Salaam kutoka Zanzibar - Hotuba kamili - Msikie SEIF SHARIF HAMAD-Si mchezo



- Tizama sasa mkuu wangu, unasema ya kumrudisha Sultani ni ya karne iliyopita, meaning kwamba unakubali kuwa yaliwahi kuwepo kwa sababu kwani karne ina miaka mingapi? Sasa eti kwa kuamini kuwa ya kurudi kwa Sultan yaliwahi kuwepo karne iliyopita unakua ni mtu mwenye elimu lakini umezidiwa na utashi na unasikitisha eti bado ina make the same sense kwako mkuu?

- Sasa unasema kwamba utuuzima na fikra zetu zinakua ni za kuburuzwa, tunaposema kwamba malengo ya CUF Visiwani sio sawa na malengo yake Bara? Ni kweli tumepata elimu ili tuweze kuitumia na in this case tuweze kuelewa kwamba hotuba za Seif anapokuwa Bara hazifanani na anapokuwa Visiwani sasa ana agenda gani mkuu kama sio u-Pemba?

U-Pemba hauna nafasi kwenye Muungano wetu, ndio maana rais anasema ataulinda Muungano kwa nguvu zote, sasa Seif analilia nini kama anaupenda Muungano?
 
1.
Quote: Ngekewa

Kuulinda nini mzee mfarakano wa Wazanzibari au nini, samahani sijakuelewa.

2.
- Mkuu wangu wewe unasema mfarakano wa Wazanzibari, Seif anasema kuna mshikamano mkubwa sana kati ya Wazanzibari,

sasa nani kati yenu anayesema ukweli mkuu?
 
 

- Mkuu wangu all this hapo juu coming from wewe mtu mmoja huoni kwamba ni incredible? Exactly what are you from neutral to Upinzani wa CCM?


- Ohhh my Gosh, sasa mkuu what is what hapa I am lost!

CUF- watamsimamisha tena Maalim kwa mkakati, kiufundi na kijamii kwa kuwa wao wanaamini anapendwa na ni kiongozi mwadilifu kwao.But, CCM hawatakubali hilo litokee abadani kuwa Maalim Seif ni kiongozi wa Znz.Tusubiri na tuone, time will tell!!

- Fair enough, watamsimamisha Seif tena, kwa sababu hawaelewi maana ya neno insanity kwamba ni pamoja nikurudia rudia the same theory ukitegemea different results.

Thanxs!
 

NI yakweli kabisa wala haya tatizo hata kdg, TATIZO NI WAHAFIDHINA WA CCM-BARA (VIBARAKA WA JK & OTHERS); KWAMBA KUIKWA NA MUAFAKA WA KISIASA CCM NDIO IMEKUFA ZNZ, MAANA ATHARI ZA MUAFAKA 1 & 2 WAMEZIONA SASA KUKIWA NA MUAFAKA WA3 NDIO KWA HERI KBS.

Jiulize kwa nini kuanzia 2000 na 2005 uchaguzi wa znz na muungano unakuwa cku moja? Waliona athari za 1995, maana ile hamasa ya upinzani kushinda znz basi uchaguzi wa bara nao unakuwa na asilimia kubwa ia upinzni uatshinda.

Kuhusu ya Nyerere kuwa na nia ya kutaka kuifuta znz nakupa home work ndogo tu; Nenda Pale Cathedral Bookshop posta ya zamani. Tafuta kitabu SINODI ya Afrika, utapata full details za why mwalimu alitaka kuifuta znz.
 
