Saido mmoja ni sawa na foward nzima ya Yanga

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001


Uwezo wa Saido hauhitaji uchambuzi mwiiiiiiiingi. Sitaki kujiba kazi ya kuchambua, kama unataka uchambuzi chambua mwenyewe. Mimi nakuwekea sinema tu. Kwa wewe ambaye hukumuona jana basi jionee, maana unaweza kupotoshwa na haters.

Ukiangalia kwa jicho lisilo na husda utakubaliana na mimi kuwa Saido mmoja ni sawa na foward yote ya Yanga.

Ni jambo la afya kuona wachezaji wa Yanga wamekataa kuwa wanafiki, wamesema "Shikamoo Saido". Kuanzia Mayele, Farid, Aucho, Boxer, Sure Boy
 
Umesahau enzi hizo alipokuwa Yanga ulikuwa unasemaje?
 
Huu usajili nakumbuka wa kwanza kuubeza ulikuwa ni wewe. Kumbukumbu ninazo, ila nilikukatalia nikakwambia Saido ni mzuri ataisaidia sana Simba. Unakumbuka?
 
Saidooo kama Mbapeee[emoji91][emoji91]
 
Nipo na na kocha naby fundi la mpira nilipomuonesha post hii amecheeka Sana

Ila ameniacha na methali hii nimetafsiriwa Kutoka kiarabu

GANDA LA MUWA LA JANA CHUNGU KAONA KIVUNO
Mpe methali hii huyu Nabi wako
MLA NI MLA LEO MLA JANA KALANI? Kisha mkumbushe kuwa Morisson alitupiwa virago Simba. Mtakie heri ya mwaka mpya.
 
Wakati huyo ni zao letu ! Sana sana mtushukuru..tena nyamazeni tutamrudisha si mnajua bado ana mapenzi na timu yake?
 
Wakati huyo ni zao letu ! Sana sana mtushukuru..tena nyamazeni tutamrudisha si mnajua bado ana mapenzi na timu yake?
Alisha sema kuwa familia yake na ndugu zake wengi ni washabiki wa kubwa wa simba na walitamani siku moja wamuone akicheza simba... hivyo ndoto yake na ndugu zake imetimia tena kwa kishindo kikuu...
 
Wakati huyo ni zao letu ! Sana sana mtushukuru..tena nyamazeni tutamrudisha si mnajua bado ana mapenzi na timu yake?
Zao lenu kivipi wakati alitoka ulaya akiwa kwenye moto wake hata aliposajiliwa hapo utopoloni kwa fedha kiduchu alafanya makubwa kwa roho zenu mbaya na mtu wa watu hapendi mambo ya majini na kuogeshana maji ya maiti akamua akimbie
Mkadhalilisha sana etu ni mtovu wa nidhan kumbe alikataa kuoga maji ya maiti
 
Ukweli Saido alichoshindwana na gongowazi ni kukataa kulambishwa yai viza katika mambo yao ya kishirikina.
 
Umbumbumbu wa nini wakati amekubali kwamba ni kweli alikuwa hamkubali na sasa amebadili mtizamo wake
Na hii ndiyo sifa mojawapo sasa ya kuitwa mbumbumbu. Leo Matola, anafaa! Kesho Matola hafai! Leo Kepten John Bocco hafai! Kesho anafaa! Leo Saidoo hafai! Keshi anafaa!!

Hizo ndizo sifa kuu za mashabiki mbumbumbu. Ukigeugeu.
 
Na hii ndiyo sifa mojawapo sasa ya kuitwa mbumbumbu. Leo Matola, anafaa! Kesho Matola hafai! Leo Kepten John Bocco hafai! Kesho anafaa! Leo Saidoo hafai! Keshi anafaa!!

Hizi ndizo sifa kuu sasa za mashabiki mbumbumbu. Ukigeugeu.
Mchezaj akiwa yanga hafai Ila huyo huyo akienda Simba ni bonge ya mchezaj ikitokea kwa Morrison na sasa saido katika vitu wanavyoongoza watanzania ni unafki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…