Uchaguzi 2020 Salum Jecha Mwenyezi Mungu hataniwi, umelipwa kwa kadri ya matendo yako, sasa subiri makubwa zaidi

Uchaguzi 2020 Salum Jecha Mwenyezi Mungu hataniwi, umelipwa kwa kadri ya matendo yako, sasa subiri makubwa zaidi

Jecha mwamwonea bure! Alitekeleza maamuzi kutoka juu. Katika chaguzi za Zanzibar hilo ni kawaida, CCM haijawahi shinda hata siku moja.
Jecha anaonekana sana kuliko wengine waliokatwa, kwakuwa alimbeba shein na kumpa haki asiyostahili.
Hivyo alitazamia kubebwa pia, na tulitazamia mumbebe.
 
Jecha amefanya kosa kubwa sana la kudhalilisha Urais wa Dkt. Shein. Kitendo cha yeye kuchukua fomu ilhali yeye ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ambaye ndiye aliyetoa maamuzi ya kufuta uchaguzi, yamepeleka taarifa mbaya kwa wananchi kuwa alifanya hivyo kulinda maslahi ya chama chake cha ccm.

Na hilo ni kosa kubwa sana kushusha hadhi ya Rais. Hivyo hakustahili hata kujadiliwa hata kidogo, na jambo la kwanza lingetakiwa kuchana fomu yake bila hata ya kuikagua.
 
😀😀😀
Sasa mnatunga mnayotamani yangetokea.. chadrama nyie hamukomi.. uliyoyaandika yameonyesha uongo.. kufikiri utawachonganisha.. kisa bado unaumia kwa kile.. unafikiri kilitokea huko nyuma.. pole sana.. ila acha kutunga
 
Wengine hawakuipigania CCM kiwango cha Jecha, kweli CCM shukran yenu ni mateke.
Kwa hiyo shida yenu ni maendeleo au kuwapa shukurani watu waliopaginia chama bila kuzingatia uwezo wao wa kuwaongoza wananchi na kuleta maendeleo?
 
Umemuelewa lkn mtoa mada?? Yaani wote walijadiliwa mmoja mmoja ispokuwa Jecha kwani lilipotajwa tu jiana lake moja kwa moja likatupwa kapuni bila hata Wajumbe kutia neno.
Hana ushahidi wowote kuthibitisha madai yake.
 
Tulikuonya mapema sana kwamba Shetani hajawahi kuwa na rafiki, ukatuona wajinga lakini taarifa za siri kutoka kwenye kikao cha CCM Zanzibar cha kuchuja wagombea wa urais wa Zanzibar, jina lako limekatwa kinyama bila hata kujadiliwa, wewe Jecha ndio mtu wa kwanza kufyekwa bila huruma.

Mwenyekiti wa kikao hicho kilichokuchinjia baharini ni yuleyule Shein uliyembeba kwa mbeleko ya chuma bila aibu wala soni, sasa subiri kudhalilika zaidi.

View attachment 1497856
Na bado yajayo yanayokuja yamtamfurahisha.
 
Hangaika na ya kwenu chadema Zanzibar hata wanachama hamna ya wazanzibari waachieni wenyewe nyie pambaneni na hali zenu.

Chadema kimekimbiwa Hadi mitandaoni mumemebaki watu msiozidi wanne ndio more active wewe ,salary slip , my son drink water na tindo.
Jipe moyo . Ipo ndani ya mioyo ya watu [emoji120]
 
Zanzibar wana huruma sana, huyo bado yuko hai? Na hapo alipo familia iko salama tu!!!!!!! Duh wazanzibar mna moyo sana. Yuko hai????
 
Back
Top Bottom