FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #21
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
UKURASA WA NANE
“Unayo nafasi ya kuweza kuyachukua maisha yangu kama ulivyo tishia hapo kwa sababu wewe ni raisi wa nchi ila unapaswa kujiuliza mswali haya, nikifa wananchi wataanza kuniulizia nipo wapi? Watauliza nani kaniua na kwa sababu zipi? Sasa hapo itatafutwa familia yangu na kuulizwa kwa mara ya mwisho nilikutana na nani, unajua watajibu nini? Watasema kwamba nilikutana na mheshimiwa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, mwisho wako utaanzia hapo kwani wataamini wewe ndiye umeniua kwa sababu unahisi kwamba nitakupokonya hiyo nafasi yako. Vipi upo tayari wananchi wajue huo ukatili wako? Unahisi watakuja kukuamini tena na kukufanya uwaongoze? Jibu ni hapana mheshimiwa” mr Apson Limo aliongea kisha akatulia kuacha hayo maneno yakae vyema kwenye kichwa cha raisi huyo kisha akaendelea.
“Kuna swali moja ambalo mimi najiuliza sana, kwanini unaniogopa sana na kuhisi kwamba mimi ni hatari kwako wakati wewe ndiye mwenye madaraka makubwa mheshimiwa? Mimi ni kiongozi wa kawaida tu huenda watu wameniamini kutokana na yale ambayo wameona nayafanya kwa muda mrefu sana. Najua unaweza ukahitaji kuniangusha ila zingatia tu usije ukafanya makosa kwenye hizo harakati zako maana kama wananchi wakijua unaweza ukajikuta kwenye nafasi mbaya sana na hata kama utapita unaweza kupinduliwa. Swali pekee la msingi ambalo unatakiwa kujiuliza ukiwa mwenyewe ni kwamba umewafanyia nini wananchi mpaka wakurudishe tena kwenye hicho kiti ulichopo? Kama hakuna cha maana ulicho kifanya basi nadhani huu ni wakati sahihi kabisa wa wewe kuandaa sababu za msingi pale ambapo wananchi hao watakuwa wanakuuliza maswali kama hayo hadharani, kama utashindwa kuyajibu maana yake utakuwa umejiondoa mwenyewe kwenye hiyo nafasi uliyopo. Nikutakie usiku mwema mheshimiwa raisi wa jamhuri ya muungano” Tajiri huyo hakumkopesha raisi wake, alimwambia ukweli wa mambo ulivyo na yale ambayo huenda yangetokea kisha baada ya hapo akatoka humo ndani kwa kuamini kwamba kiongozi wake hakuwa na cha kumfanya kwa sababu kama angemuua basi watu walikuwa wanaenda kujua moja kwa moja kwamba mhusika ni yeye kwa sababu familia yake ilijua kabisa yeye kaitwa Ikulu hivyo raisi alijikuta anabaki tu ndani akiwa mwenye hasira nyingi sana.
Aliipasua kwa kuibamiza meza ambayo ilikuwa ipo pembeni kidogo mwa sehemu ambayo ilikuwepo meza yake kubwa ya mninga ambayo ilitengenezwa kwa ubora wa hali ya juu sana. Mheshimiwa aliambiwa ukweli mtupu kwamba alipaswa kujitafakari sana na kujiuliza kwamba ni kitu gani ambacho alikuwa amewafanyia wananchi mpaka wampe tena nafasi? Hakuwa na jambo la maana sana alilokuwa amelifanya zaidi ya propaganda za mdomoni tu. Hakukuwa na ajira za kueleweka, huduma za kijamii zilikuwa duni sana hususani maeneo ya vijijini, mfumuko wa bei kila sehemu ulikuwa mkubwa sana, uchumi wa nchi ulikuwa kwenye hali isiyo ya kuridhisha, sasa angesimama vipi mbele ya wananchi kuongelea hizo habari?
“Kiongozi kuna jambo ambalo ninapaswa kulifanya?” alikuwa ni mlinzi wake ambaye sauti ya mpasuko wa meza ilimshtua na kumfanya awahi haraka sana kuingia humo ndani ambapo alimkuta mheshimiwa akiwa anapasua pasua vioo huku mkono wake ukiwa unavuja damu basi alimshika na kumtuliza huku akiwa anamuuliza ili kuona kama kuna kitu anaweza kukifanya kwa ajili ya bosi wake.
