Samsung yazidi kuwa Iphone

Samsung yazidi kuwa Iphone

Haya mambo alianzisha Apple. Na kwenye hii dunia yetu kila anachoanzisha Apple watu wanaita Innovation [emoji28][emoji28]
Ila mi najua ni mbinu tu za kibiashara. Haya makampuni Yana akili sana
SIo ni makubaliano ya watengeneza simu soko la dunia kuhusu kutunza mazingira??? 😂😂😂
 
Just imagine

Samsung Galaxy S23 Ultra ina hadi 1TB storage na bado watu wanataka sehemu ya kuwekea memory card [emoji28][emoji28]

Wakiondoa SIM Card slot basi simu itakuwa inatumia eSIM technology

Wakiondoa volume button basi simu zitakuwa zinasense pressure ukikandamiza kwenye edge na hivyo sauti itaongezeka au kupungua bila shida. Hata Xiaomi Mi Mix Alpha inafanya hivyo, haina volume buttons kabisa

Power off button wakiiondoa labda watatumia fingerprint scanner kama sehemu ya kuwashia simu, au kuwasha simu kwa kuiambia tu "Turn on"
Natamani sana technology ifikie huko ndio maana naipenda Sana Xiaomi Mi Mix Alpha [emoji116][emoji116]View attachment 2598538View attachment 2598540
Hii sasa hivi inaenda ngapi mkuu...?
 
Accessories za simu ni rahisi kupatikana na ziko very affordable

Hoja ya kusema charger uliipoteza hivyo unataka kwenye box uipate sidhani kama ina mashiko maana simu unayopewa mpya full box kumbuka pia haiji na protector wala cover ila unavinunua.

Soma uone hapa
View attachment 2598554

Mkuu hizo sio sababu za MSINGI kwa mtumiaji
Hizo ni sababu za kibiashara kwa kampuni

Nashangaa sana pale kampuni zinapotengeneza utaratibu wa kutukamua zaidi kwa sababu za kijinga kama kutunza mazingira na bado kuna watu wanaamini sababu hizo ni za msingi

Hivi kama nina iphone nataka nihamie S23 nitatumia chaja ya iPhone?
Hivi kama nina infinix nahamia S23 kweli nianze kutumia chaja ya infinix ?
Kila siku inaimbwa kwamba chaja za hovyo zinaua betrii leo unasema tukanunue chaja affordable?
Unajua bei ya hizo chaja origino?

Mnavyo maanisha ni kama ukinunua simu mpya basi huna haja ya chaji mpya kwasababu ukipewa chaji mpya wakati unayo ya zamani basi machaji yatajaa mtaani na kuwa uchafu
Yaani ni kama ukinunua simu mpya basi simu ya zamani haina kazi na chaja yake ni ziada tu...... vipi kama nataka kumpa mama yangu au mwanangu au demu wangu? Nimpe bila chaji?

Hatuna namna inabidi tukubali maana kila kitu wanapanga wao
Ila binafsi naona chaji ilikua ni muhimu sana kuwepo
 
Hii sasa hivi inaenda ngapi mkuu...?
Bei ya Xiaomi Mi Mix Alpha niliyoiona kwenye website ya Xiaomi ilikuwa ni TSh 6,700,000/=
Ingawa ilikuwa cancelled kutokana na production na distribution problem. Mfano AliExpress ilikuwa inauzwa hadi kwa shilingi milioni 13
Kwa hiyo kwa sasa kama unaitaka itapaswa uagize kutoka kwa Xiaomi wenyewe
 
Just imagine

Samsung Galaxy S23 Ultra ina hadi 1TB storage na bado watu wanataka sehemu ya kuwekea memory card [emoji28][emoji28]

Mkuu shida nyingine ni utofauti wa aina ya watumiaji kutoka sehemu moja ya dunia hadi nyingine na uwezo wao kiuchumi

Sd card mitaani ni kitu muhimu kweli kwenye kurahisisha movement za data kama movies songs nk
Dunia ya tatu watu wanahamishiana sana data kwa sd card sababu ndio njia rahisi ndio maana wanaona imekua kero
Sasa inabidi watumie Pc
 
Mimi ni mpenzi mkubwa Sana wa simu za android na simu yangu pendwa ni Samsung lakini huku tunakoelekea naona kabisa nitaisaliti chama.Sababu ni kuwa Samsung wanaiga vitu vingi Sana ambavyo havina msingi kutoka Kwa kampuni ya simu ya Iphone.

