Sallam athibitisha Harmonize kujiondoa WCB

Sallam athibitisha Harmonize kujiondoa WCB

Nampongeza sana,ndivyo inavyotakiwa kwa mpambanaji yeyote.Cha muhimu ni kujipanga tu.Unakuta mtu ameajiriwa tangu abalehe hadi uzeeni...yeye kuita wenzake boss tu.Inatakiwa ifike mahali na wewe ujisimamie mwenyewe uwe CEO kwenye kampuni yako.Nampa pongezi sana na si ajabu akafika mbali zaidi,cha muhimu ni mkakati aliojiwekea.
 
Wasanii wa TZ ambacho hawaelewi mpaka sasa hivi ni kwamba mziki wa kizazi hiki,muziki wa awamu hii hauhitaji uwe na KIPAJI peke ake kama anavyodhani HARMONIZE..mziki wa sasa hivi unahitaji KIPAJI + KIKI(pesa) ya kuufikisha kwenye PEAK.

Harmonize yawezekana amejiona kipaji anacho na Kiki anaweza...kwa haraka haraka tu Harmonize akiniambia ana kipaji cha kuimba kuliko hata DIAMOND naweza nikamkubalia 100% ila kamwe hawezi niambia ana uwezo wa KIKI za DIAMOND,ki ufupi diamond WCB ndio nyumba ya KIKI...

WCB wanapitwa vipaji na vijana wengi tu nnje ya WCB ila kinachofanya WCB ibaki on PEAK ni nyumba ya kiki yaan diamond ndio matofali,nguzo,mpk bati...kujitenga na DIAMOND utakua umebaki na KIPAJI ila KIKI huwezi tena,maisha ya KIKI anayaweza DIAMOND ndio mana anaweza maliza mwaka mzima hajatoa nyimbo ila Jina lake halikauki midomoni mwa watu.

Sasa HARMONIZE atambue tu kwamba ataondoka na KIPAJI chake ila KIKI kaziacha...akae akigundua hilo mwache ajidanganye na huyo mzungu wake..

Simuombei aanguke nataka atuthibitishie kua anaweza bila WCB.
 
Mkuu achana nae huyo, hawa ndo huwa wanaamini mchezaji ni mkubwa kuliko team... Watu wanaoangalia final product (music) wanaweza kuona kama Harmonize ni mkubwa, ila kiuhalisia bila management ya wcb huyo Harmonize angeendelea kuuza mitumba tandale hadi leo.. Harmonize kakosea sana kubadili management, Kina Sallam hawana issue nyingine kubwa za kuwaingizia kipato zaidi ya kusimamia wasanii wao, wanaspend time yao 100% kwenye music wa wasanii wao, ila hiyo management ya sasa ya Harmonize ni watu ambao tayari wana channel zao za pesa, watakua na muda kidogo wa kusimamia msanii wao, na hapo ndo Harmonize atakapoanza kupotea.. Harmonize Hawezi kuwaingizia pesa zaidi ya wanazoingiza sasa kwenye Miradi yao.
Mbona "Skylight Band" inafanya vizuri? Seba sio meneja mmbaya ni miongoni mwa wadau wakubwa wa huu mziki! Harmonize akikomaa ataendelea kuwa juu!
Seba fitna ya muziki anaijua since anatangaza njia panda clouds fm
 
Well said Mkuu, ila ukweli wa wazi ni kwamba hapa Bongo sijaona lebo nyingine zenye nguvu ukilinganisha na WCB katika kusimamia wasanii, na hili ni tatizo linadidimiza ukuaji wa sanaa ya muziki wa bongo fleva.

Tuna hitaji lebo nyingi zenye nguvu na ushindani. Mfano Harmonize anatoka WCB anaenda lebo ipi?
Hapo kwenye RED naunga mkono kwa 100%! Si kuanzisha label bali label zenye nguvu zitakazotoa wasanii wengi watoa hits na kufanya tasnia yetu kuwa competitive!!! So, Harmonize kama amejipanga sawa sawa na kutaka kuanzisha label yenye nguvu kweli kweli, ya kuweza kushindana na hata kuizidi WCB, itakuwa poa sana lakini kama anatoka kwa hoja tu kwamba hataki kuwa chini ya mtu kwavile yeye ni mkubwa, basi atafeli, kwa sababu hiyo siyo hoja ya msingi hasa ukizangatia hata wasanii wakubwa wa mbele tu na wenyewe wapo chini ya label!! Hoja nyingine labda kama anaona maslahi anayopata ni madogo na anadhani huko aendako atapata maslahi makubwa zaidi, nayo ni hoja ya msingi manake yeye hafanyi muziki kama burudani bali biashara!!
 
