Sarah Simbaulanga: Mwanamke wa kwanza kuiba pesa ndefu katika historia ya benki zote nchini

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Hivi huyu mwanamama alimaliza kifungo chake? Mnakumbuka kosa lake na jinsi ambavyo kesi yake ilikuwa ni kama simulizi la kutosadikika.

Hivi akisikia yanayofanyika hivi sasa huko aliko si anaona aliwahi kidogo tu..

-------------------





BAADHI YA MICHANGO ILIYOTOLEWA NA WADAU

 
Hivi huyu mwanamama alimaliza kifungo chake? Mnakumbuka kosa lake na jinsi ambavyo kesi yake ilikuwa ni kama simulizi la kutosadikika.. Hivi akisikia yanayofanyika hivi sasa huko aliko si anaona aliwahi kidogo tu..

Namkumbuka huyu mama, alikuwa mwajiriwa wa bank ya NBC miaka hiyo kabla wahuni hawajaitoa zawadi kwa makaburu. milioni 60 zilim.
 
Those were good old days, nakumbuka I was young then, lakini huyu mama nilimuona kama Jambazi wa hali ya juu. Lakini sasa wizi umekuwa sifa ukipata kazi nzuri after two years bila kujenga nyumba ya kifahari Jamii inakuona umezubaa. Its sad very sad.

The question is how did we get here? And can we ever go back to the good old days?
 
Hivi huyu mwanamama alimaliza kifungo chake? Mnakumbuka kosa lake na jinsi ambavyo kesi yake ilikuwa ni kama simulizi la kutosadikika.. Hivi akisikia yanayofanyika hivi sasa huko aliko si anaona aliwahi kidogo tu..

Duh mzee mimi umenikumbusha mbali huyu mama kwa sasa ndie anaweza kujitetea "vilikuwa vijisent tu"
 
Nani anajua huyu mama yuko wapi sasa? nakumbuka tulishangaa sana miaka ile mwanamke kuiba pesa kama ile!!!

Sio mwanamke tu, kipindi kile kuiba pesa ilikuwa ni jambo la aibu, yaani watu walikuwa wanakushangaa na sio wanakuadmire sahizi mtu ukiiba watu wanakusifia (hawajui kwamba hizo ni pesa zao wenye),

Kweli akili zetu zipo kwenye reverse gear for some time now, tunazidi kuwa mazuzu as days goes on (mind evolution yetu ina-move from brightness to foolishness).
 
Ninachokumbuka ni kuwa huyu Mama alikuwapua dola za marekani nyingi sana akataka kutoroka nazo nje ya nchi ila kabla hajafanikiwa dili likafumuka wakawa wanafukuzwa mpaka walipo kamatwa na hela mkononi. Nakumbuka kuna wakati yaliwahi toka mashati ya ujiuji (Kitambaa kama cha magauni ya CHARANGA kwa wanaoyakumbuka) yenye picha za dola za marekani tukawa tunayaita SIMBAULANGA.

Kweli kabisa mwanakijiji huyu mama aliwahi, maana enzi zile wizi ulikuwa haulindwi wala kusukiwa mikakati IKULU kama ilivyo sasa ambapo angechukua kiualaini na kuzikuta nje zinamsubiri badala ya kukimbia na bulungutu.
 


Kama huna kumbukumbu ya zamaniiiiii basi una matatizo, au mwenzetu umefuta kumbukumbu yako yote unaishi katika sasa tu?
 
Namkumbuka huyu mama akiitwa Sarah Martin Simbaulanga. Kusema kweli mimi ni mmoja walio frommhurumia kukamatwa. Nilimuona kama sterling fulani wa bonge la movie.

Pesa alizihamishia kwa king'asti chake Mombasa, ambaye kiumri ni ki benten, Toroha Mohamed Toroha, wakanunua mabasi ya coaster kibao ambayo nayo yalitaifishwa.

Hata aliyoyafanya Kasusura was an action movie. Kitendo cha kudakwa kirahisi ni kama sterling kauwawa, kwa kawaida Sterling huwa hauwawi.

P
 
ukishawajua ndio nini:coffee:tujuzeni jamani alikuwa nani na alifanya nini katika historia ya nchi yetu.

Hakufanya jema mkulu, huyu mama alikuwa mwizi,aliiba, aliiba fedha nyingi, alikuwa pale NBC Foreign branch sasa hivi ni makao makuu ya NMB Post mpya. Alishirikiana na kijana mmoja wa kiarabu jina lake nimesahau kigodo.Back then ilikuwa fedha nyingi approximately 60ml
 
Embu tupe data kidogo Mkuu...sijui km namfaham sana so far as navyojua ni mwanamama aggressive aliyetumia kalamu yake vizuri kuiibia serikali!...sina hakika na kumbu kumbu zangu!

Huyu mama aliiba pesa milioni 30 enzi hizo zikiwa interms of cash na travellers cheque, akakimbilia Nairobi..ambako alikamatwa akiwa na mshirika wake TOROHA Mohamed TOROHA. Walirudishwa nyumbani ambako kwanza mali zao zote zilikamatwa yakiwemo mabasi etc na baadaye walishitakiwa mahakamani.

Walihukumiwa miaka 35 na kwa kuwa makosa yote yalitendeka kwa mara moja wakala miaka 7. nadhani hawa watakuwa wameshaachiwa na atakuwa uswahilini.

Kiukweli ile kesi ilikuwa ni mfano wa kesi za mwanzoo za kifisadi lakini ajabu ni kuwa siku hizi mafisadi hawakamatwi kirahisi na hata wanaokamatwa serikali inashindwa kuwa convict.

Nadhani Sara Martin Simbaulanga na Toroha Mohamed Toroha, watakuwa wanasikitika sana kuona wenzao siku hizi wanaiba and the go away with it.
 


Nadhani Sara Martin Simbaulanga.....na Toroha Mohamed Toroha..watakuwa wanasikitika sana kuona wenzao siku hizi wanaiba and the go away with it...


ndiyo point niliyotaka kuleta.. kwanini tulikuwa very serious wakati ule..? Leo kuna mama mwingine anatuhumiwa kuiba bilioni 1.3 na hakuna watu wanaoshtuka!
 
Namjua vizuri sana mama Sarah Martin Simbaulanga ni mlokole na ni mlalahoi anaonekana maeneo ya Mwenge mara chache chache.

Anajutia sana kitendo alichofanya wakati ule, Mwenyewe anasema haukuwa utashi wake bali aliponzwa na mpenzie Toroha Mohamed Toroha.

Amemrudia Mungu na anaendelea kuishi kwa amani tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…