Tetesi: Sanamu ya Mnara wa Askari (Askari Monument) yaondolewa kupisha ujenzi wa Barabara

Tetesi: Sanamu ya Mnara wa Askari (Askari Monument) yaondolewa kupisha ujenzi wa Barabara

Gemini AI

Member
Joined
May 8, 2024
Posts
91
Reaction score
265
Kuna taarifa nimeona mtandaoni kuwa Sanamu maarufu katika jiji la Dar es Salaam, Askari Monument imeondolewa katika eneo lake kwa lengo kupisha ujenzi wa Barabara za Mwendokasi. Kama ni kweli, natumai itarudishwa na si kuondolewa moja kwa moja maana ni alama muhimu za jiji.

1718105315095.png

UPDATE: TANROADS wakanusha na kutoa ufafanuzi kuhusu tetesi hii

Soma:
- TANROADS: Mradi wa BRT Awamu ya Tatu Dar, hautaondoa wala kugusa SANAMU YA ASKARI iliyopo makutano ya Mtaa wa Azikiwe na Samora
 
Kuna taarifa nimeona mtandaoni kuwa Sanamu maarufu katika jiji la Dar es Salaam, Askari Monument imeondolewa katika eneo lake kwa lengo kupisha ujenzi wa Barabara za Mwendokasi. Kama ni kweli, natumai itarudishwa na si kuondolewa moja kwa moja maana ni alama muhimu za jiji.
View attachment 3014585
yote yanawezekana, kwa samia yote yanawezekana , kama wamasai wanafurushwa, sembuse masananu ya cement
 
KUNA KITU CHA KUJIULIZA YANI MTALII AKIJA TANZANIA HAPO DAR ANASHINDWA KUJUA MJI MKONGWE NI UPI MAANA MAJUMBA YA KIKOLONI YALITAKIWA KUBORESHWA NA KAMA UTANUZI WA MIJI NA MAJIJI KUANZISHA SEHEMU NYENGINE.
UKIFIKA WINGEREZA,ITALY,USA,URUSI NA N.K UNAONA MAJENGO NA SEHEMU ZOTE ZA ZAMANI
 
HABARI: Juni 11, 2024 - Sanamu ya Askari jijini Dar es salaam ikiondolewa leo kupisha mradi wa ujenzi wa barabara ya BRT unaoendelea sehemu mbalimbali jijini. Tunafuatilia Kinikia hili kujua endapo sanamu hio itarejeshwa tena eneo hilo au la.

Sanamu hiyo, iliyokuwa penye kitovu cha jiji la Dar es Salaam mahali ambapo mitaa ya Samora na Azikiwe (zamani: Maktaba) inakutana, ni ya askari katika sare ya kijeshi ya King's African Rifles wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia (1914-1918) akishika bunduki yenye sime nje huku ikiwa inaangalia upande wa baharini.

Sanamu hiyo ni moja kati ya tatu zilizochongwa huko London na mchongaji James Alexander Stevenson kama kumbukumbu ya askari na wapagazi Waafrika waliopiga vita hivyo katika Afrika ya Mashariki hasa kati ya Uingereza na Ujerumani ambao wengi wao walikufa. Zilipelekwa Nairobi, Mombasa na Dar es Salaam. Hii ya Dar es Salaam ilisimamishwa mwaka 1927.

Chini yake pana maandishi ya kumbukumbu kwa Kiingereza na Kiswahili kilichoandikwa kwa herufi za Kiarabu na pia kwa herufi za Kilatini kama yafuatayo:

"Huu ni ukumbusho wa askari Waafrika wenyeji waliopigana katika Vita Kuu na ni ukumbusho pia kwa wapagazi ambao walikuwa miguu na mikono ya majeshi. Ni ukumbusho pia kwa watu wote waliotumika wakafa kwa ajili ya mfalme na nchi yao katika Afrika ya Mashariki kwenye Vita Kuu toka mwaka 1914 mpaka 1918 . Ukipigania nchi yako ujapo umekufa watoto wako watalikumbuka jina lako."

Sanamu hii ilichukua nafasi ya ingine iliyosimkwa mwaka 1909 kwa kumbukumbu ya meja Hermann von Wissmann, gavana wa pili wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani, ambayo ilibomolewa na Waingereza walipoteka Dar mwaka 1916.
 
Historia ya lile sanamu si nzito kiasi hicho tuwaze kuirudisha,

Ikakae mule ndani makumbusho. Of which si necessary as well,

Hata pale askari hatukua tuna muhusudu sana zaidi ya ile round about,

Okay nadhani ikirudi itawekwa tu hata pembeni au juu ya kituo
 
Kumbe yule mwana ni mzee sanaaaa, ila mdo anaashiria mtindio wa ubongo wa Askari wengi wa nchi hii. Aondolewe watu wauzie hata Ice Cream pale.
 
Back
Top Bottom