“Hahahaa hahahaha hahaha yule mjinga kahisi kwamba labda mimi ni mtoto mwenzake sio, anahisi kwamba mimi naweza kutishiwa kirahisi sana namna hiyo? Nitamfanyia kitu kibaya sana mpuuzi yule, nahitaji kukutana na mkuu wa majeshi muda huu” aliongea kwa jaziba sana akiwa anaelekea kwenye kochi kuchukua koti lake lakini mlinzi wake ilimbidi amtulize na kumpelekea bafuni kwanza kumtuliza bosi wake ambaye alikuwa anahema kwa harisa kali mno. Walirudi sebuleni maana mlinzi huyo alimwambia mheshimiwa kwamba kulikuwa na kitu cha kukiongelea hapo.
“Mheshimiwa kuna tatizo”
“Lipi?”
“Inadaiwa kwamba kapteni wa jeshi amekutwa akiwa anaandaa mipango ambayo inadaiwa kwamba alikuwa amepanga kuja kupindua nchi”
“Whaaaaaaaat?” mheshimiwa raisi aliuliza kwa mshangao mkali isivyokuwa kawaida
“Ndiyo mkuu, hilo jambo mkuu wa majeshi alilishtukia mapema sana hivyo amemkamata haraka sana baada ya kupata habari hizo na muda wote alikuwa anakupigia simu lakini simu yako haikuwa ikipokelewa hivyo akaamua kunipigia mimi hapa ili kama unahitaji kuongea na huyo kapteni uongee naye au kama unataka wamuadhibu kwa sheria za jeshi ni wewe tu anasubiri amri yako”
“Safi sana, nilikuwa nawatafuta watu wa namna hii kweli kweli kwenye maisha yangu, nafikiri huyu anaenda kuwa wa mfano kwa kuanza naye nitawashangaza sana wanajeshi kama kuna mwingine alikuwa na huo mpango basi atajutia sana kufikiria hilo jambo” mheshimiwa alitulia kwa muda maana hizo habari ni kama zilikuja wakati mwafaka, wakati ambao alikuwa na hasira sana hivyo akafurahi kuona kuna sehemu ya yeye kutulizia hasira hizo. Ni kama kuna jambo lilimshtua ghafla akamgeukia mlinzi wake
“Inawezekana vipi kapteni kutaka kufanya jambo kama hilo na mkuu wa majeshi asijue?”
“Inawezekana mkuu, unajua mkuu wa majeshi yupo pale juu kupokea taarifa kutoka chini na kuzifanyia maamuzi au kuzipelekea sehemu zingine ambako zitahitajika lakini yeye anakuwa hajui kabisa kinachokuwa kinaendelea huko chini. Sasa kapteni yeye anazipokea moja kwa moja kutoka kwa watu wake wa chini kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba yeye anakuwa na taarifa nyingi zaidi ya mkuu wa majeshi na yeye ndiye ambaye anachagua taarifa zipi za kumpa mkubwa wake, kwa maana hiyo yeye ndiye anajua mambo mengi zaidi hivyo mpaka kufikia hapo ina maanisha kwamba alikuwa amefikia hatua kubwa sana ya mafanikio ya hicho alichokuwa anakifanya”
“Andaa msafara tunaelekea makao makuu ya jeshi wakati huu na mwambie mkuu wa majeshi aandae kabisa sehemu ambayo itatosha watu wa kutosha kuwepo na mtu huyo aandaliwe haraka sana” alitoa amri hiyo akiwa anatoka humo ndani, lilitokea jambo la haraka na yeye alihitaji kulishughulikia haraka sana maana mtu kutishia kumuondoa raisi madarakani lilikuwa ni kosa la uhaini mkubwa sana ambalo adhabu yake ni kifo tu pekee na alitaka kulifanikisha kwa mkono wake mwenyewe iwe ni kama onyo kwa watu wengine ambao walikuwa wana mawazo kama ya huyo kapteni ambaye alitoka kupewa taarifa zake muda mfupi ambao ulikuwa umepita.
