Sakata la ESCROW: IPTL na PAP Watinga Mahakama Kuu kuomba ufafanuzi wa Kisheria wa Maazimio ya Bunge

Sakata la ESCROW: IPTL na PAP Watinga Mahakama Kuu kuomba ufafanuzi wa Kisheria wa Maazimio ya Bunge

Lizaboni

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2013
Posts
33,895
Reaction score
20,392
Wadau, katika kile kinachoonekana kuwa huenda Bunge likaingia tena kwenye mgogoro na Mahakama juu ya sakata la ESCROW, Leo Mwanasheria wa IPTL na PAP, Joseph Makandege amesema kuwa wamepeleka shauri Mahakama Kuu kuomba ufafanuzi wa Kisheria juu ya Maazimio yaliyotolewa na Bunge juu ya sakata la ESCROW. Mtakumbuka kuwa IPTL na PAP walitoa taarifa ya kupinga maazimio hayo na kuyaita ni ya kipuuzi.

Inaonekana IPTL na PAP wametafskari vya kutosha na wameona kuwa kuna haja ya Mahakama Kuu kutoa ufafanuzi juu ya maazimio hayo hasa kutokana na kuonekana kuwa yanaingilia mihimili mingine ya dola na yanajichanganya.

Source: TBC1
 
Mahakama ndiyo sehemu pekee ya kupata haki safi sana PAP kutafuta haki yenu.
 
Ukweli utazidi kubainika vizuri ndipo hapo tutajua kuwa PAC ni mbugila wa hali ya juu.
 
CCM kuendelea kubaki madarakani maana yake watanzania waendelee kuhesabu maumivu!
Pole sana umefika hapo ulipo kwa ajili ya ccm leo umeota vindevu kila sehemu ya mwili unatukana hovyo bila hata kukitambua.
 
Watanzania bado tupo nyuma kwenye Capitalism. Hasara tuliyoipata kwa kushtakiwa na DOWANS ni matokeo ya wanasiasa wanaojiona ni wataalamu kwa sababu tu walishaenda semina.
Tutajifunza tu, taratibu.
 
Kweli sikio la kufa; tulitegemea hasira za wananchi Uchaguzi Serikali za Mitaa zingewaamsha mfanye maamuzi bila kulea huu upuuzi, kumbe sikio ndo lilishajiozea!!
 
Mahakama ndiyo sehemu pekee ya kupata haki safi sana PAP kutafuta haki yenu.

NA IFIKE IJUMAA
1. Na ifike ijumaa, twaisubiri kwa hamu,
hatutaki kuzubaa siku ya mashamushamu,
kusuka ama kunyoa kwao wezi wa kalamu,
na ifike ijumaa tuone hatima yao

2. mmoja kakata kamba makimbia machinjoni,
imekuwa ni kasumba, wakikosa kimbilio,
wengine wayumba yumba kama siku ya gulio,
Na ifike ijumaa tuone hatima yao

3. Ijumaa siyo mbali twangojea uamuzi
naona moshi kwa mbali wafuka bila ajizi,
walishaonja asali, mizinga hawawezi achia,
Na ifike ijumaa, tuone hatima yao.

4. Shoka limo shinani,
kukata lipo tayari,
limeanza mitaani,
kutanguliza habar,
laendelea mwakani,
na ifike ijumaa tuone hatima yao

5. majizi yote pembeni twaja mbio tupisheni,
utani weka pembeni, ofisi za umma pisheni
fedha zetu rudisheni, vifungo ni haki yenu,
na ifike ijumaatuone hatima yenu.

6. Naifike ijumaa mshiko watuletee,
kula kuku kwa mrija hakuna asiyependa,
naifike ijumaa akaunti zao zikwanguliwe,
hata zile za uswizi ukweli nazo zirudi!
 
Ukweli utazidi kubainika vizuri ndipo hapo tutajua kuwa PAC ni mbugila wa hali ya juu.

Wewe jinga tofautisha kazi ya PAC na CAG

CAG anabainisha mapungufu hapendekezi kuwajibika kwa yyt yule maana si kazi ya,
PAC wanarejea findings za CAG na wanapendekeza kuwajika/ kuwajibishwa kwa watendaji/ viongozi wazembe au waliotumia vibaya ofisi zao
 
Kama maazimio ya bunge ni ya kipuuzi onyesheni makeke yenu basi, haya makeke si mlianza tokea ripoti ya PAC inataka kuingia bungeni? ikawaje? mukatawanya repot bandia na kila aina ya mchezo lakini hatimae Zitto akaibuka mshindi sasa mwisho wenu ni kesho Ijumaa jioni mkuu wa Kaya anakuja na yake ya moyoni.
 
Kalasinga amecharuka.. Kafulila muda si mrefu atakuwa mjela jela original
 
mahakama corrupt, bunge corrupt IPTL corrupt... tunategemea nini??

Hizi sindimba dawa yake ni kutwangana bakora za m@t@k0ni
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom