Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Wakuu,
Baada ya tukio la jaribio la kumteka mfanyabiashara Deogratius Tarimo, maarufu kama Deo Bonge, lililotokea eneo la Kiluvya hivi karibuni, picha za watuhumiwa zilisambaa na kuibua mjadala mtandaoni. Mmoja wa watuhumiwa alidaiwa kuwa msaidizi wa Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, hali iliyosababisha taharuki.
Kutokana na madai hayo, Spika Tulia aliibuka kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter) na kutoa ufafanuzi akisema, "Huyo pichani si Michael msaidizi wangu, wamemfananisha. Naamini wote waliohusika watapatikana na kuchukuliwa hatua stahiki."
Sakata hili limezidi kuzua mijadala huku wengi wakitaka uchunguzi wa kina kufanyika ili kuhakikisha haki inatendeka na wahusika wanawajibishwa kwa mujibu wa sheria.
Haya wafukunyuzi wa mambo tuleteeni picha tuone kama sio yeye
Soma, Pia:
Baada ya tukio la jaribio la kumteka mfanyabiashara Deogratius Tarimo, maarufu kama Deo Bonge, lililotokea eneo la Kiluvya hivi karibuni, picha za watuhumiwa zilisambaa na kuibua mjadala mtandaoni. Mmoja wa watuhumiwa alidaiwa kuwa msaidizi wa Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, hali iliyosababisha taharuki.
Haya wafukunyuzi wa mambo tuleteeni picha tuone kama sio yeye
Soma, Pia:
- Dar: Inasemekana tukio hili la utekaji limetokea Kiluvya, kutokana na uzito wa jamaa walishindwa kumchukua. Hakuna aliyetoka kumsaidia
- Baada ya kushindwa kumteka Deo Bonge mchana, watekaji walirudi kumtafuta tena usiku
- Aliyerekodi tukio jaribio la kumteka Deogratius Tarimo (Deo Bonge) apewe maua yake