Sanduku la Agano liko wapi?

Sanduku la Agano liko wapi?

Mbona Hadi juzi juzi kipindi cha sadamu Hussein lilikuepo, hapo hapo ,
Wababylon hawakuacha kitu huko Israel ya kale,
 
Mimi pia nimeona documentary kama hiyo. Inasemekana liko Ethiopia kwenye kanisa moja dogo la kale. Pembeni yake Haile Sellasie alijenga kanisa lingine kubwa. Anayeingia kwenye chumba lilipo hilo sanduku ni mtu mmoja maalum. Akishachaguliwa mtu wa kuingia kwenye hicho chumba huwa haruhusiwi tena kutoka hekaluni kwenda uraiani mpaka anakufa, na pia haruhusiwi kuongelea details za hilo sanduku. Mtu mwingine atachaguliwa pale anapofariki huyo anayelitunza au anayelitunza akiwa hawezi tena kiafya. Watu wote waliokwisha fanya hiyo kazi hupata matatizo ya macho kutoona vizuri mara baada ya kuanza hiyo kazi.
Ngoja niitafute hiyo documentary niitazame tena, very interesting. I will share the link or upload it kwa jinsi nitakavyoipata.

Hapa kuna interesting story (ya 2021, sio zamani) kuhusu waethiopia wanavyopigana kulilinda hili sanduku SOMA HAPA
Hi hapa sio niliyoiona siku za nyuma lakini inafanana in details. Ile ni ndefu kidogo nafikiri niliiona kwenye documentaries za dstv, labda.
 
Ukisoma Samweli wakwanza..kuanzia fungu la 4

Kuna kisa hapo huwa kinanichekesha na kunifundisha sana.


Wafilisiti na waisrael walikua vitani..

Basi wafilisit,wakawapa kichapo kikubwaa waisrael, unaambiwa Waisrael walipigwaa sanaa


Walivyoona kichapo kimewaelemea, wakashauriana kufata SANDUKU LA AGANO ,eti liwalindee


Kweli wakaliletaa, wakapiga kelele sanaaa mpaka wafisiliti wakaanza kuogopa

Baadae Wafisiliti wakajawa na ujasiri wakaona bora wakapamband

Wakaenda tena kwa Waisrael, wakawatembezea kipigooo, piga saaana waisrael, pigaaa sanaaa licha ya Sanduku la agano, lkn wote walichezea kipigoo

Mpaka Wakalibeba sanduku.


Ilibidi Mungu mwenyewer aingilie kati ,kuwapa adhabu wafilisit mpaka wakalirudisha[emoji23][emoji23][emoji23].


FUNZO...Tunajifanganyaga eti ukilala na Biblia, Mashetani na wanga wa Usiku hawakuchezei

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]My Dear, kama Waisrael walichezea kichapoo licha ya kua na Sanduku la Agano. Sembuse Biblia ako[emoji23][emoji23][emoji23]

TUSALI.
 
mkuu ipo hivi israel waalipokuwa wanaasi MUNGU alikuwa anawaacha wanapigwa , na wapagani wanalibeba sanduku hawadhuriki


soma 1 SAMWELI KUANZIA SURA YA 2 LILIWAHI KUCHUKULIWA NA WAFILIST WAKALIPELEKA KWA mungu dagoni, baadae liliwaua wakiarirudisha
Kwa sehemu uko sahihi, lakini hoja yangu iko hapa kama wafilisiti waliweza kulichukua na likaweza kuwaua kwa maana kwamba bado lilikuwa na utukufu wa Mungu na kwamba amri ya kugushwa na wana wa lawi ilikuwa bado inafanya kazi ndio maana liliendelea kuwaua wafilisiti.

Je kwa sasa kama sanduku la Bwana kama bado lipo mahali hapa duniani ile hali ya kufanya makabila mengine kufa kama wataligusa sanduku la Bwana kwa kuwa siyo wana wa lawi iliondolewa ndio maana hatujasikia watu wamekufa kutokana na kugusa sanduku la Bwana? au sanduku la Bwana halipo kabisa hapa duniani ndio maana watu hawafi?.
 
Wakati wa uhai wa Yesu, hekalu takatifu katika Yerusalemu lilikuwa ndilo nguzo muhimu katika maisha ya kidini ya Kiyahudi. Hekalu ilikuwa mahali ambapo dhabihu za wanyama zilikuwa zinafanyiwa na ibada kwa mujibu wa sheria ya Musa iliyofuatwa kwa uaminifu. Waebrania 9: 1-9 inatuambia kwamba katika hekalu pazia ilitenganisha pahali takatifu zaidi ya patakatifu – mahali ambapo uwepo wa mungu uishi ulimwenguni- kutoka kwa mahali pengine Hekaluni ambapo watu waliishi.

