Sanduku la Agano yawezekana limefichwa na makundi ya siri kama Priory of Sion?

Sanduku la Agano yawezekana limefichwa na makundi ya siri kama Priory of Sion?

Jamiiforums ni kisima Cha maarifa na sio matusi. Kwa wale wenye kupenda mjadala huru na sio matusi karibuni. .

Kuna conspiracy nyingi sana mojawapo ni hiyo niliyosema kuwa ancient aliens threory Ina suggest hiki kifaa kilikuwa kama silaha. Na wanaoamini it is scientific made, ku connect na viumbe wa sayari nyingine ambao wanajulikana kama extraterrestrial 👾

Hawa viumbe waliaminika kuwa ni miungu kumbe lakini walikuwa ni viumbe vya kawaida. Mbali na wana wa Israel haya masanduku yalikuwa pia yalipatukana kwenye asili za watu wengine. Dunia ya Leo sio dunia ya kuzungumza bila ushahidi kwamba watu wanaweza connect dots kitu flani kwa nini Kiko hivi na vile. .

Mijadala hii pia haijaanza Leo hata wenzetu wakenya hapo na duniani inaendelea siku nyingi. Mfano:

https://www.JamiiForums.com.com/ind...ts-caused-nasty-sores-to-its-handlers.181778/


Sijatulia coz Niko road ila nikitulia nitaonyesha asili ambazo mpaka Leo hii wanafanya Mila za sanduku za agano kwa kirefu. Ila kifupi
1. Ethiopia
2. Zimbabwe -
3. Japan - Hawa Hawana asili kabisa na wana wa Israel ila mpaka Leo hii wanafanya Ile walk ya jangwani sanduku likiwa mbele Yao

Kuna vitabu vingi vimeandikwa na huyu jamaa anaitwa Erick Von Danineck about ancient gods. Kwa wale wanapenda kumkosea ease vitabu vyake wapate kumkosoa. .

Nitaendelea. .
 
Nianze na Japani
Kuna wajapani wanaamini sanduku lilikuwa na wazee wao kwa sababu wana observe mila ya sanduku ya kutembea jangwani. Wengi wanaamini kuwa sanduku hili liliwafikia wajapan ila cha kushangaza ni utaratibu wao wa kulitanguliza sanduku mbele kama walivyokuwa wanafanya wana wa Israel. Je kweli lilifika Japan?

Amazon product ASIN 0595694276
“The Bible says that when David brought up the ark into Jerusalem, “David was clothed in a robe of fine linen” (1 Chronicles 15:27). The same was true for the priests and choirs. In the Japanese Bible, this verse is translated into “robe of white linen.” In ancient Israel, although the high priest wore a colorful robe, ordinary priests wore simple white linen. Priests wore white clothes at holy events. Japanese priests also wear white robes at holy events”.
Arimasa Kubo

https://www.youtube.com/watch?v=R8roCXKLhMA


https://www.abovetopsecret.com/forum/thread212055/pg1
 
SHIDA SIO SANDUKU NI NGUVU ZILIZOKO SANDUKUNI,NA JINSI YA KUZITUMIA.SANDUKU WAWEZA KUPEWA NA USIELEWE WALA KUFANYA CHOCHOTE.TATIZO NI ZILE NGUVU NA UFANISI WAKE.
 
Hakuna kitu ni watu wenye akili tu ya kucheza na akili za wajinga..Ukisoma upuuzi mwengine kama unawapa viumbe nguvu kuliko MUNGU...
 
