ya Kampuni yetu na hususan Mimi binafsi , ukweli ni kwamba hakuna ufisadi wala wizi uliofanyika katika biashara hii muhimu na ya siri , kazi au biashara zinazohusu mambo ya ndani ya usalama wa Nchi zina mashariti yake na itifaki yake , ndio sababu taarifa hii inakusudia kuwatoa wasiwasi ndugu zetu , marafiki zetu na washirika wenzetu na sio kusema hadharani mienendo ya shughuli na zabuni za kazi za namna hii.

Ni uhakika kwamba Rais wetu Mh Dr John Pombe Magufuli , amedhiirisha pasipo hofu uwezo wake wa kupambana na ufisadi , wizi , utovu wa nidhamu katika utawala wake , hivyo basi kazi hii niliyoifanya na Jeshi la Polisi inaniweka Mimi na Kampuni yangu kwenye wakati rahisi wa kukamatwa na kuhojiwa juu ya tuhuma za kuibia taasisi iliyopewa mamlaka ya kupambana na uhalifu Nchini , sifikiri wala sidhani kama uhalifu wangu unasubiri Kamati ya Bunge kuthibitishwa , ni rahisi sana kwa Jeshi la Polisi kujua je vifaa hivi viko kwenye vituo vya Polisi au haviko ? na kama haviko kwanini Kampuni yangu ililipwa ? na kama nimelipwa kwa kazi ambayo sikuifanya , wale wote walio husika na mchakato wote wa kuhakiki kuwa kazi imefanyika na kuidhinisha malipo kwa kazi hiyo , wanasitahili kuwa wapi ?

Ninaona hii ni vita ya kibiashara dhidi yha Kampuni yangu , ndio sababu wengine wanahoji vitu vyepesi visivyo na ufahamu , kuwa imekuwaje mimi kupata kazi kubwa kama hii ? Ndoto yangu katika biashara zangu , hii kazi kwangu bado ni ndogo , nimefika hapa kwa kupitia maisha magumu sana , kuna wakati niliishi bila kula na bila kuwa na kazi , lakini siku zote nimekuwa nikiwaza kufanikiwa katika maisha na hapa nilipofika nimefika kwa sababu ya BIDII , MAARIFA , UTHUBUTU NA UJASIRI na safari yangu ya maisha inakwenda mbele zaidi ya hapa.

Mengi yametajwa kuhusu mahusiano yangu na Mh Riziwan Kikwete na wengine kudai kuwa ni mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya Lugumi . Ukweli ni kwamba hana hata hisa moja katika biashara zangu ila Riziwan ni rafiki yangu , wengine wanasema kuwa yeye ndio amefanikisha shughuli zangu hizi zote , ukweli ni kwamba sio kweli kama inavyosemwa kwenye mitandao ya kijamii na magazeti mbali mbali , lakini hata kama angekuwa amesaidia kwa namna moja au nyingine kufika hapa nilipo fika kibiashara , je ningekuwa nimevunja utaratibu na sheria za Nchi ?

Kwa bahati mbaya katika Nchi yetu shughuli za biashara kubwa zinaonekana kuwa ni za Watu na makundi maalumu na sio za Watanzania kama LUGUMI , ndio sababu hoja zote kwenye mitandao ya Jamii na magazeti zinahoji ninawezaje kufanikiwa katika kiwango hiki wakati Mimi ni Mtoto wa masikini ? Jibu ni rahisi , NACHUKIA UMASIKINI .

Waziri wa Mambo ya Ndani Mh Charles Kitwanga anajua ukweli wa jambo hili , kwani Kampuni yake ya INFOSYS ndiyo ilipewa dhamana kiufundi ya kuunganisha mitambo yote tuliyoisamabaza katika vituo vyote vya Polisi kama tulivyoelekezwa kwenye mkataba na Jeshi la Polisi , Je sio rahisi sana kwa Waziri kulisidia Bunge ili kupunguza gharama za utafiti na kuchafuana kwa kiwango hiki kunako endelea ?

Katika Vyombo vya habari mbali mbali imeripotiwa kuwa vituo vilivyofungwa mfumo havizidi kumi na tano , jambo ambalo , Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) anaweza kuwa na majibu mazuri kuliko Mimi , nawashauri mkamuulize , ila ripoti kutoka ofisini kwetu ambayo imesainiwa na Maafisa mbali mbali waandamizi wa Jeshi la Polisi , inathibitisha kuwa kazi hii imeshafanyika kwa asilimia zaidi ya 99%.

Mwisho , kasi ya Rais wetu katika utumishi wake ni nzuri ila wako Watu wanataka kuitumia vibaya ili kudhalilisha wengine na hatimaye kuwapora haki zao . Tunamuomba Mh Rais awe makini sana katika falsafa yake ya utumbuaji majipu , kwani wengine wanatafuta namna ya kulipa visasi.


Asanteni sana kwa kunisikiliza

Said Lugumi (MD)

LUGUMI ENTERPRISES LTD
 
Ungekaa kimya mkuu usubiri wabunge wakupandie chati,maana hawaonekani kwnyeTV hapa lazima waonekane....
 
Back
Top Bottom