Tetesi: Salim Abdallah ‘Try Again’ katika jaribio la kumng’oa Mo Dewj Simba!

Tetesi: Salim Abdallah ‘Try Again’ katika jaribio la kumng’oa Mo Dewj Simba!

Kukudanganya vibaya mnooo Mo ndo aliyemteua Try Again hivo akijua anafanya hayo anao uwezo wa kumtoa mda wowote mtu ambae ungesema anafanya zengwe habar yako iwe na maana labda Ngungu boy pole sana aise
Huna unachokijua wewe, huyo Mo sasa hivi analazwa na viatu na Try Again.

Mangungu wameungana na Try Again, sio vita rahisi kwa Mo.
 
View attachment 2966280

Moto unawaka SSC! Ni vita kubwa!
Klabu ya Simba ipo katika kipindi kigumu cha vita inayozidi kukomaa kila uchwao baina ya Mkurugenzi wa bodi ya Wakurugenzi ya Simba Salim Abdallah Mhene ‘Try Again’ dhidi ya ‘Rais wa heshima’ wa Simba Mohamed ‘Mo’ Dewj.

Wawili hao walianza kukosa maelewano baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi yake nchini ambapo taarifa za uhakika ni kwamba anaishi Dubai hadi hivi sasa.

Baada ya Mo Dewj kuhamisha makazi uwekezaji wake Simba ulisuasua, ikitaarifiwa kumuachia mzigo mkubwa wa uendeahaji timu Try Again ambao ulimuelemea!

Try Again alijitahidi kadiri ya uwezo wake baada ya ‘tajiri’ kujitenga ‘kiaiana’, akihaha huku na huko kutafuta namna ya kuinusuru Klabu ya Simba ambayo kwa msimu wa tatu mfululizo imekuwa na matokeo ya kusuasua. Jitihada zake hizo zikizaa matunda kwa kiasi kisichoendana na kipindi ambacho muwekezaji alikuwa ameshikilia usukani.

Try Again adhamiria mapinduzi, amlenga Said Salim Bakhressa!
Baada ya Try again ‘kususiwa’ timu na muwekezaji Mo Dewj, Try Again aliona uwezekano wa kupindua meza, na kama ilivyo ada ya wafanyabiashara wakubwa kuwa na jicho angavu la udhia, S.S Bakhressa hakusita kupenyeza rupia!

Vita kubwa iliyopo hivi sasa ni Try Again aliyeko kwenye mikakati thabiti ya kumpindua Mo Dewj kama muwekezaji kisha nafasi hiyo apewe muwekezaji asiye na ‘mbambamba’ S.S. Bakhressa, huku Mo Dewj nae akiwa katika mipango ya kujidhatiti kushikilia nafasi yake hiyo adhimu ambayo huitumia mara nyingi kama kielelezo cha mali zake (SSC)

Serikali yakoleza vita!
Hivi karibuni, Serikali imetoa agizo la kuanzishwa upya kwa mchakato wa undeshwaji wa kisasa kwa klabu ya Simba. Kama mtakumbuka vyema mchakato huo ulioanza miaka kadhaa nyuma, haukuwahi kukamilika.

Serikali imetoa agizo hilo baada ya kujidhihirisha kuwa mchakato wa awali ulikuwa na makosa mengi, hivyo ulikuwa batili ukikosa uhalali.

Agizo hilo limekuwa chachu kwa Try Again na timu yake, kwani endapo ukifanikiwa kuanza kuna uwezekano mkubwa wa S.S. Bakhressa na wawekezaji wengine kujitokeza na kushika hatamu katika hisa, huku ikielezwa kwamba Mo Dewj atarudishiwa fedha zake alizolipia katika mchakato huo uliohuishwa ambako alijitwalia hisa 49% za umiliki wa klabu ya Simba.

Mo Dewj atupa shilingi mechi ya Yanga!
Hii ni tahadhari kwa Klabu ya Yanga, Hersi na wenzio kama hamjaipata nawapa hii…

Mo Dewj amejipanga kuitumia mechi ya tarehe 20/04/2024 dhidi ya Yanga kama turufu yake ndani ya Simba.

Mo Dewj ambaye inaarifiwa ametenga fungu ‘nono’ kuhakikisha Simba inashinda mechi hiyo, amejipanga sawia na mkakati wake huo ambao tayari ameshaanza utekelezaji.