Daniel Mpanzi, ndilo lilikuwa jina lake mheshimiwa CDF. Vazi lake likiwa na nyota za kutosha alikuwa ameongozana na makamanda wake wakiwa eneo maalumu kabisa la kupokelea wageni kwenye makao makuu ya jeshi la nchi. Walikuwa hapo kwa ajili ya kumpokea mheshimiwa raisi ambaye alitoa taarifa muda mfupi uliokuwa umepita kwamba sio muda sana angeweza kuingia hapo kukutana na huyo mtu wake ambaye alidaiwa kwamba alitishia kuipindua nchi.
Ndani ya dakika chache msafara huo kutoka Ikulu ulikuwa unaingia ndani ya hilo eneo, alishuka mheshimiwa na walinzi wake huku akipokelewa kwa heshima sana na vijana wake hao ambao wengi kwenye hiyo nafasi aliwaweka yeye mwenyewe.
“Karibu sana mheshimiwa” CDF aliongea huku akiwa anampa mkono bosi wake.
“Asante sana, nahitaji moja kwa moja unipeleke kwa huyo mtu na waambie vijana wako waandae ulingo wa mapambano ambao utawafanya wanajeshi wengi sana kushuhudia pambano hilo ndani ya muda mchache ambao unafuata”
“Sawa mheshimiwa” hakukuwa na maelezo zaidi ya kumpeleka ndani ya chumba ambacho kilikuwa chini sana ya ardhi ambako ndiko alikokuwa amefungwa kapteni huyo ambaye alidaiwa kwamba alikuwa anahitaji kumpindua raisi huyo madarakani.
“Kwenye maisha yangu yote tangu niingie Ikulu kuna watu ambao nimewahi kuwaza kwamba wanaweza kuwa hatari kwa upande wa nafasi yangu japo hawaruhusiwi hata kuwaza kuhusu hilo jambo ila angalau wao wapo kwenye nafasi nzuri zaidi ya kufanya hilo. Kuna makamu wangu, kuna waziri mkuu, kuna spika wa bunge pamoja na jaji mkuu wa nchi, lakini hapo hapo wanaongezeka watu wawili ambao ni mkurugenzi wa usalama wa taifa bila kumsahau mkuu wa majeshi”
“Hao ndio watu ambao wana nguvu ukinitoa mimi kwa sababu wanaweza kwenda popote na kukutana na yeyote yule hivyo kwa kiasi fulani naweza kusema kwamba kama kusalitiwa basi hawa ndio walitakiwa kuwa watu wa kwanza kabisa kuweza kufanya hivyo lakini kitu cha ajabu kabisa mbwa kama wewe ndo unaanza kuwaza huu ujinga bila kuwaza madhara yake na kama mfugaji wako akikukataa nani atakulisha? Uliwahi kuwaza kwa umakini kabisa hili jambo na halmashauri ya kichwa chako ikafikia uamuzi wa mwisho kabisa wa kuwaza kunisaliti raisi wako ambaye ndiye nasaini hadi mshahara wako?” mheshimiwa alimpa maelezo na kumuuliza swali mwanaume huyo ambaye alikuwa ameketi chini akiegamia nondo ambazo zilikuwa kama kuta za chumba hicho.
Mwanaume huyo alikuwa amechakaa damu kuonyesha kwamba wakati mfupi uliokuwa umepita aliyapitia mateso makubwa sana ambayo yalimfanya achakae kwa damu. Vidole vyake vya mguuni havikuwa na kucha, zilikuwa zinaonekana chini kuonyesha kwamba mtu huyo aling’olewa kucha hizo kwa lazima. Damu ilikuwa bado mbichi sana kwenye vidole vyake, uso wake ambao ulikuwa na hofu kupita kiasi lakini wenye jeuri ndani yake ulikuwa unamwangalia raisi kwa dharau ya aina yake.
“Wewe ni kiongozi dhaifu sana, upo hapo kwa muda tu hata ukiamua kubaki hapo kuna watu ipo siku watakutoa tu” aliongea kwa jeuri mwanaume huyo akiwa ameketi hapo chini, mheshimiwa alitabasamu, mtu huyo alionekana kuwa jeuri sana isivyokuwa kawaida na alikuwa akiwahitaji sana watu wa namna hiyo kwani angewatumia kuweza kutuliza hasira zake ambazo zilikuwa zinamsumbua kwenye kichwa chake.