Sanduku la agano zimbabwe:
Kuna ushahidi wa sanduku ile mbao ambao ilitengenezea sanduku nadhani imehifadhiwa makumbusho kuu zimbabwe. Watu hawa na mapadri walitoa vinasaba vyao vipimwe na wengi walionekana wana asili na wana wa Israel. Kuna mzungu aliwahi kulikuta kabisa sanduku hili na waliporudi hawakulikuta, Je limefichwa bado Zimbabwe? Hiyo mbao waliyoitoa kwenye sanduku na kuweka nyingine je ni ya sanduku?
https://www.ctsryan.com/ark-of-the-covenant-found-in-africa-the-stories-behind-the-story/
https://www.denverpost.com/2010/05/29/profs-theory-that-zimbabwe-artifact-is-replica-of-ark-of-covenant-stirs-fierce-response/
https://www.youtube.com/watch?v=sjFDLGr5TKw
https://www.haaretz.com/jewish/2010-05-30/ty-article/scholars-ark-of-the-covenant-claims-spark-african-storm/0000017f-db82-df62-a9ff-dfd7d97b0000
 
SHIDA SIO SANDUKU NI NGUVU ZILIZOKO SANDUKUNI,NA JINSI YA KUZITUMIA.SANDUKU WAWEZA KUPEWA NA USIELEWE WALA KUFANYA CHOCHOTE.TATIZO NI ZILE NGUVU NA UFANISI WAKE.
Hili sanduku lina nguvu kubwa sana:
1. liliangusha kuta za Jericho
2. Liliwavusha wana wa Israel bahari ya shamu
3. Linasemekana bila sanduku kuwepo mana isingeshuka
4. Kulitazama tu lazima ufe ilikuwa hairuhusiwi kulitazama
5. Halikuwa linafunuliwa hili sanduku, mda mwingi lilikuwa covered
6. Image of God appeared on top on this ark of covenant
7. Kulikuwa kunafuka moshi juu ya sanduku katikati ya wale malaika wawili
8. Watu wa jamii ya yuda tu ndio walikuwa wanaruhusiwa kulihifadhi hili sanduku
9. Lazima liwatangulie wao, halijawahi kuwa nyuma yao
10. Ndani yake kulikuwa na fimbo ya Mussa , mana na
11. Wakati sanduku likuwa jangwani mbele yao kuna mwanga ukawa unawatangulia mbele yao kuwaonyesha nyia
12. Liliibiwa hili sanduku ila watu walikufa kwa mionzi, (radiation)
13. Ilikuwa lazima uvae nguo maalumu kwa makuhani waliokuwa wanahufadhi hili sanduku
14. Kuna wana wa Israel walilifungua waone ndani ukatgokea mwanga mkali ndani ya sanduku na kuwaua
nk
 
Sanduku la agano lipo mbinguni, soma ufunuo 11:19

Kisha hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la Agano lake likaonekana ndani ya hekalu lake.
Hilo sanduku lililotajwa mbinguni ni fumbo juu ya Bikira Maria sio lile sanduku la agano la kale. Sanduku la agano ni kivuli juu ya Bikira Maria! How ....

Baada ya andiko hilo uliloweka ufunuo 11:19 andiko linalofata ni ufunuo 12:1 ambalo linazungumza habari za "na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota 12."

Biblia imekuja kuwekwa chapter na verse baadae sana, kabla ya unaweza kuona Yohana anazungumzia ujumbe mmoja ambao ni Bikira Maria!

Agano la kale ilitabiriwa kuwa Bwana atajitwalia Bikira safi! Na alipoamuru kujengwa sanduku la agano alikuwa anafunua mpango wake wa ukombozi kwa mwanadamu. Kwamba atavaa mwili kupitia huyo Bikira safi na kutukomboa.

Kama mwanzisha mada alivyoandika, sanduku la agano ndani yake kulikuwa na fimbo ya haruni kuwakilisha Ukuhani, amri za Mungu kuwakilisha neno la Mungu, Mana ambayo ni mikate iliyoshuka toka mbinguni ambayo inamwakilisha mwili wake Kristo ambaye mwenyewe alisema yeye ndio chakula cha uzima.

Hivyo kwa ufupi yaliyokuwemo ndani ya sanduku la agano ni fumbo la Kristu mwenyewe na Bikira Maria ndiye sanduku la agano pale alipobeba mimba ya Yesu na fumbo la sanduku la agano likafumbuliwa.