Mkakati huu wa Mo ni kwamba endapo Simba ikishinda mechi hiyo, atafanikiwa kurudisha imani na mapenzi kwa mashabiki, hivyo kutumia hilo kama zengwe la kuwang’oa Try Again na Mangungu pale Simba.

Kila mmoja ana mpango kazi!
Try Again ambaye hapo awali alitumia ‘janja janja’ kuwang’oa aliyekuwa CEO wa Klabu bibie Barbara na Rweyemamu ambaye alikuwa meneja wa timu kwa ‘kuwachonganisha’ na muewekezaji Mo Dewj, anahaha kulinda maslahi yake kwani endapo Mo Dewj akishinda vita hii (Kwa Simba kushinda dhidi ya Yanga) amepanga kuwarejesha Barbara, Rweyemamu ambaye hivi sasa yupo Kikosi B na aliyekuwa Mkurugenzi wa bodi ya wawekezaji ambaye alijiengua Nkwabi.

Try Again ambaye wameungana na Mangungu kumuhujumu Mo Dewj, nao hawako nyuma. Wanatumia turufu yao ya ‘ujanja wa mjini’ kuhakikisha Mo Dewj anang’oka Simba kwa namna yoyote!

Inaarifiwa hata agizo la kuanza upya kwa mchakato wa uendeshaji wa kisasa wa timu umechagizwa na ‘connection’ za Try Again pamoja na S.S.B na mpaka hivi sasa mpango wao ‘umetiki’.

Je, nani ataibuka mshindi katika vita hii? Ni ‘watoto wa mjini’ Salim Abdallah, Try again au tajiri Mo Dewj?

Ni mimi na chanzo changu nyeti,

Nifah.
binafsi naitaza hivi!


simba wamedisclose some informations ili kuleta gilibu kwenye daby ya kko tarehe20, mean watu wafocus kwenye discussion za Mangunga, na mo wasahau ajenda ya msingi..



hizi wanaita siasa za mpira ni sawa na siasa za nchi tu kama mnajambo fulani so hot! kunatengezwa jambo jingine na vile waandishi wanapenda kudandia kwa mbeleee woote wanahama then mambo yanabalance kuja kurudi mambo yamepita....



cha msingi now tufocus kwenye match ya Deby then tukimalizana huko tuje sasa tujue nani ni nani!? hayo mambo yameanza mda, kwanza alianza msemaji simba, 'ohooo wanaokwenda uwanjani wawe na Roho ngumu', hatujakaa sawa, akaja mshabiki mmoja akasema timu imeachiwa msemaji, viongozi wameenda Dubai, ikatrend kidg ikaonekana imevubaa ikaja kwamba tarehe 20, baada ya match simba hata ikifungwa 1 mashabiki na viongozi wanakikao wakiwa uwanjani, hatujakaa sawa wanakuja na hii tena.....


anyway tujipe mda tarehe 20 c mbali wanasimba wana jambo lao, kwa matokeo yoyote yale tuwe na subra. cha kuzingatia tumalizie match, kwamba simba inatafuta kushinda na yanga inatafuta ubingwa match moja malengo tofauti ....



kwa hyo kwa sasa viongozi wa simba wasiwazubaishe wanachama wala yanga wasizubae kwa taarifa za mitandao na kuwa ajenda ya kila mmoja ibaki kwenye reli baada ya tarehe 20 saa1 jioni sasa tuje tujadili ajenda zote hapo juu


Mr
Bon
 
Try again amesha jiuzuru nyazifa alizonazo simba na mwanamama amerudi

Nazani kikao kilicho fanyika ktk ofisi za mo kilieleza haya

Alipost pia ktk IG yake

Kama kumbukumbu zangu zipo sawa lakini... una weza jirizisha pia kupitia IG ya muwekezaji
 
Ukweli ni kwamba kama sio SSB kupewa Simba basi bado mtaendelea kumuhitaji Dewj pamoja na drama zake zote hizo.
Hili halipingiki ila
SSB tayari ana Azam FC

Lakini kama ni kweli ameweka nia ya kuwepo simba basi kuna mpango anao wa kukwepa hicho kikwazo cha umiliki wa Azam Fc

Kwa mara ya kwanza naomba timu yangu ifungwe ili ilete chachu ya mabadiliko maana tukishinda hapa tena lawama robo fainali ijayo kama tutafika😁👍🏽
 
