Salamu kwenu Atheist wa Jamii Forums

Salamu kwenu Atheist wa Jamii Forums

We unataka Mungu hajidhirishe ili wewe umwamini kwamba yupo ila umesahau wewe hapo ulipo uneshindwa kujidhihirishA hata hapa jf una jina bandia picha bandia sisi tunaamini wewe upo kupitia maandishi yako yametosha kuthibitisha kwamba wewe upo sasa sisi hatuna shaka kwamba mungu yupo kwa vile sisi tupo vinginevyo kama Mungu hayupo na Binadamu tusingekuwepo.
Logical non sequitur fallacy.

Mtu ambaye hana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote akishindwa kujidhihirisha hakuna cha ajabu hapo, hakuna kitu ambacho hakina logical consistency.

Huyu mtu hana uwezo wote, hana ujuzi wote, hana upendo wote, inawezekana kashindwa kujidhihirisha kwa sababu hana uwezo wa kujidhihirisha tu, hajasema ana uwezo wote.

Mnaposema kuna Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, Mungu huyo hana excuse ya kutojidhihirisha.

Kwa maana mnasema ana uwezo wote, ana ujuzi wote, ana upendo wote.

Kwa nini hajajidhihirisha kuwa yupo kwa njia ambayo kila mtu atajua bila shaka atumalizie hii mijadala ya kila siku na vita za kidini zisizoisha?
 
Kuna uhusiano mkubwa kati ya kuwa Atheist na kuugua ugonjwa wa akili....
Hata kama hii ni kweli.

Kuugua ugonjwa wa akili ni uthibitisho kuwa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, asingeruhusu viumbe wake anaowapenda waweze kuumwa ugonjwa wa akili.

Kwa akili yako ndogo unaona unawabagaza atheists hapo, ika kiukweli unawaongezea atgeists hoja zao tu kuwa Mungu hayupo.
 
Kupumua kwangu kuna husiana vipi na huyo Mungu?

Kwanza thibitisha uwepo wa huyo Mungu, yeye kama yeye.

Sio kurukia kusema mifumo yangu na kupumua kwangu ni Mungu.

Hakuna Mungu anaye nifanya nipumue.

Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hatakaa awepo.

Nikisha sadiki yeye inamsaidia nini?

Huyo Mungu kama yupo ajitokeze hadharani mwenyewe ajidhihirishe yupo kama ana huo uwezo.
Nilishawahi kusema hawa wasiomwamini Mungu wote wana tatizo la Akili kama kuna mtu anataka kupima ninachoongea kama kuna mmoja unamfahamu anza kumfuatilia hapo ulipo.Yaani mwangalie huyu mjinga anatumia nguvu kubwa kutaka yeye athibishe uwepo wa Mungu eti huyo Mungu aje amthibitishie yeye kwamba yupo sasa hiyo ni kwamba Mungu anashida na wewe au una umuhimu sana kwa nani sasa ?Hata huyo Rais Samia ukimvunjia heshima yake hatokuja yeye kukushughulikia na uwenda usimuone kabisa iwe mahakamani au popote pale ila utashughulikiwa ila haiondoi kwamba yeye hana nguvu kisa tu hajajitetea mwenyewe Sisi tupo kwa ajili ya kuwa machawa wa Mungu kwa vile sisi ni Mali yake kama haumini maneno yangu nenda pale magogoni Ikulu pale kamtukane Rais uone atakuja yeye kukujibu au ni nini kitatokea.
 
We unataka Mungu hajidhirishe ili wewe umwamini kwamba yupo ila umesahau wewe hapo ulipo uneshindwa kujidhihirishA hata hapa jf una jina bandia picha bandia sisi tunaamini wewe upo kupitia maandishi yako yametosha kuthibitisha kwamba wewe upo sasa sisi hatuna shaka kwamba mungu yupo kwa vile sisi tupo vinginevyo kama Mungu hayupo na Binadamu tusingekuwepo.
Nikishaona mtu hajui tofauti ya "ajidhihirishe" na "hajidhihirishe" tu nakosa nguvu ya kuendelea kujadiliana naye kimantiki.

Huyu ni mtu ambaye hata kuandika herufi za Kiswahili tu ni mgogoro.

Sasa huyu kweli naweza kumpa link ya essays za Bertrand Russell tujadili falsafa ya dini kimantiki na kupangua logical fallacies?
 
Kumekuwa na hali fulani kwamba watu wakifanikiwa
kiuchumi au kusoma kidogo basi wengine wanasema

hakuna Mungu na kutaka logic kwenye kila jambo
linalohusu uwepo wa Mungu. Hawaamini hata immortality
life baada ya kufa.

Je nawauliza nyie ni zaidi ya Elon Musk ambaye ingawa haja
jishikiza kwenye dini ila anamini katika ukristo na uwepo wa
Mungu na kwa kipindi cha hivi karibuni amezidi kuamini sana.


Je ndugu zangu mnamkataa shetani na mambo yake na fahari
zake zote?
Elon Musk kumkubali Mungu hakuleti ukweli kuwa Mungu yupo. Hiyo inaitwa fallacy (kutumia ulaghai ili hoja ikubalike). Uwepo wa Mungu unategemea sana "correct arguments"!
 
Kwanza kuna watu hawaamini Mungu kwa sababu wao ni masikini, hivyo hoja inayounganisha kutoamini Mungu na kufanikiwa kiuchumi haina mashiko.