Hii iliashiria kuwa binadamu alitenganishwa kutoka Mungu na dhambi (Isaya 59: 1-2). Ni kuhani mkuu tu aliyeruhusiwa kupita zaidi ya hii pazia mara moja kila mwaka (Kutoka 30:10, Waebrania 9: 7) aingie katika uwepo wa Mungu kwa ajili ya waisraeli wote na kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi zao (Mambo ya Walawi 16).

Hekalu la Sulemani lilikuwa dhiraa 30 kuelekea juu (1 Wafalme 6: 2), lakini Herode alikuwa amezidisha urefu hadi dhiraa 40, kulingana na maandiko ya Josephus,mhisitoria Myahudi wa karne ya kwanza. Hakuna uhakika kwa kipimo halisi cha dhiraa moja, lakini ni salama kudhani kwamba pazia hili lilikuwa mahali fulani karibu futi 60 juu. Josephus pia anatuambia kwamba pazia hili lilikuwa na upana wa inchi nne na kwamba farasi hata wafungwe kwa kila upande hawangeweza kuirarua dhiraa hii . Kitabu cha Kutoka kinafundisha kwamba pazia hii pana iliundwa kwa mtindo kutoka samawati( buluu), zambarau, na nyekundu, na kitani kizuri cha kusokotwa.

Ukubwa na unene wa pazia unafanya matukio yanayotokea wakati wa kifo cha Yesu juu ya msalaba kuwa wa maana sana. "Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. Na tazama, pazia la Hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka."(Mathayo 27: 50-51a).

Hivyo, je,tunafanya nini kwa hili? Ni umuhimu gani dhiraa hii ilyopasuka inayo kwetu siku hizi? Zaidi ya yote, kuraruriwa kwa dhiraa wakati wa kifo cha Yesu kuliashiria kidrama kwamba kafara yake, kumwaga damu yake mwenyewe,kulikuwa upatanisho wa kutosha kwa ajili ya dhambi.Kuliashiria kwamba sasa njia ya kuingia Patakatifu pa Patakatifu ilikuwa wazi kwa watu wote, kwa wakati wote, Wayahudi na Mataifa.

Wakati Yesu alikufa, dhiraa iliraruka, na Mungu akatoka mahali pale kwamba kamwe hangeishi tenai katika hekalu zilizojengwa na binadamu (Matendo 17:24). Mungu alikuwa amemalizana na hekalu hilo na mfumo wake wa kidini, na hekalu na Yerusalemu ziliachwa "zikiuzunika kwa ukiwa" (kuharibiwa na Warumi) katika mwaka 70 A.D., tu kama Yesu alitabiri katika Luka 13:35. Bora tu Hekalu lilisimama, liliashiria kuendelea kwa Agano la Kale. Waebrania 9: 8-9 inarejelea umri uliokuwa unapita mara tu agano jipya liliimarishwa (Waebrania 8:13
 
Sanduku la agano ni kivuli tu juu ya Bikira Maria na nafikiri unajua Bikira Maria alipo.
 
Huu ni mfano wa sanduku la agano ambalo wana wa Israel waliambiwa watengeneze na Mussa wakiwa nyikani wakitoka Egypt (Misri) wakielekea promised land (Nchi ya ahadi). Sanduku hilo lilikuwa ni kama box la mbao lililotengenezwa na aina moja ya mbao inayoitwa (acacia wood) iliyofunikwa na dhahabu. Lilikuwa la urefu wa 1.15 metres, upana wa 0.7 metres na kimo cha 0.7 metres.

Ilikuwa inabebwa na mishikio miwili mirefu ambayo ilikuwa imetengenezwa kwa mbao hiyo ya acasia ambazo pia zilikuwa zimefunikwa na dhahabu. Juu ya sanduku kuliwekwa makerubi wawili waliokuwa wamegeukiana mabawa yao yakiwa yamegusana. Uwepo wa Mungu haukuwepo ndani ya sanduku bali ulikuwa juu yake katikati ya hao makerubi.

Uwepo wa Mungu juu ya sanduku hilo ulikuwa kama nuru. Kuhani mkuu alipaswa kufunika macho asiione nuru hiyo ("hakuna mwanadamu anionaye na akaishi" Kutoka 33 : 20) kila alipokuwa akiingia lilipokuwa sanduku ambapo ni patakatifu pa patakatifu.