Hataweza mbele ya serikali? Serikali ndio imetoa agizo hilo, mchakato ukianza anarudishiwa pesa zake aanze upya.
Bakheresa ana miliki timu tayari ambayo ni azam sheria za fifa haziruhusu iko kitu ni kosa

Washabiki na viongozi wa wanajaribu kutumia short cut kutatua changamoto zao kitu ambacho sio sahihi
 
Mo hisa zake kwa hiari yake atauza ila huwezi mlazimisha
Mkuu unaelewa taratibu sana. Ngoja nikufafanulie kwa mara ya mwisho…

Serikali wameagiza kuanza kwa mchakato mpya, kwa maana hiyo mchakato uliompatia hisa 49% Mo ni batili, hivyo endapo mchakato mpya utaanzishwa ni kwamba Mo atarudishiwa fedha zake alizotoa kwa ajili ya kununua hizo hisa zake.

Hapa suala sio la hiyari ya Mo tena endapo mchakato mpya utaanzishwa, ndio maana yeye kwa kulitambua hilo anafanya awezavyo ili kuzuia mchakato kuanza upya. Ndio hii mechi ya Yanga sasa inapokuja…

Kama hujaelewa basi tena, good day.
 
Hili halipingiki ila
SSB tayari ana Azam FC

Lakini kama ni kweli ameweka nia ya kuwepo simba basi kuna mpango anao wa kukwepa hicho kikwazo cha umiliki wa Azam Fc

Kwa mara ya kwanza naomba timu yangu ifungwe ili ilete chachu ya mabadiliko maana tukishinda hapa tena lawama robo fainali ijayo kama tutafika😁👍🏽
Mmiliki wa Azam ni mtoto
Miliki wa simba muwekezaji ni baba (kama atakuwa) sizani kama kuna shida

Ni kama umiliki wa timu za taasisi
Timu za jkt
Timu za jwtz huko daraja la kwanza zimejaa
Timu za polisi zipo polisi dom, polisi moro, polisi dsm
Magereza pia wanazo mikoani kama magereza musoma

Timu za halmashauri kama ilivyokuwa timu za kurugenzi (wakurugenzi wa halmashauri)

Timu za ujenzi

Timu za shirika moja la relic Yani reli kigoma, reli morogoro

Nazani kwetu ni kawaida

Pia ndg kumiliki timu ni jambo la kawaida, pale Congo dr kuna Katumbi na ndg yake wana miliki timu na zipo Ligi kuu

Salzburg RB, RB reipzig na RB zingine ni mifano ya umiliki wa taasisi moja au shabihishi
 
binafsi naitaza hivi!


simba wamedisclose some informations ili kuleta gilibu kwenye daby ya kko tarehe20, mean watu wafocus kwenye discussion za Mangunga, na mo wasahau ajenda ya msingi..



hizi wanaita siasa za mpira ni sawa na siasa za nchi tu kama mnajambo fulani so hot! kunatengezwa jambo jingine na vile waandishi wanapenda kudandia kwa mbeleee woote wanahama then mambo yanabalance kuja kurudi mambo yamepita....



cha msingi now tufocus kwenye match ya Deby then tukimalizana huko tuje sasa tujue nani ni nani!? hayo mambo yameanza mda, kwanza alianza msemaji simba, 'ohooo wanaokwenda uwanjani wawe na Roho ngumu', hatujakaa sawa, akaja mshabiki mmoja akasema timu imeachiwa msemaji, viongozi wameenda Dubai, ikatrend kidg ikaonekana imevubaa ikaja kwamba tarehe 20, baada ya match simba hata ikifungwa 1 mashabiki na viongozi wanakikao wakiwa uwanjani, hatujakaa sawa wanakuja na hii tena.....


anyway tujipe mda tarehe 20 c mbali wanasimba wana jambo lao, kwa matokeo yoyote yale tuwe na subra. cha kuzingatia tumalizie match, kwamba simba inatafuta kushinda na yanga inatafuta ubingwa match moja malengo tofauti ....



kwa hyo kwa sasa viongozi wa simba wasiwazubaishe wanachama wala yanga wasizubae kwa taarifa za mitandao na kuwa ajenda ya kila mmoja ibaki kwenye reli baada ya tarehe 20 saa1 jioni sasa tuje tujadili ajenda zote hapo juu


Mr
Bon
Hakuna tatizo wewe kuwa na mtazamo tofauti Mkuu, ni sawa kabisa.
 
Back
Top Bottom