Pili, kitu muhimu si kuamini. Kuamini ni haki ya kibinadamu ya kila mtu aamini anavyotaka. Imani inalindwa na haki ya kila mtu kuwa na faragha yake. Hii ni sehemu ya "Universal Declaration of Human Rights" tangu December 10, 1948. Ni kitu non negotiable hakihitaji mjadala wala justification. Amini unavyotaka. Usiingilie imani za wengine na uhuru wao. Ila imani ikiletwa public square kama hapa JF ni fair game tutaichambua.

Mimi sipo hapa kujadili imani ya mtu. Imani ni haki ya kibinadamu, kama ilivyo haki ya kutoamini.

Ndiyo maana kuna watu wana imani tofauti, maelfu ya dini, na wote wako sawa kuamini wanavyotaka. Hiyo ni haki yao.

Mimi niko hapa kujadili fact. Fact si haki ya binadamu kila mtu awe na yake. Fact ni objective.

Unaruhusiwa kuamini immortality na life after death. Mtu akikuingilia katika imani yako hiyo, hata mimi nitakutetea uamini unavyotaka, kwa sababu hiyo ni haki yako ya kibinadamu.

Ila, tukienda kwenye facts, immortality si fact. Hakuna evidence wala proof kwamba kuna maisha ya mtu yanaendelea baada ya mtu huyo kufa.

Swali la "nyie ni zaidi ya Elon Musk" ni logical fallacy ya argument from authority.

Kwa nini umemtaja Elon Musk? Kwani Elon Musk ana monopoly ya kuujua ukweli kuhusu uwepo wa Mungu?

Elon Musk hata si mwanatheolojia useme huyu anajua theolojia sana msikilizeni. Mimi nimebishana na Alvin Plantinga kwwnye masuala haya, na nikamshinda.

Sasa huyo Elon Musk unaweza kumlinganisha na Alvin Plantinga kwenye mambo ya theolojia?

Mbona unamuweka Elon Musk sehemu ambayo hana utaalamu nayo kwenye mambo ya theolojia? Hatushindani kuendesha kampuni ya roketi hapa, kwenye kuendesha kampuninya roketi ukitaka kunishindanisha na Elon Musk nitasema kanizidi uziefu huko, lakini kwenye faksafa ya dini Elon Musk ana credentials gani?

Pia, imani ni kitu very private and very complex.

Huyo Elon Musk unahakikishaje kweli anaamini Mungu yupo, na kwamba anapoonesha kuwa anaamini hivyo hafanyi hivyo kwa sababu inamsaidia kibiashara tu kupiga pesa, asiwaoneshe wateja wake kuwa yeye ni mtu ambaye hawatampenda? A lot of religion is virtue signaling, do you understand that?

Kama Mungu yupo, thibitisha yupo. Achana na logical fallacies za argument from authority za kumuangalia Elon Musk.

Elon Musk akila mavi na wewe utakula? Huoni kwamba unaweza kula mavi kwa kufikiri Elon Musk kala mavi, kumbe mwenzako kaitengeneza chocolate ionekane kama mavi.

Acha uvivu wa kufanya kitu kwa sababu Elon Musk kafanya, kwani wewe hunanuwezo wa kuchambua mambo ukajua mazuri au mabaya ni yapi?

Thibitisha Mungu yupo, acha longolingo za Elon Musk kimepanda kimeshuka.
Hujaelewa vizuri sijasema Elon ni Mtheolojia.

Na pia Atheists wengi ninao wazungumzia ni hawa wa Tanzania
na Afrika ambao wameacha kumuamini Mungu kisa wamesoma,

wamepata exposure na wengine wamefanikiwa kidogo kiuchumi.

Ndio nikauliza nyie ni zaidi ya Elon Musk ambaye ni mwana
sayansi na tajiri vitu ambavyo vingem tempt kusema hakuna
Mungu. Yeye nimemtumia kama mfano tuu wapo wengine wengi
 
Huyo Mungu kama yupo, Kwa nini aliumba binadamu wasio mwamini?

Huyo Mungu, Alishindwaje kuumba binadamu wema tu watakao mtii na kumwamini siku zote na wakati wote?

Hivi huyo Mungu ana jielewa kweli?
Hivyo ulivyo ndivyo imetakiwa kuwa hivyo ungeumbwa tofauti na hivyo usingeona maana ya maisha kwa sababu hicho unachokifikilia tayari kipo Mungu ameumba Malaika wao wako hivyo unavyotaka wao muda wote wako limited tofauti na wewe unafanya unachotaka Alafu akakupa Akili ikuongoze sasa hicho ndo kitu wewe umekikosa.
 
Halafu mbona ni ninyi tu binadamu mnahangaika kumwelezea Mungu na kutetea uwepo wake, Anashindwa nini kuja kujitetea na kujidhihirisha yeye mwenyewe?

Huyo Mungu kama yupo ajitokeze hadharani mwenyewe ajidhihirishe na kujitetea mwenyewe yeye kama yeye, kama ana huo uwezo.

Vinginevyo, Ni nyie tu mnahangaika kumwelezea Mungu ambaye hajawahi kuwepo, hayupo na hatakaa awepo kujidhihirisha mwenyewe.
Hata Wana wa Israel walimwambia Musa wanataka wamuone Mungu,Mwishowe , wenyewe walimwambia Musa chochote utachoambiwa huko tutakufanyia kazi! Kambi ya jeshi tuu unaogopa.
 
Back
Top Bottom