Hapa ndipo ambapo Mungu alipokuwa akiionana na Musa. Sanduku hili lilikuwa likibebwa na wana wa Walawi pekeyake hakuna mwingine aliyeruhusiwa kulishika, yeyote aliyedhubutu kulishika pasiporuhusiwa alikufa papohapo. Hao makerubi wawili wanawakilisha utukufu wa Mungu. Ndani ya sanduku hili kulikuwa na:
  • Mawe mawili yaliyokuwa yameandikwa amri kumi za Mungu
  • Fimbo ya Aron iliyoota mauwa
  • Chombo cha dhahabu kilichokuwa na manna waliyokula wana wa Israel nyikani
Sanduku hilo lilikuwa linakaa patakatifu pa patakatifu, chumba cha ndani kabisa katika hema la kukutania. Aliyekuwa anaruhusiwa kuingia mahala hapo lilipokuwa sanduku hilo ni kuhani mkuu na alikuwa anaruhusiwa kuingia mara moja kwa mwaka. Kabla ya Kuhani mkuu kuingia patakatifu pa patakatifu alikuwa ni lazima aingie na damu ya mwana kondoo kwa niaba ya dhambi zake yeye mwenyewe na dhambi za wana wa Israel.

View attachment 1760924

Sanduku la agano lilikuwa ndani ya hekalu lililojengwa na Solomon mpaka hekalu hilo lilipokujwa kuvunjwa mikononi mwa utawala wa Babylon ukioongozwa na Nebuchadnezzar. Kilichotokea kwa sanduku hilo hakijulikani ingawa haiwezekani kuwa lilichukuliwa na majeshi ya Babylon kama vilivyochukuliwa vyombo vingine vya hekalu kwasababu katika list ya vitu walivyovichukua sanduku la agano halikutajwa.

Halitajwi kati ya vyombo vilivyopelekwa Babiloni hekalu lilipohabiriwa mwaka wa 607 K.K. wala halitajwi kati ya vyombo vilivyorudishwa Yerusalemu baadaye.—2 Wafalme 25:13-17; Ezra 1:7-11

Kulingana na baadhi ya vyanzo vya habari inasemekana kuwa mfalme Josiah, mmojawapo wa wafalme wa mwisho kutawala enzi za hekalu la kwanza, kutokana na unabii uliokuwa umetolewa alijua kuwa Jerusalem itavamiwa na Babylon, akalificha sanduku la agano.

Alipolificha sanduku imekuwa kitendawili. Chanzo kingine cha habari kinasema kuwa mfalme Solomon alionyeshwa kuwa Hekalu litakujwa kuvunjwa na majeshi ya Babylon, kwahiyo akaandaa pango karibu na bahari ya shamu (dead sea) ambapo Josiah akaja kulificha sanduku.

Na pia inasemekana nabii Yeremia (Jeremiah) alilificha sanduku chini ya Hekalu lililojengwa na Solomon.

HEKALU LA MBINGUNI



Jews need the box. Christians as well as moslems. Ndio maana Yerusalemu itakuwa ngumu sana kuwa na amani. Aqsa Mosque/ Benedictine Monks Chur...Jews as well, wote wanaenda kusali wanapoamini ndipo kulikuwa na sanduku la agano
 
lilifikaje ethiopia? kuna connection gani kati ya utawala wa Babylon na wa-ethiopia ? yawezekana hawa wa-ethiopia ndiyo wakawa wana halisi wa Israel na wengi wao walikuwa utumwani Misri

Mawasli ni mengi....
Kupitia Malkia wa Sheba na kanisa kongwe la Orthodox
 
Huenda waethiopia wenyewe ndo waizrail walokusudiwa
Kuna Documentary niliangalia ya BBC/aljazera sina uhakika,wanasema lipo Ethiopia,kuna hekalu Fulani limewekwa huko ndani na huko anayeruhusiwa kuliona na kulilinda ni mtu mmoja tu na Mara nyingi hatoki nje.

Nje ya Hekalu hilo lina ulinzi mkali sana na hata mwandishi mwenyewe kwanza ilibidi apate ruhusa ya kufika huko na hata alipofika aliongea na mtu mmoja tu aliyekuwa nje ndio akamweleza hayo yite na wala hakuruhusiwa kusogea karibu na uzio wa Hekalu.
 
Back
Top Bottom