Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Afu mi ili nifaidi napikaga sato mkubwa na kiugali kidogo japo ugali matonge mawili nakula
farkhina ahsante yani samaki napenda sana kwa wiki zaidi ya mara 3 lazima nile ila si wajua usela sina oven so nampika kama unavyosema ila simgril anakuwa mbichi na mtamu balaa.Watu wanashangaaga kwa nini mbichi afu hana shombo?ha ha ha mapishi mwaya.
Shem wako juzi kaniambia kanunua oven yani atanikoma mapishi na hivi apenda kula mapenzi yatazidi wallah atatangaza ndoa lol
Hahahahahahaahaha na ugali wako taratibu....
Heaven on Earth amu Swts Ennie Chocs mimi49 BAK MziziMkavu Jawilat SHERRIF ARPAIO King'asti Ablessed Angel Nylon Fixed Point Valentina Jerrymsigwa [MENTION=16433] measkron Afro-Arabica Mrs Kharusy.na wengine...
Hahahaha unapenda sana samaki..
aki ya mama wadafa bwana mnatupatia sana kwenye menu..farkhina ahsante yani samaki napenda sana kwa wiki zaidi ya mara 3 lazima nile ila si wajua usela sina oven so nampika kama unavyosema ila simgril anakuwa mbichi na mtamu balaa.Watu wanashangaaga kwa nini mbichi afu hana shombo?ha ha ha mapishi mwaya.
Shem wako juzi kaniambia kanunua oven yani atanikoma mapishi na hivi apenda kula mapenzi yatazidi wallah atatangaza ndoa lol
Jamani, apa vp? Duuuh.
Habibty unatisha kwa mapishi. MashAllah
Siku zingine hata ugali sili samaki tu tena bakhresa katurahishia nazi zake nzuri sana
aki ya mama wadafa bwana mnatupatia sana kwenye menu..
Huna haja ya kukuna nazi kwa raha zako......
Heaven on Earth amu Swts Ennie Chocs mimi49 BAK MziziMkavu Jawilat SHERRIF ARPAIO King'asti Ablessed Angel Nylon Fixed Point Valentina Jerrymsigwa [MENTION=16433] measkron Afro-Arabica Mrs Kharusy.na wengine...
yaani dia mie nimeenda sokoni nshanunua 3 napikia mojamoja chakula cha peke yangu nishanunua njegere za kesho,maharagwe ninayo ndani yaani kwa kweli bakhresa amesaidia sana.Karibu maini rost na spagheti natamani kuweka recipe ila nasikia uvivu nkiwa fresh nitarusha hewani.
Mambo supaa........kwa ugali huyo na pilipili hizo mh mhu!!
shukran farkhina.samaki wa mishkaki ni msosi niupendao sana ila sijui huwa mnapikaje.hapo juice ya Hanjal lazima ihusike
Kumbe nawe ni mpenzi wa ugali eeh!!!! tena kwa samaki.
Mahitaji
1)Samaki mkubwa...
2)nyanya 2..
3)kitunguu thomu 1 teaspoon..
4)tangawizi 1 teaspoon
5)bizari ya njano kiasi
6)bizari ya pilau 1 teaspoon...
7)ndimu 2...
8)kitunguu maji 1..
9)chumvi kiasi
10)pilipili manga 1 teaspoon
11)pilipili mbuzi 1
12)tomato sauce
13)tui la nazi 1-1.5 kikombe...
Namna ya kutaarisha samaki
1)safisha vizuri samaki wako na umeweke alama kwa kisu ili viungo viingie ndani ya samaki..muache akolee viungo for 30minutes
2)weka samaki kwenye trey na umuunge kwa pilipili manga,chumvi,ndimu 1,bizari ya pilau,kitunguu saumu na tangawizi...
3)muweke kwenye oven moto kiasi ili awive vizuri....akiwiva upande mmoja mgeuze upande wa pili...
4)ukishawiva pande zote mbili weka samaki kwenye sahani.....
Namna ya kutaarisha sauce
1)saga nyanya,pilipili mbuzi na kitunguu maji weka maji kidogo sana au unaweza tumia tui badala ya maji..
2)weka tui jikoni,mimina mchanganyiko wako uliosaga,weka na bizari...koroga na wacha vichemke vizuri
3)weka tomato paste kiasi ili sauce iwe nzito nzito...
4)weka ndimu....acha ichemke kwa dakika 5 then epua
5)mimina sauce yako juu ya samaki ulimtaarisha kabla
Samaki wa kupaka (grilled chicken with coconut sauce) tayari kwa kuliwa...
Sasa best kama huna oven,unaweza kumkaanga???
Mpenzi kama una ile grill ya mkono ya kubanika samaki, ni vizuri sana ukamchoma na makaa kwenye seredani. Anakua very taste.
Na hayo ndo mapishi haswa ya kizamani. Sikuizi sema hatuna hayo maseredani ndo mana tunatumia ovens