Mfalme Daudi alipoletewa sanduku la agano alicheza mbele yake na lilikaa miezi 3 huko na kitu hicho hicho kilitokea pale sanduku la agano "Bikira Maria" baada ya kubeba mimba ya Yesu na kumtembelea Elizabeth aliyekuwa na mimba ya Yohana Mbatizaji, Yohana mbatizaji alicheza tumboni kwa mama yake! Bikira Maria alikaa huko miezi mitatu pia.

Inasemekana maeneo yaliyotokea hayo, Mfalme Daudi kucheza mbele ya Sanduku la Agano, na Yohana mbatizaji kucheza mbele ya Bikira Maria ni eneo lile lile!

Lakini pia Mfalme Daudi alicheza na kutumia maneno yale yale ambayo Elizabeth aliyatumia mbele ya Bikira Maria " imenitokeaje neno hili hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?" Daudi akiwa mbele ya sanduku la agano yeye alisema "Naye Daudi akamwogopa Bwana siku ile; akasema, Litanijiaje sanduku la Bwana?
2 Samweli 6:9

Hivyo ujumbe wa Mungu juu ya sanduku la agano ulishakamilika tusitegemee tena ujumbe mpya nje ya ukamilisho wa neno la Mungu kuvaa mwili kupitia Bikira Maria!

Sasa wenye alerge wakisikia habari za Bikira Maria anatajwa mniwie radhi! Kadiri unavyomfafanua Bikira Maria unazidi kumfafanua Kristo! Simulizi zima ni ukuu wa Mungu kupitia Yesu Kristo ndio maana tutaona mantiki ya sanduku la agano ni vile ilivyobeba na sio sanduku lenyewe!

Lakini huwezi kufafanua yaliyo ndani ya sanduku bila kulitaja sanduku lilotumika kuhifadhi hilo fumbo.
 
Hilo sanduku lililotajwa mbinguni ni fumbo juu ya Bikira Maria sio lile sanduku la agano la kale. Sanduku la agano ni kivuli juu ya Bikira Maria! How ....

Baada ya andiko hilo uliloweka ufunuo 11:19 andiko linalofata ni ufunuo 12:1 ambalo linazungumza habari za "na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota 12."

Biblia imekuja kuwekwa chapter na verse baadae sana, kabla ya unaweza kuona Yohana anazungumzia ujumbe mmoja ambao ni Bikira Maria!

Agano la kale ilitabiriwa kuwa Bwana atajitwalia Bikira safi! Na alipoamuru kujengwa sanduku la agano alikuwa anafunua mpango wake wa ukombozi kwa mwanadamu. Kwamba atavaa mwili kupitia huyo Bikira safi na kutukomboa.

Kama mwanzisha mada alivyoandika, sanduku la agano ndani yake kulikuwa na fimbo ya haruni kuwakilisha Ukuhani, amri za Mungu kuwakilisha neno la Mungu, Mana ambayo ni mikate iliyoshuka toka mbinguni ambayo inamwakilisha mwili wake Kristo ambaye mwenyewe alisema yeye ndio chakula cha uzima.

Hivyo kwa ufupi yaliyokuwemo ndani ya sanduku la agano ni fumbo la Kristu mwenyewe na Bikira Maria ndiye sanduku la agano pale alipobeba mimba ya Yesu na fumbo la sanduku la agano likafumbuliwa.

Mfalme Daudi alipoletewa sanduku la agano alicheza mbele yake na lilikaa miezi 3 huko na kitu hicho hicho kilitokea pale sanduku la agano "Bikira Maria" baada ya kubeba mimba ya Yesu na kumtembelea Elizabeth aliyekuwa na mimba ya Yohana Mbatizaji, Yohana mbatizaji alicheza tumboni kwa mama yake! Bikira Maria alikaa huko miezi mitatu pia.

Inasemekana maeneo yaliyotokea hayo, Mfalme Daudi kucheza mbele ya Sanduku la Agano, na Yohana mbatizaji kucheza mbele ya Bikira Maria ni eneo lile lile!

