Sakata la Warere Beach hotel kwa mtalii mgeni, Serikali ichunguze, wahusika wachukuliwe hatua, wametia doa sekta ya utalii nchini

Kipindi hiki tunataka zindua royal tour!!?
Hichi kipindi cha uzinduzi wa Royal tour ndio kipindi sahihi zaidi kwa huyo mnaigeria kulisemea, maana dunia itasikia na kulivalia njuga na huenda serikali ya Tz ikaamua kutoka usingizini ili kuchukua hatua dhidi ya wahusika.

Watanzania wote kwa pamoja tumuunge mkono huyo mnaigeria kulipigia kelele hili suala, uzalendo sio kufunika uovu. Wacha ukweli utuume lakini mwisho wa siku sote tupone.
 
Sijawahi kuwaamini wanaigeria, ni watu hatari sana linapokuja suala la pesa au kutafuta huruma kupata umaarufu.
Kama huwaamini wanaigeria basi njoo umuamini mmiliki wa Weru weru Lodge wa kule Machame ambaye alilalamika na kutoa video clip zikimhusu mkuu wa wilaya ya Hai (Ole Sabaya) aliyetinga hotelini kwake akilazimisha akalale na Nandy.
 
Hiyo Warere Beach hoteli ni ile ya Itigi?
 
Sio kudhadadia Mtanzania mwenzetu,tunataka hawa watu waliosababisha haya wachukuliwe hatua mara moja ili mambo haya yasitokee tena.
Huyo traveller kaona yeye atumie approach hii,tatizo huwa tunadharau sana watu ndo shida..laiti wangejua huyo binti anaweza leta impact kiasi hiki naamini wangelishughulikia kwa umakini kipindi limetokea
 
Isolated event

Hatuwezi kuchafuka kwa hadithi ya mtu mmoja kutoka Kiherehere hotel
Warere Mkuu
Kweli huyo Shauna yupo, tulishaenda hapo ni pazuri, shida ya zenj ni porous, mtu awezaingilia popote siyo salama hata Kwa watoto wa kiume alone!
Kulishwa drugs na kuliwa jicho na popo bawa ni rahisi!

Huyu alipewa drugs ila kiwango nafikiri kilikuwa kidogo hakuwa totally out!

Nimeshangaa hakuna receptionist overnight! Hatukuhitaji huduma Ila kawaida hotel zikiwa na wageni, huwa receptionist wanalala hata mapokezi chini! Shida tupo kimazoea!

Pole zake!
 
Sawa,
Atendewe haki, wamruudishie pesa, wazuge Tu, maneno, tunalifanyia kazi. Walinzi WA siku hiyo tumewasimamisha kupisha uchunguzi!
Blah blah blah, we take these allegations seriously! Mbona easy, hatuhitaji maguvu! Beberu anatushinda hapo! Kwenye being diplomatic & politically correct!
 
Kituo cha Polisi nao wamesemwa.
Mamlaka husika wajiridhishe kama huyu mtu kipindi hicho aliingia Tanzania alafu masuala mengine yafuate

 
Mpaka sasa dada katupiga maana kwa ushaidi wa awali vyombo vyetu vimefail sana sio muwekezaji wala polie walionesha kutaka kumsaidia dada too sad to hear that
Hilo ndilo kero kubwa!
Manager kumwambia muongo, wakati. Angemwambia tunalichukia serious, twende police, hapa ni mahali salama. Tunaangalia CCTV, vitu kama hivyo! Tunakupa baunsa WA kuzunguka naye Kwa hizi siku 4 ulizo hapa. Baunsa unamlipa 30,000 Kwa siku! Mambo mengine siasa Tu!

Siyo kila mgeni wa like anayeenda Zanzibar, kaenda kujiuza! Hiyo mentality ndiyo iliyopelekea hayo, manager kuona mgeni ni danga na police kumuona ni danga vile vile!

Customer care! Kuna comic book ya Tommy & Jenny, huwa siachi kucheka kila nikilipitia, linatusema haswa!
 
Wa maelezo yake anaonekana ni tapeli tu yule. Wanigeria kibao wanaichafua Zanzibar. Nimesoma hizo tweets yani anajichanganya tu na anaongea vitu visivyo realistic. Haya, kasema mbakaji alikuwa hajui kingereza na alielewa neno HIV pekee, ila alipoaga kuendea condom na akasema atarudi walielewana hahah.. Mbakaji anakuita baby?
 
ujinga mtupu alikuwa wapi kusema au sababu ameona mama anazindua royal tour anataka kuharibu tatizo wa Tz tunakosa uzalendo tunafuta upepo tu kila kitu
 
ww nawe unashindwa kutumia akili yako vizuri kwa hiyo Tanzania ikichafuka ww utafurahi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…