Hivi ni vitu baadhi ambavyo Samsung kaiga kutoka Kwa Iphone na vimeleta mabadiliko hasi Sana kwa watumiaji wa hizi simu za Samsung;


1 Wameiga kuondoa 3.5 mm jack kutoka kwenye simu za Iphone ;

Mwaka 2017 iphone waliondoa 3.5mm jack ya kuingiza Ear phones kutoka kwenye simu zao za Iphone 7. Matokeo yake Iphone walipondwa Sana na watumiaji wake na kukemewa vikali na kupondwa na makampuni ya simu ikiwemo Samsung.Chanzo Cha kuondoa 3.5 mm jack ilikuwa ni sababu Iphone walishindwa kutengeneza kioo full screen huku 3.5mm Jack ikiwepo.Iphone wanadai kwamba waliondoa 3.5 mm jack Ili waweze kutengeneza full screen BIla kizuizi.Kitu ambacho simu za android ilishaweza kutengeneza huku 3.5 mm jack ikiwepo.Tuseme tu android phones ZIPO mbele kiteknlolojia zaidi ya iPhone .

Swali langu ninajiuliza kwanini Samsung waliamua kuondoa 3.5 mm jack kwenye simu zao Kwa kumuiga iPhone wakati wanajua Iphone waliondoa hicho kitu sababu ya kukosa teknolojia ya kutengeneza full screen BIla kutoa 3.5mm jack?

2 Wameiga kutoweka charger na cover za simu kwenye Box la Simu mpya kama wanavyofanya Iphone ;

Nasikitika Sana kuona Samsung wamepata ujasiri wa kupakia simu tu kwenye Box BIla charger Wala Cover kama simu zingine za Android zinavyofanya.Watu wanatoa mamilioni lakini hawapati product zilizokamilika kwenye Box.Ni upuuzi mtupu.


Wakati simu zingine za Android zinajitahidi kuweka Hadi pre installed screen protector na accessories za simu zinazohitajika Sana Samsung wapo busy wanazidi kuziondoa.


Mimi ni mdau wa Samsung lakini hapa niseme tu Samsung wamefeli pakubwa.

Ni ajabu kukuta Flagship phone kama galaxy S23 ultra imekuja tu na USB Haina charger ni upuuzi mtupu tu.

NI BORA NIHAMIE KAMPUNI ZINGINE ZA SIMU MAANA SAMSUNG WAMEBADILIKA KUWA IPHONE SIO WAO TENA.

Shame on you ShameSung

Uko sahihi, ila wewe ni mteja wa Samsung ambaye hawawezi kukutilia maanani.
 
Samsung bdo itabak kuw na features nyingii zaidi compared to IPhone.
Iphone ni simu ya kilimbukeni mno
Mbona % 99 ya wazungu niliyokutana nao wanatumia simu za Iphone?, Nakushangaa unasema ni simu za kilimbukeni yani kati ya Mwafrika na Mzungu nani limbukeni wa vifaa vya Elektroniki?
 