Lakini pia Mfalme Daudi alicheza na kutumia maneno yale yale ambayo Elizabeth aliyatumia mbele ya Bikira Maria " imenitokeaje neno hili hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?" Daudi akiwa mbele ya sanduku la agano yeye alisema "Naye Daudi akamwogopa Bwana siku ile; akasema, Litanijiaje sanduku la Bwana?
2 Samweli 6:9

Hivyo ujumbe wa Mungu juu ya sanduku la agano ulishakamilika tusitegemee tena ujumbe mpya nje ya ukamilisho wa neno la Mungu kuvaa mwili kupitia Bikira Maria!

Sasa wenye alerge wakisikia habari za Bikira Maria anatajwa mniwie radhi! Kadiri unavyomfafanua Bikira Maria unazidi kumfafanua Kristo! Simulizi zima ni ukuu wa Mungu kupitia Yesu Kristo ndio maana tutaona mantiki ya sanduku la agano ni vile ilivyobeba na sio sanduku lenyewe!

Lakini huwezi kufafanua yaliyo ndani ya sanduku bila kulitaja sanduku lilotumika kuhifadhi hilo fumbo.
I am Roman Catholic na wakatoliki wengi wanaamini Bikira Maria ndio sanduku, it's a conspiracy
Na wapo walokole wengi pia nao wanaamini kuwa sanduku ni Yesu mwenyewe ndio kaja kumwaga damu ya agao lipya, pia ni conspiracy

Kifupi maana ya sanduku ni nini? Kazi yake ni nini? Ndani ya sanduku kulikuwa na amri kumi za Mungu, fimbo ya Mosses some claims Aaron, mana ambazo zilikuwa zinashuka juu wakiwa jangwani. .

Hivi vitu viliashiria nini? Kwa nini sanduku kiwe interpreted kama Yesu au Bikira Maria 😊
 
Hilo sanduku lililotajwa mbinguni ni fumbo juu ya Bikira Maria sio lile sanduku la agano la kale. Sanduku la agano ni kivuli juu ya Bikira Maria! How ....

Baada ya andiko hilo uliloweka ufunuo 11:19 andiko linalofata ni ufunuo 12:1 ambalo linazungumza habari za "na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota 12."

Biblia imekuja kuwekwa chapter na verse baadae sana, kabla ya unaweza kuona Yohana anazungumzia ujumbe mmoja ambao ni Bikira Maria!

Agano la kale ilitabiriwa kuwa Bwana atajitwalia Bikira safi! Na alipoamuru kujengwa sanduku la agano alikuwa anafunua mpango wake wa ukombozi kwa mwanadamu. Kwamba atavaa mwili kupitia huyo Bikira safi na kutukomboa.

Kama mwanzisha mada alivyoandika, sanduku la agano ndani yake kulikuwa na fimbo ya haruni kuwakilisha Ukuhani, amri za Mungu kuwakilisha neno la Mungu, Mana ambayo ni mikate iliyoshuka toka mbinguni ambayo inamwakilisha mwili wake Kristo ambaye mwenyewe alisema yeye ndio chakula cha uzima.

Hivyo kwa ufupi yaliyokuwemo ndani ya sanduku la agano ni fumbo la Kristu mwenyewe na Bikira Maria ndiye sanduku la agano pale alipobeba mimba ya Yesu na fumbo la sanduku la agano likafumbuliwa.

Mfalme Daudi alipoletewa sanduku la agano alicheza mbele yake na lilikaa miezi 3 huko na kitu hicho hicho kilitokea pale sanduku la agano "Bikira Maria" baada ya kubeba mimba ya Yesu na kumtembelea Elizabeth aliyekuwa na mimba ya Yohana Mbatizaji, Yohana mbatizaji alicheza tumboni kwa mama yake! Bikira Maria alikaa huko miezi mitatu pia.

Inasemekana maeneo yaliyotokea hayo, Mfalme Daudi kucheza mbele ya Sanduku la Agano, na Yohana mbatizaji kucheza mbele ya Bikira Maria ni eneo lile lile!