“Kuna mtu ana kisu kikali hapo?” mheshimiwa aliuliza, lilikuwa ni jambo la haraka sana, alikabidhiwa CDF ambaye moja kwa moja alimpatia raisi mkononi. Mheshimiwa alivua koti lake akiwa na kisu hicho kwenye mkono wake kisha akamsogelea mwanaume huyo ambaye alikuwa ameketi pale chini, aliwapa ishara makamanda ambao walikuwa na mkuu wa majeshi wakamnyanyua mwanaume huyo na kumketisha kwenye kiti kisha wakamfunga kwenye kiti hicho cha chuma vizuri sana kiasi kwamba akawa hana hata uwezo wa kujisogeza sehemu nyingine.
“Kweli upo sahihi kabisa mimi ni raisi dhaifu sana ila ni mimi huyu ambaye nimekufanya wewe uishi vizuri na nakulipa vizuri kwa nafasi ambayo nilikupa mjinga mkubwa wewe wakati nilikuwa nina uwezo wa kumpa hiyo nafasi mtu mwingine na mambo yakafanyika vizuri tu bila uwepo wako. Leo unanikosea heshima kiongozi wako wa nchi huku unamchukulia kawaida hata mkubwa wako wa kazi CDF hapo kwa kuamini kwamba mimi ni dhaifu hivyo hata yeye ni dhaifu kwa sababu aliteuliwa na mimi. Nimesikitishwa sana na hili jambo nilihisi huenda ungeutumia muda huu kuweza kuniomba msamaha ili nione kama naweza kukusamehe lakini ndo kwanza unaleta dharau na jeuri bado mbele yangu mimi, basi sina namna zaidi ya kukufanya ulipe kwa hiyo kauli yako ambayo umeitamka, niamini mimi hiyo kauli unaenda kuijutia sana kwa dakika hizi chache ambazo zinafuatia” mheshimiwa aliongea akiwa mwingi wa tabasamu kwenye uso wake lakini tabasamu hilo halikuashiria hali ya furaha bali hasira na uchungu kwa mtu mwenye cheo cha chini sana kwake kama hicho ambacho yeye ndiye aliye mfanikishia kukipata kumuita yeye dhaifu, alitakiwa kulipa kwa ajili ya hiyo kauli yake ya kijinga ambayo aliweza kuitamka wakati huo.
Mimi sina la ziada ukurasa wa 8 unafika mwisho.
Febiani Babuya.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
UKURASA WA NANE
“Unayo nafasi ya kuweza kuyachukua maisha yangu kama ulivyo tishia hapo kwa sababu wewe ni raisi wa nchi ila unapaswa kujiuliza mswali haya, nikifa wananchi wataanza kuniulizia nipo wapi? Watauliza nani kaniua na kwa sababu zipi? Sasa hapo itatafutwa familia yangu na kuulizwa kwa mara ya mwisho nilikutana na nani, unajua watajibu nini? Watasema kwamba nilikutana na mheshimiwa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, mwisho wako utaanzia hapo kwani wataamini wewe ndiye umeniua kwa sababu unahisi kwamba nitakupokonya hiyo nafasi yako. Vipi upo tayari wananchi wajue huo ukatili wako? Unahisi watakuja kukuamini tena na kukufanya uwaongoze? Jibu ni hapana mheshimiwa” mr Apson Limo aliongea kisha akatulia kuacha hayo maneno yakae vyema kwenye kichwa cha raisi huyo kisha akaendelea.
“Kuna swali moja ambalo mimi najiuliza sana, kwanini unaniogopa sana na kuhisi kwamba mimi ni hatari kwako wakati wewe ndiye mwenye madaraka makubwa mheshimiwa? Mimi ni kiongozi wa kawaida tu huenda watu wameniamini kutokana na yale ambayo wameona nayafanya kwa muda mrefu sana. Najua unaweza ukahitaji kuniangusha ila zingatia tu usije ukafanya makosa kwenye hizo harakati zako maana kama wananchi wakijua unaweza ukajikuta kwenye nafasi mbaya sana na hata kama utapita unaweza kupinduliwa. Swali pekee la msingi ambalo unatakiwa kujiuliza ukiwa mwenyewe ni kwamba umewafanyia nini wananchi mpaka wakurudishe tena kwenye hicho kiti ulichopo? Kama hakuna cha maana ulicho kifanya basi nadhani huu ni wakati sahihi kabisa wa wewe kuandaa sababu za msingi pale ambapo wananchi hao watakuwa wanakuuliza maswali kama hayo hadharani, kama utashindwa kuyajibu maana yake utakuwa umejiondoa mwenyewe kwenye hiyo nafasi uliyopo. Nikutakie usiku mwema mheshimiwa raisi wa jamhuri ya muungano” Tajiri huyo hakumkopesha raisi wake, alimwambia ukweli wa mambo ulivyo na yale ambayo huenda yangetokea kisha baada ya hapo akatoka humo ndani kwa kuamini kwamba kiongozi wake hakuwa na cha kumfanya kwa sababu kama angemuua basi watu walikuwa wanaenda kujua moja kwa moja kwamba mhusika ni yeye kwa sababu familia yake ilijua kabisa yeye kaitwa Ikulu hivyo raisi alijikuta anabaki tu ndani akiwa mwenye hasira nyingi sana.
