Samia: 70% wanalinyooshea kidole jeshi la polisi

Samia: 70% wanalinyooshea kidole jeshi la polisi

Hakuna ubishi kwamba wapo Polisi wabaya lakini Pia tusipofushwe macho kwamba Polisi wazuri wapo.

Tatizo la Polisi wanapambana na MAKUNDI makuu mawili Mlalamikaji Kwa upande mmoja na mlalamikiwa Kwa upande wa pili na Kwa vyovyote vile lazima mmoja ashinde na yeyote atakaye shinda lazima atakayeshindwa awachukie Polisi lakini Pia majumu Yao ya kukamata yanaongeza maadui wao kila siku mfano ukimkamata Baba yangu Kwa kosa lolote Lile lazima Mimi na familia nzima tuwachukie Polisi wote. Kwahiyo hakuna wakati wanaweza kuwafurahisha Pande zote na hiyo ndiyo sababu ya kuwachukia na kusingizia kwamba wanabambikiza kesi hovyohovyo.

Sababu nyingine ni Serikali kutokuwekeza Kwa Jeshi la Polisi wakiwaacha watumie fursa za kuombaomba ukitaka mtoto wako awe na TABIA mbaya mruhusi aanze kuishi Kwa kutegemea majirani.

Umeangazia kote huku kabla ya kuandika?

Screenshot_20230131-172039.jpg


Kwani hapo mlalamikiwa na mlalamikaji unawaona hapo?
 
Ukweli usemwe TATIZO sio Jeshi la polisi.
TATIZO ni wale wanaolitumia kuficha maovu Yao .

Polisi ni Kama kuku wa Kienyeji wameachwa wafanye wanavyotaka Kwa sababu mabosi Wao wananufaika na mapungufu ya kisheria na wananchi kutojua Haki ZAO.

SERIKALI iliyojaa rushwa kule JUU Siku zote inawapumbaza wananchi Kwa kupambana na virushwa uchwara vya polisi.

Ukitaka Ujue ni Vipi polisi wanafanya KAZI ZAO Angalia aina ya viongozi wanaopandishwa vyeo na kuwa makamishna . Wengi ni wale Wenye sifa ya kupenda anasa ,rushwa ,ngono na Ulevi. Sasa wanalewaje Kila Siku na anasa kama SIO michongo na madili ya rushwa na magendo au kushirikiana na Wahalifu. ?

Wengi ni ZAO la CCM na SERIKALI yake katika kubebena wakati Wa Uchaguzi.
Ni Vipi mabosi wanaohamasisha kuandika Faini tuu Badala ya KUTOA elimu Barabarani waweze kuwafanya askari wasilalamikiwe. Mbona Taasisi nyingine Kuna rushwa kubwa sana Lakini hakuna kelele. Jibu ni kuwa polisi wanakula rushwa lakini pia wanaosimamia Sheria zote za Nchi Hali inayosababisha Kila MTU akutane na polisi KWENYE matukio yote.

Hata hivyo tuache unafiki . Kama Kweli SERIKALI Iko sirias kulibadili Jeshi la polisi Jambo la kwanza ni kuliondoa KWENYE Médani za kijeshi na kuwa ni watoa huduma Kama walivyo watumishi WENGINE mana wanakutana na watu Wenye mahitaji mbalimblia SIO Wahalifu tuu.

Huwezi kubadili Hulka za polisi wakati mafunzo Yao ni ya kibabe ,kikatili,kujuana ,rushwa , Bila kujali kuwa wanakwenda kuwahudumia watu Wa aina zote ikiwemo Watoto na wazee. Unakuta polisi anampiga vibao na mateke mtoto Wa Miaka Mitano kisa ameletwa na mama yake kuwa hataki Shule . Chanzo ni mafunzo yaliyojaa ukorofi Badala ya KUTOA huduma Kwa weledi na kumsimamia Haki na utu .