Lakini pia Mfalme Daudi alicheza na kutumia maneno yale yale ambayo Elizabeth aliyatumia mbele ya Bikira Maria " imenitokeaje neno hili hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?" Daudi akiwa mbele ya sanduku la agano yeye alisema "Naye Daudi akamwogopa Bwana siku ile; akasema, Litanijiaje sanduku la Bwana?
2 Samweli 6:9

Hivyo ujumbe wa Mungu juu ya sanduku la agano ulishakamilika tusitegemee tena ujumbe mpya nje ya ukamilisho wa neno la Mungu kuvaa mwili kupitia Bikira Maria!

Sasa wenye alerge wakisikia habari za Bikira Maria anatajwa mniwie radhi! Kadiri unavyomfafanua Bikira Maria unazidi kumfafanua Kristo! Simulizi zima ni ukuu wa Mungu kupitia Yesu Kristo ndio maana tutaona mantiki ya sanduku la agano ni vile ilivyobeba na sio sanduku lenyewe!

Lakini huwezi kufafanua yaliyo ndani ya sanduku bila kulitaja sanduku lilotumika kuhifadhi hilo fumbo.
Nimepata mshangao mkubwa sana ambao pengine sitakuja kuusahau kufuatia ulichoandika hapa. Ngoja nikae kimya ili isionekane ninakashifu imani za watu lakini kwakweli katoliki bado sana kulielewa neno la Mungu.

Nawaombea tu neema ili macho yenu ya rohoni yafunguke mpate kumfahamu Yesu Kristo na kujua kwanini hasa alikuja duniani na nini kinatokea pale mtu anapomuamini yeye.
 
Nimepata mshangao mkubwa sana ambao pengine sitakuja kuusahau kufuatia ulichoandika hapa. Ngoja nikae kimya ili isionekane ninakashifu imani za watu lakini kwakweli katoliki bado sana kulielewa neno la Mungu.

Nawaombea tu neema ili macho yenu ya rohoni yafunguke mpate kumfahamu Yesu Kristo na kujua kwanini hasa alikuja duniani na nini kinatokea pale mtu anapomuamini yeye.
Umewaza kidhehebu, badala ya kuchallenge andiko langu umeishia kuhukumu Kanisa Katoliki kuwa halijui hata kusudio la ujio wa Kristo! Bora hata ungesema mimi binafsi sijui neno! Simply mna ignorance ya kiroho kubwa sana kama Mafarisayo!

Mnahisi mnajua neno nyie binafsi kuliko waliokusanya na kuviweka pamoja vitabu vya Biblia! Kwamba mnajua sana kuliko Kanisa lenye miaka ya 2000 likipokezana mafundisho kwa kuyatunza kwa mfumo usioweza kuvurugwa kibinadamu!

Nyie mna sehemu tu ya ukweli, ukweli mwingi utaukuta Kanisa Katoliki na ukweli wote anao Mungu pekee! Usilojua ni kiza! Pengine hili ulilosoma limekushtua kidogo! Siku ukijua kweli juu ya meza ya Bwana si utazimia? Kuwa mtafiti wa neno la Mungu kama waberoya acha mentality ya kuamini ulichosimuliwa tu! Anza kwanza ku challenge your source of facts ili uiamini.
 
Waasalam

Anaandika,
DaVinci XV,

View attachment 2408231

Naam
Inajulikana na kuelezwa dhahiri katika Imaani na maandiko tofauti tofauti ya kwamba miongoni mwa vitu vikubwa na vitakatifu basi huwezi kuacha kulitaja sanduku la Agano , au Sanduku la Ushuhuda kama wengine wanavyoliita.

Utakatifu wa Sanduku hili inaelezwa kuwa Makuhani walilazimika kulibeba kwa kulishika katika sehemu maalumu (-Fimbo) ambazo zimetengenezwa kwa ajili ya kubebea sanduku na haikupaswa kuligusa sanduku lenyewe, na sababu ni kwamba utukufu wa Mungu na uwepo wake hauwezi kuguswa na mwanadamu.
Maana sanduku lenyewe lilikuwa ni utambulisho wa uwepo wa M/mungu duniani tazama andiko la (KUTOKA 25:22)

Nadhani wengi baina yetu si wageni wa hili na wanatambua mengi kuhusu sanduku hili takatifu, sitohitaji kuingia ndani zaidi kuelezea sanduku hili , bali nitamega kidogo na kujikita zaidi katika msingi wa maada.