Mbona % 99 ya wazungu niliyokutana nao wanatumia simu za Iphone?, Nakushangaa unasema ni simu za kilimbukeni yani kati ya Mwafrika na Mzungu nani limbukeni wa vifaa vya Elektroniki?
Labda anamaanisha kwa Bongo watu wengi wananunua iPhone Kwa sababu ya kufuata mkumbo na ulimbukeni mwingi
 
Hii design sio ya 2015
Hata hivyo ni identity ya simu za Sony.
Wanatengeneza simu zenye 21:9 aspect ratio ambayo hutumika katika muvi nyingi. Sony wanasema kuwa zaidi ya 70% ya movies zilizopo Netflix zina aspect ratio ya 21:9. Kwa hiyo ukitumia hizi simu mpya za Sony kuangalia muvi yenye 21:9 ile movie itajaa kwenye screen yote bila kuacha nafasi au kuform black strips. Ndio maana simu zao zinaonekana ndefu na nyembamba kuliko simu nyingine.

Sony ipo kwa ajili ya movie fans ndio maana anaweka pixel density kubwa kwenye simu zake kuliko wapinzani mfano hiyo Xperia 1 IV ina 643ppi. Lengo ni kufanya uone details clearly ukiwa unaangalia movies.
Simu zao ni miongoni mwa simu zenye speakers bora sana tena kama hii Xperia 1 IV ina hadi base ya kutosha. Hii inaweza kuwafaa wapenzi wa mziki ila speaker Bora ni muhimu sana kwa wadau wa movie
Display ya Sony Xperia 1 IV inaweza kuswitch to 4K resolution ikiigundua tu unaplay video. Wakati hii inasababisha ulaji mkubwa wa chaji lakini lengo ni kukupa top notch experience ukiwa unaangalia movies

Bado anaweka microSD card slot ili uweze kuhifadhi movies kwenye memory card. Anakupa hadi uhuru wa kutumia 3.5mm jack ili uweze kusikiliza sauti ya kwenye movies kwa kutumia wired earphones

Ikiwa Sony imeweza kufanya mambo yote hayo ili tu ufaidi kuangalia movies basi hakuona shida kuchange aspect ratio pia ili iendane na ile ya kwenye movies. Ndio hiyo design unayoiona. Hakutaka kutumia kamera ya katikati ndani ya display area ili asipunguze nafasi ya kuangalia video/movies na wanaamini simu zao ndio Bora zaidi kwa kuangalia movies

Hiyo design inawafaa Sana wanaopenda kuangalia movies kwenye simu. Mi naona ipo poa sana
Mimi ni Sony fan hadi watapofunga kiwanda 😀!
Sahizi niko na XZ1 nainjoy unyama tu juzi nimesahau bomba maji yamejaa hadi chumbani cha ajabu simu iko kwenye maji ila haijaharibika. Kumbe kitu ni waterproof bana 😀 😀 😀
 
... charger yake aliyokuwa anaitumia kwenye simu ya zamani bado ipo.
Kijana hapo naomba usipotoshe au kuandika as wote hatuelewi humu.

Kila charger inauwezo tofauti wa kuchaji simu husika labda iwe d same phone, vinginevyo huwezi chaji Samsung kwenye charge ya Vivo ikiwa na amps tofauti.

Zingatia kila siku teknoloji inabidirika as kutoka slow to fast.
 
Duh .. wewe unachotaka ni kubishana na kuleta ushabiki
Kwa hiyo hakuna earpods zinazoharibika[emoji23][emoji23]
Mi naishia hapa
Sio kubishana. Kumbuka umesema huna experience. Na watumiaji tumekwambia mbona hatuna hilo tatizo la vitu kuharibika sana

mie sijawahi haribikiwa kabisa. Ndio maana nimekukatalia.
 
Bei ya Xiaomi Mi Mix Alpha niliyoiona kwenye website ya Xiaomi ilikuwa ni TSh 6,700,000/=
Ingawa ilikuwa cancelled kutokana na production na distribution problem. Mfano AliExpress ilikuwa inauzwa hadi kwa shilingi milioni 13
Kwa hiyo kwa sasa kama unaitaka itapaswa uagize kutoka kwa Xiaomi wenyewe
Sawa,ngoja kwanza nimalizie pagale langu hizi simu zipo tu...
 
Back
Top Bottom