Samia Scholarship ni uwekezaji wenye tija

Samia Scholarship ni uwekezaji wenye tija

Kwa mara nyingine tena Wajanja wamebuni mpango wa kujisaidia wenyewe kwakua hawa waliopata ufadhili kupitia Samia scholarship ni watoto ambao wengi wao walisoma masomo ya sayansi, yaani PCM, PCB na EGM. Watoto na wazazi walijuwa kuwa 98% ya watoto ambao wanasoma masomo ya sayansi (physics, Chemistry, Biology, Hesabu, Agriculture, Zoology kule A' Level moja kwa moja wanalenga kwenda kusoma kozi za sayansi kule vyuo vikuu, hivyo sio kweli kuwa Samia scholarships zingewavutia watoto hawa kwenda kusoma fani za sayansi, kwakuwa kwa kusoma tahasusi za sayansi kule sekondari tayari walishaamua (narrow) kusoma kozi za sayansi huko mbele ya safari vyuo vikuu, hivyo Samia Scholarship sio kwaajili ya mtoto bali ni kwaajili ya mzazi kupunguziwa gharama za kumsomesha mwanawe ambae tayari walishaamua na mwanawe kusoma masomo ya sayansi ili hatimae wasome kozi za sayansi chuo kikuu.

Dhambi iko wapi hapo? Dhambi inakuja pale Samia scholarship inapogharamia hata wale watoto waliosoma shule za ada kubwa, automatically watoto hawa wana nafasi ya kusoma vyuo vikuu kozi za sayansi hata bila Samia scholarship wala mkopo. Hii maana yake imekwenda kupunguza uwezo wa watoto masikini kupata msaada wa kusoma vyuo vikuu kozi za sayansi.

Ikumbukwe kuwa 90 ya wanafunzi wanaosoma A' Level shule nzuri kama tabora boys, tabora boys, Kilakala, dakawa, Msalato, Iliboru, nk ni watoto ambao wamesoma shule za private za msingi na sekondari (O' Level) na kuchaguliwa kwenda hizo shule za vipaji maalum,

Hii maana yake ni nini?: Ina maana kuwa elimu itakuwa kwa watoto wa tabaka fulani tu, kwakuwa watoto wanaosoma hizi shule binafsi zenye walimu na mazingira mazuri ya kusoma ndizo zinazotoa watoto wenye ufaulu mkubwa wa kuweza kupata Samia scholarships, kuchaguliwa vyuo vya serikali vyenye ada nafuu na kupata mikopo pia. Hili ni kundi la watoto ambalo wazazi wao wana uwezo mkubwa wa ku lobby kwenye bodi ya mikopo na taasisi za fedha ili watoto wao wapate mikopo au ufadhili.


Samia scholarship ungebaki kuwa mfuko wa wanyonge tu waliofanya vizuri darasani kwenye masomo ya sayanzi, na hii ndio njia madhubuti ya kupunguza pengo kati ya wenye nacho na wasio nacho nchini.
Hii kitu ni ujinga tu na imekaa kisiasa sana
 
Yaani mm sijaona lengo la hiii scholarship kwa maana watakao faulu weeng ni wale wale wanaojiweza kina feza,marian.n.k.....lengo la mkopo ni kusaidia wale wenye uwezo wa chini kujiiinua kwa kiasi chake vitu vingine vinafanyika kwa kuyokuwa na proper planning and organisation ulopita
Shule za binafsi zinaongoza kwenye udanganyifu wa matokeo, Samia scholarships ni mchongo kwa watoto wa wazazi wanaojiweza kujirudishia fedha walizotoa kupeleka watoto wao shule za private. Kwakutumia samia scholarships tujiandae kuona watoto wengi shule za private wakipata ufaulu mkubwa sana (mchongo) ili wawahi siti za mbele za samia scholarships na kupata nafasi vyuo vikuu vya serikali vyenye ada nafuu. Yaani jasho jingi wakati wa amani ili damu kidogo wakati wa vita.
 
Ndugu zangu waliostahili Samia scholarships na mikopo hawakupata kwakuwa projects zote hizo ni mbinu za kuwawezesha watoto kumudu kusoma vyuo vikuu. Mimi nina ushahidi kuwa hakuna uhaba wa watoto wa kike kwenye kozi za sayansi na elimu ya tiba kwenye vyuo vyetu kiasi cha kuhalalisha samia scholarships na mikopo kupewa hata watoto waliomaliza kwenye shule zenye ada kubwa sanakama FEZA na nyinginezo za aina hiyo. Huu ni upigaji fedha za umma sawa na upigaji mwingine. Ona sasa watoto wa masikini wamebaki nyumbani kwa kukosa ada wakati watoto wa matajiri wamepewa samia scholarships, mikopo ya students' loans board, mikopo ya NMB, scholarships za vodacom na kupewa udahiri kwenye vyuo vya serikali vyenye ada nafuu. mtoto wa mkulima, mmachinga, mvuvi, mfugaji, mama ntilie na muoka vitumbua hana access ya fursa hizi zote. Hii ni dhambi kubwa sana kutokea nchini.


 
Back
Top Bottom