Naona mtiririko wa postings unatuonyesha namna wengi wetu tunajadili mambo tusiyoyafahamu labda ni matokeo ya hutuba ya jazba ya Seif. Kwa kuanzia hebu jiulizeni wengi wa Wapemba (Iwapo tunafikiri CUF ni ya Wapemba) ni watu wa namna gani. Wengi wa Wapemba ni weusi tena weusi sana. Na jengine ni kuwa waliopo madarakani kwa jina la CCM Zanzibar kuna wengi wenye asili ya Uarabu. SASA HILI SUALA LA UBAGUZI LINAKUJAJE HAPA?
Suala la pili ni kuwa Waswahili wanasema kitanda usichokilalia hukijui kunguni wake. Ni Wazanzibari wanaojuwa raha na shida za utawala uliopo madarakani na ni wao wanaojua kiburi cha watawala kinatoka wapi. Sasa iwapo kiburi hicho kinatoka Bara nini mnategemea? Ni sawasawa na kuchokoza mwendawazimu wakati uko nyumbani kwako bila shaka mawe atakayelenga yataangukia upenuni kwako. La kufanya ni kuwaachia Wazanzibari watowane macho au wapatane wenyewe na hasa tukitilia maanani kuwa tunahubiri Amani nchini kwetu na tunapokwenda visiwani tunahubiri vita. Ivyo nani asielewa kuwa hata kama mwanao jambazi basi hutofurahia kifo kimfike . MAPINDUZI YALIWAGAWA WAZANZIBARI KWA WALIOULIWA NA WALIOUWA SIONI MANTIKI YA KUZIDI KUKUMBUSHIA MAUWAJI HAYO kama nilivyosema kifo ni kifo tu.
Ningefurahi zaidi kama ningeona yale mambo yaliyoletwa baada ya Mapinduzi yanaendelezwa lakini wapi maji kwa pesa (wala hayapo), Elimu kwa pesa, matibabu kwa pesa na megnineyo. ATI tunadumisha Mapinduzi kwa kuendelea kutawala mbona Utawala sasa ni mambo ya Demokrasia na wananchi wenyewe ndio waamue nani wa kuwaongoza. Tumeruhusu vyama vingi vya nini wakati wenye haki ya kutawala ni CCM tu? Halafu Kiongozi anaetumainiwa Afrika anasimama na kusema kuwa haki ya kutawala ipo kwa watu fulani tu. Nini tofauti na Usultani uliopinduliwa?
Wana JF tuwakataze Viongozi wenye kauli kama za Seif na pia tuwaseme viongozi wanaobariki Usultani mpya kwani Sultani si mwarabu tu bali tafsiri yake ni sawa sawa na mfalme kwa lugha yetu.
 
mi nimejaribu kuisikiliza nimeshindwa nifanye?
 

Unafikiri CUF ni upemba? Ni hasara kuamini hivyo. Kuhusu Seif kupigania Pemba ni kuwa bahati mbaya ni sehemu inayohitaji kupiganiwa kati ya Unguja na Pemba na inapokuja kwa level ya Tanzania basi Zanzibar ndiyo inayofaa kupiganiwa. Ni ubinaadamu kuwa palipo na matatizo ndipo panapotafutiwa harakati za utatuzi.
 
1.

2.

- Mkuu wangu wewe unasema mfarakano wa Wazanzibari, Seif anasema kuna mshikamano mkubwa sana kati ya Wazanzibari,

sasa nani kati yenu anayesema ukweli mkuu?

Hapa sikumnukuu Sef walaKikwete nilikuuliza wewe kwa posting yako.
 

Be fair. Kwa hesabu za haraka haraka mimi kama niko kwenye mapambano nitapenda mshindani dhaifu na kama ni hivyo kwanini CCM wanashikilia kuwa yeye ni dhaifu si waachie tu ili wapate ushindi wa kirahisi kama kule Mbeya? Uambiwapo nawe ujiambie.
 


Sasa huyo seif anawakilisha matakwa ya waarabu baada ya kutoka CCM tu ?Wacha kudanganya watu hapa mtu mzima hawi mwongo hasa wakati huu wa leo,ikiwa vijana waliokimbilia majuu huwambii kitu kurudi Zanzibar ije kuwa Sultani,hizo siasa za sultani zimepitwa na wakati huna wa kumdanganya,kama alikuwa anataka kumrudisha sultani angefanya hivyo alipokuwa Waziri kiongozi.

Hao weusi uliowaona si kutoka Afrika inawezekana kabisa umewaona wahindi ambao ni weusi kuliko sisi waafrika,huwa nakwenda Dubai kibiashala kabla sijahamia Uturuki ,sijaona watu wanaoteswa ,huo ni uongo wa kupandikiza ,nimeona wakubwa wengi wa polisi mitaani ambao ni weusi tititi nilipoulizia nikaambiwa hao ndio National wenyewe na hakuna waarabu kuliko wao wala huna la kuwaambia kama walitoka Afrika, ya Egypty siyajui naona nao ni waafrika japo weupe.halafu kwani hao waliopiga kelele juzi tu hapa Tz na kusema kuna biashala ya binadamu katika ya mikoa ya Arusha Kilimanjaro na Daresalaam ,ni waarabu hao wanaotumilisha ?