Aliipasua kwa kuibamiza meza ambayo ilikuwa ipo pembeni kidogo mwa sehemu ambayo ilikuwepo meza yake kubwa ya mninga ambayo ilitengenezwa kwa ubora wa hali ya juu sana. Mheshimiwa aliambiwa ukweli mtupu kwamba alipaswa kujitafakari sana na kujiuliza kwamba ni kitu gani ambacho alikuwa amewafanyia wananchi mpaka wampe tena nafasi? Hakuwa na jambo la maana sana alilokuwa amelifanya zaidi ya propaganda za mdomoni tu. Hakukuwa na ajira za kueleweka, huduma za kijamii zilikuwa duni sana hususani maeneo ya vijijini, mfumuko wa bei kila sehemu ulikuwa mkubwa sana, uchumi wa nchi ulikuwa kwenye hali isiyo ya kuridhisha, sasa angesimama vipi mbele ya wananchi kuongelea hizo habari?
“Kiongozi kuna jambo ambalo ninapaswa kulifanya?” alikuwa ni mlinzi wake ambaye sauti ya mpasuko wa meza ilimshtua na kumfanya awahi haraka sana kuingia humo ndani ambapo alimkuta mheshimiwa akiwa anapasua pasua vioo huku mkono wake ukiwa unavuja damu basi alimshika na kumtuliza huku akiwa anamuuliza ili kuona kama kuna kitu anaweza kukifanya kwa ajili ya bosi wake.
“Hahahaa hahahaha hahaha yule mjinga kahisi kwamba labda mimi ni mtoto mwenzake sio, anahisi kwamba mimi naweza kutishiwa kirahisi sana namna hiyo? Nitamfanyia kitu kibaya sana mpuuzi yule, nahitaji kukutana na mkuu wa majeshi muda huu” aliongea kwa jaziba sana akiwa anaelekea kwenye kochi kuchukua koti lake lakini mlinzi wake ilimbidi amtulize na kumpelekea bafuni kwanza kumtuliza bosi wake ambaye alikuwa anahema kwa harisa kali mno. Walirudi sebuleni maana mlinzi huyo alimwambia mheshimiwa kwamba kulikuwa na kitu cha kukiongelea hapo.
“Mheshimiwa kuna tatizo”
“Lipi?”
“Inadaiwa kwamba kapteni wa jeshi amekutwa akiwa anaandaa mipango ambayo inadaiwa kwamba alikuwa amepanga kuja kupindua nchi”
“Whaaaaaaaat?” mheshimiwa raisi aliuliza kwa mshangao mkali isivyokuwa kawaida
“Ndiyo mkuu, hilo jambo mkuu wa majeshi alilishtukia mapema sana hivyo amemkamata haraka sana baada ya kupata habari hizo na muda wote alikuwa anakupigia simu lakini simu yako haikuwa ikipokelewa hivyo akaamua kunipigia mimi hapa ili kama unahitaji kuongea na huyo kapteni uongee naye au kama unataka wamuadhibu kwa sheria za jeshi ni wewe tu anasubiri amri yako”
“Safi sana, nilikuwa nawatafuta watu wa namna hii kweli kweli kwenye maisha yangu, nafikiri huyu anaenda kuwa wa mfano kwa kuanza naye nitawashangaza sana wanajeshi kama kuna mwingine alikuwa na huo mpango basi atajutia sana kufikiria hilo jambo” mheshimiwa alitulia kwa muda maana hizo habari ni kama zilikuja wakati mwafaka, wakati ambao alikuwa na hasira sana hivyo akafurahi kuona kuna sehemu ya yeye kutulizia hasira hizo. Ni kama kuna jambo lilimshtua ghafla akamgeukia mlinzi wake
“Inawezekana vipi kapteni kutaka kufanya jambo kama hilo na mkuu wa majeshi asijue?”