Lakini pia Namna ya kupata Wakuu Wa Jeshi hilo ni changamoto sana mana wanapatikana kisiasa na kuteuliwa kama dili Badala ya MALENGO ya kuihudumia jamii. MTU akipewa mkoa kama Arusha ,Mbeya Mwanza ,Dar es salaam basi Ujue Kuna MTU amemuweka Ili kujinufaisha kupitia wafanyabiashara haramu na kulinda Mali za watu Fulani.

Wahali wakubwa hawawezi kuguswa kwenye mifumo Kama hiyo .

Badilisha polisi kuanzia Namna wanavyoteuliwa na kupeana Maeneo yenye ulaji Wa kushirikiana na Wahalifu wakubwa Kama wauza madawa,magendo,wakwepa Kodi na wengineo.hakuna Bosi anayependa Kwenda KUFANYA KAZI Sehemu isiyo na uhalifu mkubwa unaofanywa na matajiri . Nini Maana yake ni kwamba kuna uhusiano Mkubwa sana kimaslahi.

Ingewezekena wangepiguwa kura zansiri Ili kuwataja wale wakubwa wanaoendekeza uhalifu na rushwa Bila kujali Haki za wananchi wanyonge.

Lakini wale Wa usalama Barabarani wanapewa mamlaka na kuwa na Sheria nyingi sana za usalama Barabarani zisizotekelezeka na nyingine ni usumbufu tu.

Askari Wa Barabarani Tanzania ni Wazuri ukilinganisha na Wa nchi Jirani. Wana ustarabu ZAIDI.Barabarani Kuna kanuni nyingi ambazo zinatoa Mwanya Wa Rushwa.

Ingewezekena kungefungwa kamera na kuandika Faini zinazoweza kulipwa Bila kukamata gari kupitia akaunti za benki na miamala mingineyo.
Hii ingepunguza usumbufu na dhana ya kuonewa Barabarani japo sio kuonewa Bali ni Sheria KUTOAwanya Wa uonevu.

Umaskini ni TATIZO kubwa mana Askari Kwa Mishahara Yao midogo wakijifanya kuwa waadilifu wangi watachekwa sana wakistaafu mana Hata vinwamgongo vyao ni vidogo sana. Wale walarushwa wanasifiwa na jamii mana jamii imejaa rushwa hivyo anayekula rushwa na kujijenga anapata Heshima kubwa na pongezi nyingi hasa anapostafu.

CCM imeshindwa kusimamia Kila kitu ikiwemo Jeshi la polisi Wala wasijaribu kurusha lawama Kwa polisi.
Kila Idara imefeli mana siasa imeshika Hatamu.
 
Hakuna ubishi kwamba wapo Polisi wabaya lakini Pia tusipofushwe macho kwamba Polisi wazuri wapo.

Tatizo la Polisi wanapambana na MAKUNDI makuu mawili Mlalamikaji Kwa upande mmoja na mlalamikiwa Kwa upande wa pili na Kwa vyovyote vile lazima mmoja ashinde na yeyote atakaye shinda lazima atakayeshindwa awachukie Polisi lakini Pia majumu Yao ya kukamata yanaongeza maadui wao kila siku mfano ukimkamata Baba yangu Kwa kosa lolote Lile lazima Mimi na familia nzima tuwachukie Polisi wote. Kwahiyo hakuna wakati wanaweza kuwafurahisha Pande zote na hiyo ndiyo sababu ya kuwachukia na kusingizia kwamba wanabambikiza kesi hovyohovyo.

Sababu nyingine ni Serikali kutokuwekeza Kwa Jeshi la Polisi wakiwaacha watumie fursa za kuombaomba ukitaka mtoto wako awe na TABIA mbaya mruhusi aanze kuishi Kwa kutegemea majirani.
Sio kazi ya polisi kudeal na mlalamikaji na mlalamikiwa.

Hiyo ni kazi ya mahakama.
 
Hili jeshi linahitaji kufanyiwa mabadiliko ya maana, hasa kimfumo, kama ameshajua tatizo lipo, sasa atafute chanzo chake na aje na solution..

