Bi mkubwa anaponimaliza ni ile kutokujua kama yeye ndio amir jeshi, yeye hana wa kumlalamikia ni kuchukua hatua tu ndio amebakisha, ilo jeshi ndio linatutia aibu nchi hii, rushwa na kutotimiza wajibu wao ndio matope wanayjipaka nayo kila kukicha.
Yaani saa moja asubuhi wenzao wamedamka vibaruani na wameshonana katika daladala wao wanasimamisha dala dala bila sababu yeyote ya maana ni kuleta kero tu. barabarani ndio wanaweka barriers ili wawe omba omba usiku kucha sasa likukute jambo kama ajari ndio wamepata fursa ya kupiga pesa.
Kazi wanayoweza ni kujikomba kwa wanasiasa na kuleta shobo katika misafara. Mama kama kweli uko serious vunja kabisa hilo jeshi lote anza moja na wanajeshi washike hatamu wakati tunaandaa police wapya. waliopo wote walipwe mafao wakatafute kazi kwengine.
Hao wanajeshi wanatokea nchi Gani?
Jamii ni corrupt kuanzia JUU mpaka chini halafu utegemee kuwa na jamii yenye watumishi waadilifu?
Unajua ufisadi unaofanywa na mawizara hayo unayoyasifia . ?
Hiví unajua Miaka ya 1980 Kuelekea 90 mpaka 2000 majambazi waliokuwa wanateka mabasi na malori walikua ni Akina nani?
Unajua kama SIO mission za kimataifa Leo hii wanajeshi wetu wangekua na maisha magumu kuliko mtumishi yeyote duniani na ambacho kingetokea ni Mapinduzi.
Unajua maslahi ya mabosi Wa JUU ya Jeshi ni Kwa nini ni makumbwa ?
Leo ukiona mwanajeshi Amejenga nyumba SIO Mshahara anaolipwa na Taifa lake Bali ni pesa za UN zinazotokana na vita za kisiasa KWENYE nchi nyingine.
Tumshukuru Mungu nchi nyingine Zina vurugu mana tusingeweza kukabiliana na mtiti Wa wanajeshi Wenye njaa.
Ukitaka kujua jamii ilivyokaa Angalia Walimu wetu Wa Shule , maprofesa Wa vyuo, wakuu Wa wilaya na mikoa n.k. wanavyotumia Nguvu na ubabe na vitisho kufifisha Haki za watu.
Rushwa IPO Hata KWENYE taeuzi Kuna rushwa za ngono,vyuoni Kuna rushwa ya ngono n.k. Sasa kama maprofesa wasomi wanafaulisha wataalam Kwa rushwa ya ngono na IPO wazi lakini Kwa sababu inawahusu wasomi Kwa maslahi Yao Inaonekana ni NZURI kuliko ya polisi na Sheria za hovyo zinazoweka mianya ya rushwa.
Kama Mama Samia anataka kuwafanya Watanganyika wachukie rushwa ni vema akakubali mabadiliko ya Katiba yatakayoleta mfumo mpya Wa utumishi na kuipa Nguvu tume ya maadili. Rushwa yote ni watu kutaka kulimbikiza Mali .
Hakua MTU anayemuuliza mtumishi Wa umma kuwa amewezaje kujenga nyumba kumi Kwa muda mfupi Wakati wenzake Wenye Mshahara kama wake hawana Hata nyumba Moja? Lazima pawe na kuulizana mana ni watumishi Wa umma.Wahalali wajulikane