Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 21,741
- 26,735
Anza na kuomba kazi ya ufagizi ofisi ya Lumumba ukiwa na kadi yako ya chama mfukoni, sasa hapo kuwa mchangamfu ukifika tu jifagilishe kwenye mlango mkuu na jitahidi kupokea mikoba ya mabosi waingiapo ofisini, usiwe na aibu watakuzoea tu. Kuna siku mmoja atakuita ofisini kutaka kukufahamu zaidi hspo sasa unaingia rasmi kwenye mfumo kwani utaeleza elimu yako na kilichokulazimisha kufanya kazi ya ufagizi, amini usiamini wiki haitapita utaingizwa kazi za ofisini, hapo sasa piga magwanda ya kijani kila siku. Rudi tena kwa aliyekuingiza ofisini mwombe ushauri jinsi ya kugombea nafasi za chini na ipi itakufaa kutokana na elimu yako japo kwa CCM si kigezo.Kuwa na kiasi cha Pesa cha Kuanzia Shilingi Bilioni Moja katika Akaunti zao ni jambo la kawaida mno kama ilivyo katika Kushindana Kwao kuitafuta Shilingi Trilioni ili wawe na uhakika wa Maisha yao ya Kiujumla na Fedha ya uhakika ya kuwarejesha tena Bungeni kwa Kushinda katika Majimbo yao kila Uchaguzi Mkuu ukiwadia.
Mtakaonielewa GENTAMYCINE hasa kwa huu Uzi wangu kwa Kuusoma between the lines nawatakieni kila la kheri huku Mimi mifukoni mwangu kwa sasa nikiwa na Shilingi Elfu Moja tu na sijui hata nyingine nitaipata wapi kutokana na Maisha magumu na ya Dhiki Kubwa niliyonayo.
Ewe Mwenyezi Mungu fanya Maajabu yako Kwangu GENTAMYCINE ili nami Jina langu kamili la Kalemera Rwigyema Mazimpaka Kadogoo Kisungura lifike rasmi kwa Mteuwaji Rais Samia nami niwe Waziri ili haraka sana nianze kuitafuta Shilingi Milioni 500 kisha niwatafute Wenzangu wenye Shilingi Bilioni katika Akaunti zao kisha baadae nianze kuitafuta Trilioni kama wanavyoitafuta walioko sasa.
Nakutakia kila la kheri.