Eti nina ushahidi mwingi,ushahidi CCM mnao mwingi maana CUF ,labda nikukumbushe CUF mlikiita cha Kidini,mkakiita cha Waarabu ,mkakiita cha Binladen mkakiita ni materarist ila sasa umemwona mtu alikwenda kuterrorize WaZanzibar basi kila kitu kitaibuka kama cha waarabu ndio hivyo tunaona wale wanaotua na madege kule Arusha wakajiwindia kwa nafasi zao wameruhusiwa na CUF na kupewa vibali na CUF ,wale wanaochukua migodi ya dhahabu na kuilipa serikali vile watakavyo wao wameletwa na CUF ,wale wanaoliibia Taifa hili ni CUF waliomo serikalini ..mtu mzima wacha uongo ,uchafu unaofanywa na CCM hufiki mbali utanaswa tu na ushahidi wowote atakaouleta mwana CCM kuitetea CCM na sera zake utakuwa ushahidi wa uongo ,halafu Seif hachagui sehemu ya kusema pahala popote pale anasema mara ngapi amesharapu huko mikoani na ukitokea mkutano huko basi aliyoyasema Zanzibar atayasema huko pia naona unamtazama kwa woga ,usifikirie Seif ni Makamba ,CCM ndio iliyowakumbatia waarabu na ndio maana huko Arusha kulitokea mgogoro lakini jamaa wakatengeneza kwa vile wameshawanunua viongozi na wanyama wao upo ,wote wamechanganywa pamoja hawafurukuti ?
 
 
Hizo ni data zilizokusanywa kwa wale ambao hawakuwahi kuziona,hakujapotea kitu kila kitu kimehifadhiwa na siku ikifika basi waliohusika wajue tu watajibu,endeleeni kulinda kutetea lakini njia ya kukimbia inazidi kuwa fupi kila tukisogea japo kuna vitisho vya kulindana hivyo vingewafaa ambao wameshaonja joto la kimahakama za kimataifa ,watu ambao walikuwa na majeshi makubwa tu lakini walipoitwa majeshi na nguvu walizokuwa wakiringia hazikuwafaa ,leo Mkapa akiitwa Kikwete hana ubavu wa kumkingia kifua hata chembe.
 

Attachments


Mfumwa, hawa viongozi wetu hawajali kabisa dhamana kubwa tuliyowakabidhi kutuongoza. Huwa wanakurupuka na kutoa kauli bila kujali athari yake katika usalama na umuoja wa Watanzania. Kamwe huwezi kusikia kauli aliyoitoa Kikwete ikitolewa na Obama kuwaambia Republicans au kiongozi yeyote yule wa nchi za magharibi. Maana wanajua wakivurunda basi wataondolewa madarakani kwa kura, lakini Viongozi wa CCM na serikali sasa hivi wamekuwa na kiburi cha hali ya juu na wanajua pamoja na kuvurunda katika uongozi wao wakati wa uchaguzi ujao watawanyanyasa viongozi wa wapinzania, wanachama wao na wapenzi kwa kutumia vyombo vya dola watahujumu na kuiba kura na hatimaye kuiba ushindi.

Juzi juzi tumesikia Makamba akiwafananisha Wapinzani na Paka, lakini sijasikia hata kiongozi mmoja wa CCM kumwambia Makamba kwamba amekosea hivyo awaombe samahani viongozi wa wapinzani na wanachama wao, lakini wao wamesimama kidete kutaka Maalim Seif amuombe samahani Kikwete.

Dalili za uchaguzi wa 2010 si nzuri inaelekea kutakuwa na umwagaji damu mwingine ambao mwisho wake haujulikani utakuwa na athari gani katika usalama na umoja wa nchi yetu. Maafa yoyote yakitokea wakulaumiwa ni Kikwete na viongozi wa juu wa serikali na CCM. Pamoja na kuwa wana uwezo wa kufikia makubaliano ya kweli na CUF lakini hawakutoa uzito unaostahili katika kufikia makubaliano hayo na sasa kuna kila dalili kwamba vyombo vya dola vitatumika tena kuwaua raia wasiokuwa na hatia yoyote. Mwenyezi Mungu apishilie mbali.

Mungu ibariki Tanzania.
 

Mwiba,
Ahsante nimeangalia..sema ni ngumu kuamini..kama ni data na majina ni ya kweli...unajua siasa tena! Yawezekana kuna kutia chumvi kidogo

Hayo ya 2001 tuyaache..tusonge mbele tufanye kazi!