“Inawezekana mkuu, unajua mkuu wa majeshi yupo pale juu kupokea taarifa kutoka chini na kuzifanyia maamuzi au kuzipelekea sehemu zingine ambako zitahitajika lakini yeye anakuwa hajui kabisa kinachokuwa kinaendelea huko chini. Sasa kapteni yeye anazipokea moja kwa moja kutoka kwa watu wake wa chini kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba yeye anakuwa na taarifa nyingi zaidi ya mkuu wa majeshi na yeye ndiye ambaye anachagua taarifa zipi za kumpa mkubwa wake, kwa maana hiyo yeye ndiye anajua mambo mengi zaidi hivyo mpaka kufikia hapo ina maanisha kwamba alikuwa amefikia hatua kubwa sana ya mafanikio ya hicho alichokuwa anakifanya”
“Andaa msafara tunaelekea makao makuu ya jeshi wakati huu na mwambie mkuu wa majeshi aandae kabisa sehemu ambayo itatosha watu wa kutosha kuwepo na mtu huyo aandaliwe haraka sana” alitoa amri hiyo akiwa anatoka humo ndani, lilitokea jambo la haraka na yeye alihitaji kulishughulikia haraka sana maana mtu kutishia kumuondoa raisi madarakani lilikuwa ni kosa la uhaini mkubwa sana ambalo adhabu yake ni kifo tu pekee na alitaka kulifanikisha kwa mkono wake mwenyewe iwe ni kama onyo kwa watu wengine ambao walikuwa wana mawazo kama ya huyo kapteni ambaye alitoka kupewa taarifa zake muda mfupi ambao ulikuwa umepita.
Daniel Mpanzi, ndilo lilikuwa jina lake mheshimiwa CDF. Vazi lake likiwa na nyota za kutosha alikuwa ameongozana na makamanda wake wakiwa eneo maalumu kabisa la kupokelea wageni kwenye makao makuu ya jeshi la nchi. Walikuwa hapo kwa ajili ya kumpokea mheshimiwa raisi ambaye alitoa taarifa muda mfupi uliokuwa umepita kwamba sio muda sana angeweza kuingia hapo kukutana na huyo mtu wake ambaye alidaiwa kwamba alitishia kuipindua nchi.
Ndani ya dakika chache msafara huo kutoka Ikulu ulikuwa unaingia ndani ya hilo eneo, alishuka mheshimiwa na walinzi wake huku akipokelewa kwa heshima sana na vijana wake hao ambao wengi kwenye hiyo nafasi aliwaweka yeye mwenyewe.
“Karibu sana mheshimiwa” CDF aliongea huku akiwa anampa mkono bosi wake.
“Asante sana, nahitaji moja kwa moja unipeleke kwa huyo mtu na waambie vijana wako waandae ulingo wa mapambano ambao utawafanya wanajeshi wengi sana kushuhudia pambano hilo ndani ya muda mchache ambao unafuata”
“Sawa mheshimiwa” hakukuwa na maelezo zaidi ya kumpeleka ndani ya chumba ambacho kilikuwa chini sana ya ardhi ambako ndiko alikokuwa amefungwa kapteni huyo ambaye alidaiwa kwamba alikuwa anahitaji kumpindua raisi huyo madarakani.
“Kwenye maisha yangu yote tangu niingie Ikulu kuna watu ambao nimewahi kuwaza kwamba wanaweza kuwa hatari kwa upande wa nafasi yangu japo hawaruhusiwi hata kuwaza kuhusu hilo jambo ila angalau wao wapo kwenye nafasi nzuri zaidi ya kufanya hilo. Kuna makamu wangu, kuna waziri mkuu, kuna spika wa bunge pamoja na jaji mkuu wa nchi, lakini hapo hapo wanaongezeka watu wawili ambao ni mkurugenzi wa usalama wa taifa bila kumsahau mkuu wa majeshi”
“Hao ndio watu ambao wana nguvu ukinitoa mimi kwa sababu wanaweza kwenda popote na kukutana na yeyote yule hivyo kwa kiasi fulani naweza kusema kwamba kama kusalitiwa basi hawa ndio walitakiwa kuwa watu wa kwanza kabisa kuweza kufanya hivyo lakini kitu cha ajabu kabisa mbwa kama wewe ndo unaanza kuwaza huu ujinga bila kuwaza madhara yake na kama mfugaji wako akikukataa nani atakulisha? Uliwahi kuwaza kwa umakini kabisa hili jambo na halmashauri ya kichwa chako ikafikia uamuzi wa mwisho kabisa wa kuwaza kunisaliti raisi wako ambaye ndiye nasaini hadi mshahara wako?” mheshimiwa alimpa maelezo na kumuuliza swali mwanaume huyo ambaye alikuwa ameketi chini akiegamia nondo ambazo zilikuwa kama kuta za chumba hicho.