VILIVYOMO NDANI YA SANDUKU

View attachment 2408232

Sanduku hili takatifu lilihifadhiwa vitu tofauti tofauti vitakatifu ikiwemo

1- Mawe mawili matakatifu ambayo yaliandikwa Amri kumi za Mungu katika zama za Musa

2- Fimbo ya Harouni ambayo ina muujiza wake pale ilipochipua Maua pale MwenyeziMungu alipowaonyesha waisraeli , Kuhani aliyemchagua ambaye ni Harouni (nadhani wengi wetu wanauelewa mkasa huu)

3- Na mtungi ambao ulikuwa na Chakula Manna ,
Manna ni chakula maalumu ambacho kiliweka muunganiko kati ya M/Mungu na wanaisraeli , Na katika Imani ya dini ya kiislamu inaeleza dhahiri wakati Waisrael walipoihama misri kuelekea Nchini kwao basi M/mungu Aliwarudhuku chakula kutoka katika Pepo yake ambacho ni Manna na Salwah.

View attachment 2408236

Na vyote hivyo katika vitu vilivyomo kwenye Sanduku vilikuwa na Utambulisho au maana zake , Ambazo ni Sheria, ukuhani( ukuu), na utoaji wa M/mungu.
Na kama wanatheolojia wengi walivyoeleza.,
Nadhani pia umeona utakatifu wa vitu vilivyohifadhiwa katika Sanduku la M/mungu.

UPORAJI NA BAADHI YA MAENEO DHAHANIA JUU YA LILIPOFICHWA SANDUKU LA AGANO

View attachment 2408238

Sanduku hili lilitengenezwa kwa mbao kama biblia inavyotanabahisha vyema , kisha ikafunikwa na dhahabu safi, na sanduku hili la Agano mda wote lilihifadhiwa katika hekalu

Na mara kadhaa historia imeonyesha tawala tofauti tofauti kulipora na kuondoka nalo
Mfano wafilisti walifanikiwa kuliteka na kulipeleka kwa Mungu wao lakini Athari zake lilipelekea kuzuka kwa ugonjwa wa Tauni katika jamii yao.

Sanduku hili limeonyeshwa simulizi nyingi zinazohusu kupotea kwake na kupatikana.

Lakini mara ya mwisho sanduku hilo kuonekana ni wakati wa uvamizi wa wababyloni chini ya mfalme Nebuchadnezzer kiasi cha miaka 500 (B.C)
hivi kabla hajazaliwa masihi Yesu mtoto wa maryam walipovamia Israel na kulivunja hekalu la Suleiman na huko ndio haswa kulihifadhiwa sanduku hili la Agano.


View attachment 2408237
Nebuchadnezzer

Na vivyo hivyo Hadithi nyingi zikielezea namna tofauti tofauti ambazo namna hizo hazina ithibati ya lilipofichwa sanduku hilo la Agano
Wengine husema sanduku lilifichwa Na
Mfalme Josiah baada ya kupokea Utabiri wa uvamizi wa wababyloni

Wasomi wengine hudai sanduku hili limehifadhiwa huko Makka chini ya Al-Kaaba, na haliwezi patika kwa maana waislam hawawezi kuruhusu sehemu hiyo takatifu kuchimbuliwa ili tu kutafuta Sanduku.

Na wasomi wengine wanataja sehemu tofauti tofauti ikiwepo ethiopia na Roma huko Italy.

Nadhani kwa kiasi tumejaribu kumega muktadha wa kihistoria juu ya Sanduku la Agano, ambao wengi wetu tunautambua.