Tuombe Mungu yasitokee tena!
 
Wana JF tuwakataze Viongozi wenye kauli kama za Seif na pia tuwaseme viongozi wanaobariki Usultani mpya kwani Sultani si mwarabu tu bali tafsiri yake ni sawa sawa na mfalme kwa lugha yetu.

- Mkuu Ngekewa, angalau hapa umesema maneno yenye maana na tupo pamoja, mengine naomba kukuachia mwenyewe na hao wengine pia.
 
Haya Kikwete ni Mzanzibari? Mimi ninavyojuwa – na Profesa (Lipumba, ambaye ni Mnyamwezi na kimila ni mtani wa Kikwete) – kwamba Kikwete ni Mkwere.

Naona wewe unafahamu KIVINGINE. Wakwere asili yao ni WANYAMWEZI waliozamia Pwani/Bagamoyo. Kwa maana hiyo, Wakwere wote huheshimu Wanyamwezi kama BABU zao na hapo HAMNA UTANI.
 
Mwiba,
Ahsante nimeangalia..sema ni ngumu kuamini..kama ni data na majina ni ya kweli...unajua siasa tena! Yawezekana kuna kutia chumvi kidogo

Hayo ya 2001 tuyaache..tusonge mbele tufanye kazi!
Tuombe Mungu yasitokee tena!

Unajua huyu mtu anaejidai mtu mzima anakosa muelekeo wa mazungumzo,anaposema mambo machafu hayakufanyika kule Pemba ,mtu huyu ni mpotoshaji kama wapotoshaji wengine waliosema barabara za unguja kama mgongo wa ngisi. Aone haya yalioamuriwa

Government Orders to Use Force

Several police officers who were involved told Human Rights Watch that the regional police authorities prepared their men in several meetings at different police stations. For example, three police officers told Human Rights Watch that two days before the January 27 demonstrations, the regional police commissioner for Unguja Urban-West, Khalid Idd Nuizan, reportedly made a speech to a large gathering of policemen in Zanzibar Town, during which he said they should use all force necessary to break up the demonstrations. The police were told that it was better for them to kill than to return with their weapons and bullets. Police commissioner Nuizan reportedly said, "Kill, bring back bodies, then we will know that you have done your job.". Another police commander, who addressed some 200 police officers in a police mess in Pemba on January 26, 2001, reportedly told his men that he had received orders from his superiors to use any force necessary, including live ammunition, since the planned demonstration was banned.16 When he told the gathering to use restraint by first firing rubber bullets, several FFU riot police transferred from the mainland jeered, protesting that it would be interpreted as a sign of weakness if they did not use live ammunition.17 In another police station in Pemba, the police were reportedly given more explicit orders to use live ammunition against crowds numbering more than twenty. In Pemba, the army and the local government administration at Wete sent an intimidating message to residents on January 26, 2001, by removing the police flag at the police station and replacing it with the army flag-suggesting an arbitrary institution of martial law. Army cars then drove through town, soldiers standing atop their vehicles with guns. The entire town was under police guard.

We were sitting and chatting outside, as normal, when all of a sudden police appeared. They did not give any order for us to leave or disperse. They came there and right away they started shooting, not using sticks or anything like that, but live weapons. They didn't shoot in the air. If they had shot in the air we would have run away. They were shooting at people this side and that side. My friend was shot and died...I know the one who gave the order-[police sergeant Mahmoud Juma] Mrema. He was the one who was in charge of the group that day. He didn't shoot, himself. He was giving orders such as, "Shoot him, shoot that one."

A police officer who was on duty at Madema police station that day provided a similar account:

We went into the town around 11 or 12 o'clock, and everything was calm. Later, those who were trusted that they could do this thing were chosen; they were given weapons, and they went to town. The result was, when they returned, they had already killed, those two people ...Well, those policemen [who killed] claimed that there was disturbance, but honestly, there wasn't any disturbance.

Huyu mtu zmima muongo hapa aone kuwa uwongo kwa serikali hii haukuanza leo au jana tazama walivyoshikwa pabaya mpaka wakasema eti risasi ilipigwa juu iliporudi chini ndio ikampiga mtu. Serikali navyombo vyake ni uoza mtupu dhuluma na uongo ndio unaowaonyesha njia ya kuzitawala nchi hizi kiwiziwizi.