Mwanaume huyo alikuwa amechakaa damu kuonyesha kwamba wakati mfupi uliokuwa umepita aliyapitia mateso makubwa sana ambayo yalimfanya achakae kwa damu. Vidole vyake vya mguuni havikuwa na kucha, zilikuwa zinaonekana chini kuonyesha kwamba mtu huyo aling’olewa kucha hizo kwa lazima. Damu ilikuwa bado mbichi sana kwenye vidole vyake, uso wake ambao ulikuwa na hofu kupita kiasi lakini wenye jeuri ndani yake ulikuwa unamwangalia raisi kwa dharau ya aina yake.
“Wewe ni kiongozi dhaifu sana, upo hapo kwa muda tu hata ukiamua kubaki hapo kuna watu ipo siku watakutoa tu” aliongea kwa jeuri mwanaume huyo akiwa ameketi hapo chini, mheshimiwa alitabasamu, mtu huyo alionekana kuwa jeuri sana isivyokuwa kawaida na alikuwa akiwahitaji sana watu wa namna hiyo kwani angewatumia kuweza kutuliza hasira zake ambazo zilikuwa zinamsumbua kwenye kichwa chake.
“Kuna mtu ana kisu kikali hapo?” mheshimiwa aliuliza, lilikuwa ni jambo la haraka sana, alikabidhiwa CDF ambaye moja kwa moja alimpatia raisi mkononi. Mheshimiwa alivua koti lake akiwa na kisu hicho kwenye mkono wake kisha akamsogelea mwanaume huyo ambaye alikuwa ameketi pale chini, aliwapa ishara makamanda ambao walikuwa na mkuu wa majeshi wakamnyanyua mwanaume huyo na kumketisha kwenye kiti kisha wakamfunga kwenye kiti hicho cha chuma vizuri sana kiasi kwamba akawa hana hata uwezo wa kujisogeza sehemu nyingine.
“Kweli upo sahihi kabisa mimi ni raisi dhaifu sana ila ni mimi huyu ambaye nimekufanya wewe uishi vizuri na nakulipa vizuri kwa nafasi ambayo nilikupa mjinga mkubwa wewe wakati nilikuwa nina uwezo wa kumpa hiyo nafasi mtu mwingine na mambo yakafanyika vizuri tu bila uwepo wako. Leo unanikosea heshima kiongozi wako wa nchi huku unamchukulia kawaida hata mkubwa wako wa kazi CDF hapo kwa kuamini kwamba mimi ni dhaifu hivyo hata yeye ni dhaifu kwa sababu aliteuliwa na mimi. Nimesikitishwa sana na hili jambo nilihisi huenda ungeutumia muda huu kuweza kuniomba msamaha ili nione kama naweza kukusamehe lakini ndo kwanza unaleta dharau na jeuri bado mbele yangu mimi, basi sina namna zaidi ya kukufanya ulipe kwa hiyo kauli yako ambayo umeitamka, niamini mimi hiyo kauli unaenda kuijutia sana kwa dakika hizi chache ambazo zinafuatia” mheshimiwa aliongea akiwa mwingi wa tabasamu kwenye uso wake lakini tabasamu hilo halikuashiria hali ya furaha bali hasira na uchungu kwa mtu mwenye cheo cha chini sana kwake kama hicho ambacho yeye ndiye aliye mfanikishia kukipata kumuita yeye dhaifu, alitakiwa kulipa kwa ajili ya hiyo kauli yake ya kijinga ambayo aliweza kuitamka wakati huo.
Mimi sina la ziada ukurasa wa 8 unafika mwisho.
Febiani Babuya.
Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app