Kelele za uhuni polisi wanaowafanyia watuhumiwa wakiwa mikononi mwao sio ngeni, muhimu sasa maneno yapungue, na vitendo vya kukomesha hali hiyo vianze kwa haraka na ukamilifu wa kutosha.
 
Samia MANENO meengi utekelezaji 10%
Bingwa JOHN akuwa na maneno ya kutia MOYO yeye ukweli ukweli mtupu ikikuuma shauri yako
Kwenye utekelezaji ni 90%
akisema kitu fulani kifanyike hivi na hapo hapo halambe inaanza
Na kama aliyezingua yupo hapo anamchana LIVE iwe kumuonya au kumtumbua

UONGOZI wa mtindo wa JOHN ndivyo inavyotakiwa katika JAMII ZA AFRICA hasa zile nchi zenye UFISADI wa kutisha RUSHWA nk
Kwa TANZANIA baada ya MAGUFURI kufa ndio tuligundua kuwa tulimuhitaji sana MAGUFURI kuliko yeye alivyohitaji kuwa RAISI wa nchi hiu

Ipo siku WAPINZANI watamzunguzia MAGUFURI katika REFER za hotuba zao za MIKUTANO au maandiko yao
ukitaka kuamini hilo we wafatilie kwa makini katika HOTUBA zao au Mabandiko yao mtandaoni
utagundua tu japo wanamluka kimtindo
 
Nilikua kituo kimoja Cha polisi jijini Mwanza,nikiwa nimeenda kumtoa ndugu yangu Kwa kesi inaitwa ya uzururaji, polisi aliniweka wazi kuwa ubaoni hawezi kutoka Bure, maana mjini kila kitu ni pesa.
 
Tumpongeze rais Mama Samia kwa kuwa na ujasiri wa kulisemea hili.

View attachment 2501408

Hii ni 180° tofauti na mtangulizi wake aliyekuwa akiwamwagia sifa wasizokuwa nazo kinyume cha matarajio ya wengi.

Taasisi isiyokubalika kwa kiwango hiki ni ya nini? Kwanini taasisi hii isivunjwe ikasukwa upya na ikibidi ikaanza na watu wapya?

View attachment 2501411

Kwanini kuendelea kuwalea madhulumati hawa wanaojulikana kana kwamba hawajulikani?

--------
Source: Rais Samia aichambua magereza, jeshi la polisi ‘linavyonyooshewa kidole’
Amekose, ni 98% wanalinyooshea kidole jeshi la polisi, wananchi hawana imani tena
 
Hakuna ubishi kwamba wapo Polisi wabaya lakini Pia tusipofushwe macho kwamba Polisi wazuri wapo.

Tatizo la Polisi wanapambana na MAKUNDI makuu mawili Mlalamikaji Kwa upande mmoja na mlalamikiwa Kwa upande wa pili na Kwa vyovyote vile lazima mmoja ashinde na yeyote atakaye shinda lazima atakayeshindwa awachukie Polisi lakini Pia majumu Yao ya kukamata yanaongeza maadui wao kila siku mfano ukimkamata Baba yangu Kwa kosa lolote Lile lazima Mimi na familia nzima tuwachukie Polisi wote. Kwahiyo hakuna wakati wanaweza kuwafurahisha Pande zote na hiyo ndiyo sababu ya kuwachukia na kusingizia kwamba wanabambikiza kesi hovyohovyo.

Sababu nyingine ni Serikali kutokuwekeza Kwa Jeshi la Polisi wakiwaacha watumie fursa za kuombaomba ukitaka mtoto wako awe na TABIA mbaya mruhusi aanze kuishi Kwa kutegemea majirani.
Umenena!
 
Bi mkubwa anaponimaliza ni ile kutokujua kama yeye ndio amir jeshi, yeye hana wa kumlalamikia ni kuchukua hatua tu ndio amebakisha, ilo jeshi ndio linatutia aibu nchi hii, rushwa na kutotimiza wajibu wao ndio matope wanayjipaka nayo kila kukicha.