Human Rights Watch interviews with several eyewitnesses, victims, and police officers contradict the official government response that characterized the shootings as accidental. Laurean Tibasana, police commissioner in the Tanzanian capital, Dar-es-Salaam, announced:
In Mtendeni, due to bad luck on January 26, 2001, after Friday afternoon prayers, a police patrol car containing seven police officers on their usual patrol duty were surrounded by a group of people coming out of the mosque and throwing stones at the police. The police fired bullets in the air, whereupon the people dispersed. The patrol car continued on its rounds after the people dispersed without knowing that anyone had been injured. Later, a report was received at the station that a person had died as a result of the bullets that were fired into the air.

Halafu anazuka mtu anasema chunvi imeongezwa basi wandugu watu wanajulikana wakubwa na mkubwa wao wapo na kesi ipo mbioni.
Tutaburuzwa hivi mpaka lini ? Kinachofanywa Zanzibar msifikirie huko hakiwezi kufanywa kinachotaka kufanywa ni kuwawahi watu hawa mapema japo wanaweka vizingiti watu wasifikishe mashitaka mbele ya safari lakini vizingiti hivyo vitarukwa kama mkimbia mbio za viunzi MKAPA lazima akajibu tu kama hapo mnasua sua nae basi ajue mambo hayajesha na watu wana hasira nae ,hawakubali hawakubali hawakubali ,Mkapa ameuwa na hakuchukua hatua yeyote ile ,zaidi amewapandisha vyeo mapolisi ambao leo hii wengine wako vizimbani wakishikiliwa kwa makosa ya uuwaji ,au Zombe yupo wapi ? Hawa ndio akiwapa sifa na mivyeo kumbe nyuma ya pazia wote ni wauaji. Halafu mnasema mnatukaniwa Raisi wenu hajatukanwa Raisi hapa ,anaambiwa kweli baada ya kwenda kusema mambo ambayo si ya kiungwana na kuwakejeli watu ,watu hawana shida ya uongozi watu wanashida na maisha yao,sasa yeye aliko juu asijisahau ajue mpanda ngazi hushuka ,huo ni msemo wa kiswahili na kama wana nguvu na uwezo basi wajizuie kuzeeka.
 
[QUOTE=
Hivyo ndivyo walivyo Seif. CUF na wapambe. nashukuru unaliona hilo.
 
Mwiba wee,
Siku Muungano ukifa, Mwiba utakonda sana maana utakosa cha kuandika/kufanya. Labda uanze kuuwa MUUNGANO wa Zanzibar yaani Pemba na Unguja.

Kuna vitu huwa sikubaliani na FMes na huwa navisema. Nafikiri alichosema FMes hapa ni kuwa weusi wa Zanzibar inabidi walindwe. Haina maana Waarabu wasilindwe. Nilishaona Askari wa Kiyahudi wakilinda Waarabu. Walifanya hivyo kwani Wayahudi wenye siasa kali wangeliweza kuja na kuwauwa hawa Waarabu. Sasa ukisikia hivyo, unaweza sema WANABAGUA.
Juzi tumesikia Kibunago anavyoeleza juu ya Wanyamwezi/Wamakonde wanavyofanyishwa kazi za ovyo huko Zenji. Nikaona kabisa kumbe kuwa Mnyamwezi /Mmakonde Zenji ni aibu sana. Itabidi niende Zenji na Tshirt imeandikwa "PROUD TO BE MNYAMWEZI". Halafu nione mtu anayeninyanyasa wakati nina hela yangu mfukoni baada ya kuuza ng'ombe na mpunga. Hili la weusi kunyanyaswa na kuitwa hata Wanyamwezi ingawa unaweza kukuta ni Waha, naona lipo sana.

Mwisho, lazima mjue kitu kimoja. Kama Muungano wa Tanzania ulilazimishwa na USA/UK ili kupinga Warusi kujenga base yao hapo, sasa hivi watashindwa nini kuendelea kulazimisha hasa ikijulikana kuwa Al-qaid au ndugu zao wanataka kujenga kambi zao hapo? Ndiyo maana hata wakienda West, wanakwama kwani hizo ndevu na macho ya Maalim ukiyaona tu, unakuwa kama umewaona wale Wanafunzi wa Afghanistan.

Hivi Maalim atagombea tena URAIS? Duu, jamaa naona ni kama yule anayeimbwa na LIL WAYNE kuwa ana maisha 9 yaani zaidi ya PAKA mwenye maisha 7.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…