Sallam SK: Yanga inajua ku-brand wachezaji wao, awachana managers wa wachezaji

Sallam SK: Yanga inajua ku-brand wachezaji wao, awachana managers wa wachezaji

sinza pazuri

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2014
Posts
3,344
Reaction score
9,066
IMG_20250106_000845.jpg


Sallam SK aka Mendez ambaye ni international manager wa Msanii namba moja Africa yani Diamond Platnumz ametoa pongezi jinsi Yanga inavyofanya vizuri kwenye kuwaongezea thamani kwenye chapa zao wachezaji wake au kwa lugha nyingine branding.

Sallam SK ambaye pia ni mdau mkubwa wa soka ambaye alishafanya hapo nyuma kazi ya kuwatafutia masoko nje ya nchi wachezaji wa kiafrica, ameendelea kusema kuwa mameneja wa wachezaji wa kitanzania wamelala usingizi wa pono.

Nakubaliana na Sallam aka Jorge Mendez Wa bongo, wachezaji wetu wengi hawana managers bali wana madalali.
Managers wa TZ utawaona kwenye kipindi cha usajili ndio maana ligi imekuwa kubwa wachezaji wamekuwa mastaa ila huwezi kuta mchezaji ana endorsement ya maana kama za kina Diamond, Zuchu, Mbosso, Rayvanny, Mobetto au Nandy.
 
Dah,

Huyo jamaa aisee.... Ashukuru tu bahati yake kwa Diamond imeenda sawa ila mambo mengine ni vizur angeyaacha tu.

Mchezaji sio celebrity ni performance...

Hizi bla bla aonglee huko huko Insta watu wa maana wasimsikie.
 
Dah,

Huyo jamaa aisee.... Ashukuru tu bahati yake kwa Diamond imeenda sawa ila mambo mengine ni vizur angeyaacha tu.

Mchezaji sio celebrity ni performance...

Hizi bla bla aonglee huko huko Insta watu wa maana wasimsikie.
Wewe upo kwenye kundi la watu wa maana?

Inawezekana humjui Sallam au umemsikia kwa mara ya kwanza kupitia bongofleva.

Labda nikupe tu elimu, mpira ni biashara. Biashara ya mpira haiishii kwenye uwanja. Mchezaji anaweza kuwa tajiri mkubwa kupitia endorsements. Hao kina Messi ni matajiri sababu ya mikataba na makampuni makubwa.

Sallam SK akiongea kuhusu branding ya wachezaji ukae kimya huyo ana hang na kina Drogba, Etoo, Pogba etc kama wewe unavyocheza na wavimba macho wenzio.
 
Wewe upo kwenye kundi la watu wa maana?

Inawezekana humjui Sallam au umemsikia kwa mara ya kwanza kupitia bongofleva.

Labda nikupe tu elimu, mpira ni biashara. Biashara ya mpira haiishii kwenye uwanja. Mchezaji anaweza kuwa tajiri mkubwa kupitia endorsements. Hao kina Messi ni matajiri sababu ya mikataba na makampuni makubwa.

Sallam SK akiongea kuhusu branding ya wachezaji ukae kimya huyo ana hang na kina Drogba, Etoo, Pogba etc kama wewe unavyocheza na wavimba macho wenzio.
Embu nipishe

Alafu acha ku drag fake account kwenye level zako usije aibika..
 
Kipaji na uwezo uwanjani kwanza, mpira sio kama mziki kwamba utaendeshwa kwa skendo sijui umetoka na huyu, sijui kesho umemtukana huyo, haiendi hivyo.

Ronaldo na Messi wamefanya makubwa kwenye timu zao za taifa na vilabu walivyopitia.
Kwa hapa Tz mfano ni Mayele, alikua anauzika na kukubalika kwasababu ya kutupia magoli.

Kiwango kikishuka hata ulete drama za namna gani brand itashuka tuu. Ni kama Baloteli, alikua bonge la mchezaji, akakubalika mbaya mbovu, alivyoanza kuzingua kwenye pitch tu ule ustar wake ukaanza kupungua..

Messi na Ronaldo wanatajwa mpaka leo ni kwa namba zao huko walikotoka, wakishaachana na mpira ule unaarufu utapungua tuu maana hawakuoni ndani ya pitch.

Tofauti na celebrities wa muziki, dance au maigizo, hawa uongo uongo mwingi na sanaa kibao ila mpira ni mchezo wa wazi ukizingua fanbase inashuka.
 
Kipaji na uwezo uwanjani kwanza, mpira sio kama mziki kwamba utaendeshwa kwa skendo sijui umetoka na huyu, sijui kesho umemtukana huyo, haiendi hivyo.

Ronaldo na Messi wamefanya makubwa kwenye timu zao za taifa na vilabu walivyopitia.
Kwa hapa Tz mfano ni Mayele, alikua anauzika na kukubalika kwasababu ya kutupia magoli.

Kiwango kikishuka hata ulete drama za namna gani brand itashuka tuu. Ni kama Baloteli, alikua bonge la mchezaji, akakubalika mbaya mbovu, alivyoanza kuzingua kwenye pitch tu ule ustar wake ukaanza kupungua..

Messi na Ronaldo wanatajwa mpaka leo ni kwa namba zao huko walikotoka, wakishaachana na mpira ule unaarufu utapungua tuu maana hawakuoni ndani ya pitch.

Tofauti na celebrities wa muziki, dance au maigizo, hawa uongo uongo mwingi na sanaa kibao ila mpira ni mchezo wa wazi ukizingua fanbase inashuka.
Unaelewa maana ya branding?

Kwa hiyo kwa uelewa wako branding inafanyika kwa wanamuziki tu?

Nakuelewesha kwa kifupi, mchezaji kama Neymar analipwa mshahara mkubwa lakini brand yake nje ya uwanja imempa utajiri mkubwa kupitia endorsements za Puma, Redbull na Beats by Dre.

Branding kwa mchezaji inafanyika ndani ya uwanja na nje ya uwanja ndio maana unaona baadhi ya wachezaji siku wanapigania kuwa na social media power sababu wameshastuka kuna pesa nyingi sana nje ya uwanja.

Mayele alifanikiwa sana kujibrand ndani ya uwanja kwa style yake ya ushangiliaji lakini nje ya uwanja hakuwa na impact kibishara.

Anachosema Sallam ni wachezaji na managers wao kufikiria namna ya kuzipata pesa za makampuni makubwa zipo nyingi sana zinahitaji watu smart kuzipata.
 
Back
Top Bottom