View attachment 2408250

JE, INAWEZEKANA SANDUKU LA AGANO LIMEFICHWA NA JAMII ZA SIRI (Kama PRIORY OF SION)

Priory of sion au Prieure de sion (au makundi mengine ya siri kama Illuminant), ni nini??? Hiyo ni mada nyingine inayohitaji nyuzi yake


View attachment 2408240

Unakumbuka kuhusu Last supper ??, mlo wa mwisho wa Bwana Yesu na wanafunzi wake
Unaikumbuka vyema ile picha iliyochorwa na mchoraji na mwanasayansi hodari Leornardo Da Vinci aliezaliwa huko Vinci Italy???

Basi kama ujuavyo katika karamu yoyote , au hafla vitumikavyo ni vyombo.
Ushawahi kusikia kuhusu Holy grail kile kikombe alichotumia bwana yesu kunywea kinywaji katika mlo ule wa mwisho na wanafunzi wake.???
View attachment 2408249
Kikombe ambacho katika nyaraka tofauti tofauti zilizofichwa kimeelezwa kuwa na maajabu yaso kifani kwa yoyote aliyekitumia.

Kuna ambao , walitumia kunywa kinywaji kwa kutumia holy grail na kufanikwa kupona maradhi sugu na wasiumwe tena, kupata nguvu sisizo kifani, Kufa na kufufuka, kusafiri moja kutoka sehemu mmoja au nyingine ya umbali wa kilometa tele kwa mda mchache sana usio wa kawaida, kuwa na ufahamu mpana sana, mamlaka , na Amani ya moyo
Kuna waliotumia wakawa na ufahamu usio kifani na ujuzi wa kuvumbua mambo mengi ambayo kwa wengine si kawaida kama wanasayansi mashuhuri akiwemo Leornado Da Vinci mwenyewe ambaye baadhi ya maandiko yake ya siri yamefichua haya
Lakini ikumbukwe huyu Leornardo DaVinci ni member mkubwa sana Wa kundi la Priory of sion ambalo limehusishwa na kuwa na viongozi wengi wa kidini kama Mapapa na hata wanasayansi wakubwa na watu maarufu kama Sir Isaac Newtons , Boticelli ,na wengineo.
Na ndio kusema kwamba , wanasayansi wengi (sio wote) walikuwa katika makundi makubwa ya Siri, kutokana na uwezo uliopatikana kutoka kwao.

View attachment 2408248
Sir Isaac

Cha Ajabu zaidi usichokijua ni baadhi ya nyaraka hizo zinadai kwamba Kutokana na neema na maajabu ya holy grail kikombe hiki kimehifadhiwa kusikojulikana na mhusika mkuu ni hili kundi la priory of sion kama baadhi ya nyaraka za siri za mwamba Leornardo da Vinci zinavyodai, na si tu holy grail bali vitu vingi vitakatifu vimehifadhiwa na kufichwa kusikojulikana na makundi haya siri ili viendelee kuwanufaisha na kuwapa faida.

N.B Lakini nyaraka hizi hazina ushahidi wa kutosha kuzipa nguvu ili kiwe kitu cha kuaminika
Nani anajuaye????


(Tuachane na hapo Hii mada Holy grail panapo majaliawa tutaitafutia nyuzi yake)

Wakati mmoja nilipata kupitia documentary moja ambayo muandishi wake anadai yeye ni katika member wa makundi kati ya kundi mojawapo la siri na kubwa hapa duniani.

Moja kati ya vipengele vya documdntary hiyo vinaelezea.

Dunia yetu imeaminishwa ya kwamba sanduku takatifu la Agano limepotea na yakitajwa maeneo tofauti tofauti yakwamba huenda limehifadhiwa huko

Documentary inadai makundi haya makubwa (priory of sion, Illuminati ) , au jumuiya nyingine ya siri yoyote ya siri Huenda wana uhusiano na kupotea kwa sanduku la agano.