Wewe ni kati ya wasioujua muziki lakini una ujuaji mwingi ilhali huna ulijualo.
Unasema Lavalava sio msanii na nyimbo zake hazieleweki? Mimi sio shabiki wa hiyo WCB yenu ila Lavalava ndio msanii wangu bora pale WCB na hizo nyimbo zake unazosema huzielewi ndio nimejua hujui muziki.

Unathubutuje kusema mtu mwenye vibao vitamu kama Bora Tuachane, Utatulia, Go Gaga na wimbo wangu bora wa muda wote kwa Lavalava, Kilio sio msanii?
Wewe jamaa umejua kuniharibia asubuhi yangu!
Lavalava hamna kitu bhn naww...n lebel tu inambeba yule muimba kaswida
 
Hivi ile lebo ya wcb mmiliki si dayamondi?
Ndugu kama hujui mambo bora ukakaa kimya na huyo harmonize mnaempa kichwa nyie mtakuja kuanza kumuonea huruma wenywe kwa vile hujui ngoja nikwambie kwan WCB Mondi mwenywe akifanya shoo 30% ya pesa aliyoingiza inaenda kwa hao mameneja wa tatu yaani mshahara maana ndo makubaliano yeye harmonize ni nani mpaka asitoe hiyo 30% kwa mameneja na pesa kidogo kwenye mfuko wa lebel kwa Mondi kurudisha pesa zke.

Af watu hamjui uzito wa LEBEL mfano KANYE WEST na mipesa yake yote ile lakini yupo chini ya Jay Z na halalamiki na anakatwa asilimia flani kama kawaida.
Na lebel cku zote huwa zinamashabiki wake mfano tu kwa maono yangu lavalava sio msanii kiviile na nyimbo zake Mara nyingi huwa hazieleweki lakin lakini akitoa ngoma kaa kama siku nne hivi af ingia YouTube uone alivyopata viewers wengi na ndo mashabiki hao wa WCB ndo wanao mpa support wakati huohuo rich mavoko anatoa ngoma kupata 500k ni kwa tabu sana kwa hiyo nachotaka kusema kuwa lebo ina mashabiki wake harmo akiondoka WCB asilimia kubwa atajitenga nao na kuwa maadui wake
 
Kwahiyo ata dayamondi unaweza kuta hana kitu kabisa??
Mkuu acha kabisa kuna siku huyo rayvan kakosa hela ya mafuta kutoka kwake tabata mpaka Mbezi .. Wengi Wa mashabiki wanadanganywa na zile picha za Instagram tu ...


Watu hawawezi amini kuwa rich mavoko licha ya kutoa zile hitsong alikuwa hana hata mia mfukoni na akipata show hao utatu mtakatifu wanachukua cha kwao na Wcb kwa ujumla na kinachobaki ndio anapewa...


Kuna Dogo mmoja diamond alimchukua kutoka Sweden ndio kachukua nafasi ya Moses iyoyo kama dancer instructor Wa wcb, nimekutana nae face to face na anajuta kuingia wcb ... Huyo Dogo ndio kabuni dance styles kwenye nyimbo zote za wcb kuanzia mwaka Jana . nyegezi, tetema, inama n.k ...
 
kweli mzee..wcb ndo ilikua kila kitu kwake sasa amenyea kambi atakua kama mavoko

halafu mbaya media zingine pia haziivi sa cjui nae atafungu radio na tv
So long as ataondoka kwa njia muafaka, Wasafi hawataacha kupiga ngoma zake! Ni ngumu kwa Wasafi kupiga ngoma za Mavoko kwa sababu Mavoko alitoa tuhuma za kunyonywa!! Sasa mtu kama huyo lazima uwe na tahadhali ili kesho na kesho kutwa asije tena akasema Wasafi wanapiga ngoma zangu bila kunilipa!!! Harmonize hawezi kufika huko! Harmonize angependa sana kuondoka WCB lakini bado akiwa na ties na WCB kwa sababu anafahamu potential yake! Na hata kuhusu hizo media ambazo hawaivi; kimsingi "mgomvi" wa hizo media sio Harmonize bali Diamond! Na media za Bongo zilivyo za ajabu, utaona sasa watakavyoanza kumchangamkia Harmonize kama namna ya ku-deal na Diamond! Usishngane ndani ya wiki 2 zijazo baada ya kila kitu kuwa sawa, ukakuta jina la Harmonize linakuzwa pale Clouds kuliko msanii mwingine yeyote!! Hata hivyo, itakuwa ni upepo tu! Kama upepo wa EFM kwa Ruby enzi Ruby anaingia kwenye conflict na Clouds!!
 
