Salma Kikwete apongezwe, amesaidia Wenza maskini wa Wastaafu. Historia itamkumbuka

Salma Kikwete apongezwe, amesaidia Wenza maskini wa Wastaafu. Historia itamkumbuka

Salma Kikwete alaaniwe kwa kuwa mwanamke mroho,mbinafsi na mwenye roho mbaya,alaaniwe yeye na uzao wake wote
 
Kifafanuacho wafu mbele ya Mungu, si cheo kikubwa, si daraja , si sifa
matendo mema yataufungua mlango wa mbingu.

ukija duniani unatafuta , unatumia, unaviacha
Mungu hapa ndipo alicheza hasa, huondoki na chochotee
 
Super? sababu amekupa interview sio, ni sawa pia unavyomsifia Makamba sababu wanakupa interview.

Unalipwa kiasi gani kutetea huu ujinga? Wewe ni objective, serious journalist?
Mkuu ruaharuaha , she is super for the contents, umesikiliza contents au umeishia kukodolea shavu dodo na ile baby face?.

Mimi ni mwandishi wa kujitegemea kwa kujitolea, silipwi na yeyote, uandishi na utangazaji naufanya bure kabisa just for the love of it!.

P
 
Kifafanuacho wafu mbele ya Mungu, si cheo kikubwa, si daraja , si sifa
matendo mema yataufungua mlango wa mbingu.

ukija duniani unatafuta , unatumia, unaviacha
Mungu hapa ndipo alicheza hasa, huondoki na chochotee
Sahihi vingine hata hutavifaidi .mtu awaye yeyote hata apewe bilioni kwa mwezi mifisadi mingi na mikwapua pesa za wanyonge au za umma au kuonea wanyonge kwa rushwa nk au kula kodi za walalahoi inaunwa kuanzia visukari na migonjwa kibao na haiwezi kula chakula kitamu chenye sukari,chumvi au mafuta ,nyama nzuri red meat nk Mwenyezi Mungu kawavizia kawatenda kitu kibaya na mamilioni na mabilioni yao chakula tu chenye chumvi,mafuta au sukari hakipandi wakati lofa anaweza bugia chumvi au sukari kavu bila kuunga mboga yuko fresh tu au chakula aweza kula chenye mafuta kibao na yuko fresh tu

Mungu kawapiga marufuku kula vitamu na mabilioni yao wanakula chukuchuku na miradhi kibao juu Hiyo mipesa hata hawafaidi

Lofa na elfu 3 yake kwa siku anafaidi afya safi,chumvi ruksa,sukari ruksa ,mafuta ruksa ,red meat ruksa nk

Mungu fundi Mwacheni Mungu aitwe Mungu
 
Mkuu ruaharuaha , she is super for the contents, umesikiliza contents au umeishia kukodolea shavu dodo na ile baby face?.

Mimi ni mwandishi wa kujitegemea kwa kujitolea, silipwi na yeyote, uandishi na utangazaji naufanya bure kabisa just for the love of it!.

P

Hahaha, Shavu tena! Pascal jikite kwenye hii topic ya mleta mada Jaji mfawidhi. Usikwepe swali maswali ya wadau.

Contents mmezungumzia mambo mengi mengine hadi kuhusu uhusiano wao. Sisi hayatuhusu.

Maoni yako ni yapi kuhusu hii topic? Jikite kwenye muswada wake.
 
Hahaha, Shavu tena! Nazungumzia hii topic ya mleta mada Jaji mfawidhi.

Contents mmezungumzia mambo mengi mengine hadi kuhusu uhusiano wao. Sisi hayatuhusu.

Maoni yako ni yapi kuhusu hii topic? Jikite kwenye muswada wake.
Sahihi ulichosema

Maoni yake atoe Pascal Mayala kwenye hoja iliyopo
 
Salma Kikwete ambaye ni Mwalimu Mstaafu wa Oystrbay Primary, Mbunge huko Mtwara na pia Mmiliki. wa WAMA -NGO ya Kitajiri:

Wenza ni :
1. Maria Nyerere.
2. Siti Mwinyi.
3 Anna Mkapa.
4. Salma Kikwete
5. Janeth Magufuli


Bunge lijalo , kama atatokea kiongozi mwengine basi ipendekezwe na watoto wa wastaafu wapewe mafao, baba zao na mama zao wametumikia nchi, wametumia muda mwingi kufikiria taidfa na kuliongoza taifa.

Kifungu kipya cha 13 ambapo makamu wa rais anapofariki akiwa madarakani, au baada ya kustaafu (kabla hajalipwa mafao yake), wategemezi wake (dependants) watalipwa kiasi cha fedha sawa na mshahara wote wa makamu wa rais alioupokea wakati akiwa madarakani. Mfano, kama makamu wa rais alikaa madarakani kwa miaka 10, akalipwa TZS 2B kama mshahara, basi wategemezi wake watalipwa kiasi hiko cha TZS 2B kama pension. Ifahamike, kwa mujibu wa sheria hii, neno "dependants" limefafanuliwa kwenye kifungu cha 4, na maana yake ni mke au wake, mume, watoto (ambao walikuwa ni tegemezi kwa marehemu), pamoja na wazazi wa marehemu (wategemezi).
Badiliko la JEDWALI la sheria hii linalotaja nyongeza ya mafao ya viongozi.

1. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka magari 2, sasa atapata magari 3 yasiyopungua uzito wa tani 3 (yaani hawezi pewa Corola, bali ni gari kubwa kama V8 ,vxr nk, ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.

2. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 2 na sasa atapewa 3.

3. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.

4. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.

5. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.

6. Makamu wa Rais atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.

7. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Makamu wa Rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama Makamu wa Rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.

8. Makamu wa Rais atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.

9. Waziri Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.

10. Warizi Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.

11. Waziri Mkuu mstaafu atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.

12. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Waziri Mkuu mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake atakapofariki.

13. Waziri Mkuu atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.

14. Mjane wa Rais mstaafu, kwa sheria ya sasa anapata 40% ya mshahara wa rais aliye madarakani kila mwezi kama "maintenance allowance", asilimia hii imepanda sasa atalipwa 60%.

15. Sheria ya sasa inatoa gharama za matibabu kwa mjane wa Rais mstaafu kwenye hospitali za ndani ya nchi tu, lakini badiliko la sheria mpya, atalipiwa na Serikali matibabu ya hospitali za nje ya nchi pia.

16. Mjane wa Rais mstaafu ameongezewa huduma za gari toka gari moja mpaka magari mawili, na dereva 2 kufanya shughuli zake za kila siku. Serikali inalipia gharama za mafuta pia. Magari haya yatakuwa yanabadilishwa kila baada ya miaka 5. Pia, ameongezewa mpishi, mfua nguo na mtunza bustani. Atapata ulinzi wa TISS.

17. Mjane wa Makamu wa Rais, anapata stahiki kama za mjane wa rais isipokuwa tofauti yake ni moja, yeye atapata gari moja la Serikali na dereva mmoja.

18. Mjane wa Waziri Mkuu mstaafu anapata stahiki za ziada kama mjane wa Makamu wa Rais, isipokuwa gari analotumia la Serikali litakuwa linabadilishwa kila baada ya miaka 7.

19. Hili ni badiliko linalohusu Waziri, Naibu Waziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wastaafu ambapo watapata ziada ya mafao yao: wind-up allowance, Diplomatic passport kwao na wenza wao, gari moja ambalo atapewa jipya kila baada ya miaka 5, Ulinzi wa TISS, Msaidizi mmoja, Bima ya Afya bure yeye na mwenza wake, Matumizi ya VIP lounge.

20. Hii ni nyongeza kwa Spika wa Bunge kwenye mafao yake: gari moja, Bima ya Afya yake binafsi, matumizi ya VIP lounge, pia anapata stahiki nyingine kama LITA 70 za mafuta kwa wiki.

NOTE: Pongezi kwa Wenza, walikuwa wanaishi kimaskini Sana !

View: https://www.youtube.com/watch?v=fYGKoLzTWRg
View attachment 2814342

Mama Salma kaupiga mwingi. Anastahili pongezi kwa kuwapigania wanyonge. Wabunge wa aina hii ndio wanatakiwa wawe wengi kule mjengoni ili kuharakisha maendeleo ya wananchi. Safi sana
 
Hongera Salma Kikwete bado watoto wenu waongezwe humooo.....umewasahau....low IQ sana na milelee
Mungu hataniwi hata Siku moja na sio mtani wa yeyote duniani na hatarqjii kuwa mtani wa yeyote kodi za wanyonge ziheshimiwe

Sio kisa tu mtu ana mamlaka anatakodi zote ziende kwake na familia yake

Mungu ana tabia ya upole lakini pia ni mkali na mkorofi kwa wakorofi waonea kodi za wanyonge kisa tu wana position juu
 
Hastahili pongezi yoyote uongozi kwa Tanzania imegeuka ajira yenye kipato kinono.

Licha ya yeye kuwa mbunge na atapata kiinua mgongo cha ubunge , bado miradi na biashara zingine nyingi za pembeni bado anadai mafao.

Wake wa hao marais wamekua n mifuko mingi na miradi mingi ambayo 'accountability ' ya fedha za mifuko hiyo hakuna anayehoji.

Ila sishangai asilimia kubwa ya wanaowaongoza ni wajinga ndio maana maonyesho ya kupanda trekta, punda na ngamia yanachukua kurasa za mbele huku nchin ikiwa kwenye lindi zito la umasikini.
 
Hakika. Tunawajibika kupambania haki.

Kitu kingine, kwa wenye wake wawili kama mwinyi na ghalibu bilal sijui wake wote wawili watalipwa!
Ndio, wake wanatambuliwa wanne, kwa wenye imani ya Kiislamu, kwa wakristu ni mke mmoja kama una suria huyo utamhusumia kwa fedha za posho za safari.
 
Kuna siku Raisi Mama Samia aliwahi fokea Watendaji kuwa mihela yote mnaiba mtaenda nayo peponi?

Haya hiyo mifao yote umiza walipa kodi aliyopigania Mama Kikwete kuanzia yeye na wengine wataenda nayo peponi? Mihela kibao hiyo loo .
 
Mungu hataniwi hata Siku sio mtani wa yeyote duniani na hatarqjii kuwa mtani wa yeyote kodi za wanyonge ziheshimiwe

Sio kisa tu mtu ana mamlaka anatakodi zote ziende kwake na familia yake

Mungu ana tabia ya upole lakini pia ni mkali na mkorofi kwa wakorofi waonea kodi za wanyonge kisa tu wana position juu
Tag Salima Babu Seya ......atakujibuu
 
Back
Top Bottom