Nimepita katika pitapita zangu mitandaoni, pale mjini Instagram nakutana na page inayoitwa @samia.app nikawa natazama ajali ya kariakoo ambayo bwana Alikiba alikuwa anahojiwa na page hiyo ya Samia.app kuhusu ajali hiyo ambayo yeye pia alifika kutoa msaada na kuangalia namna zoezi linavyokwenda.
Nikajiuliza ngoja niingie Playstore kuangalia kama kuna App inayoitwa Samia App. Kuingia Playstore nakutana na App hiyo ambayo imetengenezwa na developer aliyetengeneza Application ya CCM.
View attachment 3155819
Nakatika muktadha huo, Rais Samia Suluhu Hassan anakuwa Rais wa kwanza Nchini Tanzania kuwa na Application yake kwa ajili ya habari zake za kisiasa na uongozi. Hakuna rais aliyewahi kuja na Historia hiieo