Hivi ile lebo ya wcb mmiliki si dayamondi?
Hata kama angekuwa anaimiliki WCB kwa 100%, bado share ya showz lazima iende kwa mameneja wake! Mtoa hoja hakumaanisha mapato ya label ya WCB bali mapato ya shows za Diamond kama msanii, ambae nae yupo managed na hao mameneja watatu!!! Ukiona akina Tale wanaenda na familia zao Ulaya, hayo ni matokeo ya mgao wanaopata kutoka kwenye shows za Diamond!!
 
Kasumba tuliyonayo waswahili kondeboy Ana explore new ventures na opportunities hakina sababu ya kumbana WCB.

Tunahitaji wanamuziki wakubwa Kama nchi za wenzetu . Hongera Sana Harmonenga kwa kuchanja mbuga inshaalah mola akuwekee wepesi.

#Achawoga Kondegang kesho la mtu moko
# Jembejembe tunakuamini usimtose kijana wetu

#Independentisgrowth
 
Mbona "Skylight Band" inafanya vizuri? Seba sio meneja mmbaya ni miongoni mwa wadau wakubwa wa huu mziki! Harmonize akikomaa ataendelea kuwa juu!
Seba fitna ya muziki anaijua since anatangaza njia panda clouds fm
Hiyo skylight band imefika level ya kimataifa? Huyo Seba kamfikisha msanii gani level ya kimataifa? Harmonize alikua amefika level ya kimataifa so tunategemea awe juu zaidi ya hapo, na hilo ndo tunalosubili.
 
Mbona mwishoni umeoeta uchawi mkuu.
Come on mentality gani hio,unadhani dunia ingekua na mentality hio Leo kungekua na jamiiforum?
Haswaa kaanza vzr huko mwisho sasa kaleta uchawi wake kwani Mbona inaonesha km imewauma Sana mmakonde kuondoka na wkt mnajinasibu kaondoka kiustaarabu?
 
Wabongo ni wanafiki tu.

Kipindi kile wasanii wakiachana na CMG au THT tunaambiwa wamejitambua na blah blah kibao ila huyo jamaa kutoka WCB imekuwa nongwa Why?
Sindano imewaingia kinoma hii sindano ni ya kutibia ng'ombe jooh yaani wameumia kinomaa ndo maana wanaweweseka mara oooooh atapotea utazani wao ndo sir God
 
Mkuu achana nae huyo, hawa ndo huwa wanaamini mchezaji ni mkubwa kuliko team... Watu wanaoangalia final product (music) wanaweza kuona kama Harmonize ni mkubwa, ila kiuhalisia bila management ya wcb huyo Harmonize angeendelea kuuza mitumba tandale hadi leo.. Harmonize kakosea sana kubadili management, Kina Sallam hawana issue nyingine kubwa za kuwaingizia kipato zaidi ya kusimamia wasanii wao, wanaspend time yao 100% kwenye music wa wasanii wao, ila hiyo management ya sasa ya Harmonize ni watu ambao tayari wana channel zao za pesa, watakua na muda kidogo wa kusimamia msanii wao, na hapo ndo Harmonize atakapoanza kupotea.. Harmonize Hawezi kuwaingizia pesa zaidi ya wanazoingiza sasa kwenye Miradi yao.
Kwani WCB mama yake mkuu Mbona munaumia Sana?
 
Sasa mkuu, mbona hakushikiwa mtutu kumwaga wino kwenye huo mkataba, si alikubali yeye mwenyewe
mikataba ya kichifu kimangungo. nilishawahi kuratibu event moja ambayo tulimualika mbosso kuja ku perform. dogo alijituma sana stejini mpaka akakaukiwa sauti.

nilihuzunika sana niliposikia licha ya kujituma kwake kote kule, asilimia karibia 70% ya pesa tuliyomlipa ilienda kwa hao jamaa watatu na management ya wasafi.
 
Back
Top Bottom