Sakata La Kanisa Lililolipotiwa Kupiga Muziki Saa 24 Na Kujengwa Kuziba Barabara Serikali Yachukua Hatua Lapigwa Stop Mchungaji Akaidi ( 3 ) .

King Kisali

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2019
Posts
1,041
Reaction score
1,349
Sakata la kanisa lililoripotiwa kupiga muziki mkubwa sana masaa 24 na lililojengwa katikati ya barabara , limeingia sura mpya baada ya serikali kuchukua hatua na kulizuia kuendelea kujengwa na kuendelea na shughuli zozote za ibada , baada ya maofisa wa serikali kufika kanisani hapo Jana na kubandika zuio hili , ambapo baadhi ya waumini wa kanisa hilo walikuwepo . Baada ya maofisa wa serikali kuondoka mchungaji aseme hawambabaishi , akabandua zuia hilo na kusema hawawezi kumfanya kitu na jumapili ataendelea na ibada kama kawaida hawawezi kumfanya kitu chochote yeye ni mwamba serikali haimuwezi kwa lolote .
 
Nilikwambia amehonga huyo na sasa wamemgeuka haamini macho yake.

Mungu ana utaratibu. Mungu hafanyagi mambo yake kimkiki mkiki
 
Chizimaarifa njoo mchungaji uchwara mwenzio kaishaangukia pua .
 
Atakuwa na udugu na nabii Tito
 
Andika vema ili kama mtu ni mgeni wa hili tukio aweze kujua na kuelewa unalokusudia kutihabarisha
 
Uchongezi = barua ya serkali + maneno ya mtoa mada - barua ya mchungaji/voice note/video/pic
 
Tulisema humu kuwa huyu mchungaji uchwara ,Hana kibali , kujenga kuziba barabara ,anapiga muziki mkubwa sana , watu wakatubeza , wanapinga licha ya vielelezo vyote , sasa hayo yametimia , wachangiaji muwe mnachangia kwa fact na sio mihemiko ya kilokole uchwara , walokole uchwara jifunzeni kufuata sheria za nchi .
 
Andika vema ili kama mtu ni mgeni wa hili tukio aweze kujua na kuelewa unalokusudia kutihabarisha
Ok hii ni nyuzi ya tatu ikihusu Kanisa la Bethel Kariakoo Tabora , ambapo Lililipotiwa kujengwa kuziba barabara , kupiga muziki mkubwa sana , kujenga bika kibali nyuzi ya kwanza ilikuwa "Kanisa Lajengwa Katikati Ya Barabara Lapiga Muziki Masaa 24 ":, 2 "Sakata La kanisa lililojengwa katikati ya barabara na kupiga muziki mkubwa sana masaa 24 lajengwa usiku kucha kuwahi kulimaliza " na huu Uzi ndio mwendelezo wa tatu .
 
Tumwache watoto washindwe kusoma shule mbili , Westland primary school na Itetemia shule ya Msingi washindwe kusoma kwa sababu ya upumbafu wa mchungaji uchwara kupiga muziki mkubwa sana kama vichaa , wazee wetu na wagonjwa wateseke kwa sababu yake ?
 
Uchongezi = barua ya serkali + maneno ya mtoa mada - barua ya mchungaji/voice note/video/pic
Ukisema ukweli unakuwa mchochezi ? Documents sio uchochezi ni supporting documents .
 
Shukrani kwa kujali na kuheshimu mawazo ya wadau
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…