Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 51,303
- 40,190
Wewe Ritz hujui chochote kabisa bora ukae kimya. Its does not need you to be magician to clear any cargo, its simply the matter of principals and procedures.
HSC ni wezi wakubwa katika nchi hii. Tena majambazi, taratibu za clearing ukimaliza unampa mteja documents zote za mzigo wake( file zima) waulize hao wafanya biashara kama wana documents hasa zinazoonyesha TRA ushuru ulikuwaje. Na kama wangekuwa nazo wangedai in reference to those old documents.
Sasa kwa taarifa tuu hii ishu imeanzia IMF wakiilalamikia TZ hawakusanyi kodi na wakatoa moja ya reference.
Endeleeni kumwonea mmnyonge tuu ila ipo siku ukweli utadhiirika zaidi ya hapo.
Wewe kazi yako kubwa ni kutetea kitu chochote chenye element ya "uislam" hata kama ni upuuzi ukidhani ndio unausaidia huo "uislam" kumbe unawapeleka wenzio motoni kwa shetani. Wasaidie kwa kusema kweli ili wabadilike.
Ndugu yangu mambo ya Uislam yanatoka wapi tena au wewe ndiyo una chuki na hao Waislam.
Naomba nikuulize wewe umepakia mzigo wako CBM 2 unataka upewe documents za TRA? Mimi nijua kukuzidi wewe ambaye unaongozwa na chuki.
Kwa hiyo unataka kutuambia maclearing wanatoa mizigo isipokuwa HSC tu.
Wewe ndiyo hujui chochote wafanyabiashara wenyewe wanashirikiana na mawakala kuiibia serikali wataomba documents za nini.
Mfanyabiashara anafunga kontena yake ya kitenge kwenye paking list kaandika miamvuli hapa utamlaumu clearing. Halafu acha uongo na habari zako za vijiweni kuhusu IMF.