Yaani saa moja asubuhi wenzao wamedamka vibaruani na wameshonana katika daladala wao wanasimamisha dala dala bila sababu yeyote ya maana ni kuleta kero tu. barabarani ndio wanaweka barriers ili wawe omba omba usiku kucha sasa likukute jambo kama ajari ndio wamepata fursa ya kupiga pesa.

Kazi wanayoweza ni kujikomba kwa wanasiasa na kuleta shobo katika misafara. Mama kama kweli uko serious vunja kabisa hilo jeshi lote anza moja na wanajeshi washike hatamu wakati tunaandaa police wapya. waliopo wote walipwe mafao wakatafute kazi kwengine.
 
Tuanzie kwenye uchama dola, vunja hii kitu vinginevyo gizza litazidi kutanda.
Pili unda upya jeshi la pollisi 1. Mfumo na 2. Uelewa wao, jinsi ya kuhudumia wananchi3. Uhusiano wao na watawala.
 
You are right. Polisi wakianza kusimamia maadili wasije wakaanza tena kuwavuta upande wao.

Misingi ya utendaji wa polisi kwa 70% imeshajihishwa na chama cha ccm sababu mwenyekiti wa ccm ndio anateua na kufanya mawasiliano ya karibu na IGP.

Na polisi ndio hasa mbeleko ya ccm. Nje ya vyombo vya dola, CCM ni bora TLP. Siku polisi wakisema wanafuata sheria ndio mwisho wa hicho chama cha majizi.
 
Tumpongeze rais Mama Samia kwa kuwa na ujasiri wa kulisemea hili.

View attachment 2501408

Hii ni 180° tofauti na mtangulizi wake aliyekuwa akiwamwagia sifa wasizokuwa nazo kinyume cha matarajio ya wengi.

Taasisi isiyokubalika kwa kiwango hiki ni ya nini? Kwanini taasisi hii isivunjwe ikasukwa upya na ikibidi ikaanza na watu wapya?

View attachment 2501411

Kwanini kuendelea kuwalea madhulumati hawa wanaojulikana kana kwamba hawajulikani?

--------
Source: Rais Samia aichambua magereza, jeshi la polisi ‘linavyonyooshewa kidole’
Amepunguza asilimia sana, ukweli hakuna mtanzania mwenye imani na Police kabisa,niliibiwa Simu nikaenda kureport pale Msimbazi,wanataka Laki moja na nusu ili waitafute.........baada ya kuondoka na kuona hawana msaada,yule aliyenipokea baada ya kuona kimya alikuwa ananipigia Simu zaidi ya miezi 3 bila aibu anauliza lini nitamtumia Hela,Kifupi jeshi la police limeoza kabisa
 
Trafiki wakike gongolamboto ananilazimisha kuwa gari langu halina bima. Nikamuuliza mbona hujakagua.huku anasimu ya kitochi. hawa watu ni hatari sana.
 
Samia MANENO meengi utekelezaji 10%
Bingwa JOHN akuwa na maneno ya kutia MOYO yeye ukweli ukweli mtupu ikikuuma shauri yako
Kwenye utekelezaji ni 90%
akisema kitu fulani kifanyike hivi na hapo hapo halambe inaanza
Na kama aliyezingua yupo hapo anamchana LIVE iwe kumuonya au kumtumbua

UONGOZI wa mtindo wa JOHN ndivyo inavyotakiwa katika JAMII ZA AFRICA hasa zile nchi zenye UFISADI wa kutisha RUSHWA nk
Kwa TANZANIA baada ya MAGUFURI kufa ndio tuligundua kuwa tulimuhitaji sana MAGUFURI kuliko yeye alivyohitaji kuwa RAISI wa nchi hiu

Ipo siku WAPINZANI watamzunguzia MAGUFURI katika REFER za hotuba zao za MIKUTANO au maandiko yao
ukitaka kuamini hilo we wafatilie kwa makini katika HOTUBA zao au Mabandiko yao mtandaoni
utagundua tu japo wanamluka kimtindo

Hakuna mpinzani anamfagilia Rais muovu. Kwa taarifa yako huyo John hakuwa rais, bali muhalifu aliyepata madaraka.
 
Back
Top Bottom