Salome Makamba aomba Serikali itumie magari ya "Washawasha" kuwaondoa Wamasai Ngorongoro badala ya kudhibiti Wapinzani

Wamasai wanalo...!!
Kufuata historia, je? Ni Wamaasai wameingilia hifadhi ya wanyama au wanyama waliwakuta Wamaasai pale?
Mbona hili jambo limeshikiliwa kidedea leo?
Hapa kuna siri kubwa. Kama kipindi cha mtawala fulani walijenga kwenye njia ya Tembo!! Kwanini tusiamini hata sasa kuna mtawala ana taka eneo???
 
Naanza kuamini kuwa hili sakata la Ngorongoro lina yaliyojificha nyuma ya pazia.
Kwanza kabisa, tukubali lipo tatizo la Uhifadhi Ngorongoro.
Tena tatizo kubwa.
Tatizo lenyewe ni Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Siyo Wafugaji wa Kimasai.
Nguvu ya rushwa inahamishia tatizo kwa Wafugaji, badala ya kulielekeza kwa Mamlaka ya Hifadhi.
Kwa nini?
Mbuga inayoingiza takriban Shs. Bilioni 150 kila mwaka, kwa nini wenyeji wa mbuga hiyo waishi kwa mashaka?
Wenyeji wa Hifadhi hiyo ni Wafugaji na Wanyamapori.
Kwa nini ishindikane kuboresha mazingira wakati kila mwaka pesa nyingi zinapatikana?
Let us focus on the corruption and inefficiencies of Ngorongoro Conservation Authority.
Kelele zote hizi zinaelekezwa kwa Wafugaji na rushwa inayotolewa na Viongozi wa Mamlaka.
Ambao wametoa Vibali haramu vya Ujenzi ndani ya Hifadhi.
Watanzania, tufumbueni macho tuone uhalisia.
 
Huyu amekosa Busara..., mara zote hususan katika jambo ambalo wananchi wenyewe ndio walinzi sio vema kutumia mabavu..., cha maana ni kutoa knowledge ili waelewe wenyewe wataondoka na kulinda wenzao zaidi wasichafue....

Let them know manufaa ya hio hifadhi na wafanye wawe wanufaika wa hio hifadhi (sasa kama faida yote wanakula wachache unategemea nini)?

Kuliko gharama za kupeleka magari wawatafutie sehemu bora zaidi kuliko hio (win win for all)
 
Daaaah ndo wabunge tulionao bungenii kwakuwa hili jambo halimgusi yeye walaaa jamiii yake moja kwa moja atasema watolewe hata kwa mtutuuuu sasaa ila lingekuwa linamgusa yy asingesema ivoooo
 
Wamasai wamewakosea nini?
 
Posho mkuu
 
Yaan wanasiasa!

 
Huo ni uonevu maasai ni sehemu ya utalii pia, pili masaai Ali nyama pori sioni athari ya yeye kukaa hifadhini.
 
Usikute kuna mwarabu anatembeza mpunga kama enzi zile za Mwinyi maana wengine muhimu kwao Pesa.
 
Njia pekee ni kuwapunguza idadi yao Ili waendane na ecologia tena kiungwana kwa kuwapeleka maeneo mengine salama.
 
Mmaasai akakae ghorofani😁😆 na MBUSI inakaa wapi?
Ugolo na mate atawatemea mpaka nawaonea huruma, kisha huwa wanakojoa popote Tu! Shuka pembeni ananyunyuzia, nawaza akiwa ghorofani!😆😁
 
Kuna wajanja wananufaika na uwepo wa wamasai
Kuna wajanja watanufaika ikiwa wamasai wataondolewa Ngorongoro...Kuna watu wanaplan kwenda kujenga mahoteli yao pale kwa kuwa ni ngumu mmsai kuuza kipande Cha ardhi yao ya urithi kutoka kwa mababu zao.
 
hii nchi ina wabunge waajabu sana , yaani wamasai ni wanyama kama wanyama wengine tu lakini bado watu wanashupaza shingo eti wawaondoe , uliona wapi mtu anapishana na simba ama tembo na hawadhuriani? wanaweza kulazimisha kuwaondoa hao masai ikawa ndio mwisho wa hiyo crater. Kuwa fisiemu kunahitaji ngozi ngumu sana , imagine anaweza akaja mbunge mmoja siku moja akaamua kuleta hoja kuwa serikali itumie nguvu kwa watu flani wabadilishe dini ama kabila na wakamshangilia.
 
Na chadema miaka mingi walikuwa wanatoa solution ya matatizo.

Lkn sasa wapo kimyaa ndipo wananchi watatia akili.

Sasa wananchi hawana wa kuwasemea
 
ha ha ha ,haya bana ,watu tunataka bwawa lianze kufua umeme,wanatuhamisha mawazo na wamasai .
 
Serikali haiwezi ua 80% ya kabila la raia wake. Hakuna jamii ya watu fulani eneo fulani inaweza pigana na serikali na ikashinda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…