View attachment 2408244
Wasomi wale wanaijua Biblia vizuri sana, kuliko kawaida, ni miongoni mwa kitabu chao cha mwongozo.
Wanaelewa maneno ya siri na yenye faida juu ya kutawala .
Wameweza kuwafanya watu kuwa mpumbavu na wajinga juu ya maandiko na mafumbo tofauti tofauti ya dini.
Wana uelewa mkubwa sana juu ya Faida za ulimwengu wa kiroho unaopatikana kutokana na sanduku lile, na vitu vingine vitakatifu vilivyofichwa hivyo wakatengeneza nadharia nyingi sana kuaminisha ulimwengu juu ya sanduku ili kuwapoteza watu na wao kuendelea kufaidika na vilivyomo.

Sanduku halikufichwa huko Ethiopia kwa malikia wa Sheeba, wala halikufichwa kwa waarabu pale Makka wala halikufichwa kwa Wayahudi pale Israel, wala halipo kwa waitaliano pale Rome.

View attachment 2408245

Akili , Maarifa na Nguvu za utawala za makundi haya zinatokana na vitu kama hivyo vitakatifu ambavyo vimehifadhiwa na kutumika katika ulimwengu wa kiroho zaidi kama vilivyohifadhiwa vitu vingine
(Holy grail, Kinubi cha mfalme Daudi na hata hilo sanduku la Agano na vinginevyo)

Vitu kama hivyo (sanduku la Agano) vinawapa nguvu.
hawaogopi kifo, inawafanya wawe na nguvu Inawapa udhibiti wa akili na mwili wao na wanadamu wengine.
Inawapa mamlaka ya kutawala dunia na nguvu nyingine nyingi
Endapo vitu hivi vitarudi katika mkono sahihi basi hapo hapo ndipo nguvu itarud kama ilivyo kawaida

Na hapa ndipo kiu ya kumsubiri mwana wa Adamu (Issa au Yesu mtoto Wa marym) inapozidi kuwa kubwa ili aje kufichukua mengi msiyoyajua.

Naam nikipata wasaa nitaambatanisha jina la documentary ile

Kipindi fulani wakati najaribu kupata darasa kuhusu
Holy grail jinsi ilivyofichwa na kutumika kunufaisha watu ndipo nikajiuliza yawezekana hata sanduku la Agano ambalo sisi bado hatujui lilipo nalo limehifadhiwa na hawa mabwana wakubwa wa Dunia. Ili waendelee kunufaika na matunda ya faida zake

Wewe unadhani vipi!??

Shuqraani

DaVincii XV
shukran
 
Jamiiforums ni kisima Cha maarifa na sio matusi. Kwa wale wenye kupenda mjadala huru na sio matusi karibuni. .

Kuna conspiracy nyingi sana mojawapo ni hiyo niliyosema kuwa ancient aliens threory Ina suggest hiki kifaa kilikuwa kama silaha. Na wanaoamini it is scientific made, ku connect na viumbe wa sayari nyingine ambao wanajulikana kama extraterrestrial 👾

Hawa viumbe waliaminika kuwa ni miungu kumbe lakini walikuwa ni viumbe vya kawaida. Mbali na wana wa Israel haya masanduku yalikuwa pia yalipatukana kwenye asili za watu wengine. Dunia ya Leo sio dunia ya kuzungumza bila ushahidi kwamba watu wanaweza connect dots kitu flani kwa nini Kiko hivi na vile. .

Mijadala hii pia haijaanza Leo hata wenzetu wakenya hapo na duniani inaendelea siku nyingi. Mfano:



Sijatulia coz Niko road ila nikitulia nitaonyesha asili ambazo mpaka Leo hii wanafanya Mila za sanduku za agano kwa kirefu. Ila kifupi
1. Ethiopia
2. Zimbabwe -
3. Japan - Hawa Hawana asili kabisa na wana wa Israel ila mpaka Leo hii wanafanya Ile walk ya jangwani sanduku likiwa mbele Yao

Kuna vitabu vingi vimeandikwa na huyu jamaa anaitwa Erick Von Danineck about ancient gods. Kwa wale wanapenda kumkosea ease vitabu vyake wapate kumkosoa. .

Nitaendelea. .
Shukraan kwa mchango mkuu.
 
Back
Top Bottom